Thursday 23 March 2017

[wanabidii] JPM KUMKINGIA KIFUA MAKONDA: HATA JK ANGEKUWA NA MAMLAKA ANGEZUIA KIFO CHA AMINA CHIFUPA:

Kama kuna jambo baya alilowahi kulifanya Mwalimu Nyerere katika uhai wake, ni kushirikiana na Dr. Milton Obote wa Uganda na Jomo Kenyata wa Kenya kumnyanyasa Field Mashal John Okello baada ya kufanikisha mapinduzi ya Zanzibar. Inasemekana mara baada ya kuupindua usultani wa Zanzibar, John Okello alionekana tishio kwa mataifa ya Afrika Mashariki na hivyo kutupwa tupwa huku na huko na akakosa mwelekeo na kupotelea kusikojulikana. Katika kitabu chake John Okello anasema kusudi lake kubwa haikuwa kuzipindua serikali halali bali alitaka kuelekea kusini kuzipindua serikali za huko na alitaka kuanzia Angola. Myaka yetu hiyo ungekutwa na kitabu hicho ungewekwa kizuizini.
Wakati fulani waIsrael wakipigana na waFilisti waliwatanguliza wenzao ambao walikimbia mbele ya wafilisti. Huo ulikuwa mtego wa kuwaondoa askari wa wafilisti mjini ili waisrael wauchome moto na kuwapiga kutokea pande zote. Vita ina mbinu nyingi. Hii hutegemea na adui unayepigana naye.
Nani haoni mafanikio ya vita ya madawa ya kulevya? Pita mitaani kama utakuta watu wakisinzia hovyo hovyo kama ilivyokuwa kabla ya vita kuanza! Hakuna kitu kibaya kama watu kutoona kinachoendelea na badala yake kuona kisichokuwepo.
Magufuli alichofanya ilikuwa kumtanguliza Makonda. Makonda toka amewataja wauza madawa biashara hii imeathirika sana Tanzania. Haiingii akilini kuwa Makonda alitamka majina bila kuwa na habari kamili. Kama inavyojulikana duniani wafanya biashara wa madawa wana nguvu nyingi. Wana hela nyingi. Wanaweza kumnunua mtu yeyote kama tunavyoona. Wanayumbisha serikali nyingi. Wanaofikiri vita hii ingeanza bila kuwataja wauza unga hawajaelewa vizuri vita yenyewe au ni wanufaika. Kitendo cha Makonda kuwataja tu; mizigo iliyokuwa njiani ilikomea huko huko. Iliyokuwa imeingia nchini ndiyo inapata shida kuwafikia wateja. Kazi ya kwanza na muhimu ilikuwa imekamilika. Ndipo na tume ya madawa ikatajwa. Ingetajwa kabla ya kuwataja wahusika tume hiyo ingeishia hapo hapo kwenye sherehe ya kuiapisha. Tungeshtukia magorofa yanaota na ukifuatilia kila mjumbe wa tume angemiliki moja.
Faida nyingine ya kuwataja, ilisaidia mamlaka kujua nani zaidi wanahusika na nani ni wanufaika. Tukawasikia walioanza kusema "heshima za watu zimeharibika". Wenye akili tukaongeza kwenye orodha. Watu wakahoji " inakuwaje watu watajwe kabla ya uchunguzi". Utendaji wa polisi kwa kiwango tulicho nacho na tulivyozoea ni Mamlaka ikipata fununu inamchukua mtuhumiwa na kwenda kumhoji. Sasa kama ndicho kilichofanyika kwa nini watu waone shida kuwataja watuhumiwa? Nani amewapeleka gerezani, ambako huenda waliohukumiwa? Watu wameitwa Polisi ili uchunguzi ufanyike. Utawaitaje Polisi bila kuwataja? Mboja list of shame ilitajwa na ndipo mengine yakafuata? Baada ya kutajwa mtu anachukua juhudi zake kujisafisha. Iweje watake kusafishwa? Mbona wezi wa kuku hujisafisha kila siku?

