Thursday, 9 October 2014

Re: [wanabidii] TUSHIRIKIANE ILI KUPATA KATIBA HALALI

Lucas ukitaka isomwe weka picha ya gazeti la udaku juu chini bandika hii la hutusomi

On Oct 9, 2014 6:24 AM, "'lucas haule' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com> wrote:
Nimeipenda na nita i print kisha naiweka katika njia na mitini.
--------------------------------------------
On Thu, 10/9/14, 'Bart Mkinga' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

 Subject: [wanabidii] TUSHIRIKIANE ILI KUPATA KATIBA HALALI
 To: "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>
 Date: Thursday, October 9, 2014, 2:02 PM

 Bunge Maalum la Katiba chini ya
 Mwenyekiti wake Samwel Sita limehitimisha kazi yake ya
 kuandaa katiba itakayopelekwa kwa wananchi kwaajili ya
 kupigiwa kura. Zoezi hilo lili lilihitimishwa kwa kupigiwa
 kura na wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kwa namna ambayo
 haijawahi kushuhudiwa hapa nchini wala Taifa jingine lolote
 hapa Duniani. Baada ya kuwa na mashaka makubwa ya
 kutopatikana kwa theluthi mbili kutoka upande wa Zanzibar,
 Mwenyekiti alibuni njia mpya ya upatikanaji akidi ya
 theluthi mbili kutoka pande zote mbili za Mwungano. Hatimaye
 wajumbe walitangaziwa kuwa akidi amepatikana, jambo ambalo
 liliwafanya wajumbe wa Bunge la katiba waliokuwepo ukumbuni
 kuonesha furaha yao ambayo huenda ilikuwa ni vigumu sana
 kuielezea kwa maneno. Walio wengi waliionesha kwa kucheza na
  kushangilia.
 Lakini
 kwenye huu mchakato uliotengeneza hii katiba
 inayopendekezwa, kuna mambo ya msingi ya
 kujiuliza:Uhalali wa Katiba unatokana na
 nini?Je, katiba inayopendekezwa ni
 halali?Wajumbe wa Bunge la Katiba na viongozi wao,
 wanaelewa utofauti wa katiba na ushindani wakati wa
 uchaguzi?Ni nani mwenye haki ya kufurahia
 kupatikana kwa katiba nzuri inayopendekezwa, ni waandaaji au
 wananchi?Tunajua kwa nini mataifa mbalimbali huweka
 hitaji la theluthi mbili katika kupitisha katiba lakini
 huweka asilimia hamsini au ushindi wa uwingi tu wa kura bila
 ya kujali ni asilimia ngapi kwenye uchaguzi?
 UHALALI WA KATIBA HUTOKANA NA
 NINI?
 Nilimsikia
 mara kadhaa Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba akisema
 kuwa atawashangaa Watanzania kama
  hawataikubali katiba hiyo kutokana na mambo mazuri yaliyomo
 ndani yake. Na jana pia nilikatishwa tamaa zaidi na
 Mheshimiwa Rais ambaye alitumia muda mwingi sana kuelezea
 mambo mazuri yaliyopo ndani ya katiba
 inayopendekezwa.
 Kuna
 kitu cha msingi sana katika demokrasia mnapofanya uamuzi.
 Katika mfumo wa kidemokrasi unaheshimu mamlaka ya umma,
 hakuna kitu muhimu kama kitu kilichoamuliwa kuwa 
 'halali'. Na uhalali hautokani na ubora au uzuri
 bali hutokana na uhalali wa mchakato wa ushirikishwaji. Kama
 lengo letu lingekuwa kupata tu
  katiba iliyo nzuri bila ya kuzingatia 'uhalali'
 sidhani kama kungekuwa na haja ya kuunda Tume ya Kukusanya
 maoni wala kusingekuwa na haja ya kuwa na Bunge Maalum la
 Katiba au hata upigiaji kura katiba inayopendekezwa.
 Tungepata katiba iliyo nzuri zaidi kama tungewatafuta
 wanasheria wazuri kabisa ndani na nje ya nchi, wakajifungia
 mahali, wakachambua katiba mbalimbali Duniani, wakafanya
 utafiti wao binafsi, na baadaye wakatuletea Watanzania na
 kutueleza kuwa hii ndiyo katiba mpya. Na huenda katiba hiyo
 ingekuwa bora kuliko katiba ya nchi yoyote ile Duniani
 lakini nina uhakika isingekuwa katiba halali.
 Nina
 hakika watanzania walichokuwa wanataka siyo katiba nzuri tu
 bali muhimu zaidi walitaka iwe 'halali'. Na
 ikumbukwe pia uhalali wa kitu hautokani na sheria pekee
 yake. Kuna nchi ziliwahi kutawaliwa na viongozi madikteta na
 wauaji lakini katika nchi hizo hata walipokuwa wanawaua watu
 wao ovyo walikuwa wakitumia sheria. Hata makaburu kule
 Afrika Kusini wakati wa utawala wa kibaguzi walikuwa
 wakiwakamata Waafrika na kuwafungulia mashtaka ya kukiuka
 sheria za kibaguzi. Kwa hiyo walikuwa wakitumia sheria. Hata
 Yesu alihukumiwa kuuawa kwa kutumia sheria. Hapa
 tunachotakiwa kujiuliza, mtu anaposema kuwa mchakato wa
 upatikanaji wa katiba inayopendekezwa ni halali kwa sababu
 umefuata sheria, Je, sheria yenyewe halali? Tutambue kuwa
 uhalali ni zaidi ya sheria maana hata sheria yenyewe inaweza
 kuwa sheria halali au sheria ya kibaguzi au sheria
  gandamizi. Sisi sheria yetu ya mabadiliko ya katiba ilikuwa
 halali? Kwangu mimi sheria ile haikuwa halali maana
 haikulenga kuufanya mchakato wa upatikanaji wa katiba
 usihodhiwe na makundi fulani, na hasa Bunge la Jamhuri ya
 Mwungano, na wanasiasa na vyama vya siasa.

 KATIBA INAYOPENDEKEZWA NI
 HALALI?
 Katiba
 inayopendekezwa na Bunge Maalum la katiba inaweza kuwa ni
 nzuri lakini siyo
 halali. Wanaoipigie debe ikiwa ni pamoja na
 Mheshimiwa Rais, wameelezea vizuri sana uzuri wa katiba hiyo
 lakini hawajaelezea ni kwa namna gani katiba hiyo ni halali.
 Katiba inayopendekezwa siyo halali kwa sababu mchakato wake,
 kuanzia sheria iliyotumika kuitengeneza haikuwa
 halali.
 Katiba
 ya wananchi ni lazima itengenezwe na wananchi wenyewe na
 wala kusiwe na kundi la kuhodhi mchakato wake. Katika
 mchakato wa utengenezaji wa katiba ilistahili kuondoa dalili
 zozote zile za kuonesha kundi fulani ndilo lenye mamlaka ya
 kuandika katiba kwaajili ya watu wengine. Tangu awali
 ilitakiwa kuyatambua makundi ambayo yatabanwa zaidi na
 katiba mpya. Kundi mojawapo kubwa ilikuwa ni wabunge wa
 Bunge la Jamhuri ya Mwungano. Katiba mpya tulitaka idhibiti
 ununuaji wa madaraka na uwakilishi kwa njia ya rushwa wakati
 wa uchaguzi. Malalamiko mengi ya rushwa yamekuwa wakati wa
 uchaguzi yakihusisha wagombea wa nafasi za ubunge na
 mawakala wao. Kundi la wabunge ambamo ndani yake kuna wengi
 wanajitambua kuwa nafasi zao wamekuwa wakizipata kwa njia ya
 rushwa hawawezi kuwa ni watu sahihi wa kutunga katiba
 itakayodhibiti rushwa wakati wa uchaguzi.
 Wananchi
 wengi wamekuwa wakilalamikia upeo na uwezo mdogo wa baadhi
 ya wabunge kutokana na elimu zao kuwa ndogo kupindukia.
 Itawezekana vipi wabunge ambao ni darasa la pili, la nne au
 la saba wapitishe katiba inayotamka kuwa hitaji la chini la
 elimu ya mtu anayetaka kuwa mbunge ni kidato cha nne? Hivyo
 wabunge wa Bunge la Mwungano walistahili kuwakilishwa kwenye
 Bunge Maalum la katiba kama taasisi nyingine lakini siyo
 kila mbunge kuwa mjumbe na hivyo kuwa na maamuzi ya mwisho
 juu ya Katiba inayopendekezwa. Kama Bunge la Jamhuri ya
 Mwungano wa Tanzania
  wangewakilishwa na wajumbe wachache kama taasisi nyingine,
 kungekuwa na uwakilishi mpana zaidi wa wananchi kuliko
 kulifanya Bunge la Jamhuri ya Mwungano kuhodhi mchakato wa
 katiba.

 Jambo
 la pili la kujiuliza ni kuwa kulikuwa na ulazima gani Rais
 kuteua wajumbe waliopendekezwa badala ya taasisi na makundi
 mbalimbali kuwateua moja kwa moja?
 DHAMIRA CHAFU HAIZAI KITU
 HALALI
 Uhalali
 wa kitu kwanza hutokana na dhamira safi na wala hautokani na
 uzuri wa kitu. Ningependa kuwalizeni - Mathalani nyumbani
 kwako ulikuwa na upungufu wa visu na ulikuwa unahitaji sana
 kisu kizuri chanye
  makali lakini bahati mbaya huna uwezo wa kukipata. Siku
 moja jambazi mmoja akaenda kutafuta kisu chenye makali sana
 huku akiwa na dhamira kuwa akija nyumbani kwako akutoe uhai,
 na baada ya hapo atoweke na mali zako. Lakini usiku aliokuja
 akiwa anafikiria kuwa wewe upo pekee yako, akakukuta upo na
 majirani waliokuja kukufariji kutokana na msiba wa ndugu
 yako uliotokea kijijini kwenu. Jambazi alipoingia akawakuta
 watu wengi ambao hataweza kukabiliana nao, hivyo naye
 akajifanya ni mmoja wa waombolezaji. Baadaye yule jambazi
 akagundua wapishi hawana visu vizuri vya kukatia nyama, naye
 akatoa kisu chake ambacho alikichukua kwaajili ya kuja
 kufanyia ujambazi. Wote mkafurahi maana tatizo la kisu
 limekwisha. Kisu cha jambazi kinaonekana ni kizuri,
 kimetatua tatizo lakini kisu hiki ni haramu kutoka na
 dhamira mbaya ya aliyekuwa amekileta. JAMBO BAYA LIKIFANYIKA
 KWA NIA NJEMA MUNGU HULITAKATIFUZA LAKINI JAMBO JEMA
 LIKIFANYIKA KWA NIA MBAYA MUNGU
  HULINAJISISHA.
 Wale
 waliofuatilia vizuri hotuba ya Mheshimiwa Rais Kikwete
 watakuwa walimsikia Rais akisema kuwa alipotaka kuanzisha
 mchakato wa uandaji wa katiba mpya, CCM haikutaka lakini
 akachukua maamuzi yake. Nadhani kwaajili ya kumheshimu Rais,
 CCM waliamua kumkubalia lakini miyoyo yao haikuridhia. Kuna
 mengi yaliyotokea, na kwa kiasi kikubwa ndiyo
 yaliyochelewesha upatikanaji wa katiba mpya, ukijiuliza
 huelewi kwa nini mchakato umeenda kwa namna ulivyoenda.
 Jambo lililodhahiri ni kuwa CCM japo walishindwa kumkatalia
 Mheshimiwa Rais
  lakini waliamua kuchukua njia nyingine kuhakikisha katiba
 mpya haipatikani, na hilo lingewezekana kwa kuhodhi mchakato
 wa upatikanaji wa Katiba. Mahali pekee ambapo waliona
 wanaweza kuhodhi bila shida ni kuhakikisha Wabunge wa Bunge
 la Jamhuri ya Mwungano ndiyo wanaokuwa na maamuzi makubwa
 kuhusu katiba mpya, wakitambua kuwa ndani ya Bunge la
 Jamhuri ya Mwungano, wabunge wa CCM ni zaidi ya 75%. Wabunge
 hawa wa CCM nia yao kubwa haikuonekana kutengeneza katiba
 mpya bali ilikuwa kuzuia kupatikana kwa katiba mpya. Dhamira
 hiyo inaonekana wazi kwenye Katiba mpya
 inayopendekezwa.
