Sunday 29 June 2014

Re: [wanabidii] BARUA KUTOKA KWA MUME WA FLORA MBASHA KWENDA KWA MCHUNGAJI GWAJIMA


 
Mchungaji anayetajwa hapa ni nani-Millionaire Gwajima mzee wa kutoa Mizukule? hivi alivyobega kwa bega na mke wake mpaka kanisani na kila wanakokwenda-namuona hupita hapa kwetu kijijini ataweza kumuacha na kumshabikia huyo mke wa mtu. Kutwa kazungukwa na bodyguards. juzi tu salasala kaumpa msikiti maji ya buree! na anauza maji salasala kama mchezo atakosa hela ya kumsaidia mtu mwenye matatizo kama Flora kwa upendo tu wa kawaida?
Anyway-kupenda ni kidonda hata mtu wa dini sana anaweza akapenda akafanya makosa. Binadamu wengi hujisahau na kufanya makosa.
Utasikia wanakwaya na waswalihina wa kikristu wamepeana mimba huko kwenye kwaya; wakristu kugombania vyeo vya kamati mbali mbali makanisani kipaumbele- hela; viwanja vya vigango vya makanisa kununuliwa bila kushirikisha waumini kikamilifu-hela 10%.

Kwenye dini ulaji haukosi na pia masuala ya mapenzi hata kwa hao ndio tunawaamini sana. Mimi ninaomba daima Mapadri na masista Katoliki waruhusiwe kuoa jamani hawa ni binadamu wana hisia. Kumtumikia Mungu unaweza kufanya vizuri hata kama umeoa. Ni kuwatesa kuwakataza wasioe au kuolewa nao wanahizia zote kamilifu.

Pia kuna nguvu za giza hata katika dini zote zipo zinafanyakazi. Hutashangaa kusikia mzee wa kanisa anayeongoza sala na kupokea hostia kanisani akiwa wakwanza kukutwa na fuvu la binadamu au na tunguli na mizukule. Sheikh akawa mchawi wa kupiga watu majini, chuma ulete na mikosi mingine. Kusali sana kunaweza kuwa kiini macho pia. Nasafi ya uongozi hata mahala pa sala ikatumika vibaya na viongozi wa dini wakagoimbea madaraka.
Kwenye kulala nje katika mikesha ya sala mapenzi yakashamiri. Baadhi ya mashoga niliohoji waliniambia walianza kamchezo walipokuwa wakilala nje kwenye kupiga DUFU- kwenye maurid. na hivyo ndivo baadhi ya watu wadini kupatikana na makosa ya kulawiti vitoto, kubaka wanawake, wasichana, sodomy ndani ya ndoa na kupangia vitoto vishoga nyumba.Ubushoke nao unaweza ukawa na makosa ndani yake. Mungu atusaidie tutende yaliyomema. Flora na Mumewe wamejiaibisha kwa kupeleka matatizo yao hadharani badala ya kutumia wazee wao na ndugu kwao kwanza. wapo wengi wanayo kuliko hayo. Kutumia mitandao na magazeti hakufai kwani kesi ipo mahakamani. Kama kabaka si msichana alipimwa vidhibiti vipo ataadhibiwa? hayo yao mengine watumie mahakama sio kutumia media.


On Saturday, 28 June 2014, 23:57, jones konga <lufj.24@gmail.com> wrote:


kwanza niseme,,,tuu kuwa maneno ya manabii yameshatimia  kuwa kutakuwa
na watu watakaotumia jina la messiah ili kujitajirisha, watu watajali
sana fedha kuliko uzima wa milele,,,,Lakini kwa hapa ilipo fika hii ni
issue kubwa,,,,

On 6/28/14, Abdalah Hamis <hamisznz@gmail.com> wrote:
> "Mchungaji ...yapata kama wiki mbili zilizopita nilihoji kupitia vyombo vya
>
> habari juu ya 'utajiri' wa ghafla wa mkewangu Mara baada ya mgogoro kutokea
>
> kati yangu na yeye, bila kupoteza muda mkewangu akanijibu kupitia gazeti
> moja la udaku kuwa amechangiwa fedha kiasi cha milioni 9 na waumini
> kanisani kwako.
>
> Mchungaji, naomba uelewe kuwa nafahamu juu ya mipango yote mnayoipanga
> kuliko unavyodhani!! Kwanza ni kweli kuwa mlipitisha harambee ya kumchangia
>
> mkewangu, lakini kiwango kilichopatikana kilikuwa ni milioni 2 na laki tatu
>
> na si milioni tisa kama mlivyotangaza!! Lakini mlitangaza uongo huo
> makusudi iwe rahisi kutimiza malengo yenu ya kidhalimu mliyoyapanga juu
> yangu!!
>
> Mnamo tarehe 3 mwezi juni mwaka huu, mlifungua akaunti mpya kwa jina la
> mkewangu katika benki ya crdb morogoro, na siku nne baadae mkewangu
> aliingiziwa fedha kiasi cha milioni 18 kutoka akaunti ya MWANAMAPINDUZI
> FOUNDATION ambayo hyo accnt ipo nmb mwanza! Ambapo asasi hii inamilikiwa na
>
> mchungaji wako msaidizi Maximilian Machumu pamoja na mbunge wa viti maalumu
>
> kutoka mikoa ya kaskazini!
>
> Nashukuru kama ulimpa fedha hizi kwa nia ya kumsaidia, lakini hofu yangu ni
>
> kuwa kwanini kitendo hiki kifanyike kwa kificho?? Kwanini mtumie njia za
> siri ambazo si rahisi watu kujua kama mmempa fedha??
>
> Pia napatwa na mashaka zaidi kwani siku moja baada ya fedha hizi kuingizwa
> taarifa ya benki inaonyesha kuwa kiasi cha milioni sita cash zilitolewa na
> siku hiyo hiyo wapo waandishi watatu wa magazeti ya udaku ambao wanaonekana
>
> waliingiziwa fedha kiasi cha milioni moja kila mtu na aliyedeposit hizo
> fedha ni moja ya viongozi wako hapo kanisani!! Kuna nini hapo??
>
> Mchungaji, naomba tusizunguke mbuyu! Ni dhahiri shahiri kuwa umekuwa na
> uhusiano wenye utata na mkewangu kwa muda mrefu sasa!
>
> Binafsi nilianza kupata wasiwasi mwaka jana mwezi desemba tulipoenda katika
>
> mkutano wako wa injili pale morogoro! Mimi na mkewangu tulifikia hoteli ya
> kingsway msamvu na wewe ulifikia Nashera Hotel maeneo ya forest hill!!
>
> Baada ya siku tatu za mahubiri mkutano wako ulipigwa marufuku na serikali
> kwasababu ya maneno yakichochezi uliyokuwa unahubiri, hvyo ikatulazimu
> waimbaji wote turejee dar es salaam!!
>
> Lakini uliniomba mkewangu abaki na wewe kwani ulipanga uwe unawafanyia watu
>
> maombi pale kanisani kwako kihonda kwa muda wa siku nne!! Nilikubali na
> nikamuacha mkewangu nyumbani kwa dada yako pale mazimbu!! Lakini kesho yake
>
> dada yako alisafiri kwenda mwanza na ikabidi mkewangu arudi hotelini
> kingsway!!
>
> Kwaa taarifa nilizonazo na nimezithibitisha kupitia wahudumu wa pale
> hotelini ni kuwa mkewangu hakuwahi kulala pale hata siku moja ingawa chumba
>
> kililipiwa kwa siku zote zile!! Unaweza kunijibu alikuwa analala wapi?? Je
> unaweza kunieleza kwanini mkewangu alikuwa analetwa nashera hoteli na taxi
> kila siku usiku!! Sibahatishi katika hili kwani hata namba ya dereva taxi
> ninayo!!
>
> Yote haya nilivumilia, na hapa kati kati kuna mengi sana yametokea lakini
> nikajifanya mjinga nikajishusha nikavumilia kwa lengo la kulinda ndoa yangu
>
> isiharibike lakini naona wenzangu hambadiliki wala hamjishitukii sana sana
> mapenzi ndio yanzidi kuwa motomoto kati yenu!! Ulikuwa unategemea nivumilie
>
> mpaka lini, nijishushe kiasi gani, niwe mjinga kiasi gani Nilikuvumilia
> sana mchungaji lakini sasa imefika point hapana, imetosha lazima
> nikuondelee uvivu watanzania na dunia ikufahamu jinsi ulivyo na kitendo
> ulichonifanyaia na unataka kuniziba mdomo kwa kunitishia jela miaka 30!!!
>
> Wewe ni mpuuzi na shetani anaishi ndani yako... na nataka nikuahidi kitu
> kimoja kuwa NITAKUSHINDA! Najua utanisumbua sana kutokana na hela zako but
> at the end, I will be the last man standing!! Narudia tena, nitakushinda.!!
>
> Bila kusahau naomba niongee na wewe pia mkewangu, hivi ni nini
> kilichokukuta ndani ya moyo wako How did we get here?? Je ni fedha
> zilizokufanya ukengeuke kiasi hicho au kuna kingine?? Kama unanichukia mimi
>
> kiasi hiki je, uwahurumii hata watoto wetu?? Mbona tunawatengenezea mikosi
> wakiwa wadogo hivi?? Hivi unadhani watoto wanajisikiaje watakaposikia kuwa
> baba ameenda jela kwa kosa la kubaka lakini aliyechongesha muvi yote hiyo
> ni mama?? Hivi kisaikolojia hawa watoto watakuwaje Si watakuwa huku
> wanatuchukia sisi wote wawili kwa aibu na mikosi hii tunayowatengenezea
> Kwanini tunataka kuwataabisha watoto kwa dhambi ambayo hawajaitenda
>
> Yes nafahamu nimekukosea mengi and am very sory for that, lakini basi embu
> kumbuka mkewangu nimekuvumilia mambo mangapi mkewangu, kumbuka makosa
> mazito uliyonifanyia lakini nikakusamehe ni sijamsimulia hata ndugu yako
> ama ndugu yangu ili kulinda heshima yako!! Kumbuka jinsi tulivyopogana na
> changamoto mbalimbali mpaka leo hii umefikia kuwa moja ya icons wa muziki
> wa injili hapa nchini?? Kumbuka shida, manyanyaso, dhuluma, kuchekwa na
> kudharauliwa ambako tumepitia mpaka leo hii tuko hapa!!!
>
> Mkewangu, kwa miaka yote hii nimekubali nionekane bushoke tu huku watu
> hawajui kuwa mimi ndiye ninayechora ramani ya kila ishu yako!! Mimi ndiye
> nimekuwa nafatilia na kufanikisha kila kitu chako from scratch!!!
>
> Lakini nimekubali jamii inione bushoke kwani nilikuwa najua nini mimi na
> wewe tunatengeneza kwa maisha yetu ya sasa na baadae!!! Nini
> kilichokubadilisha mkewangu Fedha Au huyo mchungaji mwanamazingaombwe
>
> Hivi kweli kabisa umefikia hatua ya kulipa waandishi wa habari ili
> wanikandamize nionekane sifai katika jamii Ni nini kilichokuoata mkewangu??
>
> Naomba uelewe kuwa binafsi siogopi kwenda jela kwasababu ya hiyo muvi
> mliyonizushia, kwani ni bora nikakae jela kuliko kuishi huru huku
> mkininyanyasa kiasi cha kuondoa utu wangu kama bidamu, lakini kinachoniuma
> ni familia yetu!! Kwanini watoto wateseke kwa sababu ya tamaa zetu
> binafsi!! Nikifikiria hilo naumia sana!
>
> Najua kwa sasa inaonekana kama vile ni impossible kwa mimi na wewe
> kurudiana tena, lakini binafsi naamini tunaweza!! Najua haitakuwa rahisi
> kwani tumeharibu mno, lakini ni heri ya kujaribu kuliko kuendelea kufanya
> huu upuuzi tunoufanya sasa!!
>
> Kumbuka hiki tunachokifanya sasa hatujajipaka matope sisi tu pekee, bali
> mziki wote wa injili Tanzania, na tusipotubu tukajirudi Mungu atatuhukumu
> kwa dhambi hii!!
> Kumbuka kuwa hakuna kati yenu atakayeshinda katika hii vita, vyombo vya
> habari pekee ndivyo vitakavyo nufaika lakini mimi, wewe na mchungaji wote
> tuta loose!!
>
> Mwisho nimalizie na wewe mchungaji, tulipokutana mara ya kwanza
> nilikuchukulia kama kaka na kama mlezi wetu wa kiroho!! Lakini umegeuka
> shetani mwenye pembe saba, umeparaganyisha familia yangu, umeleta maumivu
> makali kwenye ukoo!!
>
> Nakuonya tena kwa mara nyingine, muache mkewangu!! Huyo ni mkewangu,
> nilimtolea mahali mimi mwenyewe na wazazi wake waliniamini na
> kunikabidhi!!! Nasema niachie mkewangu!!
>
> Wewe ni nyoka, imefika time watanzania wakujue ukweli wako wewe mbwa mwitu
> mkali uliyevaa ngozi ya kondoo!!!
>
> Umedanganya watu vya kutosha na umefarakanisha ndoa nyingi sana kwa sababu
> ya kiburi cha pesa zako chafu za sembe!! Umeudhalilisha ulokole kiasi cha
> kutosha imefika time tuwaeleze watanzania ukweli na wakufahamu kuwa wewe ni
>
> nyoka!!
>
> Sitakubali kuona ukiendelea kuitesa familia yangu, nitapambana na
> nitakushinda!!! Siogopi fedha zako wala connection ulizonazo, ni bora nife
> nikiwa nimesimama kuliko kuishi nimepiga magoti!
>
> Nitapambana na wewe mpaka mwisho ili historia isomeke vizuri ili hata
> wanangu wakiwa wakubwa wajue kuwa baba yao sikuwa lofa kiasi cha kupiga
> magoti na kuelekeza shingo kibla kuruhusu mdhalimu kama wewe uichinje
> familia yangu, bali licha ya umasikini wangu nilisimama kiume na kupigana
> kutetea familia yangu!!!
>
> Narudia tena mchungaji, nitapambana na nitakushinda.."
>
> --
> Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
>
> Kujiondoa Tuma Email kwenda
> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha
> ukishatuma
>
> Disclaimer:
> Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal
> consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be
> presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to
> this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
> ---
> You received this message because you are subscribed to the Google Groups
> "Wanabidii" group.
> To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an
> email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
> For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
>

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment