Mtu asiyeelewa sera na mikakati ya nchi katika sekta fulani asipoteze watu. Niielewavyo kiasi sekta ya Afya serikali ina jinsi inavyoweka viwango vya huduma za afya. Iwapo hakuna hospitali ya wilayani au zahanati ya Kata au Health Centre ya GVT inaweza ikachagua yoyote iliyopo private hapo ambayo ina viwango ikawa designated health facility. Hiyo inaweza ikawa ya bakwata, Aga khan, St Kizito etc. Kama ni ya Kiwilaya-Ikawa designated District Hospital. Ikiwa ya Kitaifa pia na rufaa zote toka zahanati zikaenda health centre hiyo au ya DDH (iwe ya dini ya kikristu, anglican, islam, Lutheran, suni,etc).
Ikachagua hupata mchango wa GVT. Kuna health Kit ya mwezi au kila baada ya miezi kadhaa ambapo wilaya huzinunua kwa facility zilizo wilayani kwake. Zile za Kitaifa huzipata Kitaifa Ki-wizara. Hospitali za Rufaa kimkoa-Kitaifa si zote za GVT ni za madhebebu sio ya Kikristu pekee hii mbona inajulikana? Na siku hizi mahospitali makubwa yameongezeka unaweza ukaambiwa uende ukapige picha au uchunguzi fulani hospitali mojawapo-zinatambulika na capacity na kuna ushirikiano na upelekaji vijana kujifunza, kutibu. Serikali hupeleka watumishi inaowalipa mshahara katika designated health facilities kama mchango wake kwani haiwezi kuweka hapo tena facility kama hiyo. Ndio maana KCMC (ni ya kanisa)inatumika kama referral hospital; Ipo DDH ya Dini Serengeti Mjini; Health Centre ya Mikumi ni ya kanisa na ni ya serikali kwa matumizi wanatoka wagonjwa tarafa nzima ya Mikumi na nje yake wanakwenda pale hata wagonjwa wa ajali barabarani.
Aga Khan Hospital, Hindu Mandal nani anasema inachukua wahindi tu? Udini upo wapiila uwezo wa mtu tu na nyingine tele za dini (Wahindi) zinatambulika kitaifa na zahanati za Bakwata.
Ni kweli bahadhi ya madhehebu yapo nyuma katika kujenga mashule, huduma za afya na vyuo vikuu. Lakini baadhi za dini zinatoa mafunzo ya wauguzi yanayotambuliwa kitaifa na kimataifa, Wana miradi ya extension services kimkoa taifa inayoitambua (Aga Khan, KCMC). Aga Khan wana miradi ya maendeleo ya kilimo cha kulima mpunga na umwagiliaji maji, shule za watoto wagogo you name it wanayo.Na akija kiongozi wao Taifa linamtambua na kumpokea. Sio tu viongozi wa kikristu.
Baadhi ya madhehebu huduma zao bado hazijakua. Wenzao ni michango ya waumini katika madhehebu yao wanafika kuwa hata na vituo vya kulelea yatima, wazee etc, mashule yenye standard nzuri. Michango ya shs 200/= kwa kila muumini kwa siku inafika laki 6 sala moja mpaka jioni milioni 4. Kwa mahekalu 10 katika mji ni milioni 40 kwa siku, kwa mwezi, mwaka, miaka-wanajenga huduma mojawapo kutoa huduma kumtukuza Mungu. Kanisa la Efatha Mwenge limeanzisha na Bank inatoa mikopo kwa waumini wake. Mama Lwakatare ana kanisa lake ana misaada huko, mashule na magari kibao, waumini anabeba bure kwa makari yake.
Dini yoyote inaweza ikaweka huduma nzuri ikitaka na kama wanaona umuhimu wake-kusitakiwe kushika mchawi. Pia kutumia misaada yao itokayo e.g. Uarabuni kwa matajiri, Ulaya kwa wazungu wa madhehebu yao au kwa Aga Khan kuboresha shule na Zahanati/hospitali yao/zao. mashule na vituo vya watoto, kuwa na miradi ya shamba darasa etc na shule kuleta hata walimu/wataalamu toka nje wakawaomba wahisani wao. Tuone mbali badala ya lawama na chuki. Nani kwa mfano anazuia hekali lako lisiwe na shule ya watoto wadogo au zahanati kwa michango yenu na kuzingatia sheria ya nchi na wakafundisha watoto wenu mliosomesha elimu dunia na ahera au elimu ya Bwana yesu na ya Kizungu?? Lakini kama tutajali maslahi binafsi michango itolewapo au unapoletwa toka wahisani-inakuwa tatizo.
Tanzania utakuta mtu anaamua kutumia zahanati ya Bakwata, ya Kilutheri au Aga khan au ya serikali kwa uwezo wake na hazijali dini hizo kama asemavyo Muhigo na wengineo. Hata kama wametundika misalaba au mwezi ukutani na mlangoni wewe angalia huduma tu kwa uwezo wako.Mzazi anaamua mwenyewe mwanao aende St Mary Bagamoyo au Kinondoni Muslim au St Augustne au Tegeta college ya wahindi au aishie Madrasa tu na atibiwe Bakwata/Mwananyamala. Mzazi anunue health card 10,000/= watibiwe watu 6 kwa mwaka au wanafuzi 5 kwa elfu 10 kwa mwaka au anywe ujimbi na atumie maelfu anapopata dharura ya ugonjwa.
From: ELISA MUHINGO <elisamuhingo@yahoo.com>
To: wanabidii@googlegroups.com
Sent: Saturday, 22 September 2012, 11:09
Subject: RE: [wanabidii] Re: NILICHOSIKIA KONGAMANO LA KIISILAMU ARUSHA
To: wanabidii@googlegroups.com
Sent: Saturday, 22 September 2012, 11:09
Subject: RE: [wanabidii] Re: NILICHOSIKIA KONGAMANO LA KIISILAMU ARUSHA
Wewe unaamini kuwa Serikali inatoa mabilioni hayo kuimarisha ukristo? Ipo Serikali ya Namna hiyo? Kama serikali itatoa fedha kwa hospitali za missioni kwa sababu zinatoa huduma wala si biashara huko ni kuimarisha ukristo? Kuna hospitali yoyote inayotoa huduma kama hizo inayonyimwa ruzuku kwa sababu siyo ya kikriso? Kwanza hospitali hizo zinaendeshwa na makanisa tu lakini ni za wagonjwa bila kujali ni wa imani gani. Tunaziona za Agakhan. ni commecial/bussiness as usual. Ni hospitali za wagonjwa tatajili. Mvumi ya Dodoma au Kilimatinde ni za wagonjwa wote. ndiyo maana serikali huzipa ruzuku. Tusiwe wapumbavu kama ndugu zetu hawa ila tujaribu kuona namna gani tutakwenda nao. Wanakoelekea wanaweza kuleta sokomoko. Kama wakikubaliana kuwa uislamu ni kuua na kuuawa itakuwa balaa kwa sababu ipo siku watalaumu kuwa jua halijawaka sana kwenye maeneo yao
|
0 comments:
Post a Comment