 Mambo
 ambayo wananchi wengi waliyaona ni muhimu kwenye katiba mpya
 ni pamoja na:Kupunguza
 madaraka ya Rais katika uteuzi. Kwenye hili wananchi wengi
 wanaona kuwa uteuzi wa Rais kwa nafasi fulani, japo ni
 nafasi muhimu sana kwa maisha yao ya kila siku lakini
 wanaoteuliwa wanapewa kama zawadi maana baadhi yao
 hawaonekani kuwa na uwezo wa kuzimudu kazi zao. Lakini pia
 kudhibiti uteuzi wa Rais kungesaidia wateule hawa kufanya
 kazi kwa kujiamini zaidi kuliko pengine kufanya kazi kwa
 lengo la kumfurahisha aliyewateua. Pia kuna ukweli kuwa
 ikitokea bahati mbaya mkampata Rais dikteta ni vigumu sana
 kuweza kumdhibiti Rais ikiwa wasimamizi wa ofisi zote kubwa
 za umma ni wateule wakeWananchi walitaka kuona katiba
 ambayo ina miongozi mikali kwenye mambo ya kudhibiti rushwa
 maana wananchi wengi wanaamini hili ni tatizo kubwa kwa nchi
 yetu kwa sasa, na linahitaji
  kudhibitiwa kwa nguvu zoteWananchi walitaka kuona nchi
 inakuwa na dira. Dira hiyo ielezwe na tunu zetu kama Taifa.
 Sababu kubwa ya kuwekwa tunu hizo ni kwa vile watu wengi
 wanaamini kuwa pamoja na katiba yetu inazungumzia usawa wa
 binadamu lakini kiuhalisia inaonekana kuna Watanzania
 wengine na hasa viongozi na matajiri, wao ni binadamu zaidi
 kuliko wengine. Kutambua tunu za Taifa kungesaidia kuundwa
 kwa sheria kali kwa watakaokiuka au kutenda kinyume na yale
 ambayo Taifa limeyaweka kama mambo makuu ambayo Taifa
 linaamini.
 Wajumbe waliobakia Bungeni
 wameyaondoa mambo hayo ambayo yalichangiwa na wananchi walio
 wengi na badala yake kumekuwa na majigambo sana kuwa katiba
 inayopendekezwa imetambua haki za makundi mbalimbali kama
 vile wafugaji, wakulima, walemavu, wasanii, n.k. Kwangu mimi
 haya yanayotajwa ni sawa na mtu ambaye ana paka wake ambaye
 ana njaa, na paka huyu wakati Bwana wake anakula naye
  anataka apande juu ya meza ili apate kushiba. Bwana wake
 anachukua mfupa anaurusha nje, paka anaufuata mfupi nje, na
 kisha Bwana wake anafunga mlango. Paka alirushiwa mfupa nje
 alidhani kilio chake cha njaa kimesikika kwa Bwana wake
 kumbe Bwana wake alikuwa na nia ya kumwondoa ndani ya nyumba
 asimsumbue tena. Paka atalamba mfupi na kisha kuendelea na
 njaa yake.
 Ukiwa
 na katiba inayotambua na kuzingatia haki na usawa wa watu
 wote na mahitaji yao yanayoendana na hali zao, tayari
 mlemavu naye atakuwemo, mkulima yumo, mfanyabiashara yumo,
 mvuvi,
  mfugaji, na wengine wote. Tunatajiwa haki za makundi lakini
 hatuambiwi ni wapi ndani ya katiba kiu yetu ya kuona
 wanaoteuliwa wanapata nafasi hizo kwa uwezo wao na siyo
 sababu nyingine. Maana hawa wateule katika baadhi ya maeneo
 wamekuwa ni kikwazo kwa maendeleo ya wananchi au kutokana na
 maadili yao au uwezo wao mdogo. Ndani ya katiba hatuambiwi
 ni wapi tumedhibiti kikatiba kuhakikisha watu hawapati
 madaraka kwa kutumia pesa au vyeo vya wazazi na ndugu zao.
 Ndani ya katiba hatuambiwi ni wapi tumedhibiti uwezekano wa
 mikataba mibovu, n.k.
 MTU
 SAFI
  UKIGUNDUA MWENZIO AMEFANYA KOSA AU HILA KWA MAKUSUDI NA
 WEWE UKAUNGANA NAYE, WEWE NI MHALIFU ZAIDI. MTU MWADILIFU
 ANATAKIWA KUSIMAMA KIDETE NA KUSEMA KUWA ULICHOFANYA SIYO
 SAHIHI. TUNAPOFANYA HIVYO KWA DHAMIRA SAFI NA SIYO KWA
 MASLAHI YAKO AU KIKUNDI FIULANI, KAULI HIYO ITAKUWA NI
 TAKATIFU.
 Napenda
 kuwaambia watanzania wenzangu kuwa ni aheri katiba
 isipatikane kuliko kukubali watu wengine kutumia sheria
 zisizo halali kuhalalisha katiba isiyo halali.
 WABUNGE WA CCM
 WANAELEWA UTOFAUTI WA KUPATA KATIBA YA WOTE NA USHINDANI WA
 UCHAGUZI?
