Saturday 15 September 2012

[wanabidii] Bendera Ile Ya Taifa Kijijini Mtandika, Tafakari...

Ndugu zangu,


Ni kweli, Watanzania tunaendekeza sana siasa za vyama na kuiasahau Tanzania yetu. Leo asubuhi sana niliianza safari yangu kutoa Msamvu , Morogoro kuja Iringa. Ni kawaida kando ya barabara kwenye makazi ya watu au vibanda vya biashara kukuta ikipepea, ama, bendera ya CCM, Chadema, CUF, Simba au Yanga. Lakini, ni nadra sana kuiona ikiperushwa bendera ya taifa letu.

Leo pale kijijini Mtandika, nje kidogo ya Ruaha Mbuyuni niliona kwenye banda moja la biashara ikipepea bendera ya taifa. Nilishtuka kuiona , niliguswa pia. Nlipunguza hata mwendo kumwangalia kijana yule aliyekuwa akifanya biashara yake ya vitunguu huku bendera ya nchi yake ikipepea.

Maana, bila shaka kijana yule kwa mapenzi ya nchi yake aliitafuta mwenyewe bendera ile ya taifa. Kwa vile, unapoona mahali kuna vijana wanapeperusha bendera za vyama yaweza kuwa na tafsiri ya ama, ni wapenzi wa vyama hivyo, na kuwa wamezitafuta wenyewe, au kuna kada wa chama husika aliyekuja na kugawa bendera hizo kwa vijana hao.

Ndio, tunahitaji kufanya jitihada za kuwafanya watu wetu waipende nchi yao waliyozaliwa, kutoka ndani ya mioyo yao. Na moja ya jitihada hizo ni kuwapa maarifa yatakayowawezesha kujitambua, kujiamini na kuthubutu.

Maggid,
Iringa.
0788 111 765.
http://mjengwablog.com

--
Karibu Jukwaa la www.mwanabidii.com
Pata nafasi mpya za Kazi www.kazibongo.blogspot.com
Blogu ya Habari na Picha www.patahabari.blogspot.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
 
 

0 comments:

Post a Comment