bandugu, maggid mjengwa kapata dhamana. kawekewa dhamana na saed kubenea na mbarakah islam usiku huu yapata saa tatu hivi. nakumbuka leo asubuhi yapata majira ya saa nne hivi nilipigiwa simu na maggid mjengwa akanambia yuo makao makuu ya polisi gorofa ya saba chumba namba 704 na kwamba alikuwa ananihitaji nifike huko polisi nimshuhudie akitoa/akiandika maelezo yake kuhusiana na kuhusika kwake au kutohusika na masahibu yaliyompata absalom kibanda ya kutekwa, kuteswa na kujeruhiwa. pamoja na kumhurumia maggid mjengwa kama rafiki na mdogo wangu katika fani ya uandishi wa habari nilimweleza kuwa nisingeweza kumsaidia kwa sababu tuhuma zinazomkabili zinagusa maslahi ya mteja wangu absalom kibanda ambaye mimi ndiye ninayemtetea katika kesi yake ya uchochezi inayoendelea katika mahakama ya hakimu mkazi kisutu. hata hivyo nilijitahidi kumtafutia wakili mwingine ambapo nilimpata wakili aitwaye jacquiline rweyongeza ambaye nilimsindikiza hadi polisi makao makuu na mimi mwenyewe kumtambulisha kwa maggid mbele ya mapolisi yapatayo matano chini ya advocate nyombi aliyepata kuwa rpc mbeya na sasa yuko makao makuu ya polisi. nadhani taarifa hii inasaidia kumaliza kiu ya habari hii ya kukamatwa maggid kwa wanamabadiliko. kicheere, tungi, kigamboni, tanganyika territory --- On Sat, 4/13/13, heche suguta <hechesuguta29@yahoo.com> wrote:
|
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
0 comments:
Post a Comment