Thursday 25 October 2012

[wanabidii] CHADEMA – ARUSHA: Nassari (Mb) anusurika kukung’utwa; MOSHI: Madiwani wakung’utana; SHINYANGA: Mwenyekiti achomwa mkuki - Mwanzo

MBUNGE wa Jimbo la Arumeru, mashariki, Joshua Nasari  amenusurika kipigo kutoka kwa wananchi ambao walichukizwa na kitendo chake cha kuhamasisha wafuasi wa Chama chake, CHADEMA, kuwashambulia wanachama wa CCM na kumjeruhi Katibu kata wa  CCM, kata ya Usariver, baada ya kuzuiliwa asifanye kampeni za uchaguzi wa wenyeviti wa vitongoji katika mji mdogo wa Usariver kabla ya wakati.

Tukio hilo ambalo limethibitishwa na Katibu wa CCM wilaya ya Meru, LANGAEL AKYOO, amesema  katika vurugu hizo zilizotokea katika  eneo hilo la Usariver, katibu wa kata ya Kisambare wa Chama cha mapinduzi, alijeruhiwa kichwani mdomo  na mkono ambapo amefungua jalada kituo kikuu cha polidsi wilayani Arumeru, USRIVER/RB 4397 /2012.

Ammesema chanzo cha tukio hilo ni mbunge huyo kuanza kupita nyumba hadi nyumba na kwenye vilaub vya pombe za kiasili na kuwanunulia pombe akihamasisha wananchi kukichagua Chama chake kabla ya muda wa kampeni haujaanza.

Kampeni zimepangwa kuanza Oktoba 28 mwaka huu.


http://wotepamoja.com/archives/9704#.UIl9ZH6Jjb0.gmail

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

0 comments:

Post a Comment