Wednesday 22 May 2013

[wanabidii]

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII

 

 

 

 

TANGAZO KWA UMMA

 

Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kupitia Tangazo lake kwenye Gazeti la Habari Leo la tarehe 20 Aprili, 2013 siku ya Jumamosi na la tarehe 23 Aprili, 2013 siku ya Jumanne na kwenye tovuti ya Wizara, ilitangaza nafasi mbalimbali  za kazi za Kada ya Afya zikiwemo za Maafisa Ustawi wa Jamii, Maafisa Ustawi wa Jamii Wasaidizi, Walezi wa Watoto, Maafisa Lishe na Maafisa Lishe Wasaidizi.

 

Wizara inapenda kuwajulisha waombaji wa nafasi za Kada tajwa hapo juu zitashughulikiwa na Ofisi ya Rais, Sekretarieti ya Ajira.

 

Hivyo, waombaji wote waliotuma maombi yao Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, wanajulishwa kuwa maombi yao yatapelekwa Sekretarieti ya Ajira kwa ajili ya uchambuzi na usaili.

 

Tangazo hili halihusu waombaji walioomba Kada mbalimbali za Afya ambazo zitashughulikiwa moja kwa moja na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii.

 

 

 

Kaimu Katibu Mkuu

WIZARA YA AFYA NA USTAWI WA JAMII

22 Mei, 2013

 

 

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

0 comments:

Post a Comment