Tuesday 28 May 2013

[wanabidii] POLICCM NA MKAKATI MPYA WA KUBAMBIKA KESI YA UGAIDI.

Wadau nyeti mbili usiku wa leo ambazo pro CHADEMA mnapaswa kujiandaa kuzikabili kama CCM wataendelea na mpango wao kama ulivyopangwa ufanyike kuanzia kesho.
Kwanza kesho Team Lowassa, CCM na polisi kupitia gazeti moja ambalo mmoja wa wahariri wake ni mtu unethical kupindukia na karibuni ameweka rekodi ya kujitenga na wenzake, wamepanga kutunga na kupika stori ikiwa ni mwendelezo wa kukipaka matope CHADEMA na issues za ugaidi.

Watamtumia mwana CCM mmoja kutoka Mbeya ambaye aliwahi kuwa CHADEMA kabla hajahama miaka takriban miwili iliyopita, baada ya kuuza 'ubunge' mara mbili, mara ya kwanza kwa kujifanya amekosea namna ya kutekeleza masharti ya kisheria.

Atanukuliwa na gazeti hilo akijitambulisha kuwa eti aliwahi kuwa mjumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya CHADEMA, na katika kikao kimoja chini ya uenyekiti wa Kamanda Mbowe, walipanga mipango ya ugaidi.
Gazeti hilo litalotumika ni moja ya magazeti ambayo CCM, wakiwemo Team Lowassa na polisi wameamua kulitumia kusukuma agenda ya kukipaka matope CHADEMA na viongozi wake wakuu kwa kashfa za kupika, lengo ikiwa ni kuwahusisha viongozi wakuu wa chama hicho na hatimaye CCM watekeleze wanachokitaka.

PILI
Kwa takriban zaidi ya siku 10 sasa, polisi mkoani Mtwara wamekuwa wakimshikilia Kaimu Katibu wa CHADEMA Mkoa wa Mtwara, anayeitwa Melikizedeki, nimefanikiwa kupata jina moja kwa hataka niliyokuwa nayo kuleta hii habari hapa jamvini.

PolisiCCM wa Mtwara walimkamata tangu Ijumaa ya Mei 17. Tangu wakati huo amenyimwa haki zake za msingi, ikiwemo kuonana na mwanasheria wake, hata wakati wa kuandikishwa maelezo yake! Hajaruhusiwa kabisa kukutana na ndugu zake. Mwanzoni hata chakula hakuwa akipewa. Hadi sasa kwa siku zote hizo, amenyimwa kabisa dhamana.

Hiyo tisa, kumi ni kwamba polisi walipomkamata walimyang'anya simu yake. Sasa baada ya kukaa nayo muda wote huo, wameikagua bila kuwepo mtu yeyote mwingine kama shahidi, wameshinikizwa wamfungulie kesi ya ugaidi na uchochezi, kisa eti kwenye simu yake wamekuta picha za nyumba ya Hawa Ghasia na George Mkuchika na meseji zingine.
Polisi wanatumika vibaya sasa, kuliko hata ile mipira...hivi kweli mtu unawezaje kuchukua simu ya mtu, umekaa nayo huko, hakuna anayejua umeifanya nini, umeingiza vitu gani, kisha huo ndiyo uwe ushahidi mahakamani? 

Habari zinasema kuwa hata ndani ya jeshi la polisi huko Mtwara wanabishana sana kupeleka hiyo kesi mahakamani. Wengine wachache waliobakiwa na akili za kupembua chenga, mchele na pumba, wanaopenda kutumikia jeshi hilo kwa weledi na taaluma na maadili, wanaona hicho kitu hakikubaliki. Walio mafisadi, polisiCCM wanasukuma kesi ifikishws mahakamani ikibidi hata kesho.

Ni mtu mgeni huko Mtwara, yaani si mzaliwa wa huko. Amekwenda kikazi. Asilia, kwao ni Kagera. Anaelezwa kuwa mtu mwenye msimamo kwa sababu anajua vitu. Lakini kinachoonekana ni kwamba baadhi ya viongozi wa CHADEMA wasiokuwa waaminifu huko Mtwara hasa ngazi ya wilaya wamemsaliti mwenzao. Kwanza walichelewa sana kutoa taarifa makao makuu ili hatua za haraka zichukuliwe.

Pili, baadhi yao wamekuwa hawatoi ushirikiano wa dhati kumsaidia Melikizedeki ambaye anatajwa kuwa mfanyakazi wa moja ya NGO inayoshughulikia watoto yatima. Viongozi hao hivi karibuni, wakati wa sakata la gesi lilipoibuka mara ya kwanza kabisa, walirubuniwa na watu wa usalama wa taifa wilayani na DC, wakaletwa Dar es Salaam kuonana na Waziri Mkuu, bila hata kukitaarifu chama chao na kushirikisha uongozi. 
Bwana Melikizedeki kwa kutambua msimamo wa chama hicho katika masuala yanayoweza kuonekana kuwa ni kuwasaliti Watanzania ambao kimekuwa kikiwatetea, akapinga hiyo move ya hao wenzake, kwenye vikao na hata hadharani katika mahojiano na redio. Wakamchukia.

Taarifa zinasema Makao Makuu wamechukua hatua ya kutuma wanasheria haraka kwenda Mtwara.
Ni hayo kwa leo, wakati kesho tukisubiri Gazeti la kuendelea kutumika na kuzidi kujitangaza kuwa ni 'adui wa umma' kwa kupika na kutengeneza stori.

Chanzo: jamiiforums
Sent from my BlackBerry® smartphone provided by Airtel Tanzania.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.

0 comments:

Post a Comment