Wanabidii, Janga lililomkumba Ikongoro ni kwa kuwa tu (kwa taarifa zilizopo) ameoa askari tena traffic. Kw hiyo wakati vurugu zinaanza kutoka kwa wananchi walengwa walikuwa askari. Na nyumba hiyo watu walikuwa wakisema ni ya askari huyo trafiki na siyo mwandidhi wa habari. Siku ya pili ikawa zamu ya askari kilipiza kisasi baada ya kuwa jana yake wamepokea kipigo cha kuridhisha kutoka kwa wananchi, hapa ndipo ile methali ya " Mtenda akitendewa ..........." ikatimia. Sasa lawama ziko kwa askari na wala siyo kwa wale waliosababisha vurugu hizi kwa maslahi binafsi. MTIZAMO mwingine ni kuwa mwandishi huyu anaripotia chombo cha umma ambacho nacho watu wamelazimishwa kuamini kwamba hakitoi taarifa sahihi kama vile wanavyotaka. Maana siku hizi mtu asipoandika kama wewe unavyotaka ni rahisi kusema anatumiwa au analipwa kuchafua wengine. Utaona sasa katika mazingira kama haya ni vigumu kwa wanahabari kuwa salama kwa namna yoyote ile. Usalama tu ni pale wananchi wote watazingatia wajibu wao wa msingi wa kulinda amani yao wao wenyewe kwanza bila kulazimishwa au kuingiliwa. Kama itatokea unanunuliwa basi uwe makini na tayari kwa kile kitakachotokea. Shibe yakomisije kuleta maafa kwa wengine. Kwangu mimi naona ikitokea hivi ni vizuri ukaweka wazi mapema msimamo wako kabla ya mambo hayajahafibika. Mfano mzuri ni magazeti ya UHURU na Tanzania Daima yana misimamo inayoeleweka na waandishi wake wanajulikana na hata kama hoja ikiandikwa katika magazeti haya yenye ujumbe mzito huoni watu wanahangaika kuuliza kwa nini kwa vile wanategemea gazeti kama hili liandike hivyo. Tatizo linakuja pale unayemwamini, na ambaye unajua hana upande wowote katika jambo linalobishaniwa anapoamua kuchukua upande na kupotosha kwa wazi wazi kabisa. Tuwe wawazi ili tuipeleke nchi yetu mbele. Hakuna anayetaka vurugu kama hizi ziendelee kutokea labda kama siyo mtz. Sent from Yahoo! Mail on Android |
From: salum mkango <salumkango@yahoo.com>;
To: wanabidii@googlegroups.com <wanabidii@googlegroups.com>;
Subject: Re: [wanabidii] Ujumbe Muhimu kwa Wadau wa Habari
Sent: Sat, May 25, 2013 10:18:41 AM
LINGONET LINDI Kwa aina ya polisi tulionao na kwa jinsi wanavyofanya kazi kwa hasira na kulipiza kisasi naamini inawezekana. Tumeshuhudia haya maeneo mengi ya nchi hasa panapokuwa na maandamano au shughuli nyingine za kisiasa hasa zinazowahusu wapinzani. Lkn wasipokuwepo polisi mkutano au maandamano yanaweza kufanyika pasipo vurugu yoyote ile. Lakini pia na nyie waandishi wa habari kwa nini mnatoa taarifa bila kuzithibitisha? Eti daraja limevunjwa, huwezi kuingia wala kutoka Mtwara lkn hakuna hata picha inayoonesha daraja hilo lililovunjwa. Mara ooh watu wengi wameuawa, jamani kwa nini tunafanya kazi kwa kubahatisha kwa kiasi hiki kana kwamba hawa waandishi sio professional??? Na hii sharia ya kumuingilia mtu ndani na kumpiga na kumkamata polisi wameitoa wapi? Unavunja duka au mlango wa nyumba eti ili umkamate mhalifu au uibe mali zake??? Na ulijuaje kama ndani ya hiyo nyumba kuna mhalifu wakati vurugu inaendelea nje??? Tuna kazi kubwa ya kuvitengeneza vyombo vyetu vya dola hasa polisi kufanya kazi kitaalamu bila kutumia nguvu kubwa kiasi hiki katika kudhibiti vurugu. Ni maoni yangu tu. Nawasilisha.
From: LINGONET Lindi <lingonetlindi@yahoo.co.uk> To: wanabidii@googlegroups.com Sent: Saturday, May 25, 2013 12:03 PM Subject: Re: [wanabidii] Ujumbe Muhimu kwa Wadau wa Habari wandugu vurugu za mtwara zimetawaliwa na habari za kishabiki sana ,nadhani hii ni moja ya mambo yanayokoleza sintofahamu katika kadhia yote ya gesi kusini mwa tanzania ,kwa bahati mbaya hata serikali imejiingiza katika kutumia propaganda kukabiliana na yanayojiri mtwara ,iliyofikia kuandaa vipindi maalumu kwa ajili ya kueneza uongo ili wananchi wa kusini waonekane ni wahalifu,waziri mkuu alikwenda mtwara akaongea na wananchi na kufikia makubaliano amabyo mpaka leo hajayatekeleza inayomwia vigumu tena leo kwenda mtwara kwa sababu hana majibu ya maswali atakayoulizwa kufuatia makubalano yao. lakini turudi katika vurugu za tarehe 22/5/2013 wananchi walibaki majumbani mwao ama kutekeleza wito wa vipeperusi au kwa hofu ya vurugu na biashara zote zilifungwa,ni askari tu waliokuwa wanaranda mjini na kupiga mabomu ya machozi bila ghasia zozote,kitendo kilichoamsha makundi ya vijana kuwarushia mawe kama hujuavyo katika jambo lolote kuna watu wanaoshabikia fujo,lakini la msingi walioanzisha vurugu ni polisi,baada ya kuzidiwa na gari ya kurusha maji ya kuwasha kushindwa kufanya kazi,wanajeshi waliingia kusaidia na maeneo yote ambayo jeshi waliwajibika hakukuwa na madhara makubwa kama yale ambayo polisi walikuwepo kwa kukamata wanaume na kuvunja maduka na kupora vitu,kwa bahati mbaya sana vyanzo vya habari vilizusha taarifa zisikuwa na ukweli na kueleza kuwa daraja la mikindani limevunjwa na huwezi kuingia mtwra jambo ambalo si sahihi,siku ya pili ya tarehe 23/5/2013 ndipo polisi walipofanya fujo kubwa sana katika maemeo ya magomeni,chipuputa,mangowela mdenga na tandika.maeneo yote ya madukani shangani railway ambayo wanajeshi walikuwepo hakukuwa na vurugu kwa vile wanajeshi walikuwa wanafanya kazi bila kupora mali wala kuingia majumbani kuwachomoa watu. hivyo dhamira yangu hapa ni tujitahidi kueleza hali halisi ilituweze kupata muafaka huku tukijitahidi kuondoa tabia ya wananchi kufanya vurugu wakati wakudai haki na kuwa na jeshi la polisi linalofanya kazi kwa mujibu wa taratibu na sheria wakati waandishi wa habari kama huna chanzo cha habari usizushe taarifa ambayo inaweza kuharibu amani yetu,mwandishi amekimbia fujo amejificha kuogopa kupigwa lakini anasema daraja limevunja bila kuona haya ndio mambo yanayozidisha sintofahamu --- On Thu, 23/5/13, denis Matanda <denis.matanda@gmail.com> wrote: From: denis Matanda <denis.matanda@gmail.com> Subject: Re: [wanabidii] Ujumbe Muhimu kwa Wadau wa Habari To: "wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com> Date: Thursday, 23 May, 2013, 17:49
Hamna justification ya violence Salum Mkango. Kuna tofauti sana kati ya justification na explanation. Mimi rai yangu kule mabadiliko imekuwa ni kutafuta suluhu ya kweli kwa hizi pande mbili zinazotofautiana kutafuta a common ground. Yaani kila upande ujaribu kuelewa kwa nini upande mwingine unayachukulia mambo tofauti na wao wanavyoyachukulia. Busara itawale, huu sio wakati wa kuonyeshana umwamba. Two wrongs don't make it right nafikiri.................. -- Send Emails to wanabidii@googlegroups.com Kujiondoa Tuma Email kwenda wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma Disclaimer: Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines. --- You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group. To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com. For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
|
-- Send Emails to wanabidii@googlegroups.com Kujiondoa Tuma Email kwenda wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma Disclaimer: Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines. --- You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group. To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com. For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out. |
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit
https://groups.google.com/groups/opt_out.
0 comments:
Post a Comment