Thursday, 14 April 2016

Re: [wanabidii] Ni Afadhali Mtu Mmoja Afe

Mimi nadhani issue ilikuwa kuhusu kazi ngumu ya kuwa rais na kardinary akawa anamtia moyo kwamba ni afadhali alikubali kuwa rais (kufa kwa ajili ya wengi). Hivyo, yalikuwa mazungumzo ya hao wawili na siyo kwa ajili ya mtu mwingine.

2016-04-14 14:16 GMT+03:00 'ELISA MUHINGO' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>:
Nikijikita kwwa maneno aliyoyatumia Kardinali mimi nitafikiri kuwa hawa wawili walikuwa wanaongea juu ya mtu fulani ambaye Rais anasita kumchukulia hatua. Kardinali akamshauri kuwa ''Heri kumtosa (kufa) huyo kuliko kulinyima (kuteketea) haki taifa.
Nani haoni yanayotokea? mathalan: Polisi kusita kuleta mkataba unaoonyesha mabilioni yameliwa. Nani anajua kama mkataba ukiletwa mbele kuna mtu ataumbuka? kama wawili hawa waliona kuumbuka huko ni 'kufa' kwa nini Kardinali asimshauri kumuumbua huyo kuliko bilioni 37 kuyeyuka kama pelemende kwenye ulimi? Kwa ufupi sijatafsiri 'kufa' na ''kuteketea' kama kifo hasa kama cha Sokoine. Au nimepotea?
Elisa
--------------------------------------------
On Thu, 4/14/16, 'Bart Mkinga' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

 Subject: [wanabidii] Ni Afadhali Mtu Mmoja Afe
 To: "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>
 Date: Thursday, April 14, 2016, 11:22 AM

 Magazeti
 leo yameandika kile alichokisema Mwadhama Polycarpo Kadinali
 Pengo wakati wa ibada ya kumbukumbu ya Hayati Edward Moringe
 Sokoine aliyefariki kwenye ajali ya gari 12 Aprili 1984. Kwa
 wale ambao walikuwa hawajazaliwa, ni kwamba kifo cha Sokoine
 ni kifo kilicholeta simanzi kubwa kwa karibia Watanzania
 wote kuanzia tuliokuwa wadogo wakati huo mpaka kwa wakubwa.
 Na watu wengi mpaka leo hawaelewi ilitokeaje gari ya Waziri
 Mkuu kugongwa na gari nyingine, mbele kukiwa na magari,
 nyuma kukiwa na magari, Waziri Mkuu akiwa amekaa kiti cha
 nyuma, lakini akafariki yeye pekee yake. Lakini kwa sababu
 ya heshima na imani kubwa ambayo Watanzania tulikuwa nayo
 kwa kiongozi wetu mkuu, Mwalimu Nyerere ambaye naye msiba
 huo ulimchanganya sana hadi kulia hadharani, hatukuhoji
 zaidi maana katika hotuba yake ya simanzi kubwa alituambia,
 'Watanzania tukubali kuwa Sokoine amefariki kwa ajali ya
 gari', wote tuliyachukua maneno hayo kwa imani kubwa
 mpaka leo. Mungu amjalie raha ya milele marehemu Sokoine
 kutokana na mapenzi yake na matumizi ya vipawa vyake
 alivyopewa na mwenyezi Mungu kwaajili ya faida ya watu
 wanyonge na maskini.
 Ni kwenye ibada hiyo ya Kumkumbuka Hayati Sokoine
 ndipo Mwadhama Polycarp Kadinali Pengo alipoeleza kuwa Rais
 Magufuli akiwa Chato alimpigia simu, na kati ya mambo ambayo
 Rais Magufuli alimwambia yeye Kadinali ni kuwa, 'Kama
 ningejua Urais ndiyo hivi nisingegombea', naye Kadinali
 akamwambia Rais, 'Ni afadhali mtu mmoja afe lakini Taifa
 lisiteketee'.
 Wengi tunaendelea kutafakari, ni nini hawa watu
 wawili waliongea mpaka kufikia huko? Japo ni rahisi kusema
 kuwa kwa mzalendo wa kweli, huwa yupo tayari kufa kwaajili
 ya watu wengine lakini kifo ni kigumu na bahati nzuri
 hutokea bila ya kuwa na taarifa ya kabla. Sisi wengine
 tutaendelea kuomba kusiwepo na wa kufa na pia Taifa
 lisiteketee.
 Binafsi ningekataa tamaa kama ningesikia kuwa Rais
 Magufuli alimwambia Kadinali kuwa anamshukuru Mungu
 amemsaidia kuwa Rais na sasa anafurahia nafasi aliyopewa ya
 kuwaongoza Watanzania. Tafsiri rahisi ingekuwa hajali shida
 za wananchi. Nchi hii ina watu asilimia kubwa wanaoishi kwa
 shida na kwa kubahatisha kuliko idadi ya wenye uhakika wa
 maisha. Kuna watu wanakufa muda usio wao kwa sababu ya
 kukosa matibabu, kupata matibabu duni au kutibiwa kwa dawa
 zilizo chini ya viwango. Kuna watu wanakufa kila siku
 kwaajili za magari, pikipiki, mitumbwi na basikeli kwa
 sababu ya udini wa vyombo wanavyosafiria, barabara mbaya,
 ukosefu wa wataalam na vyombo vya uokoaji, n.k. Lakini pia
 kuna watu wasiopata chakula cha kutosha au chakula bora,
 kuna watu wana makazi duni kabisa, kuna watu wanafikiria ni
 kwa namna gani watanunua hata blanketi au shati. Kuna watoto
 pia ambao Mungu kawajalia vipaji mbalimbali lakini kutokana
 na umaskini wa wazazi wao kamwe vipaji vyao havitakuja
 kuonekana.
 Hayo yote yanatokea wakati tukiwa na rasilimali
 ambazo kila mmoja anazijua. Hayo yote yanatokea Tanzania
 ikiwa na uongozi wa kwake yenyewe kwa zaidi ya miaka 50.
 Hayo yote yanatokea tukijidai kuwa tuna uongozi bora, sera
 na mipango mizuri ya uchumi, tuna sheria na vyombo vya
 kusimamia utawala wa sheria, vyombo vya kusimamia maadili ya
 uongozi wa umma, tuna taasisi mbalimbali za kusimamia
 mipango ya kuondoa umaskini usiondoka. n.k.
 Kama miaka yote tumekuwa na hayo yote lakini nchi
 haikupiga hatua, ina maana vyombo hivyo ama vyote au vilivyo
 vingi vina matatizo makubwa. Na mahali pa kuanzia siyo
 kuviboresha bali kuviunda upya vikiwa na maelekezo mapya,
 sheria mpya za kuviendesha na za kuvisimamia. Ili kuweza
 kuyafanya haya kuna watu wanatakiwa kuondolewa, na kuna watu
 wapya wenye fikra mpya wanatakiwa kuingizwa. Na hapa ndipo
 ugumu wa kazi ya Urais unapokuja.
 Maana wanaotakiwa kuondolewa ni watu ambao nyuso
 zao siyo ngeni kwa Rais Magufuli. Wengine ni makada wa Chama
 aliowafahamu kwa miaka mingi. Wengine ni marafiki
 aliowafahamu kwa miaka mingi. Wengine huenda waliwahi kuwa
 wakubwa zake katika utumishi wa umma, wengine ndugu au
 marafiki wa viongozi wenzake. Wengine ni watu aliowategemea
 sana kuwa msaada katika uongozi wake lakini anagundua kuwa
 siyo msaada bali ni 'majipu'. Kuweza kuwachukulia
 watu wa karibu yako, ambao sura na sauti zao unazijua, kwa
 faida ya watu ambao hata majina yao huyajui, inahitaji roho
 ya pekee, na roho hiyo iwe ya Kimungu.
 Mheshimiwa Membe aliwahi kudokeza ilivyo ngumu
 kumchukulia hatua mtu unayemfahamu na uliyemteua
 mwenyewe.
 Lakini tunachoweza kumwambia Mheshimiwa Rais ni
 kuwa utendaji bora hupimwa katika ugumu na siyo katika
 urahisi. Ni aheri amegundua mapema kuwa kazi ya Urais ni
 ngumu, hasa unapoongoza nchi ambayo mifumo mbalimbali
 haifanyi kazi, sera zipo kwenye mafaili lakini hazifanyiwi
 kazi, sheria zipo kwenye makabrasha lakini zinapindishwa kwa
 namna watu wenye malaka wanavyotaka, n.k.
 Jambo la kujiuliza, je watendaje wengine wote nao
 wanatambua kuwa kazi zao ni ngumu? Mawaziri wote wanatambua
 kuwa uwaziri ni kazi ngumu? Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa
 Wilaya wanatambua kuwa kazi yao ni ngumu? Polisi wanatambua
 kuwa kuwalinda wananchi, tena kwa haki bila upendeleo ni
 kazi ngumu? Mahakama zinatambua kuwa kutoa hukumu kwa wakati
 wake na kwa haki ni kazi ngumu? Mifuko ya kijamii wanajua
 kuwahakikishia maisha mazuri wanachama wao badala ya
 kuhangaika na majengo ya kifahari yasiyowasaidia moja kwa
 moja wanachama wao ni kazi ngumu? Madaktari wanatambua kuwa
 kuwahudumia watanzania kwa upendo na uadilifu ni kazi ngumu?
 Au hawa wengine wanasali na kumshukuru Mungu kuwaweka mahali
 walipo?






 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya
 kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment