Friday 17 August 2012

Re: [wanabidii] Fahari ya Tanzania . . .

Matinyi.
Tunajitangaza vya kutosha sema tu tunajitangaza kijinga, kipuuzi,
kidhaifu, kipoyoyo na kisegemnyeke kwenye mboni za wastaarabu. [ongeza
neno lingine lisilo na ncha kali ukipenda]

1. Walio weka fedha Uswis wameitangaza Tanzania kuwa ni nchi yenye
mfumo mzuri wa kudhibiti fedha chafu zisiwekwe kwenye mabenki ya
Tanzania. Fedha huwekwa nchi za nje kama Uswis na visiwa vya Jersey na
hata ikigundulika mmiliki hakuna tatizo maadamu ameziweka nje. Swala
kuwa ni chafu au safi sila serikali.

2. Tumejitangaza vya kutosha kwenye elimu na ina paswa tuanze mchakato
wa kuingia kwenye vitabu ya maajabu ya dunia. Tanzania ni nchi pekee
ulimwenguni ambayo wanafunzi wamefaulu mitihani ya taifa lakini
wanafunzi hao hawajui kusoma wala kuandika majina yao. Ajabu hili
linapatikana Tanzania pekee nchi ya maziwa na asali.

3. Kwa mujibu wa utetezi wa Tundu Lissu kwenye kamati ya maadili na
haki ya bunge. Yupo jaji ambae kateuliwa kwa majukumu ya kijaji lakini
hana shahada ya sheria na ndio kwanza anasoma kwa njia ya mtandao
shahada yake ya kwanza. Kwa hiyo kwa sasa ndio anajifunza "what is
tort law" ana weza ku-suppliment pepa, au jioni akitoka kuhukumu kesi
anapitia madesa kwa vijana wake pale udsm, akifika nyumbani anafanya
assaignment huku anakula valuer bila wasiwasi na mwisho wa mwezi
anakamata mapene yake ya ujaji. Hii ni tanzania pekee.

4. Tumejitangaza kwenye utalii vya kutosha kwa kujibia wanyama wetu
wenyewe na kuruhusu dege la nje kuingia anga ya Tanzania kuwabeba
wanyama hao huku wakipata escourt ya walinzi wa ndani halafu baadae
kinasanuka kuwa kumbe tulijiibia! Wanafukuzwa wakurugenzi bila
kufilisiwa walichopata maisha yanakwenda.

5. Akiwa nje ya Tanzania na kuhojiwa na mwandishi wa ufaransa. "Mr
president, what do you think are the main causative of poverty in your
country". Majawabu hayakuwa ya kuumiza kichwa ilikuwa rahisi kama
"kupiga mbizi" ili "upepo upite" na "liwalo na liwe" "hata mkila
nyasi" "go to hell" HAJUI.

6. Tanzania ni nchi pekee ulimwenguni ambayo wezi wakubwa wa fedha za
nchi wameombwa na raisi kupitia bunge wazirejeshe fedha walizo iba
huku vibaka wa kuiba ndala na wezi wa kuku wakichomwa moto hadi kufa
na kuwaacha Mafisadi wakidunda mtaani.

7. Tanzania ni nchi pekee ulimwenguni yenye bunge la kidemokrasia
ambalo spiker wake akitaka kupitisha hoja kwa kura, wanao sema sioooo
wakiwazidi wanao sema ndiooo hoja husika inapita bila wasiwasi. Chezea
mama wewe!

8. Tanzania ni nchi pekee ulimwenguni inayojinasibu kuwa ina serikali
sikivu lakini serikali hiyohiyo yanapoibuka makundi yenye madai
mbalimbali hukimbilia mahakamani kuziba sauti za makundi hayo ili
kuziba miale ya sauti zao zisisikike kwa serikali husika.

9. Tanzania ni miongoni mwa nchi pekee ulimwenguni iliyo sababisha
waziri wa nchi nyingine kujiuzuru kwa sakata la Rushwa [Mama rada]
halafu pesa tuliyolipa zaidi tukaiitia chenchi kana kwamba tulinunua
bidhaa ya 5000/ na sisi tukatoa 10000/ kwa hiyo wanaturudishia 5000/
yetu kwa fedha ya malipo halali ya kitanzania. Walio sababisha tulipe
zaidi hawana makosa.

10. Mashindano ya olimpiki yaliyo kwisha Tanzania ni miongoni mwa nchi
iliyopeleka washiriki wachache (4) lakini msafara wa viongozi
wasindikizaji ulikuwa mkubwa (watu zaidi ya 15) na hatukupata medali
hata moja.

Matinyi.
Kwa haya ukijumlisha na umiliki wa mlima mrefu kuliko yote Afrika
ambao unajulikana sana kuwa uko Tanzania unataka tujitangazaje zaidi?
Au labda tubadilishane tuhamie Ulaya wao waje huku ndio utajua kuwa
tunajitangaza kwa viwango vya dahari?

On 8/17/12, lilian ruga <lilian.ruga@yahoo.com> wrote:
> Matinyi,
> Ukweli ni kwamba, kama haina vijisenti vya kuweka kwenye account ya majuu
> then...WHO CARES!??!
>
> --- On Wed, 8/15/12, Mobhare Matinyi <matinyi@hotmail.com> wrote:
>
> From: Mobhare Matinyi <matinyi@hotmail.com>
> Subject: [wanabidii] Fahari ya Tanzania . . .
> To: "Wanabidii googlegroups" <wanabidii@googlegroups.com>, "Mabadiliko"
> <mabadilikotanzania@googlegroups.com>
> Date: Wednesday, August 15, 2012, 8:51 PM
>
>
>
>
>
>
>
> Cheki mgeni anavyotutangaza kwenye gazeti maarufu Uingereza la Daily
> Mail..........................sisi wenyewe je?
>
> So
> what shall we do today boys...hunting again? Africa's fearsome predators put
>
> their paws up as they contemplate next meal
>
>
>
>
> The three-year-old lions were snapped on the edge of the Serengeti, in
> Tanzania, Africa. Within another five minutes, three of the six predators
> had
> fallen asleep. The photo was captured by Daniel Dolpire who spotted the the
>
> lions lounging on the edge of the Salt Lick, a tributary of the Grumeti
> river,
> during a trip around Tanzania and Kenya with his wife. They pair had stopped
>
> over at the picturesque Klein's Camp on a group safari when they saw the six
>
> lions which make up the 30-strong Black Rock Pride.
>
>
>
> --
>
> Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
>
> Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
>
> Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
>
>
>
> Kujiondoa Tuma Email kwenda
>
> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha
> ukishatuma
>
>
>
> Disclaimer:
>
> Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal
> consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be
> presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to
> this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
>
>
>
>
>
> --
> Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
> Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
> Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
>
> Kujiondoa Tuma Email kwenda
> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha
> ukishatuma
>
> Disclaimer:
> Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal
> consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be
> presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to
> this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
>
>
>


--
"Tukosoane, Turekebishane, Tuwajibishane, ndipo Tusameheane". Regia Mtema.
--
+255 (0) 713 (784) 24 67 64.

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.

0 comments:

Post a Comment