Waliogomea kuandika habari za kiPolisi wanaamini kuwa POLISI HAWAJALI KUHUSU JAMII.
LABDA NI KWELI.
Na...Ni kwa sababu hiyohiyo naamini kuwa kwa kuwa habari za kipolisi haziwanufaishi polisi bali jamii, kugoma kuandika ni kuipa adhabu ya pili jamii.
Huwezi kumkomoa mtu kwa kutenda kile asichojali
Nakuunga mkono.
ANDIKA TU....KWA MANUFAA YA JAMII
On Wednesday, September 5, 2012 6:04:33 PM UTC-4, maggid mjengwa wrote:
--Ndugu zangu,
Kufuatia mauaji ya kutisha na ya kusikitisha ya mwandishi Daudi Mwangosi ambapo askari wa Jeshi la polisi wanatuhumiwa kuhusika, kumekuwa na mitazamo na mikakati tofauti miongoni mwa wanahabari ikiwamo kugomea kuripoti habari zinazotoka kwenye jeshi la polisi.
Mjengwablog, kama chombo cha habari na mawasiliano ya kijamii, ina mtazamo wa kuendelea kuripoti habari za kipolisi, za kutoka ndani na nje ya jeshi hilo ikiwamo taarifa za kichambuzi.
Tunafanya hivyo tukiamini, kuwa habari za kipolisi kwa kiasi kikubwa ni habari zenye kuihusu jamii.
Maggid Mjengwa,Mwenyekiti Mtendaji,Mjengwablog.Iringa0788 111 765
http://mjengwablog.com
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
0 comments:
Post a Comment