Wednesday 29 April 2015

[wanabidii] WANAZUONI WAJADILI MUSTAKABALI WA TANZANIA DEMOKRASIA YA VYAMA VINGI

Habari za asubuhi,

Tafadhali pokea CODES.


<a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/Jaji-Francis-Mtungi-akifunguja-mkutano-wa-wadau-wa-siasa-wa-uimatishaji-demokrasia-ya-vyama-vingi.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-134536" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/Jaji-Francis-Mtungi-akifunguja-mkutano-wa-wadau-wa-siasa-wa-uimatishaji-demokrasia-ya-vyama-vingi.jpg" alt="Jaji Francis Mtungi akifunguja mkutano wa wadau wa siasa  wa uimatishaji demokrasia ya vyama vingi" width="640" height="427" /></a>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Jaji Francis Mtungi akifungua mkutano wa wadau wa siasa wa uimarishaji demokrasia ya vyama vingi.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Na <span style="color: #0000ff;"><a style="color: #0000ff;" href="http://www.modewjiblog.com/">Modewji Blog team</a></span></strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Dk. Benson Bana wa Chuo Kikuu cha Dare s salaam ambaye amebobea katika masuala ya siasa amewataka wadau wa siasa na wananchi kwa ujumla kuzuia uvunjifu wa amani kuelekea uchaguzi mkuu kwa kufuata Sheria na kutobeza mamlaka.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Dk Bana alisema hayo jana akijibu swali la msimamizi wa mdahalo wenye lengo la kuimarisha demokrasia ya vyama vingi ulioandaliwa na Msajili wa Vyama vya siasa kwa ufadhili wa UNDP, Profesa Bernadetta Killian.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Profesa Killian  alitaka kujua baada ya maelezo ya awali ya Dk Bana juu ya mtazamo wake kuhusu ukuaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Tanzania , nini kinastahili kufanya kuepuka uvunjifu wa amani hasa katika muda huu ambapo viashiria vipo.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Dk Bana alisema kama watu hawatafuata utamaduni wa vyama vingi, utamaduni wa kufuata sheria na kutobeza mamlaka, taifa litaingia katika machafuko.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alisema watu kama wanaona wanaonewa wanatakiwa kufuata taratibu na kama taratibu hizo zinaonekana ni tatizo bado wanatakiwa kuwa na subira na kuondoa taratibu hizo zenye matatizo kwa kufuata utaratibu.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Katika shauri hilo la viashiria vya mizozo Profesa Rugumamu, aliyebobea katika masuala ya kutanzua mizozo aliihimiza Ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa kutengeneza mfumo wa utambuzi wa viashiria vya hatari (early warning) ili iweze kukabiliana navyo mapema.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Akizungumzia kama Tanzania ni nchi ya demokrasia Dk. Bana alisema kwamba kuna maendeleo makubwa yamepatikana tangu mtindo wa vyama vingi kuingia nchini miaka 23 iliyopita.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alisema demokrasia haijengwi kwa siku moja, ina safari ndefu yenye milima na mabonde  na wakati mwingine watu wasifike.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/Mkurugenzi-UNDP-Philippe-Poinsot-akizungumza-katika-mdahalo.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-134542" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/Mkurugenzi-UNDP-Philippe-Poinsot-akizungumza-katika-mdahalo.jpg" alt="Mkurugenzi UNDP Philippe Poinsot  akizungumza katika mdahalo" width="640" height="427" /></a></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong> Mkurugenzi wa Mkazi wa Shirika Maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP, Philippe Poinsot akizungumza na wawakilishi wa vyama mbalimbali vya siasa na kiraia katika mkutano huo.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Aidha alisisitiza kwamba demokrasia sio suala jepesi, lakini watanzania wanastahili kujivuna kwa hatuha waliyofikia katika mambo mbalimbali ambayo hata mataifa mengine ya Ulaya hayajafikia.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alisema mwaka 1994 wakati taifa linaingia katika vyama vingi taifa lilikuwa na vyama 13 kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka 1995 lakini sasa tunapozungumza kuna vyama 22 vyenye usajili wa kudumu, wigo wa kuwania dola ukiwa umetanuka zaidi.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Pia alisema mafanikio mengine ni namna ambavyo vyombo vya habari vina nafasi kubwa ya kuandika inavyoona sawa, japo kumekuwa na tukio la kufungiwa kwa gazeti la Mwanahalisi, Mtanzania na Mwananchi, lakini kadhia hizo haziondoi ukweli kuwa kumekuwepo na uhuru mkubwa wa vyombo vya habari.</strong></span></p>
<a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/Dk-bana-akizungumza-katika-mdahalo.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-134537" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/Dk-bana-akizungumza-katika-mdahalo.jpg" alt="Dk bana akizungumza katika mdahalo" width="640" height="427" /></a>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Dk Benson Bana akizungumzia demokrasia ya vyama vingi.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alisema taifa hili halina sababu ya kuomba radhi kwa mafanikio yaliyopo na changamoto zake katika siasa kwani uelewa katika masuala ya siasa unazidi kutanuka.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alisema pamoja na mafanikio hayo bado kuna mapungufu mengi hasa ya kutokuwa na utamaduni wa vyama vingi, utamaduni unaoambatana na vyama kuwa na  aidolojia (itikadi), kukosekana kwa lugha za kistaarabu katika majukwaa ya siasa na hata mitafaruku ya ndani ya kivyama.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alisema kutanuka kwa wigo wa ushiriki wa kuwania dola (vyama vingi vya siasa)  kunatakiwa kwenda sanjari na kujenga utamaduni huo wa kuimarisha ustawi wa utamaduni wa vyama vingi.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alisema pia kuna haja ya kuimarishwa kwa taasisi zinazosaidia utamaduni huo kama Tume huru ya Uchaguzi, Bunge na hata mfumo wa utawala ambapo wakuu wa mikoa na wilaya wasiwe katika hali ya kikada bali wale wanaoweza kutekeleza majukumu yanayostahili katika maeneo yao.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/jaji-Mutungi-akiwa-na-Mkurugenzi-UNDP-Poinsot.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-134543" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/jaji-Mutungi-akiwa-na-Mkurugenzi-UNDP-Poinsot.jpg" alt="jaji Mutungi akiwa na Mkurugenzi UNDP Poinsot" width="640" height="427" /></a></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Jaji Mutungi akiteta jambo na Mkurugenzi UNDP, Bw. Poinsot.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Aidha alisema kwamba vyama vingi vya siasa vinafanyakazi ya uanaharakati badala ya kuwa na itikadi ya kuifuata .</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alizungumzia pia haja ya vyama vya upinzani kujivunja na kuanzisha chama kimoja na kutengeneza mkakati wa kutwaa dola huku akisema muungano wa Ukawa kwa sasa una mushkeri zaidi badala ya kusaidia kujiandaa kutwaa dola.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Katika mdahalo huo ambao ulielezwa na Msajili wa vyama vya Siasa jaji  Francis Mutungi, si mkusanyiko wa kufanya kampeni ya uchaguzi bali jukumu la ofisi ya msajili hasa kuelekea uchaguzi mkuu, washiriki wake pia walielezwa changamoto za siasa za vyama vingi.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Profesa Rugumamu alisema kwamba katika tafiti aliyoifanya yeye na wenzake katika nchi 15 za bara la Afrika wamekumbana na changamoto  takribani saba ambazo ni kikwazo katika kupata na kukuza utamaduni wa demokrasia ya vyama vingi.</strong></span></p>
<a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/IMG_4917.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-134538" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/IMG_4917.jpg" alt="IMG_4917" width="640" height="427" /></a>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Jopo la wanazuoni kuanzia kulia Dk Bana, Profesa Meena, Profesa Rugumamu na mwishoni ni msimamizi wa mdahalo Prof Bernadetta Killian.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Miongoni mwa changamoto hizo ni vyama vikongwe na utamaduni wake kushindwa kuainisha kati ya mamlaka ya dola na vyama vyenyewe, kuwepo kwa vyama vya kikanda na kidini katika  kipindi cha mpito katika demokrasia ya vyama vingi, wanasiasa kubadili katiba waendelee kutawala, vyama na wanachama kutojua haki na wajibu wao kutokana na kutofundishwa uraia tangu awali.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Pia alizungumza uadui unaojijenga kwa nchi ambazo zimetoka vitani na uanzishaji wa makundi ya ulinzi ya vyama ambavyo husababisha mitafaruku wakati wa uchaguzi au kwenye uchaguzi na matumizi ya fedha yasiyojulikana kwa ama kukosa sheria au sheria kuwapo na watu kutoizingatia.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alisema dosari zote hizo zinatikisa ujenzi wa utamaduni wa demokrasia ya vyama vingi.