Thursday 9 May 2013

Re: [wanabidii] Zitto Kabwe : Taifa lina nyufa

Inawezekana wanayaona, ila wanayaona ya kawaida tu hayawezi kuleta madhara yoyote. Mpaka wayaone madhara ndio watasema ningejua!
 
Nitatoa mfano wa kwanza:  nina ndugu yangu, mtoto wake wa kidato cha tatu alimnunulia simu ya mkononi na wanamjazia hela za maongezi. Ukimpigia simu, kijana anapokea kama vile ni mtumishi. Kisa wanavijisenti wazazi.
Nilipomueleza kuwa huyu mtoto ni mdogo bado hajajifahamu vizuri, hii tabia ya matumizi ya simu inampunguzia muda wa kujisomea. Majibu ya kidato cha nne yakitoka mabaya nitawaomba msimseme mtoto. Wazazi mtakuwa mmechangia kwa kiasi kikubwa matokeo ya mtoto kuwa mabaya.
 
Juzi matokeo yametoka, nikawauliza vipi mtoto kafauluje? mtoto amepata division four inayokaribia zero!. Na wanamsema mtoto, nikawakumbusha na kuwaomba wasimseme mtoto.
 
Mfano wa pili:
Marehemu baba wa taifa aliona mbali kuwa Dini na ukabila vinaweza vikawa tatizo la umoja wetu. Pengine wengine walimuona kama anaota tu! Yale maono yake leo yanaanza kujitokeza na yakiwa na sura mbaya. Pengine kama mtapata nafasi kuongea na viongozi wenzie wa wakati ule, wataeleza namna walivyomuona yupo ndotoni.
 
Hitimisho: maono ni karama ambazo zinatolewa na mwenyezi mungu. Si kila mtu anazo hizo karama. 
Tuendelee kuwapenda viongozi wetu, tuyafanyie kazi mawazo ya jirani zetu hata kama wao wenyewe hatuwapendi. Kwa namna hii wote tunaweza kwenda peponi. 
 
 
 
 
 
From: denis Matanda <denis.matanda@gmail.com>
To: wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>
Sent: Thursday, May 9, 2013 11:41 AM
Subject: Re: [wanabidii] Zitto Kabwe : Taifa lina nyufa
Mhandisi, bila ya kuingilia uhuru wako wa kumkubali mheshimiwa Zitto, hivi ni kweli aliyoyasema kuna watu walikuwa hawajayaona?
On Wed, May 8, 2013 at 3:42 PM, ezekiel kunyaranyara <ekunyaranyara@yahoo.co.uk> wrote:
Mara nyingi huwa nasema huyu kijana anao uwezo mkubwa wa kuona mambo kwa mtizamo ambao wengi huwa hatuwezi kuuona kwa urahisi. Kwa mara nyingine katika maelezo haya amezidi kulithibitisha hilo kwa mtizamo wangu wzndugu.
KEM
Sent from Yahoo! Mail on Android
From: BILLEGEYA, Mussa <msbillegeya@yahoo.com>; To: wanabidii@googlegroups.com <wanabidii@googlegroups.com>; Subject: Re: [wanabidii] Zitto Kabwe : Taifa lina nyufa Sent: Wed, May 8, 2013 12:30:08 PM
Ati taifa lina Ufa? Au ni taifa gani mnazungumzia? kama ni Tanzania Mbona Kuta nyingi karibu zote za Vyumbani zimeshabomoka??? Ukuta wa nyuma na wenyewe umenagushwa na nanihii hivi majuzi!!!... Ufa upi mliouona leo?
 
BILLEGEYA, Mussa,
Twitter: @MBillegeya
From: ELISA MUHINGO <elisamuhingo@yahoo.com>
To: hamisznz@gmail.com; wanabidii@googlegroups.com
Sent: Wednesday, May 8, 2013 3:18 PM
Subject: Re: [wanabidii] Zitto Kabwe : Taifa lina nyufa
Lo! Nani hakuelewa hotuba hii? Swala la BAKWATA mbona kaliweka sawa? Natumaini anayetaka ukweli amegundua. Ni swala la kukubali tu. ----------Sent from my Nokia Phone------Original message------From: Abdalah Hamis <hamisznz@gmail.com>To: "Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com> Date: Wednesday, May 8, 2013 11:16:33 AM GMT+0300Subject: [wanabidii] Zitto Kabwe : Taifa lina nyufaNDUGU KABWE Z. ZITTO, MB – BUNGENI TAREHE 6 MEI, 2013Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili niwezekuchangia leo katika mjadala huu muhimu sana.Hapa Afrika kulikuwa kuna nchi, na bado ipo, inaitwa Ivory Coast. Ilikuwani nchi ambayo inasifika sana kwa amani na utulivu; na ilikuwa ni nchi ya kupigiwa mfano. Leo hii Ivory Coast imegawanyika vipande vipande. Ukiendaleo Ivory Coast unakuta wanaoitwa Ivorite na wanaoitwa wageni ambao wazaziwao walienda Ivory Coast kufanya kazi miaka mingi sana. Lakini pili katika mgawanyiko huo kuna mgawanyiko mkubwa sana wa kidini kati ya watu wa IvoryCoast wanaotokea Kaskazini na watu wa Ivory Coast wanaotokea Kusini.Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikuwa tuna Sierra Leone nchi ambayo wageni walikuwa wanakirimiwa katika hali ambayo haijawahi kutokea hapa duniani.Lakini leo Sierra Leone ina rekodi kubwa sana ya watu wenye ulemavu kwasababu ya vita ya wenyewe kwa wenyewe.Naomba nichukue nafasi hii kufuatia matukio ambayo yametokea hivi karibunina hasa jana na siku zilizopita ninanukuu hotuba ambayo Rais wa Awamu yaTatu Mheshimiwa Benjamin Mkapa aliitoa katika Bunge hili tarehe 4 Novemba,1998. Alisema: "Mr. Speaker, after three years of my presidency, I can dare to modify thewords of famous Zanzibar maestro Siti Binti Saada by saying, Tanzania is agood country, let one who wishes to come do so. God has showered blessings on our country. It is a country of unity, peace, love, rejoicing andexciding generosity. It is a country of people who love equality andjustice. Our national unity brings from our firm believe in equality ofhuman beings before God and before the Law. A Unity reinforced by correct policies of national building. Policies based on the principles of socialjustice, peace, harmony and development for all. A unity which is extrasensitive to policies, statements behavour and actions which may sore seedsdiscard hatred and suspicious among Tanzanias"Mheshimiwa Mwenyekiti sitatafsiri. Lakini naomba kila Mbunge ajiulize leoiwapo Rais Mkapa tukimpa fursa ya kuja kuhutubia Bunge hili anaweza akayatumia maneno haya tena? Hakuna mtanzania yoyote anayeweza kuthubutuleo kutumia maneno haya tena kwa sababu nchi yetu ina nyufa. Ina nyufaambazo kwa kujua au kwa kutokujua sisi kama watu ambao tumepewa wajibi na wananchi wa kuitunza nchi hii na kuipeleka pamoja tumejikuta tukiingiakatika kutoa kauli, maneno na vitendo ambavyo ni "irresponsible"vinavyopelekea kugawanya nchi; na yanayotokea sasa ni matumizi ya nyufahizo. Asubuhi hapa Mheshimiwa Lissu amesema, ametoa rekodi ya namna ambavyowanasiasa wa chama kinachoongoza (CCM) wamekuwa wakitoa kauli dhidi yavyama vya upinzani kuhusiana na masuala haya ya kidini. Wametoa mfano kuhusu chama cha CUF kilipoitwa chama cha waislam, wamekitolea mfano kuhusuCHADEMA kinavyoitwa mpaka sasa chama cha wakristo.Mheshimiwa Mwenyekiti, inawezekana ikawa ni rahisi sana tuka-"pointfingers" kwa wenzetu nyie, ni rahisi sana; lakini CUF wakati wanaitwa ni chama cha waislam ambao walikuwa hawaitwi ni chama cha waislamhawakunyoosha mkono kupinga. Wakati CHADEMA kinaitwa cha cha Kikristo ambaohawaitwi hivyo hawakunyoosha mkono. Matokeo yakeni nini? Tumejenga hofukubwa sana katika Taifa na hii ni lawama kwa wote. Wote kama nchi ili tuseme kwamba hapa tumekosea na tuanze upya.Mheshimiwa Mwenyekiti, adui anapokuja kwenye nyumba anaangalia ni wapiambapo ni rahisi kamba kukatika. Tumeji-"expose", tumejiweka wazi. Leo mtuanayetaka kuishughulikia Tanzania ata-deal na udini tu. Kwa sababu anajua watanzania hivi sasa wamegawanyika katika misingi hiyo. Jana limetokeatukio Arusha, angalia kwenye mitandao ya kijamii mara moja watanzaniawenyewe kwa wenyewe na ukiangalia majina ya watu wanaojadiliana wanaanzakusemana kwa dini zao. Ndiyo hatari ambayo tumeifikia; na ndio anachokitakaadui. Ni hicho. Atakuja, wanaitwa "Agent Provacateur", watapiga, mtabaki mnagombana ninyi. Tukiruhusu NYUFA hizi ziendelee hatutakuwa taifa. Nilazima sote kwa pamoja tusimame imara.Mheshimiwa Mwenyekiti, waislam na wakristo nchi hii hawana chuki kwa sababuwanaishi pamoja, ni marafiki, ni ndugu na kama ingekuwa kwa mfano waislam wanawachukia wakristo waislam wangevunja makanisa au wangechoma makanisa auwangewalipua wakristo. Wakati wa tukio la Mwembechai ndipo ambapo Polisiwaliingia mskitini wakaua watu, wanawake wakateswa kwenye magereza na kadhalika, watu wakakaa miezi mitano gerezani bila kushtakiwa lakinihapakuwa na mtukio yoyote ya namna hii. Waislam na wakristo wa nchi hii niwamoja. Wananchi wetu ni wa moja lakini sisi viongozi kwa kutoa kauliambazo ni "very irresponsible" tunawagawa watu wetu na ni lazima tukataehali hii. Tunafanya nini?Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima twende mbele. Kwanza ni lazima sasa Serikaliijenge utamaduni wa kufuatilia "grievances" zote ambazo wananchi wanazo bila kujali dini zao. Pili turuhusu watu kuwa huru kusema. Nimesikia hapawatu wanasema kwamba maandamano ni tatizo nakadhalika. Maandamano sitatizo, ukimzuia mtu kuandamana akiweka hasira zake kesho atafanya nini? Atatoka na bomu. Turuhusu "honest discussions" miongoni mwetu kama wananchi.Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu ni lazima sasa tuseme ya kwamba ni marufukukuwa na kauli za chuki "hate speeches". Kama hatuna vipengele vya kisheria tutunge sheria kwa sababu kumekuwa na "hate speeches" nyingi sana katikahii nchi na hakuna hatua ambazo zinachukuliwa.Mheshimiwa Mwenyekiti, state, dola, ihakikishe inajiondoa kwenye shughuliza uendeshaji wa mambo ya kidini. Ijiondoe kabisa. Kwa mfano kuna lawama yamuda mrefu sana ya waislam kuhusu BAKWATA, Waislamu miaka mingi toka mwaka1969 wakati Serikali imeunda BAKWATA wanalalamika. Leo hii Serikali ikitaka kuzungumza na waislam inafanya nini? Inaenda kuwaita BAKWATA. Hawanalegitimacy ya waislam, hamtaweza ku-addres masuala ya waislam lakini nirahisi sana kuweza kuongea na CCT kwa sababu CCT ni chombo ambacho kina uhuru wake. Kwa hiyo Serikali ijiondoe kwenye uendesheji wa shughuli zakidini. Hapa ndipo tutakapoweza kuhakikisha kwamba tunakuwa na nchi mojanchi ambayo ina amani.Mheshimiwa Mwenyekiti, namaliza kwa kusema nchi hii si ya waislam peke yake, nchi hii si ya wakristo peke yake. Nchi hii si ya CCM au ya CHADEMA,CUF au ya NCCR-Mageuzi au TLP na kadhalika. Nchi hii ni moja, nchi hii niya Jamhuiri ya Muungano wa Tanzania. Lazima wote tusimame kuhakikisha tunailinda Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaMheshimiwa Mwenyekiti, nakushuru sana asante.-- Send Emails to wanabidii@googlegroups.comKujiondoa Tuma Email kwenda wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma Disclaimer:Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines. --- You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out. -- Send Emails to wanabidii@googlegroups.comKujiondoa Tuma Email kwenda wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma Disclaimer:Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines. --- You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
mailto:wanabidii%2Bunsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to mailto:wanabidii%2Bunsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 
--
Wasalaam,
 
Denis Matanda,
Mine Planning Supt,
Tanzania.
 
" Low aim, not failure, is a crime"
-- Send Emails to wanabidii@googlegroups.com   Kujiondoa Tuma Email kwenda wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma   Disclaimer: Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines. --- You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group. To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com. For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.    

0 comments:

Post a Comment