 Ukifuatilia
 toka mwanzo wakati wa utengenezaji wa sheria ya kusimamia
 mchakato wa kupata katiba mpya, ni dhahiri kuwa mchakato
 uligeuzwa kuwa ni ushindani kati ya CCM na CHADEMA, na
 baadaye kati ya CCM na UKAWA. Hili lilikuwa ni kosa kubwa
 sana. Ni ukweli huo ndiyo uliowafanya wabunge wa CCM
 kushangilia sana baada
  ya kuelezwa kuwa kura zilizopigwa kwa fax, email na sms
 zimefanya akidi ya theluthi mbili kufikiwa. Furaha ile
 ilikuwa ni kushangilia kuwa CCM imewashinda UKAWA kama vile
 kulikuwa na kiti kinachogombaniwa kati ya CCM na
 UKAWA.
 Ni
 fikra hizo ndizo zilizomfanya Mwenyekiti wa Bunge Maalum la
 Katiba hata kubuni upigaji kura ambao haujawahi kutokea nchi
 yoyote katika sayari hii. Yote hiyo ilifanyika ili CCM ipate
 ushindi dhidi ya UKAWA. Wajumbe hawa na Mwenyekiti wao
 hawakujua kuwa ilistahili Watanzania wote tufurahie kuwa
 tumepata katiba mpya
  ambayo ina 'ownership' ya watanzania wote kama
 mchakato wake ungekuwa umelenga kuwashirikisha wananchi wote
 na siyo wanasiasa kuhodhi mchakato mzima. Leo tuna katiba
 inayopendekezwa na CCM ambayo ownership yake ipo kwa CCM.
 Hawa ndiyo watakaohitajika kuwashawishi wananchi waikubali
 na huku UKAWA na sisi wengine tunaoamini kuwa haitakuwa
 katiba halali tukiwashawishi wananchi waikatae kwa kuwa
 katiba iliyotengenezwa imehusisha kundi dogo ambalo lina
 msimamo unaofana kisera. KWENYE JAMBO HILI NI LAZIMA
 WATANZANIA TUSIMAME NA TUTAMKE KUWA TUNATAKA KATIBA YETU
 AMBAYO SISI WENYEWE TUTAIPIGIE DEBE, TUTAIFANYIA KAMPENI KWA
 WATANZANIA WENZETU. HATUTAKI UUNDWAJI WA KATIBA MPYA
 UBADILIKE NA KUWA NI MASHINDANO KATI YA CCM NA
 UKAWA.
 KWA NINI MATAIFA MBALIMBALI HUWEKA
 HITAJI LA THELUTHI MBILI KWENYE KATIBA?
 Katiba
 husimamia masuala yote kwa ujumla ya kila mwananchi na ndiyo
 msingi wa sheria zote za nchi. Msingi huu ni lazima uwe
 imara, mzuri lakini muhimu zaidi uwe halali. Katika nchi
 ambazo watu hutanguliza dhamira njema, viongozi
  wanaosimamia upatikanaji wa katiba huwa hawataki washinde
 bali huwa wanataka kujiridhisha kuwa angalao watu walio
 wengi kabisa kama si wote, wanaafiki katiba walioitengeneza
 ili wailinde, waitetee na wajivunie. Na ili hayo yafanyike
 ni lazima kuwe na 'ownership'. Hii katiba
 inayopendekezwa ikipitishwa ni lazima kutakuwa na kundi
 kubwa (significant number) ambalo haliwezi kujivunia na
 huenda wasiilinde katiba ambayo imetengenezwa na wajumbe wa
 CCM na kisha kupelekwa kwa wananchi. Katiba hailindwi na
 Polisi, Usalama wa Taifa, mahakama au Jeshi bali hulindwa na
 wananchi wenyewe. Katiba mbovu na isyopendwa itazaa sheria
 mbovu na zisizopendwa. WATANZANIA TUSIKUBALI KUWA SEHEMU YA
 KUWEZESHA UTENGENEZAJI WA SHERIA MBOVU KWA KUPITISHA MSINGI
 AMBAO HATUAMINI KUWA MCHAKATO WAKO UMEBEBA UHALALI WA
 DHAMIRA SAFI.
 NINI CHA KUFANYA
 KWA
 MTU MWADILIFU KABISA KABISA, KUUNGA MKONO KITU UNACHOJUA
 WAZI SIYO SAHIHI NI UHAINI DHIDI YA NAFSI YAKO MWENYEWE.
 Kama wananchi tunaamini kwa dhati ya mioyo yetu kwa kadiri
 ya utashi wetu, kuwa katiba hii
  haikukidhi vigezo vya uhalali wa kimaadili na uhalisia
 (siyo kisheria), tutakuwa tumelisaidia sana Taifa letu la
 leo na vizazi vyetu vingi vijavyo kwa KUIKATAA. Na tufanyapo
 hivyo, isiwe kwa nia ya kushindana, isiwe kwa nia ya
 kuishinda CCM au kumshinda Mwenyekiti wa Bunge au kwa nia ya
 kukomoana, bali tufanye hivyo kwa dhamira safi kwaajili ya
 faida ya watu wetu wote. Kuna watu ni wanaCCM, wengine CUF,
 CHADEMA, n.k. lakini ninyi nyote mtambue kuwa katiba yetu ya
 nchi ni moja tu. Tunataka katiba ambayo itatoa uhakika wa
 kila mtu kuishi katika Taifa letu kwa kujivunia Uraia wake
 na wala siyo fedha, cheo, kabila, dini, ukoo au familia
 yake. Tunataka katiba ambayo itamfanya kila mmoja akimwona
 Mtanzania mwenzake aone ni mtu wa karibu kwake kuliko mtu wa
 Taifa jingine lolote. Tunataka katiba itakayoyaweka mamlaka
 ya umma juu ya kitu chochote.
 Kuna
 siku nilikuwa nasafiri, nilikuwa na haraka sana. Nilipokuwa
 naondoka nilihisi gari yangu haikuwa vizuri sana, kwanza
 nilifikiria niahirishe safari yangu kwa siku moja ili
 niifanyie matengenezo. Lakini kwa kufikiria umuhimu wa
 safari ile niliamua kusafiri bila hata ya kujua kwa undani
 tatizo la gari langu, nia ilikuwa moja tu kuwa nisichelewe
 kwenye program niliyoipanga. Siku ya pili ya safari yangu,
 gari iliharibika kabisa, chombo kilichoharibika sikukipata
 duka lolote, nilikokuwa nawahi sikufika. Siku ya tatu
 nilitarajia nifike Mbeya nipande ndege. Nilikopanga kwenda
 sikufika, mbeya nilichelewa ndege
  iliyotakiwa kunichukua kwenda Dar ili nikapande ndege
 nyingine, Tiketi zote za ndege zilipotea.

 Nimeelezea
 kisa hiki kwa sababu wapo watakaosema kuwa gharama ambayo
 Taifa limeingia kwenye uandaaji wa katiba inayopendekezwa ni
 kubwa mno na hivyo kitendo chochote cha kuufuta au
 kuurekebisha mchakato mzima ni upotevu wa fedha na muda.
 Ukweli ni kwamba, kwa Taifa letu kuwa na katiba ambayo haina
 uhalali wa kimaadili ni gharama ambayo haiwezi kupimika.
 Tusipoliona hili sasa, tunaweza kulipia maradufu huko
 mbeleni. KWA
  KUUJUA UKWELI HUO NAPENDEKEZA YAFUATAYO:
 Wananchi WAIKATAE katiba
 inayopendekezwa lakini iwe ni kwa dhamira safi na siyo
 ushindani au kukomoana Baada ya katiba inayopendekezwa
 kukataliwa, mchakato urudi nyumaSheria ya
 mabadiliko ya katiba iangaliwe upya ili kuhakikisha sheria
 hiyo inalenga kuhakikisha hakuna mtu au kundi linalohodhi
 mchakato wa upatikanaji wa katibaMchakato wa katiba
 uanze na uteuzi wa wajumbe wa Bunge la Katiba kwa
 kuhakikisha hakuna kundi au taasisi ambayo inakuwa na
 wawakilishi zaidi ya 10% ya wajumbe wa Bunge la Katiba
 (Bunge la Jamhuri  lichukuliwe kama taasisi ambayo
 itawakilishwa na wajumbe wachache)Wajumbe wa Bunge
 la Katiba
  wachaguliwe na makundi yao moja kwa moja na idadi yao
 iongezweKwenye Bunge la Katiba wawepo pia wataalam
 huru wa mambo ya katiba ambao kazi yao itakuwa ni kushauri
 na kuandika katiba kwa muundo unaokubalikaMuundo wa
 Mwungano upigiwe kuraBart
 Mkinga






 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya
 kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment