Sunday 3 March 2013

[wanabidii] Ni Ushauri Wangu Tu; Kwenye Masuala Ya Kitaifa Tuwe Na Salaam Za Kitaifa, Si Za Kivyama au kidini...

Ndugu zangu,

Moja ya changamoto kubwa katika ujenzi wa Umoja wetu wa Kitaifa ni kuchanganya salamu za kivyama na kidini kwenye masuala ya kitaifa.

Hakuna dhambi ya kutumia salamu za kivyama, lakini, hizo ziwe kwenye shughuli za vyama husika, si za kitaifa.

Hakuna pia dhambi ya kutumia salamu za kidini, lakini, iwe ni kwenye mikusanyiko ya kidini na si ya kitaifa.

Ni makosa na ni kuchangia kuligawa taifa pale Mtanzania anaposimama kwenye kusanyiko lisilo la kidini na kuanza na salamu kama ; " Bwana Yesu Asifiwe! Au Asalaam Aleikum!"

Hizo ni salamu za kidini na zinapaswa zitolewe kwenye kusanyiko la wenye dini husika. Fikiri kama kwenye kusanyiko la Watanzania kuna WaTanzania wenye kufuata imani za jadi, au imani za Kihindu, nao watajisikiaje kutengwa kwenye salamu hiyo.

Tungeweza kabisa kuwa na salamu ya kitaifa, napendekeza ifuatayo; "Udumu Umoja Na Mshikamano Wa Watanzania... Jibu ni Udumu!"

Na ingetosha kabisa, kuwa mwisho wa mazungumzo yetu kutamka tu; " Mungu Ibariki Tanzania". Maana, Mungu huyu ni wa wote.

Hakika, kwa hali ilivyo sasa tunachangia wenyewe kwenye hili la udini. Kwa mambo tunayoyaona ni madogo.

Ningeshauri pia kwa viongozi kuacha kutumia mavazi au alama za kidini kwenye masuala ya kitaifa. Huwa nashangaa kuwaona Wabunge wamevalia kanzu bungeni wakati wakifanya kazi za kitaifa. Ingependeza, na ni katika kudumisha umoja wa kitaifa bila kujali dini, kwa wenye imani husika wangevaa mavazi hayo baada ya kutoka jengo la Bunge. Si kuna vyumba vya kubadilishia mavazi?

Ningeshauri pia, kwa wanasiasa na watendaji , ambao kimsingi ni watumishi wa umma wenye watu wa imani tofauti, waache kutumia milio yenye sauti za kidini kwenye simu zao.

Ni ushauri wangu tu...!

Maggid Mjengwa,
Iringa.
0788 111 765
http://mjengwablog.co.tz

--
Jobs in Africa - www.wejobs.blogspot.com
International Jobs - www.jobsunited.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/groups/opt_out.
 
 

0 comments:

Post a Comment