Tuesday 28 August 2012

RE: [wanabidii] Neno Fupi La Usiku Huu; Usidanganywe Na Miguu Ya Tembo...!

Mr Majid

Nimefurahia ujumbe wako, japo niko tempted kuuliza kama unayo majina tuweze kuwafahamu wanariadha wa mbio hizo.

 

 

F.K

 

 


From: wanabidii@googlegroups.com [wanabidii@googlegroups.com] on behalf of maggid mjengwa [mjengwamaggid@gmail.com]
Sent: Tuesday, August 28, 2012 12:32 AM
To: wanabidii; mabadilikotanzania
Subject: [wanabidii] Neno Fupi La Usiku Huu; Usidanganywe Na Miguu Ya Tembo...!

Ndugu zangu,


Inakaribia saa sita za usiku hapa Iringa. Kabla sijafunga kazi zangu za usiku huu nimeona niseme japo neno fupi la usiku huu.


Ndio, nimelipitia jarida la kila wiki ( Pichani) . Limesheheni vichwa vya watarajiwa Urais 2015. Inahusu Urais 2015. Si mnajua, Watanzania hatuna ndoto ya taifa, nyingi ni za vyeo tu, ikiwamo Urais.


Na Urais Bongo ni vita, tena si ya mchezo. Na kwenye vita kuna ya muhimu haya; Uwanja wa vita kwa maana ya uwanja wa kupigania. Kuna mikakati, kuna makamanda wa vita na wapiganaji. Lakini, vita pia ni sharti iwe na malengo.


Ndio, babu yangu alipata kuniambia; porini usidanganywe na miguu ya tembo. Tembo ni mnyama makini sana. Unaweza kuifuata miguu ya tembo ardhini ukadhani unayemfuatilia ni tembo mmoja. Hapana, tembo hukanyaga nyayo za tembo aliyemtangulia. Nyuma ya tembo mmoja yumkini kuna tembo mia moja.


Inahusu Uongozi pia, leadership. Nyuma ya kiongozi mmoja yaweza kukawa na kumi wanaomfuatia nyuma yako. Mzee Kenyatta alitamka; " Fuata Nyayo!"- Na kwa tembo ni " Kanyaga Unyayo!"


Naam, usidanganywe na miguu ya tembo, ukadhani ni mmoja, kumbe wako mia moja.
Na hilo ni Neno Fupi La Usiku Huu.
Alamsiki.
Maggid,
Iringa.
0788 111 765
http://mjengwablog.com

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 
*************************************************************************************** *************************************************************************************** This e-mail and any attachments are proprietary to NMB PLC. Any unauthorized use or interception is illegal. The views and opinions expressed are those of the sender, unless clearly stated as being those of NMB PLC. This e-mail is only addressed to the addressee and NMB PLC shall not be responsible for any further publication of the contents of this e-mail. If this e-mail is not addressed to you, you may not copy, distribute or disclose the contents to anyone nor act on its contents. If you received this in error, please inform the sender and delete this e-mail from your computer.

0 comments:

Post a Comment