Thursday 2 August 2012

[wanabidii] Asah Andrew Mwambene Ateuliwa Kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO)

Bw. Asah Andrew Mwambene ameteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Habari
(MAELEZO) katika Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
kuanzia tarehe 01 Julai, 2012. Bw. Mwambene anachukua nafasi
iliyoachwa wazi na Bw. Clement Mshana ambaye mwaka jana aliteuliwa
kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).

Bw. Mwambene (41) kabla ya uteuzi huu alikuwa Kaimu Mkuu wa Kitengo
cha Mawasiliano Serikalini katika Wizara ya Mambo ya Nje na
Ushirikiano wa Kimataifa. Aidha, Bw. Mwambene amewahi kufanya kazi
katika Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) akiwa mwakilishi wa
Kampuni hiyo huko Zanzibar.

Idara ya Habari (MAELEZO) ndiyo Msemaji Mkuu wa Serikali hapa nchini.

IMETOLEWA NA
WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI
NA MICHEZO, AGOSTI 1, 2012

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.

0 comments:

Post a Comment