Saturday 29 September 2012

[wanabidii] Msafara wa CCM wapata ajali Chunya , 1 Afariki

Habari za kuaminika nilizopata sasa hivi kutoka katika kijiji cha
Matundasi wilayani Chunya ni kwamba mwanachama mmoja wa CCM amefariki
dunia kwa ajali ya gari aina lori na wengine wengi wakiwa wamejeruhiwa
vibaya. Chanzo cha ajali waliokuwemo humo wanasema ni kitendo cha
dreva kuongea na simu na huku akiwa amechia usukani wa gari hilo
ambalo lilikuwa katika mwendo mkali na kulikuwa na kona eneo hilo.
Misafara hiyo ya wanachama ni kwa ajili ya kukutana mjini Chunya
kufanya uchaguzi wa viongozi mbalimbali ambao majina yao yamepitishwa
na NEC-CCM hivi majuzi.

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.

0 comments:

Post a Comment