Niombe waislamu safi wajitokeze kwa wingi kulaani matendo haya ya uvunjifu wa amani. Redio za kiislamu zisitumike kuchochea vurugu bali zilaani vurugu na kutoa mafundisho safi km Mtume Mohamad SAW alivyofundisha.
Wahuni wachache ambao kwa bahati mbaya sana wanatumia majina yatumiwayo na waislamu safi wakikamatwa na polisi, tuwaache sheria ichukue mkondo wake bila mashinikizo ya kuwataka waachiwe. Misikiti kamwe isitumike kama kijiwe cha kukutanikia kuanzisha mashambulizi ya kisasi dhidi ya makanisa. Viongozi wa dini km kweli hawawatumi hao wahuni wawakatae na wasikubali misikiti kutumika kama kinga mara wahuni hao wakutanapo na rungu la dola. Tukiwaendekeza nchi
hii haitatawalika na waislamu safi ambao sasa wanakaa kimya nao watakosa pa kuishi kwa amani.
Polisi ichangamke isiendelee kulala, amani haipo tena. Sasa tunaanza eti kufikiria kukaa nyumbani au kutokuwa maeneo ya kanisani ifikapo siku za jumapili saa za mchana. Ofisi za balozi mbalimbali eti zinaanza kutoa taadhali kwa wafanyakazi wao kuwa waangalifu siku za ijumaa. Tunakwenda wapi?
William Kihigwa
William Kihigwa