Ndugu Wanabidii Mara nyingi sipendi kuchangia mada kama hizi zinazohusu dini za watu bila kuwa na ushahidi wa kutosha kuhusu kile ninachotaka kuchangia lakini kwa upotoshwaji huu tena unaofanywa na mtu niliyekuwa na muamini kama Yona Maro naanza kupata wasiwasi na madhumuni ya uwepo wa forum hii ya wanabidii. Mwanzoni nilijua ipo kwa ajili ya wanajamii wote wapendao mabadiliko japo baadae nikaona inaelekea zaidi katika mrengo wa kiCDM zaidi japo hilo halikunisumbua sana kwa sababu ziku zote naamini katika mabadiliko hasa yenye positive results bila ya kuathiri values zetu. Lakini kwa hili aliloandika Ndugu Yona Maro katu siliachi lipite hivihivi. Kwanza tatizo la kwanza ni hii historia tuliyosoma. Historia iliyopikwa kwa kuwaita wengine washeni na wengine wastaarabu. Ni nani asiyejua kuwa hawa watumwa walikuwa wakipelekwa katika mashamba ya mabepri huko Ulaya??? Nani hapa wakulaumiwa muuzaji au mnunuzi???? Na wale walioingia kwa kujiita Wamissionari na kujifanya eti wana malengo ya kuleta "ustaarabu" lkn mwishowe walitutawala na kuchukua maliasili zetu na kuuwa mababu zetu waliowapinga, mbona historia haiwasemi????? Sasa kwa hili la "Vurugu za Ukanda wa Pwani" eti kuhusisha mataifa ya Mashariki ya Kati?????? Haliniingii akilini kabisa. Ni kweli mimi si mwana historia, nimesomea Uhandisi (Engineering) lakini historia niliyosoma ya sekondari school na kwenye vitabu na mitandao mbalimbali inatosha kabisa kulisemea hili. Ndio maana naliita ni UPOTOSHWAJI A MAKUSUDI. Ni nani asiyejua kuwa vurugu zote zinazohusu rasilimali duniani chanzo chake ni mataifa ya Magharibi hasa Marekani???? Ukiondoa Israel ni taifa gani la Mashariki ya kati lenye jeuri ya kuja Afrika na kugombania mafuta au gesi au madini???? Hizi tunazoziita vurugu za Pwani ni matokeo ya mfumo uliojengwa siku nyingi sana katika nchi yetu hii. Na inapotokea kundi fulani la watu linakosa msaada linalouhitaji kwa muda mrefu na kuhisi halisikilizwi huamua kujichukulia sheria zake lenyewe. Ni ujinga kufikiri eti hao wanaofanya vurugu wanatumwa eti na mataifa ya Mashariki ya Kati??????? Ni aibu kwa kijana msomi wa karne hii kuwa na fikra finyu kama hizi. Inasikitisha sana. Ndio maana huwa naamini upendo wa kweli miongoni mwa Watanzania hakuna. Ni chuki na hasama za kidini ambazo hazina nafasi katika karne hii. Nina wasiwasi na mafunzo tunayopata kutoka kwa viongozi wetu wa dini. MUNGU IBARIKI TANZANIA. AHSANTENI SANA. Kwa mawasiliano. 0713322553 --- On Thu, 10/18/12, Emmanuel Sulle <esulle17@gmail.com> wrote:
|
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
0 comments:
Post a Comment