Thursday 23 March 2017

Re: [wanabidii] JPM KUMKINGIA KIFUA MAKONDA: HATA JK ANGEKUWA NA MAMLAKA ANGEZUIA KIFO CHA AMINA CHIFUPA:

Elisa Muhingo,
Nchi yetu imefika pabaya sana. Mambo ya msingi hayana maana tena bali ushabiki umewakwa mbele. Tunashabikia bila kuhoji, wasomi na wanazuoni wamepofushwa macho. Wenye ujasili kama wako ni wachache mno. Kuna mambo ya kujadiliwa lakini hayapewi umuhimu. Nilitegemea wasomi wangejikita kwenye masuala kama ya usafirishaji wa mchanga kwenda nje ya nchi. Faida na hasara zake, uendelee kubebwa au hapana. Mchanga huu una nini? Hakuna anayehangaika na hilo. Suala la vyeti vya Makonda limekuwa ndiyo hoja. Anatakiwa kuonyesha vyeti vyake mtandaoni lakini wanaodai hivyo hakuna hata mmoja aliyeweka vyake kama mfano tuvione.
Hawatuthibitishii kwa kumleta Paul Christian halisi ili atuthibitishie ukweli wa jambo lenyewe. Sina sababu ya kumtetea Makonda kama alifoji vyeti, lakini pia sina sababu ya kuamini bila uthibitisho kuwa Paul Makonda ndiye Daudi Albert Baahite. Nitaamini hili atakapojitokeza Paul Christian halisi.
Elisa, tumelaani sana suala la kuwataja watu hadharani kwa kuwa tu limefanywa na Makonda mwana CCM lingefanywa na Mbowe na genge lake lingekuwa halali na lisingekuwa udhalilishaji. Ndiyo, iliwahi kutokea mwembe yanga miaka ya nyuma watu walitajwa kama mafisadi papa na haikuwa udhalilishaji. 
Kama alichofanya Makonda ni udhalilishaji wahusika wanajua taratibu wangezifuata. Thngeona kesi za kudhalilishwa zinafunguliwa dhidi yake. Badala yake wanahangaika na kesi za kikatiba kwanini, kwa vile wanajua ukweli na wanajua wataumbuka. Tumwache Makonda afanye kazi tumpe nafasi rais wetu kusafisha papasi waliongia ndani ya nyumba yetu kwa njia ya soko huria. Haha rais mstaafu ambaye ndiye aliasisi sera hii mzee Ruksa alikiri kuwa wazo la kufungua milango lilikuwa zuri ila matokeo ya kufungua milango ndiyo yaliyotufikiaha hapa tulipo. Amesema ukifungua mlango kwa ajili ya kupata hawa safi wataingia pia mbu, mende, papasi nk. 
Anachofanya JPM  ni kuondoa papasi tubaki na hewa safi. Makonda ameamua kwa dhati kumsaidia mzee kuondoa uchafu lakini wanufaika wa uchafu wanaleta vikwazo. 
Sisi tunaochukia uchafu thsikate tamaa tuendelee kusema mavi ni uchafu hata kama wengine watauita mbolea. Tusijali matusi yatakuwa mbolea au mafuta ya ustawi wa taifa letu.
Usikate tamaa songa mbele bila kujali wengine wanasema nini

On Thu, 23 Mar 2017 at 21:34, 'Mohamed Mnzava' via Wanabidii
<wanabidii@googlegroups.com> wrote:
Asante sana, . . . .  "Mahala pa kuonyesha uzalendo ni hapa. Ni sasa. Hatuna budi kuiunga mkono serikali yetu kila inaponusa usaliti". . . . . 

Sent from my iPad

> On 23 Mar 2017, at 4:34 PM, 'ELISA MUHINGO' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:
>
> Kama kuna jambo baya alilowahi kulifanya Mwalimu Nyerere katika uhai wake, ni kushirikiana na Dr. Milton Obote wa Uganda na Jomo Kenyata wa Kenya kumnyanyasa Field Mashal John Okello baada ya kufanikisha mapinduzi ya Zanzibar. Inasemekana mara baada ya kuupindua usultani wa Zanzibar, John Okello alionekana tishio kwa mataifa ya Afrika Mashariki na hivyo kutupwa tupwa huku na huko na akakosa mwelekeo na kupotelea kusikojulikana. Katika kitabu chake John Okello anasema kusudi lake kubwa haikuwa kuzipindua serikali halali bali alitaka kuelekea kusini kuzipindua serikali za huko na alitaka kuanzia Angola. Myaka yetu hiyo ungekutwa na kitabu hicho ungewekwa kizuizini.
> Wakati fulani waIsrael wakipigana na waFilisti waliwatanguliza wenzao ambao walikimbia mbele ya wafilisti. Huo ulikuwa mtego wa kuwaondoa askari wa wafilisti mjini ili waisrael wauchome moto na kuwapiga kutokea pande zote. Vita ina mbinu nyingi. Hii hutegemea na adui unayepigana naye.
> Nani haoni mafanikio ya vita ya madawa ya kulevya? Pita mitaani kama utakuta watu wakisinzia hovyo hovyo kama ilivyokuwa kabla ya vita kuanza! Hakuna kitu kibaya kama watu kutoona kinachoendelea na badala yake kuona kisichokuwepo.
> Magufuli alichofanya ilikuwa kumtanguliza Makonda. Makonda toka amewataja wauza madawa biashara hii imeathirika sana Tanzania. Haiingii akilini kuwa Makonda alitamka majina bila kuwa na habari kamili. Kama inavyojulikana duniani wafanya biashara wa madawa wana nguvu nyingi. Wana hela nyingi. Wanaweza kumnunua mtu yeyote kama tunavyoona. Wanayumbisha serikali nyingi. Wanaofikiri vita hii ingeanza bila kuwataja wauza unga hawajaelewa vizuri vita yenyewe au ni wanufaika. Kitendo cha Makonda kuwataja tu; mizigo iliyokuwa njiani ilikomea huko huko. Iliyokuwa imeingia nchini ndiyo inapata shida kuwafikia wateja. Kazi ya kwanza na muhimu ilikuwa imekamilika. Ndipo na tume ya madawa ikatajwa. Ingetajwa kabla ya kuwataja wahusika tume hiyo ingeishia hapo hapo kwenye sherehe ya kuiapisha. Tungeshtukia magorofa yanaota na ukifuatilia kila mjumbe wa tume angemiliki moja.
> Faida nyingine ya kuwataja, ilisaidia mamlaka kujua nani zaidi wanahusika na nani ni wanufaika. Tukawasikia walioanza kusema "heshima za watu zimeharibika". Wenye akili tukaongeza kwenye orodha. Watu wakahoji " inakuwaje watu watajwe kabla ya uchunguzi". Utendaji wa polisi kwa kiwango tulicho nacho na tulivyozoea ni Mamlaka ikipata fununu inamchukua mtuhumiwa na kwenda kumhoji. Sasa kama ndicho kilichofanyika kwa nini watu waone shida kuwataja watuhumiwa? Nani amewapeleka gerezani, ambako huenda waliohukumiwa? Watu wameitwa Polisi ili uchunguzi ufanyike. Utawaitaje Polisi bila kuwataja? Mboja list of shame ilitajwa na ndipo mengine yakafuata? Baada ya kutajwa mtu anachukua juhudi zake kujisafisha. Iweje watake kusafishwa? Mbona wezi wa kuku hujisafisha kila siku?
>
> Ninafahamu na ninaamini waliotajwa ni wahusika tu. Kinachoweza kukosekana ni ushahidi wa kimahakama. Kwa hiyo ilikuwa ni hatari kutumia njia ya kimya kimya. Wangekuwa wanaendelea na mitaani waathirika wangekuwa kama kawa. Sasa hatuwaoni. Kwa nini Makonda alitumika, alitumiwa au alitumia njia sahihi.
> Baada ya hapo tunaona maajabu. Mtu anaibuka na hoja ya vyeti vya Makonda. Anawakusanya watu kwa wingi kumuunga mkono. Kuwa tuache agenda ya madawa yanayoharibu vijana wetu tushughulikie vyeti vya Makonda. Sisemi makonda hakufoji. (Japo sisemi alifoji, maana sijui). Ninasema kuacha wahalifu wa madawa ya kulevya kwa sababu ya vyeti ni ujinga. Kama si ujinga (kwa wasionufania) na ni  mbinu ya wahusika (kwa wahusika wa madawa hayo.
> Mtu kutarajia kuwa rais atamchukulia hatua zozote za kumfanya Makonda asishughulikie madawa hayo ni kumdharau rais. Kumfanya hana akili. Hajui malengo yake. Kama rais ana dhamira njema na ndiye anayeongoza taifa kupambana na madawa ya kulevya hawezi kuanza kumshughulika na vyeti vya Makonda. Akifanya hivyo nitamdharau. Nitajua hana agenda. Anaweza kuyumbishwa na jambo lolote na kutelekeza agenda yake. Hata wasaidizi wake wasingeendelea kumsaidia. Kama rais mstaafu Jakaya Kikwete alikuwa na dhamira ya kupambana na madawa. Akampata Amina Chifupa, na kwa ujasiri akawa tayari kuwataja wahusika kama alivyosema; Kikwete angekuwa na mamlaka ya kuamurisha kifo angekiamuru kisimguse Amina Chifupa. Watu aina ya Makonda au Chifupa sio wengi. Wao ni mashujaa wa taifa hili na hawapatikani. Mmoja nimemuuliza "wewe ukiwa msifuni ukagundua kuwa dereva wako hana liseni. Utamteremsha msituni na kurudi mjini kutafuta dereva mwenye liseni? Akasema atakuja mjini na dereva huyo hadi mjini na akifika anambadilishia kazi. Nikasema tumuache Magufuli atoke msituni. Yuko msituni kwa sababu ni watu wachache walio na nia ya kupambana na madawa kama alivyo Makonda. Huwezi kumtelekeza ukafikiri vita itaendelea.
> Kama taifa litakosa ushahidi wa kuwapeleka mahakamani wahusika lakini angalau biashara yao imeingiliwa na haitiririki kama ilivyokuwa. Huenda isirudie pale ilipokuwa. Angalau wauza unga wanajua kuna serikali. Juhudi zao za kuiyumbisha zinawayumbisha kuliko serikali inavyoyumba. Pia watanzania wameona kuwa hakuna mtu anayeweza kujihakikisha kutoshughulikiwa kwa sababu ya nafasi aliyo nayo kisiasa au kiuchumi. Hakuna tena mtu kufikiri kwa sababu ana fedha basi atawaamrisha waliotumwa kumkamata.
> Mahala pa kuonyesha uzalendo ni hapa. Ni sasa. Hatuna budi kuiunga mkono serikali yetu kila inaponusa usaliti na kuufagia. Kanunu za mchezo wa ngumi zipo. Ukizitumia kuuendesha mchezo wa ngumi na mateke hutafika. Huu si mchezo wa ngumi. Ni mchezo wa mateke na ngumi. Mbinu zote zinatakiwa ili kushinda.
> Lakini ninajisikia kuumia. Kuna watu ninajua wanaelewa. Wamesikia kelele za mlango na kuamua kujitenga. Vita ikiisha nitawaita na kuwashauri. Wasijisikie vibaya. Hata wakati wa vita ya Uganda zilipotumika silaha nzito, (nasikia) kuna askari wetu walikimbia kwa kudhani ni za adui. Hapana ndiyo vita.
> Elisa Muhingo
> 0767 187 507
> elisamuhingo@yahoo.com
>
>   
>            --
>         
>           
>       
>       
>            Send Emails to wana...@googlegroups.com
>         
>           
>       
>       
>             
>         
>           
>         
>       
>          Kujiondoa Tuma Email kwenda
>         
>           
>         
>       
>          wanabidii+...@ googlegroups.com
>       
>       
>            Utapata Email ya
>       
>       
>            kudhibitisha ukishatuma
>         
>           
>       
>       
>             
>         
>           
>         
>       
>          Disclaimer:
>         
>           
>       
>         
>            Everyone
>        posting to this Forum bears
>          the sole
>         
>            responsibility
>         
>            for any legal
>        consequences of his or
>          her postings,
>         
>          and
>       
>       
>            hence
>         
>            statements and facts must be
>        presented
>          responsibly.
>       
>       
>          Your
>         
>            continued membership signifies that
>          you agree to
>         
>          this
>         
>            disclaimer and pledge to abide by
>        our
>          Rules and
>         
>            Guidelines.
>         
>           
>         
>       
>          ---
>         
>           
>         
>            You received this
>        message because you
>          are subscribed
>         
>          to
>       
>       
>            the
>         
>            Google Groups "Wanabidii"
>          group.
>         
>           
>         
>       
>          To unsubscribe from this group and
>       
>        stop receiving
>         
>       
>        emails
>         
>            from
>        it, send an email to wanabidii+...@
>       
>        googlegroups.com.
>         
>       
>         
>         
>            For more
>        options, visit
>         
>            https://groups.google.com/d/
>          optout.
>         
>           
>         
>       
>       
>         
>         
>       
>       
>          --
>         
>          Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
>         
>         
>       
>       
>          Kujiondoa Tuma Email kwenda
>         
>          wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
>        Utapata Email ya
>       
>        kudhibitisha ukishatuma
>         
>         
>         
>       
>        Disclaimer:
>         
>          Everyone
>        posting to this Forum bears the sole
>       
>        responsibility
>          for any legal consequences
>        of his or her postings, and
>        hence
>          statements and facts must be presented
>        responsibly. Your
>          continued membership
>        signifies that you agree to this
>       
>        disclaimer and pledge to abide by our Rules
>  and
>          Guidelines.
>         
>          ---
>         
>       
>        You received this message because you are
>    subscribed
>      to
>        the
>          Google Groups
>        "Wanabidii" group.
>         
>          To unsubscribe from this group and stop
>        receiving emails
>          from it, send an email
>        to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

>         
>          For more options,
>        visit
>       
>        https://groups.google.com/d/optout.
>         
>       
>         
>       
>     
>      --
>      Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
>     
>      Kujiondoa Tuma Email kwenda
>      wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
>      Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
>     
>      Disclaimer:
>      Everyone posting to this Forum bears the sole
>    responsibility
>      for any legal consequences of his or her
>  postings,
>    and
>    hence
>      statements and facts must be presented
>  responsibly.
>    Your
>      continued membership signifies that you agree to
>    this
>      disclaimer and pledge to abide by our Rules and
>    Guidelines.
>      ---
>      You received this message because you are
>  subscribed
>    to
>    the
>      Google Groups "Wanabidii" group.
>      To unsubscribe from this group and stop receiving
>    emails
>      from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
>      For more options, visit
>      https://groups.google.com/d/optout.
>
> --
> Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
>
> Kujiondoa Tuma Email kwenda
> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
>
> Disclaimer:
> Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
> ---
> You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
> To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
> For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment