Sunday 29 June 2014

Re: [wanabidii] UAMUZI WA JULIUS MTATIRO NA GIZA NYUMA YA PAZIA


Ludo

Una swali mpaka hapo?

On Jun 29, 2014 8:46 PM, "Reginald Miruko" <rsmiruko@gmail.com> wrote:
HONGERA MHE. MAGDALENA SAKAYA (MB).

Iam proud of you dada #MagdalenaSakaya#(MB), NAIBU KATIBU MKUU MPYA, Chama Cha Wananchi CUF - Tanzania Bara.

Wewe pamoja na sekretariati mpya ya chama, nawatakia kila la heri katika majukumu ya kujenga chama chetu.

Nakuahidi wewe binafsi, viongozi na wanachama wetu wote ushirikiano mkubwa sana wakati wote ambapo mtakuwa mkipambana kukijenga chama.

Jambo moja ambalo ni muhimu, mimi naamini sana katika uwezo wa kina mama. Wewe umekuwa mbunge wetu muhimu sana na umeing'arisha CUF ndani na nje ya Bunge.

Natumai kuwa utatumia uzoefu wako mkubwa kukilinda na kukijenga chama katika nafasi ya NAIBU KATIBU MKUU BARA ambayo tumekukabidhi leo.

Nitumie fursa hii pia kuwashukuru viongozi wetu wakuu wa chama, Prof. Lipumba, Juma Duni Haji na Maalim Seif Hamad bila kumsahau Makamu Mwenyekiti mstaafu Mzee Machano Khamis Ali. Katika nyakati zote tulizofanya kazi pamoja nimejifunza mengi kutoka kwenu, nidhamu ya uongozi, uvumilivu, busara, hekima, mashirikiano na mengine mengi.

Miaka mitatu ambayo nimeongoza ofisi ya Naibu Katibu Mkuu Bara nimekuwa mkomavu sana, nimekuwa kiongozi imara na nimechota hekima, busara, uadilifu na nidhamu kutoka kwenu. Kupumzika majukumu haya makubwa ni faraja kwangu na kunanipa sasa muda wa kutosha wa kukamilisha shahada yangu ya tatu ya sheria.

Sitasita kuzidi kutumia uzoefu niliopata kuineza CUF na kuhakikisha inaweka mizizi Tanzania Bara. CUF ni kila kitu kwangu na bado najiona NINA DENI KUBWA katika chama changu, bado leo, kesho na kesho kutwa ntakuwa nafikiria NINI NIKIFANYIE CHAMA CHANGU na siyo CHAMA KINIFANYIE NINI.

Baraza Kuu lililochaguliwa hivi sasa lina uwezo mkubwa sana kuliko lililopita, hili lina wajumbe wengi vijana, wengi wanawake na wazee washauri wachache. Baraza hili litatuvusha vema chini ya uongozi wenu.

Nitazidi kuwa balozi wa chama changu usiku na mchana. Nimekuwa Mkurugenzi wa kitaifa wa chama nikiwa na miaka 26 na nimekuwa Naibu Katibu Mkuu nikiwa na miaka 28, ni nadra sana vijana kupata fursa kwa umri huo. Ni mara chache sana vijana wanaaminiwa kiasi hicho.

Naishukuru sana familia yangu, mke wangu Zakia Hassan na watoto wangu Faustina, Alexander, Elvis na Alma kwa kuwa wavumilivu wakati wote ambapo nilitingwa na majukumu ya kitaifa. Nawashukuru sana ndugu zangu wote ambao walinipa ushauri muda wote, marafiki na wote wenye mapenzi mema na kila aliyekuwa na mchango muhimu katika utendaji wangu.

Julius Mtatiro,
Naibu Katibu Mkuu Mstaafu,
Chama Cha Wananchi CUF,
Tanzania Bara.
28/06/2014.

RSM


2014-06-29 15:43 GMT+03:00 <bonnyluv84@hotmail.com>:

Hapa kuna maswali mengi zaidi ya majibu. Mtatiro akipata nafasi basi atolee maelezo.

--
Sent from myMail app for Android

Sunday, 29 June 2014, 02:06PM +0300 from Fakhi Karume <fkarume@gmail.com>:

Hakuna kijana au mzee wa Taifa hili asiyejua mchango wa Julius Mtatiro kwenye siasa za Upinzani hapa Tanzania. Ni mfano wa kijana anayeweza kuthubutu kujenga hoja na kuibua tafakuri ambazo ni zenye kujnga mustakabali chanya katika siasa ndani ya CUF na nje pia.
Kuna wakati Chama cha CUF kiliyumba na baadhi ya viongozi wake pia kukata tamaa lakini akiwa Naibu Katibu Mkuu Taifa alisimama akapigana akakifikisha Chama mahala kilipo  akiwa ndio Kiongozi kijana mwenye mvuto kwa tabaka hili muhimu.
Leo safu mpya ya uongozi Mtatiro hayupo. Kuna wakati pengine watu waliamini angeweza kutumikia chama katika nafasi zaidi ya ile ya Naibu Katibu Mkuu lakini haikuwa hivyo. Magdalena Sakaya amepata nafasi hiyo nandiye Naibu Katibu Mkuu mpya. Mtatiro hajafikia uwezo wa kushindana na Maalimu Seif na Lipumba? Na kama ndio wanamuandaa kuwa mrithi hapo baadae hawaoni kama alipaswa awe ndani ya Uongozi ili aendelee kupata uzoefu? Ama kaogopa yasimtokee ya Zitto Kabwe na je unadhani nini hatma ya kukosekana kwake katika safu hii inayoendelea kuongozwa na wakongwe Prof Lipumba na Maalim Seif?
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to  wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com .
For more options, visit  https://groups.google.com/d/optout .

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment