Thursday, 18 October 2012

Re: [wanabidii] Vurugu Ukanda wa Pwani una Mkono wa mataifa ya Mashariki ya Kati

Fahamu kuwa upo ktk taifa la mchanganyiko sio kama kwa wengine. Jee, iwapo askari naye ni wa dini hiyo na anakubaliana na hayo wasemayo atakwenda mapema kukamata? Jee, kama walikwisha kuwahi kuua askari wakamkata kichwa na anayekwenda anakwenda kwa gari inayopita barabarani sio helikopta si ataogopa petroli, mawe na magogo atauawa na umma nao wapo wachache? Askari mmasai au mkurya atakwenda kukamata wa makabila hayo ambao ni wezi wa mifugo wanaoua watu? Ilibidi yale mauaji ya Serengeti-mkoa wa Mara na mapigano yaliyozagaa mpaka kufikia kuteka vituo vya polisi kuvivamia ili wenzao watolewe kufanyike kazi ya ziada. Mwaka 1993-1994 walipeleka askari Mugumu na maeneo mengine huko na hao askari walitolewa Zanzibar kwani jeshi la Tanganyika bara ni watu wa Mkoa wa Mara kama si 80% enzi hizo basi ni 50%. Na mkoloni alifanya hivi ili kupunguza mapigano, wizi wa mifuko na vurugu nyingine ambazo zilionekana kuathiri productivity na wamasai akatengeneza Maasai resrrve kutoka humo ni kwa kibali kuelekea kokote kule (soma Colonial District Books National archives). wapigane Wanyanjali na askali ni Mnyanchali kutakuwa na ufanisi? 
 
Hata akina Suleiman Kova au rais akikemea ataambiwa tayari amekwisha kubatizwa. Lawama zitakuwepo na ni hivyo wakimuwinda na kumtishia Kadhi kwa vile labda hakubaliani nao mambo fulani. Kama ni Mafuta na Gas-bara ni mengi Mtwara, Songosongo, Mafia labda na maeneo mengine.
 Kwa sasa Mtwara si ile tena ya zamani wamejaa sasa hivi karibuni itakuwa another capetown.
  
Mafia wapo busy wafaransa baharini miaka wakichimba na mpaka meli ya uchimbaji ikavamia miaka ya karibuni na wasomali wakitaka kuiteka.
 
Ujenzi wa bandari Mafia na ujenzi wa International Airport Mafia wanauona na kuusikia. Gas na mafuta yanachimbwa kabla hawajagundua yao, mbona sisi hatukufanya vurugu kusema hatuwataki kwa vile tumegundua hiki au kile? Viongozi wa dini  na wanasiasa wahusike kuelimisha jamii sio kuangamiza na kuchochea-tujifunze kutoka kwa wenzetu tunaona ktk TV. Mbona hata huko ktk dini moja kubwa ya aina moja (Somalia, Syria, Afganistan, Misri, Libya, Mali etc) vikianza haviishi wenyewe kwa wenyewe hakuna usalama wanapigana tu. Hivi hapa petu suala ni dini ya Kiislamu kweli kuwa inaonewa na wakristo hili ni la ukweli kweli.
 
Ugomvi kidogo kuchoma makanisa-yamekosa nini? Huko Mafia 2008 wavuvi tika ZNZ walipokuwa wanavua ndani ya Marine Park Mafia na jamaa zao wa kule na kutakiwa kuondoka wakaenda na petroli kama silaha ikawa vurugu ya ki-dini kumbe hoja ilikuwa kuvua ndani ya conservation area ya samaki. Serikali haikujibu mapigo yao ya mabomu ya petroli, iliweka patrol tu na askari ikiwatazama na mitutu mkononi. Huku kutazama tu kutatuponza. Mfano wakiingia shule mojawapo ya kanisa na kuchoma wanafunzi itakuwaje? Jee, wakristu wakiamua kulipiza kisasi-tutafika? Hebu kuwekwe kongamano zirushwe na radio na TV kuelimisha.
God Bless us.
 


--- On Thu, 18/10/12, Yona Maro <oldmoshi@gmail.com> wrote:

From: Yona Maro <oldmoshi@gmail.com>
Subject: [wanabidii] Vurugu Ukanda wa Pwani una Mkono wa mataifa ya Mashariki ya Kati
To: "wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com>, "Wanazuoni" <wanazuoni@yahoogroups.com>
Date: Thursday, 18 October, 2012, 14:20

Vurugu Ukanda wa Pwani una Mkono wa Waarabu


Ndugu zangu


Hizi virugu nyingi zinazoendelea haswa upande wa pwani wa afrika mashariki zina mkono wa Mataifa makubwa ya kiarabu ambayo yanafikiri huu ugunduzi wa mafuta na gesi kwenye ukanda huu unaweza kuathiri biashara yao ya mafuta .


Hii imetokea Niger Delta kwa kuanzisha uasi ambao unaendelea mpaka leo na huko kaskazini mwa naigeria kwa kisingizio cha Dini .


Katika mipango hii kuna viongozi wa vyama vya siasa wanaotumika kwa kujua kwamba wanatetea dini zao kumbe wanaowafadhili wameangalia eneo kubwa zaidi .


Ni vizuri wananchi waambiwe ukweli haswa hao wanaokubali kutumika kwenye hila na hujuma dhidi ya taifa lao .


Pia ni vizuri vyombo vyetu vya usalama haswa idara ya usalama wa taifa ibadilishe mtindo wake wa utendaji na uwajibikaji na ushirikiano wake na vyombo vingine vya dola na taasisi binafsi uongezwe maradufu .


Inashangaza kuona askari walichelewa kwa dakika zaidi ya 30 huko Zanzibar baada ya wananchi kuanza kujikusanya ina maana kulikuwa na hitilafu ya taarifa hapa .


Huku mbagala pia kwa kitendo cha mhalifu kupelekwa kituo cha polisi ilitakiwa kuclick vichwani kuhusu uwezekano wa vitu kama hivyo kutokea lakini yote inaonyesha taarifa zilichelewa au ushirikiano ulikuwa hafifu .

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

0 comments:

Post a Comment