Sunday 29 January 2017

Re: [wanabidii] WANYONGE MKIUNGANA-SHAIRI

Dear
Group Admin, please add me.

2014-11-16 11:01 GMT+03:00 Novatus Kambota <novakambota@gmail.com>:
Na Nova Kambota, +255712 544237
Jumapili, 16 Novemba 2014
Dar es salaam, Tanzania.
Tano miongo yapita, taifa ladidimia
Wengi wameshastuka,dawa wajitafutia
Viongozi kadhalika, mali walimbikizia
Wanyonge mkiungana, minyororo mtakata

Tazama kwenye ramani, utaona hiyo nchi
Nchi ya wasio soni, wenye tabu wananchi
Raia wapo kinuni, watwangaji wana mchi
Wanyonge mkiungana, minyororo mtakata

Chama kisicho na dira, kimekamata hatamu
Wanakula kwa papara, hamu ya kula utamu
Roho zao za harara, mikono yao ya damu
Wanyonge mkiungana, minyororo mtakata

Wameileta rasimu, bila maoni ya watu
Kutawala wana hamu, roho zimekosa utu
Chama kisicho nidhamu, mfumo wake wa kutu
Wanyonge mkiungana, minyororo mtakata


Unganeni masikini, mijini na vijijini
Zinduka jitambueni, enyi tabaka la chini
Mmefanywa kuwa duni, jitoeni kitanzini
Wanyonge mkiungana, minyororo mtakata

Ondoeni hilo giza, enyi wana afrika
Hakuna cha kubakiza, pigeni kura ya zika
Nchi yazidi kuviza, inakumbwa na gharika
Wanyonge mkiungana, minyororo mtakata

Si dawa si pembejeo, hazipo tele nchini
Heri jana sio leo, taifa la watu duni
Amebanwa kwa koleo, hana hali masikini
Wanyonge mkiungana, minyororo mtakata

Zindukeni kina mama, mlete mabadiliko
Kataeni hiko chama, cha hao wavuta kiko
Idondosheni zahama, kataeni matambiko
Wanyonge mkiungana, minyororo mtakata

Vijana msitumike, bendera fata upepo
Lazima mmakinike, msiwe mfano popo
Pigeni ngumi na teke, hao walamba makopo
Wanyonge mkiungana, minyororo mtakata

Tamati nimefikia, beti kumi natulia
Wavuja jasho sikia, mwongozo fatilia
Unyonyaji kukataa, nchi ipate kupaa
Wanyonge mkiungana, minyororo mtakata.

Mtunzi wa shairi hilini Nova Kambota, ni mchambuzi na mwandishi wa
siasa anayeishi jijini Dar es salaam, anapatikana kwa simu 0712-544237
, barua pepe; novakambota@gmail.com , waweza kutembelea Blog yake;
http://novakambota.wordpress.com

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment