Monday 1 April 2013

[wanabidii] Taarifa ya CCM-SA kuhusiana na tuhuma za utapeli wa Paul Mkoba

KUKANUSHA  TAARIFA ILIYOCHAPISHWA NA  JAMII FORUMS (TAREHE 28 MARCH 2013) KUHUSU UTAPELI ULIOFANYWA NA ALIYEHAWI KUWA KATIBU WA CCM, TAWI LA SOUTH AFRICA, NDUGU  PAUL PIUS ALBINO MKOBA

Mimi, kama mwenyekiti wa CCM, tawi la Afrika Kusini,  Ndugu, Kelvin Nyamori, nimesikitishwa na Habari, zilizochapishwa kwenye blogsite mbalimbali, pamoja na Jamii Forums, kuhusu utapeli uliofanywa na aliyekuwa katibu wa CCM, tawi la South Africa, Ndugu Paul Pius Albino Mkoba, Wenye Thamani ya Shilingi Millioni 37 za Kitanzania (RAND 200,000).

Napenda kuwaatarifu, Watanzania wenzangu waishio Afrika Kusini na kwengineko Duniani, kuwa taarifa zilizotolewa na vyanzo vya habari si sahihi, kabisa.

Chama hakiusiki kabisa na utapeli uliofanywa na ndugu, Paul Pius Albino Mkoba, ambaye alikuwa ni katibu  wa CCM, ila alikuwa na kampuni yake binafsi ya Investement (Forex & Stock Marketing) aliyokuwa akiimiliki, nchini South Africa, iliyosajiliwa kwa jina la mke wake, Betty Outsource Service.

Ila sisi kama Chama cha Mapinduzi, hatukuhusika na wala wanachama wetu hawakuhusika katika hiyo Biashara, na wala hakuwahi kutumia jina la chama katika kutangaza hiyo kampuni yake ya Investment, kama ilivyoripotiwa kimakosa na Jamii forums, na Blogsite nyinginezo.

Nimesikitishwa zaidi, na watu wa Jamii Forums kuichapisha hiyo habari ya mtuhumiwa huku wakiweka  picha ya mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na mtuhumiwa.

Ninachojua Rais ni kiongozi wa watu wote hivyo ana haki ya kusalimiana na hata kupiga picha na mwananchi yeyote yule. 

Napenda kuwaatarifu Watanzania wenzangu, sisi kama Chama cha Mapinduzi tawi la South Africa,

Tutawapa ushirikiano wa kutosha, waliotapeliwa na ndugu Paul Mkoba. Tumeshatoa taarifa ubalozini, na kituo cha polisi, tunamtafuta na kumsaka mtuhumiwa ili tumfikishe kwenye vyombo vya sheria, kwa kufanya utapeli kwa kutumia jina la chama kimya kimya. Kamati , Tulishafanya kikao cha dharura kumsimamisha kazi yake ya
ukatibu, baada ya kupata tarifa hizo, kutokana na malalamiko ya waliodhulumiwa, pamoja na vyombo vya habari.

Pia napenda kukanusha, kwa wale wanaosambaza taarifa kwamba mimi Mwenyekiti wa CCM, South Africa, kwamba nahusika na utapeli huo, ama kujua chochote kuhusu utapeli huo wa Mr. Paul Mkoba, uhusiano wangu na
Paul Mkoba ulikuwa ni kwa shughuli za kichama tu, na siyo vinginevyo kama watu wanavyonituhumu.

Hatukanushi tuhuma dhidi ya mtuhumiwa ila tunakunusha utapeli huo kuhusishwa na Chama Cha Mapinduzi, kama ambavyo Jamii Forums walivyoripoti.

Kwasababu kuu mbili.  Mosi  , Ndugu Paul Pius Albino Mkoba aliwadanganya wafanyakazi wa Ofisini kwamba anaenda Capetown kwenye semina ya kikazi (Forex & Stocks  Workshop) badala yake akaenda Tanzania kimya kimya.

Mwaka jana mwezi wa 9 Ofisi  ya Chama iliwahi kuibiwa vifaa vya ofisi vyenye thamani  karibu ya shilingi Millioni 15.
Ambavyo ni  Laptop  nne (4),  Giant Computers, Apple Macintosh mbili, pamoja na printer.

Wakati huo mimi kama mwenyekiti wa chama sikuwepo Johannesburg, nilienda kwenye shughuli za kichama   Western Cape. Nikaja kupokea simu kutoka kwa aliyekuwa katibu (Paul Mkoba) kwamba vifaa vya ofisi vimeibiwa.

Na yeye mwenyewe  ndugu Mkoba ndiye aliyezisambaza taarifa za ofisi za chama  kuibiwa kwa kutumia BBM na Facebook Page ya CCM. Ila uchunguzi wa polisi ulifeli, kutokana na mazingira ya wizi ulivofanyika. Napenda kuhitimisha kwa kuwaomba, Watanzania wenzangu waishio South Africa na Kwengineko, Wasipotoshwe na ripoti zisizo sahihi zilizotolewa na Jamii Forums na blogsite mbali mbali za nchini Tanzania.

Hawakufanya sahihi kumhusisha mtuhumiwa na Chama, kama alifanya dhuluma hiyo aliifanya kwa dhamira na hulka yake yeye mwenyewe na wala siyo Chama cha Mapinduzi.

Kwani inaonekana baadhi ya watu wanataka kuitumia habari hiyo kiuchochezi  zaidi.

Nawathibitishia Watanzania na wana CCM, wenzangu tuko  pamoja kumsaka na kumfikisha kwenye vyombo vya sheria mtuhumiwa, kwa kutapeli kwa kutumia jina la chama kimya kimya, ambacho ni kinyume na taratibu na kanuni, popote duniani. Kwani kwa sasa hata Chama , hakijui wapi alipo mtuhumiwa.

Kwa ushirikiano zaidi kwa mtu atakayejua wapi alipo Ndugu Paul Pius Albino Mkoba asisite kuwasiliana na Chama Cha Mapinduzi South Africa, au kutoa taarifa kituo chochote cha polisi nchini Tanzania au South Africa

Tunaambatanisha picha ya mtuhumiwa kwa ushirikiano zaidi, Asanteni sana.

Kidumu Chama cha Mapinduzi.

Mwenyekiti wa CCM Tawi la South Africa
Kelvin. A .Nyamori
Johannesburg  HQ
Phone: +27731688316
Email: Kelvinmartin39@hotmail.com
Or:  Mwenyekiti@ccmza.org

Source: http://www.wavuti.com/4/previous/2.html#ixzz2PC9KCzA9

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

0 comments:

Post a Comment