Sunday 26 August 2012

[wanabidii] Fwd: Wizi wa Mizigo British Airways (BA) na Mashirika Mengine



---------- Forwarded message ----------
From: abel makubi <makubi55@gmail.com>
Date: 2012/8/26
Subject: Wizi wa Mizigo British Airways (BA) na Mashirika Mengine
To: mabadilikotanzania@googlegroups.com


Wanamabadiliko

Inashangaza hii tabia wa dokoa dokoa kwenye Bags za kusafiria mashirika ya ndege kama British Airways ana mengine imekuwa kitu cha kawaida. Mimi nimesafiri juzi toka Boston-USA kupitia London kuja Dar, lakini bag ambalo nilicheck-in likachelewa siku 2 na kufika jana. Nilikuwa nimefunga na kuweka kufuli baada ya kukaguliwa Boston . Cha kushangaza bag nakuta liko zima pamoja na kufuli likikiwa intact lakini pair zangu za viatu na nguo za watoto wameiba. Vitu vingine wameacha bila kuiba. Hii ni mara ya pili kuibiwa kwenye mashirika ya Ndege, kwani mwaka 2006 pia niliibiwa viatu ndani ya bag nikiwa nasafiri ka KLM. Sasa najiuliza tutakuwa tunaweka wapi mizigo yetu? Maana yote huwezi kupanda nayo ndani ya ndege bila check-in.



--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

0 comments:

Post a Comment