Thursday 30 October 2014

Re: [wanabidii] MHESHIMIWA SHYROSE BHANJI AIDHALILISHA TANZANIA

MVUTANO mkubwa unaoendelea ndani ya Bunge la Afrika Mashariki (EALA) umekwamisha shughuli za Bunge hilo kutokana na baadhi ya wabunge kugomea, wakitaka kwanza Mbunge kutoka Tanzania, Shyrose Bhanji achukuliwe hatua za kinidhamu kwa kile wanachodai kuwa ni utovu wa nidhamu.

Shyrose, anatuhumiwa kutoa lugha chafu kwa baadhi ya wabunge wenzake na viongozi wakuu wa nchi za Rwanda, Uganda na Kenya, wakati wa ziara ya viongozi wa EALA iliyofanyika Brussels, Ubelgiji wiki mbili zilizopita.

Kutokana na tuhuma hizo, wabunge wenzake wanamshinikiza Spika wa EALA, Margaret Zziwa aruhusu mjadala kuhusu Shyrose, lakini kiongozi huyo hakuwa amekubaliana na suala hilo, hivyo kusababisha miswada ya sheria na taarifa za kamati ambazo zilipangwa kujadiliwa na vikao vya Bunge hilo kuwekwa kando.

Tanzania daima ilishuhudia mwenendo mzima wa kikao cha Bunge hilo juzi, majira ya saa 8:30 mchana (saa za Rwanda), ambako Spika Zziwa alitoa taarifa kwamba, suala la utovu wa nidhamu kwa baadhi ya wabunge lilikuwa likishughulikiwa na Tume ya Bunge.

"Tulifanya kikao Jumanne iliyopita, Oktoba 21, 2014 na pia Jumatano, Oktoba 22, 2014 suala hilo lilijadiliwa kwa pamoja na mawaziri wa Afrika Mashariki. Kutokana na tuhuma husika kuwa nzito, hatukuweza kupata hitimisho," alisema Zziwa.

Kwa maelezo ya Spika huyo, tume yake ilitarajiwa kukutana tena jana huku akiahidi kwamba, uamuzi ambao ungelifanywa, taarifa zake zingetolewa kwa wabunge.

Baada ya maelezo hayo, Zziwa alitoa maelekezo ya kuanza kwa mchakato wa kupitisha muswada wa sheria ya Ushirika ya Afrika Mashariki, lakini kabla ya suala hilo kuingia katika hatua ya kupata maelezo ya kamati husika, ilitolewa hoja ya kutaka shughuli hiyo isitishwe ili kutoa fursa ya kujadiliwa kwa kanuni na miongozo ya Bunge hilo.

Hoja hiyo iliyotolewa na Judith Pareno, iliungwa mkono na wabunge wengi, hivyo Spika Zziwa kuelekeza kwamba kuanzia jana mjadala kuhusu kanuni ungepewa nafasi ya kwanza.

Hata hivyo, baada ya mwongozo huo, ilitolewa hoja nyingine kwamba Bunge liahirishwe ili kuwapa fursa wabunge muda wa kujiandaa, hoja ambayo pia ilipitishwa hivyo kusababisha kikao hicho kudumu kwa dakika 25 tu.

Baadaye akizungumza na waandishi wa habari nje ya ukumbi wa Bunge la Rwanda vinakofanyika vikao vya EALA, Pareno alisema lengo la hoja yake ni kuwezesha Bunge hilo kuendeshwa kwa kuzingatia utawala bora.

Watanzania wakutana

Kuahirishwa kwa kikao cha Jumanne kabla ya muda uliotarajiwa, kulitoa fursa kwa wabunge wa Tanzania EALA, kukutana kwa faragha ili kupata ukweli kuhusu suala hilo kutoka kwa Shyrose mwenyewe ambaye pia ni Katibu wa wabunge hao.

Kikao hicho cha dharura kilidumu kwa takribani saa tatu, lakini habari zinasema hakukuwa na muafaka wa pamoja ambao ulifikiwa kuhusu suala hilo, kutokana na kile kilichoelezwa kuwa misimamo iliyokinzana miongoni mwao.

Akizungumza baada ya kikao hicho, Shyrose alisema kuwa anashangazwa na tuhuma zilizosambazwa katika mitandao ya kijamii juu yake na kwamba, alikuwa hajapokea taarifa rasmi kutoka kwa uongozi wa EALA ili aweze kujibu.

"Hata mimi nasikia mengi sana tu lakini hadi sasa sijaletewa wala sijaambiwa chochote, lakini kama ni za kweli wanaonituhumu waziwasilishe kwangu kwa maandishi na mimi nipo tayari kuzijibu," alisema Shyrose.

Mmoja wa wabunge wa Tanzania, Makongoro Nyerere, alisema hawakuweza kuwa na mjadala wenye afya katika kikao chao, kwani ni kweli kwamba hakukuwa na orodha ya tuhuma zinazomkabili Shyrose.

"Sisi tungekuwa na cha kusema kama tungekuwa na hizo tuhuma rasmi na pengine ni vizuri kujua ni nani anamtuhumu, yaani mlalamikaji ni nani tofauti na sasa ambapo tunasikia manung'unuko tu, watu wananung'unika, ukiwauliza nani mlalamikaji hakuna anayejitokeza," alisema Nyerere.

Mwelekeo wa hatma ya Shyrose, ulitarajiwa kufahamika jana jioni baada ya Spika Zziwa kutoa taarifa ya tume, ambayo ilipanga kukutana jana asubuhi.

