Thursday 18 October 2012

Re: [wanabidii] Re: [Mabadiliko] Neno La Leo: Ya Mbagala Na Bedui Aliyekojoa Msikitini....

 
 
Naipenda nchi yangu na kuhudumia jamii kwa kujitolea. Lakini inafika wakati kichwa kinakuuma unasononeka unapoona watu kila mnalokubaliana haliendeleo ila kuna kiswahili cha kisengerenyuma. Vijana nao walaumiwe pia kwa kukosa ari ya kujituma kutaka rahisi rahisi.
 
Panapo vurugu vibaka wa aina yote watatafuta nafasi ya kujinufaisha. Hata panapokuwa na maurid na watu wamevaa vibarghashia wamekaa foleni ya mkao wa Kula baadhi ya waliokaa hapo si waislamu -hasa vijana. Wameweka kikofia upande anasubiri wali-beche. Siku itakuwa imeingia. Kaazima kikofia apate mlo. Ukianzisha vurugu, hatari ni kwamba penye mamba kenge hawatokosa wanaingia kwa nia ya kujifaidisha binafsi. Utashangaa, ugomvi ni wa kidini sasa kukwanyua betri ya gari, kioo cha gari mpita njia, kupora pochi ya wapitao, kuchukua Laptop na viti kanisani inahusiana vipi?
 
Lakini-Ni vizuri pia kuangalia pia tabia za uvivu za vijana wetu wasiopenda kujituma. Fuatilia pale CBO, NGO local/International walikoanzisha miradi ya vijana na kuwafundisha life skills uone kinachoendelea. Baada ya training ya kupata na posho, capital-hela imetolewa, hakuna kinachoendelea au kikundi kimevurugika kutokana na majungu na uroho wa madaraka ili kula fedha. Ardhi ipo kijiji kimewapa hakuna kinachoendelea. Jembe hilo la mkono vizee vinalima, mahindi yanapatikana ila wao waliowengi wapo kuwaibia vizee hao, kuvuna mahindi usiku yanaletwa DSM ktk mafuso tunachomewa. 
 
Fika Lindi maendeo ya traditional irrigation mabonde safi Aga Khan Foundation ina wataalamu inasaidia kilimo uangalie ni vijana wangapi wanalima. asubuhi mapema wapo wanacheza pool kwenye meza za udongo na kuchoma vihindi vichache. Nyumba nyasi mpaka mlangoni, minazi imejaa kama mchicha lakini mtu unamchungulia ndani, ukuta wa udongo umeporomoka, choo makuti yamechakaa na hakina hifadhi, paa limeenguka na wingu limetata juu itanyesha. Wapo barazani wanakula story, mudaukifisa-sala. Unajiuliza-tumemkosea nini Mungu tuna macho lakini hatuoni. Tuna nguvu na viungo lakini tu wavivu. Ukiangalia msitu-pori lina miti, udongo wa bure, michungwa ipo msituni anachuma hivyo hivyo  iki kuuza. Nazi zimejaa, vifuu na makumbi yake ambayo unaweza ukatengeneza zuria za kuuza kupitia makumbi, vifuu na nazi. Miembe kibao wanaweza kujiunga kusafirisha hata nje ya nchi. Udongo na maji hayauzi. Mbuzi za na ng'ombe za maziwa miradi imesaidia (FAO, CONCERN, TASAF) kwa nini hakieleweki?
 
Ufuta ni ALMASI unakua sana Lindi-Mtwara na lori zinafika hata kama barabara si za lami na wakijiunga kwa kilimo watapata mkopo wa kununua Fuso na Power tiller. Mhisani anatoa power tiller msaada-kujengea kibanda na kuituza tatizo na miti imejaa, inakaa nje, watoto wanachezea, wanang'oa nati na kuchana viti (Evidence na picha zipo). Mzungu Mhisani anakuja anaona mnatafuta pa kuweka uzo. Yale yote mliyokubaliana ulipoondoka wamebaki kubishana tu hakuna kinachoendelea. waliomba wao, wakapewa, kazi kulifanyia kazi, shida kung'oa visiki ili lilime (walipwe posho ya kung'oa visiki ili walime watoto wao wa shule wapate uji) na  kuboresha mashamba yao. Tumelogwa. Ina maana huyu kijana ili ajikwamue abebwe mngongoni? Lazina kurudisha yale masomo ya stadi za kazi kuanzia darasa 3 na kila shule iwe na vifaa vya ufundi, kushona, mapishi kama ilivyokuwa 1960s-mzungu alikuwa hakukosea. Tusingojee VETA pekee. Leo mtoto wa foirm 3 hajui hata jinsi ya kupanda mahindi au mbegu za viazi na muhogo atapenda kulima huyu? Tunapima viwanja vya nyumba hadi vijijini hakuna pa kulima na tunaongeza miji kupanuka kuingia vijijini vizee haviwezi tena kulima nje ya nyumba. DSM inaingia kigamboni, Changanyikeni, Makoko, Salasala, Tegeta, Bunju, Mbagala Mkuranga, Kibaha, Bagamoyo ni plot tu ni mji/miji marufuku mashamba kama zamani na hakuna social security  (Mshahara wa mwezi kwa wasio ajira) ili wapate kula na kuishi bila wizi. Sasa ipitako barabara ya Kikwete DSM-bagamoyo-Chalinze mashamba yote yanauzwa ni minara ya majengo ya Bar tu na majumba sio tena mpunga, minazi, miembe na mananasi. Hivi tunajipenda kweli hawa vijana tutawafanya nini? Mbona ulaya kuna mashamba makubwa nje kidogo ya miji ngano, mifugo miti ya matunda wide farms zinaonekana? 
 
 
Unafika Ruaha mbuyuni si mbali sana kuna Mwega Irrigation system, bonde la kilimo cha vitunguu, nyanya, mpunga, ndizi. Linaendelea hadi Ulaya, Zombo-Kilosa. Wakulima ni wazee, vijana wenyewe wapo kulangua vitunguu toka Ruaha hadi Mikumi na kuendesha bodaboda na bajaji kutwa na baiskeli na sasa taxi zimeingia zinajaza vibaya sana. Vijana wa Iringa Ilula na kwingineko walijitahidi sana wamelima nyanya, wameuza, wametajirika sasa wanakula na kuishi vema matenga ya nyanya tunayaona. Ila ujambazi unakatisha tamaa kuvamia wanaojituma.
 
Kufanyike mapinduzi ya kifamilia pia kubidiisha wazazi wawe wanawafanyisha kazi watoto wao kazi asifanye houseboy/housegirl tu wao wanaangalia TV au wapo nje wanatoa story au wanawafanyia wao wazazi. Watoto watajifunza na kujituma lini na kudaka wajibu wao? N i bomu ndio lakini kutokupenda kujituma, kutaka rahisirahisi ni tatizo letu. Atakujaje Mchina, Mkorea akulimishe kwa jembe la mkono na utalima lakini pekee hulimi na ardi ni yako. Ataingia Mnyarwanda atakuajiri wewe utakata miti, utabeba mbao hapo kijijini kwako atakutumikisha na ataingia na ming'ombe kibao ataharibu mazingira mbele ya macho yako upo upo tu. Aina hizi za ujinga budi tuepuke tujikanye badala ya kulalamika na kuonani bomu, Uvivu wetu na mtazamo wetu finyu ktk kujikwamua ni bomu hasa; land use planning mbovu ni bomu la masafa marefu; ulimbikizaji mifugo bila ya maendeleo na kilimo kisicho endelevu pamoja na kuwa na mbolea ya mifugo ipo na ya mboji inayotengenezeka ni baruti ya kuumiza vizazi vya sasa na vijavyo.
 