Ninafahamu na ninaamini waliotajwa ni wahusika tu. Kinachoweza kukosekana ni ushahidi wa kimahakama. Kwa hiyo ilikuwa ni hatari kutumia njia ya kimya kimya. Wangekuwa wanaendelea na mitaani waathirika wangekuwa kama kawa. Sasa hatuwaoni. Kwa nini Makonda alitumika, alitumiwa au alitumia njia sahihi.
Baada ya hapo tunaona maajabu. Mtu anaibuka na hoja ya vyeti vya Makonda. Anawakusanya watu kwa wingi kumuunga mkono. Kuwa tuache agenda ya madawa yanayoharibu vijana wetu tushughulikie vyeti vya Makonda. Sisemi makonda hakufoji. (Japo sisemi alifoji, maana sijui). Ninasema kuacha wahalifu wa madawa ya kulevya kwa sababu ya vyeti ni ujinga. Kama si ujinga (kwa wasionufania) na ni mbinu ya wahusika (kwa wahusika wa madawa hayo.
Mtu kutarajia kuwa rais atamchukulia hatua zozote za kumfanya Makonda asishughulikie madawa hayo ni kumdharau rais. Kumfanya hana akili. Hajui malengo yake. Kama rais ana dhamira njema na ndiye anayeongoza taifa kupambana na madawa ya kulevya hawezi kuanza kumshughulika na vyeti vya Makonda. Akifanya hivyo nitamdharau. Nitajua hana agenda. Anaweza kuyumbishwa na jambo lolote na kutelekeza agenda yake. Hata wasaidizi wake wasingeendelea kumsaidia. Kama rais mstaafu Jakaya Kikwete alikuwa na dhamira ya kupambana na madawa. Akampata Amina Chifupa, na kwa ujasiri akawa tayari kuwataja wahusika kama alivyosema; Kikwete angekuwa na mamlaka ya kuamurisha kifo angekiamuru kisimguse Amina Chifupa. Watu aina ya Makonda au Chifupa sio wengi. Wao ni mashujaa wa taifa hili na hawapatikani. Mmoja nimemuuliza "wewe ukiwa msifuni ukagundua kuwa dereva wako hana liseni. Utamteremsha msituni na kurudi mjini kutafuta dereva mwenye liseni? Akasema atakuja mjini na dereva huyo hadi mjini na akifika anambadilishia kazi. Nikasema tumuache Magufuli atoke msituni. Yuko msituni kwa sababu ni watu wachache walio na nia ya kupambana na madawa kama alivyo Makonda. Huwezi kumtelekeza ukafikiri vita itaendelea.
Kama taifa litakosa ushahidi wa kuwapeleka mahakamani wahusika lakini angalau biashara yao imeingiliwa na haitiririki kama ilivyokuwa. Huenda isirudie pale ilipokuwa. Angalau wauza unga wanajua kuna serikali. Juhudi zao za kuiyumbisha zinawayumbisha kuliko serikali inavyoyumba. Pia watanzania wameona kuwa hakuna mtu anayeweza kujihakikisha kutoshughulikiwa kwa sababu ya nafasi aliyo nayo kisiasa au kiuchumi. Hakuna tena mtu kufikiri kwa sababu ana fedha basi atawaamrisha waliotumwa kumkamata.
Mahala pa kuonyesha uzalendo ni hapa. Ni sasa. Hatuna budi kuiunga mkono serikali yetu kila inaponusa usaliti na kuufagia. Kanunu za mchezo wa ngumi zipo. Ukizitumia kuuendesha mchezo wa ngumi na mateke hutafika. Huu si mchezo wa ngumi. Ni mchezo wa mateke na ngumi. Mbinu zote zinatakiwa ili kushinda.
Lakini ninajisikia kuumia. Kuna watu ninajua wanaelewa. Wamesikia kelele za mlango na kuamua kujitenga. Vita ikiisha nitawaita na kuwashauri. Wasijisikie vibaya. Hata wakati wa vita ya Uganda zilipotumika silaha nzito, (nasikia) kuna askari wetu walikimbia kwa kudhani ni za adui. Hapana ndiyo vita.
Elisa Muhingo
0767 187 507
elisamuhingo@yahoo.com

   
           --
       
          
       
     
           Send Emails to wana...@googlegroups.com
       
          
       
     
            
       
          
       
       
         Kujiondoa Tuma Email kwenda
       
          
       
       
         wanabidii+...@ googlegroups.com 
       
     
          Utapata Email ya
       
     
           kudhibitisha ukishatuma
       
          
       
     
            
       
          
       
       
         Disclaimer:
       
          
     
       
           Everyone
      posting to this Forum bears
        the sole
       
          responsibility
       
           for any legal
      consequences of his or
        her postings,
       
         and
       
     
          hence
       
           statements and facts must be
      presented
        responsibly.
       
     
         Your
       
           continued membership signifies that
        you agree to
       
         this
       
           disclaimer and pledge to abide by
      our
        Rules and
       
          Guidelines.
       
          
       
       
         ---
       
          
       
           You received this
      message because you
        are subscribed
       
         to
       
     
          the
       
           Google Groups "Wanabidii"
        group.
       
          
       
       
         To unsubscribe from this group and
       
      stop receiving
       
       
       emails
       
           from
      it, send an email to wanabidii+...@
       
      googlegroups.com.
       
       
        
       
           For more
      options, visit
       
          https://groups.google.com/d/
        optout.
       
          
       
       
     
       
       
       
     
        --
       
        Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
       
         
       
     
        Kujiondoa Tuma Email kwenda
       
        wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com 
        Utapata Email ya
       
      kudhibitisha ukishatuma
       
         
       
       
      Disclaimer:
       
        Everyone
      posting to this Forum bears the sole
     
      responsibility
        for any legal consequences
      of his or her postings, and
        hence
        statements and facts must be presented
      responsibly. Your
        continued membership
      signifies that you agree to this
       
      disclaimer and pledge to abide by our Rules
and
        Guidelines.
       
        ---
       
       
      You received this message because you are
  subscribed
    to
        the
        Google Groups
      "Wanabidii" group.
       
        To unsubscribe from this group and stop
      receiving emails
        from it, send an email
      to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
       
        For more options,
      visit
     
      https://groups.google.com/d/optout.
       
     
         
     
   
    --
    Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
   
    Kujiondoa Tuma Email kwenda
    wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com 
    Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
   
    Disclaimer:
    Everyone posting to this Forum bears the sole
    responsibility
    for any legal consequences of his or her
postings,
  and
    hence
    statements and facts must be presented
responsibly.
  Your
    continued membership signifies that you agree to
  this
    disclaimer and pledge to abide by our Rules and
    Guidelines.
    ---
    You received this message because you are
subscribed
  to
    the
    Google Groups "Wanabidii" group.
    To unsubscribe from this group and stop receiving
  emails
    from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
    For more options, visit
    https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment