Monday 1 April 2013

[wanabidii] WATANZANIA TUCHAPE KAZI TUACHE POROJO

Ndugu zangu

Sijui kama mmegundua kwamba Katika Afrika mashariki nchi ya Tanzania ndio inayoongoza kwa watu haswa vijana kurandaranda kwenye mitandao haswa ya kijamii zaidi Facebook , katika kutumiana salamu , mazungumzo tu na masuala mengine binafsi kuliko kujadili masuala mbalimbali haswa yale yanayogunsa maisha yao kama elimu , ulinzi , usalama ,kilimo .

Tabia hii imekuwa kubwa na inaleta janga lingine kwa taifa ambalo pengine limeanza kuchomoza katika utendaji kazi wa baadhi yetu haswa kule maofisini , mashuleni , vyuoni na katika baadhi ya vyombo vya ulinzi na usalama .

Kwa viongozi wa idara kama ni mashuleni basi wabadilike , kwa serikalini watengeneze miongozo kwa majumbani wazazi waangalie mienendo ya watoto wao katika matumizi ya vyombo hivi .

Kwa sisi tuliojiajiri haswa kwenye fani hii ya TEHAMA kama mimi nawaomba haswa vijana wenzangu tubadilike , tusiendeleze sana tabia hii , tuwe na muda maalum kwenye mitandao hii angalau tusipoteze nguvu ya taifa kubwa kwenye mitandao ya kijamii .



--
www.wejobs.blogspot.com Jobs in Africa
www.jobsunited.blogspot.com International Job Opportunities

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

0 comments:

Post a Comment