Saturday 8 September 2012

[wanabidii] Harambee Ya Mjane Wa Daud Mwangosi; Waliochangia, Namna Ya Kuchangia, Na Kiasi Kilichopatikana Hadi Sasa...

1. Chris Cremence                                     100,000
2. Anonymous                                             500,000
3. Maggid Mjengwa                                     100,000
4. Raymond Kasoyaga                                   20,000
5.Edward Mgogo                                            10,000
6.Joachim Kiula                                                5,000
7.Libory Muhanga                                             5,000
8.Geofrey Kagaruki                                        10,000
9.Sadiki Mangesho                                         10,000
10. Edwin Namnauka                                      40,000
11.Daud Mbuba                                               10,000
 12. Anonymous                                             200,000
13.Mikidadi Waziri                                              6,000
14. Bungaya Mayo                                             5,500
15. Abraham Siyovelwa                                    50,000
16. Godfrey Chongolo                                       22,222
17. Jacob Mwamwene                                       51,000
18. Denis Bwimbo                                        153,683 
19. Zanzibar Ni Kwetu                                     150, 464
20.Felex Mpozemenya                                       10,000
21.Rweyendera Ngonge                                     11,000
22. Festo Temu                                                      10,000
23.  Azaria Mulinda                                                 10,000
24.Khatibu Kolofete                                                   5,000
25. John Bukuku                                                  25,000
26. Abel                                                                10,000
27. Hafidh Kido                                                     10,000
28. George Mtandika                                            16,000 
29. Shy-Rose Bhanji                                          200,000
Jumla:                                                   1,605,464   ( Milioni Moja Na Laki Sita Na Tano Na Mia Nne Na Sitini Na Nne)

Kiasi kilichobaki kutimiza lengo?  595,000 ( Kiasi cha shilingi lakini tano na tisini na tano elfu
)

Unaweza kuchangia kwa kutumia; M-Mpesa, Tigo Pesa, Airtel Money au NMB Mobile. Kwa namba 0754 678 252, 0712 95 61 31, 0788 111 765 ( Kwa walio nje mnaweza kutuma kwa Western Union, jina la mpokeaji- Maggid Mjengwa, Crdb A/ c 01j 2070759000 Maggid Mjengwa, NBC account ni 028201037642 jina Maggid Mjengwa. Tafashali nijulishe kama utatuma kwa njia ya Western Union au Benki)
 
Background:
Ndugu zangu, 
 Daud Mwangosi ambaye pia alikuwa ' Mwanakijiji' mwenzetu hapa  Mjengwablog hatunaye tena.
Nimemfahamu Daud Mwangosi  tangu mwaka 2004 nilipofika Iringa. Tangu wakati huo, amekuwa akiinipa ushirikiano mkubwa kwenye kazi ya kutangaza shughuli za kijamii kwenye  Vyuo Vya Maendeleo ya Wananchi. Ni  kwa kupiga picha za televisheni na kurusha habari kwenda Channel Ten; Iwe ni kwenda naye Ilula au Njombe, Daud Mwangosi  alikuwa tayari kila nilipomwomba aongozane nami kwa shughuli ya kijamii.

Mara nyingi nilimkuta Daud ofisini kwake  ( Picha ya kwanza juu) akichapa kazi na   huku mkewe akimsaidia kazi nyingine. Daud Mwangosi alikuwa mbunifu. Alikuwa ni mwenye kiu ya kujifunza mambo mapya kwenye teknolojia ya habari na mawasiliano.

Najua Daud Mwangosi alikuwa na  malengo ya kuendeleza shughuli zake za ujasiriamali.  Mbali ya mambo mengine, alikuwa na Photocopy machine ya kumwongezea kipato  ambayo iliharibika mwaka jana. Akawa na ndoto ya kuwa na studio ndogo ya kupiga picha za vipande ( Passport Size). Yote ni katika kumwongezea kipato kutunza familia yake.

Leo Daud Mwangosi hayuko nasi. Ameacha familia, mjane  na watoto wanne;  Itika Mwangosi ( Mjane) Nehemia Mwangosi ( 17) Kidato cha Nne Malangali Sekondari, Hetzgovina Mwangosi  (12) Bathsheba Mwangosi (9) na Moria Mwangosi ( 2)
Namini Daud Mwangosi angependa shughuli alizokuwa akizifanya ziendelee na zije kuwasaidia watoto wake pia.

Jana na leo nimewasiliana na mjane wa marehemu Mwangosi ambaye bado yuko Tukuyu. Nikamwambia kuna ' Wanakijiji ' wa Mjengwablog walioguswa na msiba wa Mwangosi na wangependa kutoa pole yao imsaidie katika kupata mwanzo kutoka hapa alipo sasa. Mjane wa Mwangosi amefarijika sana kusikia habari hizo. 

Kwa vile tayari ameahidiwa msaada wa kusomeshewa watoto. Msaada anaouhitaji kwa sasa ni kupata photocopy machine ( Used)  na kodi ya pango la ofisi. Jumla yake kwa yote hayo mawili haitazidi shilingi za Kitanzania milioni mbili na laki mbili. Hivyo msaada anaouomba kwa wenye mapenzi mema ni shilingi 2, 200,000 ( Shilingi milioni mbili na laki mbili). Shughuli hizo zitamsaidia kujikimu.

Kutokana na hali aliyo nayo sasa, Mwenyekiti wenu napendekeza nichukue jukumu la kuratibu michango hiyo.  Shime tushirikiane kufanikisha hili ili tumsitiri mjane wa mwenzetu Daud Mwangosi.
 Napendekeza ifikapo mwisho wa mwezi huu  ( Septemba) tuwe tumefanikisha zoezi hili kwa yeyote aliye nacho, hata kama ni shilingi elfu tano, ni msaada mkubwa.

Mjengwablog bado tuna rekodi nzuri katika kuchangishana kuwasaidia  wenye kuhitaji. Itakumbukwa, huko nyuma,  kwa pamoja, tulifanikisha kukusanya michango ile ya watoto wa Somalia na kuikabidhi UNICEF, Dar es Salaam. Ni zaidi ya shilingi milioni mbili.
Tulifanikisha mchango wa kusaidia ukarabati  wa maktaba ya Kijamii kijijini Mahango, Madibira. Zaidi ya shilingi milioni nne.
Sasa ni zamu ya kumchangia mjane wa mwenzetu Daud Mwangosi. Kinachohitajika ni milioni mbili na laki mbili.
Naam, kutoa ni moyo, usambe ni utajiri.
 Mwenyekiti wenu na familia yangu naanza kwa kuchangia shilingi laki moja.
Na kama kawaida, taarifa za waliochanga na kiasi kilichopatikana kitawekwa kwenye blogu kwa kila mmoja kuona.

Namna ya kuwasilisha michango: Tumia M-Mpesa, Tigo Pesa, Airtel Money au NMB Mobile. Kwa namba 0754 678 252, 0712 95 61 31, 0788 111 765 ( Kwa walio nje mnaweza kutuma kwa Western Union, jina la mpokeaji- Maggid Mjengwa)

Natanguliza Shukrani.

Maggid Mjengwa,
Iringa.

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

0 comments:

Post a Comment