Monday 15 October 2012

[wanabidii] Mukama Aitolea Uvivu CHADEMA, Asema Inakabiliwa na Ukame wa Viongozi Waliopikika Kimaadili - Mwanzo

KATIBU Mkuu wa CCM, Wilson Mukama amesema Chadema hakiwezi kuwa chama chenye tija na hatma njema kwa taifa kutokana na kulazimika kuokoteza hata wagombea wake kutokana na wanaoshindwa kwenye michujo au chaguzi ndani ya CCM. Alisema, Chadema na vyama vingine vya upinzania hapa nchini, vinazama katika hali hiyo, kutokana na kutokuwa na tanuru imara linalowawezesha kutoa viongozi waliopikika kimaadili, kama ilivyo ndani ya CCM. Amesema, Chadema wanaposema, kwamba kwa CCM kutowafukuza au kuwanyima uongozi baadhi ya wana-CCM ni kuizika CCM, huko ni kulia kinyume kwamba kwa kutofanya hivyo CCM imewakosesha watu ambao wangehamia kwao hivyo chama chao kinakufa.
http://wotepamoja.com/archives/8792#.UHw15uZTcyI.gmail

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

0 comments:

Post a Comment