Mbunge Peter Mathuki kutoka Kenya, alisema mgogoro unaoendelea ndani ya EALA umewagawa wabunge na kwamba, hali ya kutoheshimiana miongoni mwao ni sababu kubwa ya athari zinazojitokeza sasa katika uendeshaji wake.

Vikao vya Bunge la Afrika Mshariki vinavyoendelea jijini Kigali Rwanda, vilianza Oktoba 20 na vinatarajiwa kumalizika leo, huku likiwa limeshindwa kukamilisha kazi hata moja kati ya zote zilizokuwa zimepangwa kwenye orodha yake.


On Thursday, October 30, 2014 3:06:12 PM UTC+3, john mushi wrote:
Hivi Mwandishi, naomba kuuliza. Nchi yetu inapomchagua mtu kuiwakilisha nje hapekuliwi?(vetting) au anajiendea jinsi alivyo?Kama ndivyo basi kuna tatizo mahali fulani.Au Uchaguzi wa kishabiki ndio matokeo hayoo!wala tusimshangae Huyu Mdada kapigiwa kura na walio wengi!


On Friday, October 24, 2014 9:19 AM, 'Happiness Katabazi' via Wanabidii <wana...@googlegroups.com> wrote:


Kweli jamani?

Sent from my iPad

On Oct 24, 2014, at 8:16 AM, "'Reuben Mwandumbya' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

Mchunguzi;
Kama haya ni ya kweli,,basi kuna shida kubwa ya kimaadili kwa huyu Mdadaa.
 
Reuben


From: "mchunguzihuru@gmail.com" <mchunguzihuru@gmail.com>
To: wanabidii@googlegroups.com
Sent: Thursday, October 23, 2014 5:56 PM
Subject: [wanabidii] MHESHIMIWA SHYROSE BHANJI AIDHALILISHA TANZANIA

Shyrose Bhanji kazua balaa kwenye Bunge la EAC huko Kigali jana na leo! Walioandika trh 8 kwenda Brussels kwenye Bunge la EU members wote wa Tume yao na Wenyeviti wa Kamati. Wakiwa safarini kwenda ndani ya ndege sijuwi kukosa ile lishe aliyoizoea? Akawa anakunywa kama kichaa! Crews wakamzuia kuwa kwakuwa ndege ni ya mchana asinywe kupitiliza. Akaanza kutukana crews matusi yote unayoyajua!
Akawaambia hawajuwi kama yeye ni mbunge wa EAC? Akaanza kufanya fujo ndani ya ndege, akachukua chupa akapasua! Hapa security ndani ya ndege wakamkamata na kumtia pingu! Maneno yakawa yanamtoka ovyo. Wenzie walipojaribu kumtuliza wa kutoka Rwanda na mwingine Uganda (names withheld) akawageukia, tukana hadi marais wao hya kutosha! Hapo walikuwa juu ya anga ya Cairo.
Pilot akakataa kuendelea na safari akataka kushusha ndege Cairo. Walimsihi sana Pilot ndio akakubali kwa masharti Shyrose adhibitiwe!
Walipofika Brussels vituko havikuishia hapo. Kwenye mikutano anabwabwaja ovyo. Mbaya zaidi akaandika ki-note na kukiweka mgongoni ili walio row ya nyuma yake wakisome. Kiliandikwa kuhusu yule mbunge/Waziri wa EAC aliyefariki kuwa amekufa kwa UKIMWI, na kwa kuwa amelala na Wabunge wanawake wa EALA (kawaandika majina kwenye ki-note) nao wana UKIMWI kwa kuwa wanaumwa mara kwa mara.
Wakamaliza ziara ambayo hata Spika wa EALA alikuwepo, Wabunge toka Tz waliokuwepo pamoja na Shyrose ni Kimbisa na Angella Kizigha; kwa rekodi mbaya!
Sasa Bunge la EALA limeanza vikao juzi, jana Bunge limevunjika, hawataki kujadili Miswada wala nini hadi Shyrose ajadiliwe Bungeni kwa mambo ya aibu aliyoyafanya ktk ziara hiyo. Bunge likavunjika!
Leo asbh kulikuwa na kikao cha House Business, ambacho kwa huku Bongo ni kama Kamati ya uongozi. Agenda ni Shyrose na kuvunjika kwa Bunge jana. Kikao kimevunjika na Wajumbe wote wamejiuzulu! Wanasema kwanini Spika hakumkemea Shyrose alipofanya ujinga kwenye ndege? Kwanini hamuwajibishi kwa kumfukuza Bungeni ilhali anajua sifa zote mbaya za Shyrose tangu ameingia EALA? Sasa hivi wote wamejiuzulu na sasa si tu wanataka Shyrose afukuzwe bali na Spika ajiuzulu mara moja!
Wajumbe wanadai walipojitoa na kujiuzulu, Spika peke yake hajajitoa, hivyo naye aende na maji! Yaani hakuna kinachoendelea, Wabunge wanasema Bunge halitaendelea wala kufanyika hata kwa miaka 10 ijayo hadi Shyrose na Spika waondoke!
Hii ni aibu kubwa kwa nchi yetu! Kila Shyrose anapopita hukosi kusikia kapigana, kagombana, katukana au kufanya mambo ya aibu! Hapo EALA kagombana na watu wengi kuanzia Wabunge wenzie hadi staff.
Nitaendelea kuwajulisha kinachoendelea. Vilugho mnyetishie ta Nanka.
Fuatilieni website ya Eac na ile ya Bunge lao huwa wapo live www.eala.org
Majanga!
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
--
Send Emails to wana...@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+...@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment