Wednesday 22 August 2012

Re: [wanabidii] Anguko la Kafumu na Mapinduzi ndani ya CCM-UTENZI

Very cool pal

Sent from my iPhone

On Aug 22, 2012, at 11:59, "Mashaka Mgeta" <mgeta2000@yahoo.com> wrote:

Kafumu amevuliwa ubunge,
Makosa Ya 'wahafidhina' wa CCM,
Wale wasioyaona mabadiliko,
Wasiotaka kuyaishi mabadiliko,

Wasioyakubali mabadiliko.
Wamefanya 'uvundo wa kisiasa',
Wameukasirisha umma,
Wameumbuliwa na Mahakama,

Pole sana Kafumu!
Pole sana mwana mawasiliano mwenzatu.
Kwa jeuri na ulevi wa madaraka,
Wasiostahili, wamekusababishia usichostahili.

Hukumu imeshatoka,
Taji la ubunge umevuliwa,
Mjengoni hawatakuona,
Pumzika, anza upya.

Ole wako CCM,
Ole kwa jeuri ya waliomo ndani yako,
Wakitumia rasilimali za umma,
Wanakiuka yaliyo ya umma.

Wanajivisha jeuri ya kutoguswa,
Wafanye wanalolitaka,
Watishie pasipo soni,
Wakiuke kwa matarajio,
Kwamba watadumu siku zote.

Amka enyi mlio wa CCM,
Mapinduzi ya haki myaibue,
Hasira zenu ziwaondoe wasioistahili jamii.
Watoke, watoke kabla hamjatoka.

Msibwete enyi wana wa CCM,
Mkayaona mabaya na kuyaacha,
Kwa vile yanatendwa na wenye majina,
Mkashindwa kuwakemea, kuwatimua.

Mtayaonja mauti ya kisiasa,
Kwa uzembe wa wasio haki,
Wakitisha na kukiuka,
Ubunge wenu mkavuliwa.



....Mwenye beti za tenzi zaidi anaweza kuziongeza. Tuone kama CCM sikivu itatusikiliza.









--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

0 comments:

Post a Comment