Yote yanahitaji ufumbuzi itufanye watu wa Taifa hili tuwe wachapakazi tunaojituma badala ya kusubiri kuletewa na tukipewa tuvidumishe  (Ona kiambata)
 
Vijana wajiajiri hata wasomi.Mbona msomi wa PhD na masters Ulaya anafagia mtaani akikosa ahira husika? Wenye hela matajiri waungane waunde makampuni ya kuchimba mafuta, gas, kilimo cha mashamba makubwa, ufugaji wa kisasa wa viwanda vya maziwa waje waajiri wazungu wa kutoa mafunzo na uzoefu ktk  sekta husika (madini etc) ili makampuni ya wazawa yatoe ajira kwa vijana kwa wingi. Wasichangie mashindano ya Mpira tu na Miss-Tanzania kuacha madini aje kuchimba mchina au m-canada.
 
 
 
--- On Thu, 18/10/12, ngwananzela@yahoo.com <ngwananzela@yahoo.com> wrote:

From: ngwananzela@yahoo.com <ngwananzela@yahoo.com>
Subject: Re: [wanabidii] Re: [Mabadiliko] Neno La Leo: Ya Mbagala Na Bedui Aliyekojoa Msikitini....
To: wanabidii@googlegroups.com, "mabadilikotanzania@googlegroups.com" <mabadilikotanzania@googlegroups.com>
Date: Thursday, 18 October, 2012, 7:10

Maggid,
Umenena kweli, sio sababu za kuchoma makanisa maana baadhi yao ni wakina John pia nao wamekamatwa, kweli tutafakari elimu yetu, ajira za hawa vijan zikoje au ndo wanashinda vijiweni siku nzima?

Kiongozi mmoja alisema kuna bomu la vijana na ajira tukambeza kwa kutoa data za uongo, huu ni mwanzo tu, tutaona makubwa kutoka vijana ili mradi apatikane wakuuwasha moto huo.

Ni kweli bila subira na hekina tutaangamia kama taifa, serkali yetu ianze kuchua tahadhari mapema kabla mambo hayajawa nje ya uwezo wake.

Siku njema!
Sent from my BlackBerry® smartphone from Vodacom


From: maggid mjengwa <mjengwamaggid@gmail.com>
Sender: mabadilikotanzania@googlegroups.com
Date: Thu, 18 Oct 2012 06:53:18 +0100
To: wanabidii<wanabidii@googlegroups.com>; mabadilikotanzania<mabadilikotanzania@googlegroups.com>
ReplyTo: mabadilikotanzania@googlegroups.com
Subject: [Mabadiliko] Neno La Leo: Ya Mbagala Na Bedui Aliyekojoa Msikitini....

Ndugu zangu, 

 Moja ya hadithi za Mtume Muhammad S.A. W ni pale Mtume Muhammad alipokuwa msikitini na maswahaba wake. Mara akaingia msikitini mtu wa kabila la Mabedui na kuanza kukojoa. Maswahaba wa Mtume wakasimama kwa hamaki kutaka kumwadhibu Bedui yule. 

Mtume akawasihi maswahaba wake wasifanye jambo lolote litakalomdhuru Bedui yule. Hapo ikavutwa subira. Bedui yule akakojoa na akamaliza. Mtume Muhammad alipomuhoji Bedui yule ikabainika kuwa alikuwa ni mtu wa hovyo na wala hakujua kuwa alimokuwa ni msikitini. Bedui yule akaelimishwa, akaelewa. Akarudi kwenye ustaarabu. 

Ndio mkojo ule ulifutwa kwa maji na amani ikawepo. Wahenga walinena; Subira yavuta heri. Siku zote, hamaki si jambo jema. Kwa kutanguliza subira na kutumia hekima Mtume Muhammad aliivuta heri na kuepusha shari. 

Maana, kama Mtume alisingewaasa maswahaba wake kuvuta subira, basi, makubwa matatu yangetokea ndani ya msikiti ule; Mosi, zingezuka vurugu na watu kuumizana na hata kutoana roho. Pili, mkojo wa Bedui yule ungesambaa msikitini kwa vile alishaanza kukojoa na isingekuwa rahisi kwake kukatisha mkojo wake. Tatu, Mkojo una madhara ya kiafya pia. 

 Naam, kwa mwanadamu, ni muhimu kuwa na subra na kutafakari kabla ya kufanya maamuzi. Kwa ndugu zangu Waislamu, tunaona Mtume Muhammad ameweza kuonyesha hilo. Na kwa ndugu zangu Wakristo, kuna mifano pia ya Yesu Kristo kuonyesha subra. 

Ndio, Uislamu, kama ilivyo kwa Ukristo na dini nyingi za humu duniani, msingi wake ni amani na upendo. Kitendo cha mtoto yule wa Mbagala kukojolea korani kitazamwe kwa sura ya kitendo kilichofanywa na mtoto . 

Na kama ilivyokuwa kwa Bedui yule, kama pale Mbagala subira na hekima vingetangulizwa, basi, yumkini tungebaini kuwa mtoto yule hakujua madhara ya kitendo chake. Naye angekanywa kama tuwakanyavyo watoto wetu. Na hata kitendo hicho kingefanywa na mtu mzima, bado tulikuwa na haja ya kutanguliza subira na hekima kumhoji aliyetenda, yaweza akawa kama Bedui yule kwenye msikiti alimosali Mtume na maswahaba wake. 

Na kwa kuangalia picha zile za Mbagala naiona hatari iliyopo sasa, kuwa tuna vijana wengi wasio na kazi; Wakristo kwa Waislamu. Vijana wasio na dogo. Ni kama moto uliofifia. Akipatikana kwa kuchochea kuni wanalipuka. 

Ni vijana wanaopatikana wakati wowote na mahali popote. Hata jambo likianza saa tatu asubuhi wao wapo. Hawana ofisi wala bosi wa kumwomba ruhusa ya kwenda kuandamana na kurusha mawe. Ndio hawa wanaonekana wamevaa ' Kata kiuno' na wengi wao hawajahi hata kuingia misikitini au makanisani. 

Inakuawaje kijana wa kweli wa Kiislamu achome kanisa na kuiba kompyuta. Inakuawaje kijana na muumini wa kweli wa Kiislamu aonekane saa mchana wa jua kali akivamia baa na kukimbia na kreti za bia? Ni maswali yanayotutaka tutafakari kwa makini. 

Maana, ninavyoamini mimi, uchumi na elimu duni ndio hasa vinavyochochea  vurugu za kijamii, iwe za kidini au kisiasa, na hususan inapohusisha vijana.   Vijana wetu hawana misingi mizuri ya elimu, na wengi hawana ajira pia. Haya ni sawa na makombora yasiyo na gharama kubwa kuweza kutumiwa na wanasiasa wasio waadilifu na hata viongozi wa kidini wenye mitazamo mikali.  Ni makombora yaliyoanza kutulipukia. Tuliziona ishara, tukazipuuzia.

Leo  Kuna vijana watakaotumiwa au kutumia fursa hiyo kutenda maovu kwa kisingizio cha dini. Ni hawa wataoshiriki kuchafua taswira za dini husika pia. Tujiadhari, kabla ya hatari kubwa inayotujia. Hatujachelewa.

 Na hilo ni Neno La Leo. 

Maggid Mjengwa, 

Iringa. 

0788 111 765
http://mjengwablog.com
--
Unapokea Email hizi kwa sababu umejiunga na Jukwaa la 'Mabadiliko'.
Kuchangia mada tuma kwenye Email hii: mabadilikotanzania@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda; mabadilikotanzania+unsubscribe@googlegroups.com
Utapokea Email ya kudhibitisha kujiondoa kwako.
 
TEMBELEA Facebook yetu:
http://www.facebook.com/MabadilikoForums?ref=hl
 
For more options, visit this group at:
http://groups.google.com/group/mabadilikotanzania?hl=en?hl=en
 
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Mabadiliko Forums" group.
To post to this group, send email to mabadilikotanzania@googlegroups.com.
To unsubscribe from this group, send email to mabadilikotanzania+unsubscribe@googlegroups.com.
 
 
--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 
--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

0 comments:

Post a Comment