Sunday 28 October 2012

[wanabidii] WAISLAMU TUWE MAKINI SASA

natoa angalizo juu ya vurugu na pia huo ujumbe unaotolewa na kusambazwa mitaani kuna uwezekano hautolewi na waislamu au taasisi yoyote ya ki-slamu, upo uwezekano wa jambo hili likafanywa na wale wanaouchukia uislamu, ili uislamu uonekane kama dini siyofaa, isiyopenda amani na dini ambayo haitakiwi popote duniani hata mbinguni...nasema hivi kwa sababu kuna kundi la vijana walitokea irani enzi hizo nipo mlimani mwaka wa pili2005, na kuleta mitafaruku chungu mzima katika msikiti wa chuo unaojulikana kwa jina la MSAUDI, vijana hawa tuliwabaini na tulichokifanya ni kutowasikiliza katika mambo yao, then...
kuna mwaka mmoja hapa tanzania palitokea chama flan cha siasa kilianzisha vurugu na kuharibu mali zao wenyewe kw siri ili wapinzani wao waonekane wamefanyia vurugu na jamii iwachukie na iwaone kama wapenda vurugu.....,je tumesahau kuna siku vyombo vya habari viliripoti uamsho zanziba wameanzisha vurugu na kuharibu vitu huku wakiwa wameandamana cha kushangaza picha iliyowekwa front page ilikuwa ni ya maandamano yaliyowahi kufanyika zamani Morogoro....... kuna tetesi kuwa jengo la WTC na pentagon lilipigwa na wamarekani wenyewe ili ku justify kuivamia afganstn na iraq, staili kama hiyo huenda ikatumika kuharibu uislamu ambao ulikuwa unakuja juu sana kwa hoja zilizo za wazi.....napenda kuchukua fursa hii kuwa kanya na kuwatahadharisha waislamu wenzangu kuwa, tutulize akili zetu na tutafakari maisha ya tanzania na watanzania wenzetu mustakabali wa nchi yetu ambao mambo yanaenda mrama kila secta...nchi inaharibika na sisi tunaoitwa wasomi wala hatujiulizi nini cha kufanya... tunaichekea CCM na rushwa yao nje nje, vijana wamekata tamaa na maisha....upi mwaisho na mustakabali wa nchi yetu

0 comments:

Post a Comment