Thursday 30 October 2014

Re: [wanabidii] URAIS 2015 - Bernard Kamilius Membe

Tuambie mtu huyo aggressive anayetufaa tupate muda wa kumpima pamoja na wenzake, watu waandike juu yake kama alivyofanya huyu aliyetuletea habari za Membe. Tunataka tuwafahamu vizuri hawa wanaotaka kugombea urais 2015, mzee Makamba kaweka wazi kuwa mwanaye anaweza kwa kuwa anaweza kutumia ipad si kama hao waliozaliwa enzi za ujima. Kama hiyo nayo ni sifa basi tutampima kwenye mizani na wenzake. Tutajie jina la hao unaoona wanaweza ili tuwaweke kwenye mizani na wenzao. Yawezekana kwa maoni yako Membe hafai kwa kuwa ni legelege kama unavyodai, ingawa hujatueleza ulegelege wake ulipo. Tunawafahamu wengi wanaotaka urais kama Membe walishakuwa na madaraka wakayatumia vibaya, wengine waliuza hadi viwanja vya mnazimmoja kwa wahindi hadi wananchi wakaingilia kati kugawana mabati ya uzio ulioanza kujengwa lakini leo wanadhani tumesahau. Ni vizuri tuwaweke wazi tuwajadili kwa pamoja bila upendeleo kwa kuwa ushabikihaulisaidii taifa.


On Wednesday, October 29, 2014 1:45 PM, 'ngupula' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:


Sitaki kusumbuka kutafutiza sifa za mtu kana kwamba nimeelekezwa na mganga wakati wenye sifa wapo kibao tu. Mi membe namjua,anaweza akawa rais lkn mjue kuwa ata underperform sana,therefore,hatufai katika phase ya 2015 tunayohitaji a really aggressive person. Kuna kitu fulani Membe anacho,ni mtu vuguvugu na asiyeelezeka kirahisi....ana upole fulani kwa kizubavuzubavu....binafsi hata navyoelekezwa na maandiko,vuguvugu huwa hawafai kwa Mungu na Shetani pia. Zaidi ya yote,Membe sikumpenda pale alipozunguka nchi nzima halafu kwa unafiki akawa anawatapeli viongozi wa dini kuhusu Oic na Mahakama ya kadhi...tulimtimua bhana na tukamuonya Jk kamwe asiwatume watu kama hawa kuongea na watu wenye akili....halafu leo msanii huyu ndio awe rais wangu. Na ndio maana naongea sasa ili lizone,na wengineo wajue kabisa,haiwezekani.

'Fred Hans Kipamila' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

Ngupula,
kwa nini unakuwa na negative attitude linapotajwa jina la Membe? Huyu bwana anajaribu kutuonyesha wasifu wa Membe kwa yale anayoyajua, tena katja na majina ya vyanzo vya taarifa yake. Hii ndiyo njia sahihi kwa mtazamo wangu kutuonyesha mazuri na mabaya ya kila mgombea badala kutuaminisha tu kuwa huyu ni jembe anafanya maamuzi magumu bila kutueleza maamuzi hayo ni yapi. Leteni sifa na udhaifu wa kila mgombea tumpime. Mimi simjui yeyote kati ya wanojitangaza kuutaka urais lakini sitaki kuwa dodoki kumezeshwa tu uzuri wamgombea nataka kura yangu iende kwa mtu ninayeamini ataweza kukidhi matarajio yangu kama mwananchi wa kawaida. Yaelekea unayajua mengi yanayomhusu Membe tuandikie kama alivyofanya huyu bwana ili tumjue vizuri, na vilevile tuandikie wasifu wa huyo jembe unayemtaka ili tumpime mizani moja na wengine tutajua upi ni mchele na zipi ni pumba.Narudiatena mimi natamani sana Joseph Sinde Warioba angeomba nafasi hii, ukitaka nikupe sababu nitakuwa tayari pale mtakapoanza kuweka wazi wasifu wa mgombea mmoja mmoja.


On Saturday, October 18, 2014 7:03 PM, 'ngupula' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:


Mtanisamehe jamani,nimeshindwa hata kusoma kufika mwisho...sio kweli kwamba Membe hakuhonga kwenye ujumbe wa kamati kuu..kwa taarifa sahihi kabisa ridhione na mama kikwete na maafisa kadhaa ndio waliofanya kaz hiyo...na hata sasa ridhione ndiyo mfadhili mkuu wa friends of membe to ikulu na kimsingi labda upepo ukatae tu,membe ndiye chaguo haswa la familia ya jk..na hizo CV zote mnazotafutiza labda kama mnatafuta mkuu wa wilaya lkn sio rais na kamanda in chief wa majeshi ya tz.....eti ana msimamo kwa kuwa tu alionyesha tu mapenzi kwa mugabe...membe tulimfukuza mza kwa unafiki wa kuwadanganya maaskofu kuhusu oic na mahakama ya kadhi. Membe ni msanii  na ni wasanii tu ndio watampenda.
Membe huyuhuyu ndiye alikuwa akigawa laki 2 kwa wenye viti wa ccm mpk jk akakemea.......aliyetamka hadharani kuwa atapokea hela kutoka kwa shetani je si membe lkn leo eti ni muadilifu......ngupula.

Katika mfululizo wa makala hizi zinazochambua wasifu wa wagombea urais katika uchaguzi mkuu ujao, leo tunamwangalia bernard kamillius membe, mbunge wa jimbo la mtama mkoani lindi na waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa.

Kama tutakavyoona katika uchambuzi huu, huyu ni mgombea mwenye historia
fupi lakini tajiri katika siasa za tanzania na kimataifa.

Katika uchambuzi huu nimetumia vyanzo mbalimbali vya taarifa, vikiwamo machapisho mbalimbali ndani na nje yanayomhusu membe, mahojiano na baadhi ya watu waliopata kusoma na kufanya naye kazi, taarifa za maendeleo yake kitaaluma shuleni na vyuo alikosoma, na taarifa za utekelezaji wa ilani ya ccm katika jimbo la mtama.

Aidha, katika maandalizi ya makala haya, nilipata bahati ya kufanya mazungumzo ya ana kwa ana na membe jijini dar es salaam.

Kuzaliwa, malezi na familia

bernard kamillius membe alizaliwa novemba 9, 1953 katika kijiji cha rondo-chiponda, wilaya ya lindi vijijini, akiwa ni mtoto wa pili katika familia ya watoto saba wa mzee kamillius anton ntanchile na mama cecilia john membe.

Membe alifunga ndoa ya kikristo na dorcas richard masanche mwaka 1986, na wamejaliwa kupata watoto watatu-wawili wa kiume na mmoja wa kike.

Membe tunaweza kusema alizaliwa na kukulia katika hali ya maisha ya mtanzania wa kawaida aliyezaliwa kijijini. Alizaliwa katika kijiji ambacho maji ilikuwa shida na hivyo kulazimika kutembea kilometa nyingi kufuata maji; hali hiyo ikifanya kuoga mara moja tu kwa wiki-siku ya jumamosi.

Hapakuwa na hospitali na kwa hivyo uhai ulitegemea zaidi kudra za mwenyezi mungu na hekima na akili za wazazi na wazee wengine kijijini. Kimsingi haya ndiyo maisha ambayo watanzania wengi tumekulia, hasa katika miaka ambayo membe alizaliwa.

Baba yake membe alikuwa mwindaji aliyelazimika kuwa hivyo. Akiwa bado mtoto mdogo miaka kama mitano hivi, wakiwa shambani, kamillius anton ntanchile alishuhudia simba akimnyatia na kisha kumdaka mama yake na kutokomea naye, na walikuja kupata baadhi tu ya viungo vya mwili w
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


0 comments:

Post a Comment