Thursday 12 June 2014

[wanabidii] Re: SOKO LA MITUMBA MCHIKICHINI LATEKETEA KWA MOTO



On Thursday, June 12, 2014 9:59:40 AM UTC+3, Abdalah Hamis wrote:

 

 

 



On Thursday, June 12, 2014 7:44:23 AM UTC+3, kilalo cha lugamba wrote:
Soko maarufu la kuuza viatu na nguo za mtumba mchikichini, limewaka na kuteketea ghalfa usiku wa kuamkia leo. Moto mkubwa ulizuka mnamo saa nne na nusu usiku na kuenea haraka katika maeneo yote ya soko hilo lililojengwa kwa vibanda vya mbao na kuezekwa mabati. Kwa mujibu wa mashuhuda, Moto huo umewaka na kuenea ghafla mno, kiasi cha kuwatisha majirani na wote wanaoishi na kufanya shughuri zao katika soko hilo.
Katika siku za hivi karibuni kumekuwepo na mgogoro kati ya mkandarasi aliyetakiwa kulijenga upya kwa upande mmoja na wafanyabiashara waliotakiwa kupisha ujenzi huo kwa upande mwingine, bila kuelezwa watahamia wapi wakati wa ujenzi huo. Baadaye ilikubalika kuwa mkandarasi huyo itabidi alijenge kwa awamu, atumie eneo la stand ambapo atajenga vibanda vya kutumika kwa muda wakati akijenga upande wa pili. Likikamilika ndipo warudi kaitka maeneo yao, kabla ya kuteketea kwa soko lote usiku wa kuamkia leo katika mazingira yenye utata mkubwa, kwani mashuhuda  wanashindwa kuelewa kasi ya kusambaa kwa moto huo na kuteketeza soko lote kwa wakati mmoja bila kuopolewa chochote sokoni hapo.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment