Tuesday 4 September 2012

[wanabidii] TAMKO LA PPAT KULAANI KIFO CHA MWAKILISHI CHANNEL TEN IRINGA DAUDI

KUMB.Na:GS/PPAT/
01/2012
04/09/2012

MHARIRI WA HABARI
………………………………

YAH: TAMKO LA PPAT KULAANI KUSHAMBULIWA NA KUSABABISHA KIFO CHA
MWAKILISHI CHANNEL TEN IRINGA DAUDI
Chama cha Wapigapicha za Habari Tanzania (PPAT) kinapenda kuungana na
jamii ya wanahabari nchini, watanzania wote kutoa pole kwa Familia ya
Marehemu Daud Mwangosi na KULAANI mauaji ya kikatili ya Mwandishi Daud
Mwangosi wa Channel Ten mkoani Iringa.

Mwangosi ambaye pia alikuwa ni Mwenyekiti wa Klabu ya wanahabari
Mkoani Iringa (IPS) alifikwa na umauti Septemba 2, 2012 majira ya saa
10 jioni wakati wa vurugu za Polisi na Wafuasi wa CHADEMA.

PPAT inalaani kwa nguvu zote kitendo hicho cha kinyama na ambacho
kimetishia kwa kiwango kikubwa usalama wa waandishi wa habari hasa
Wapigapicha kama Mwangosi ambao hutakiwa kuwa mstari wa mbele katika
kupiga picha za matukio mbalimbali.

Polisi ikiwa ni chombo pekee cha usalama wa raia na mali zao wakati
wote ilishindwa kuhakikisha Mwandishi, Daud Mwangosi anakuwa salama na
kutekeleza wajibu wake vyema.

Ni hao hao Polisi tumewaona katika picha kadhaa wakimshambulia na
hatimaye kutawanyika baada ya kufa kwa Mwangosi lakini ajabu tunasikia
kupitia taarifa zao kuwa Mwangosi alikuwa wakati akikimbia kutoka
upande wa Wananchi.

PPAT inapenda kutoa wito kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP
Said Mwema na kuwaajibisha Askari wote waliohusika katika tukio lile
akiwepo RPC wa mkoa wa Iringa na kisha yeye mwenyewe pia kuwajibika
kutokana na mauaji hayo ya kinyama.

PPAT pia inaungana na vyama vyote vya Waandishi wa habari nchini
Tanzania katika kutaka uchunguzi huru na wahaki ulio katika uwazi
katika kuchunguza kifo cha Mwandishi Mwenzetu Daudi Mwangosi na majibu
yake yawekwe hadharani mapema iwezekanavyo .

Pia PPAT inawaunga mkono Chama cha Waandishi wa Habari Mkoani Iringa
(IPC) kuwazuia wanachama wake kuandika Habari zozote za Jeshi hilo
Mkoani Iringa. PPAT inaomba vyama vyote vya mikoa na Jukwaa la
Wahariri TEF kusitisha uandikaji wa habari zozote zinazolihusu Jeshi
la Polisi nchini hadi watakapo wawajibisha waliotenda mauaji hayo.


Mroki Mroki
Katibu Mtendaji PPAT.
0717002303/0755 373999

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.

0 comments:

Post a Comment