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Awali akimkaribisha Jaji Mutungi kufungua mkutano huo Mkurugenzi wa UNDP nchini, Philippe Poinsot alisema Umoja wa mataifa  umefurahishwa kwa wadau wa siasa nchini Tanzania kuwa na mazungumzo yenye lengo la kustawisha amani  kuelekea uchaguzi na kutengeneza mfumo wa majadiliano kama kukiwepo na kutokuelewana.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alisema mkutano huo walioufadhili ni sehemu ya makubaliano ya Ofisi ya Msajili na UNDP kupitia mradi wake wa kuimarisha demokrasia (DEP) yenye kulenga kujenga uwezo na kuimarisha demokrasia ya vyama vingi na kuleta maelewano ndani ya vyama na kitaifa wakati nchi inaelekea katika uchaguzi mkuu.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><a style="color: #000080;" href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/IMsimamizi-wa-mdahalo-Prof-Bernadetta-Killian.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-134539" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/IMsimamizi-wa-mdahalo-Prof-Bernadetta-Killian.jpg" alt="IMsimamizi wa mdahalo Prof Bernadetta Killian" width="640" height="427" /></a></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Msimamizi wa mdahalo Prof Bernadetta Killian.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alisema ni matumaini yake kwamba mkutano huo utatengeneza mustakabari bora wa Tanzania kuwa na uchaguzi huru na  wa amani.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alisema kutokana na ushindani, uchaguzi unaweza kuleta matata kwa hiyo ni vyema kama wadau wataliangalia hilo na kuona namna ya kutanzua matata ili taifa libaki  na amani na kusonga mbele katika maeneo yote ya jamii.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Naye Jaji Mutungi aliwaasa washiriki kutambua kwamba hakuna sababu ya kukamiana  na kukomoana miongoni mwa vyama vya siasa kwani wote wanajenga nyumba moja na kimsingi hawana sababu ya kugombania fito.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alitaka wadau kucheza mchezo wa siasa kwa maridhiano ili wasibomoe misingi ya amani ya taifa na mafanikio yake.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alisema lengo la mkutano huo ni kuweka sawa dhana ya demokrasia ya vyama vingi na kutafuta majibu ya changamoto zinazokabili pasipo kuvunja amani ya nchi.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/Profesa-Ruth-Meena-akizungumzia-ushiriki-wa-kijinsia-katika-demokrasia-ya-vyama-vingi.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-134544" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/Profesa-Ruth-Meena-akizungumzia-ushiriki-wa-kijinsia-katika-demokrasia-ya-vyama-vingi.jpg" alt="Profesa Ruth Meena akizungumzia ushiriki wa kijinsia katika demokrasia ya vyama vingi" width="640" height="427" /></a></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Profesa Ruth Meena akizungumzia ushiriki wa kijinsia katika demokrasia ya vyama vingi.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/Profesa-Rugumamu-akizungumza.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-134545" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/Profesa-Rugumamu-akizungumza.jpg" alt="Profesa Rugumamu akizungumza" width="640" height="427" /></a></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Profesa Rugumamu akizungumza.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><a style="color: #000080;" href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/IMG_4861.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-134540" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/IMG_4861.jpg" alt="IMG_4861" width="640" height="427" /></a></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Baadhi ya washiriki wakijadiliana.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><a style="color: #000080;" href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/IMG_4879.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-134541" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/IMG_4879.jpg" alt="IMG_4879" width="640" height="427" /></a></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Washiriki wa mkutano wakijadiliana.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/wanamdahalo-wakiwa-makini.jpg"><img class="aligncenter size-full wp-image-134546" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2015/04/wanamdahalo-wakiwa-makini.jpg" alt="wanamdahalo wakiwa makini" width="640" height="427" /></a></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Wanamdahalo wakiwa makini.</strong></em></span></p>

KAWAIDA

Jaji Francis Mtungi akifunguja mkutano wa wadau wa siasa  wa uimatishaji demokrasia ya vyama vingi

Jaji Francis Mtungi akifungua mkutano wa wadau wa siasa wa uimarishaji demokrasia ya vyama vingi.

Na Modewji Blog team

Dk. Benson Bana wa Chuo Kikuu cha Dare s salaam ambaye amebobea katika masuala ya siasa amewataka wadau wa siasa na wananchi kwa ujumla kuzuia uvunjifu wa amani kuelekea uchaguzi mkuu kwa kufuata Sheria na kutobeza mamlaka.

Dk Bana alisema hayo jana akijibu swali la msimamizi wa mdahalo wenye lengo la kuimarisha demokrasia ya vyama vingi ulioandaliwa na Msajili wa Vyama vya siasa kwa ufadhili wa UNDP, Profesa Bernadetta Killian.

Profesa Killian  alitaka kujua baada ya maelezo ya awali ya Dk Bana juu ya mtazamo wake kuhusu ukuaji wa demokrasia ya vyama vingi nchini Tanzania , nini kinastahili kufanya kuepuka uvunjifu wa amani hasa katika muda huu ambapo viashiria vipo.

Dk Bana alisema kama watu hawatafuata utamaduni wa vyama vingi, utamaduni wa kufuata sheria na kutobeza mamlaka, taifa litaingia katika machafuko.

Alisema watu kama wanaona wanaonewa wanatakiwa kufuata taratibu na kama taratibu hizo zinaonekana ni tatizo bado wanatakiwa kuwa na subira na kuondoa taratibu hizo zenye matatizo kwa kufuata utaratibu.

Katika shauri hilo la viashiria vya mizozo Profesa Rugumamu, aliyebobea katika masuala ya kutanzua mizozo aliihimiza Ofisi ya Msajili wa vyama vya siasa kutengeneza mfumo wa utambuzi wa viashiria vya hatari (early warning) ili iweze kukabiliana navyo mapema.

Akizungumzia kama Tanzania ni nchi ya demokrasia Dk. Bana alisema kwamba kuna maendeleo makubwa yamepatikana tangu mtindo wa vyama vingi kuingia nchini miaka 23 iliyopita.

Alisema demokrasia haijengwi kwa siku moja, ina safari ndefu yenye milima na mabonde  na wakati mwingine watu wasifike.

Mkurugenzi UNDP Philippe Poinsot  akizungumza katika mdahalo

 Mkurugenzi wa Mkazi wa Shirika Maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP, Philippe Poinsot akizungumza na wawakilishi wa vyama mbalimbali vya siasa na kiraia katika mkutano huo.

Aidha alisisitiza kwamba demokrasia sio suala jepesi, lakini watanzania wanastahili kujivuna kwa hatuha waliyofikia katika mambo mbalimbali ambayo hata mataifa mengine ya Ulaya hayajafikia.

Alisema mwaka 1994 wakati taifa linaingia katika vyama vingi taifa lilikuwa na vyama 13 kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka 1995 lakini sasa tunapozungumza kuna vyama 22 vyenye usajili wa kudumu, wigo wa kuwania dola ukiwa umetanuka zaidi.

Pia alisema mafanikio mengine ni namna ambavyo vyombo vya habari vina nafasi kubwa ya kuandika inavyoona sawa, japo kumekuwa na tukio la kufungiwa kwa gazeti la Mwanahalisi, Mtanzania na Mwananchi, lakini kadhia hizo haziondoi ukweli kuwa kumekuwepo na uhuru mkubwa wa vyombo vya habari.

Dk bana akizungumza katika mdahalo

Dk Benson Bana akizungumzia demokrasia ya vyama vingi.

Alisema taifa hili halina sababu ya kuomba radhi kwa mafanikio yaliyopo na changamoto zake katika siasa kwani uelewa katika masuala ya siasa unazidi kutanuka.

Alisema pamoja na mafanikio hayo bado kuna mapungufu mengi hasa ya kutokuwa na utamaduni wa vyama vingi, utamaduni unaoambatana na vyama kuwa na  aidolojia (itikadi), kukosekana kwa lugha za kistaarabu katika majukwaa ya siasa na hata mitafaruku ya ndani ya kivyama.

Alisema kutanuka kwa wigo wa ushiriki wa kuwania dola (vyama vingi vya siasa)  kunatakiwa kwenda sanjari na kujenga utamaduni huo wa kuimarisha ustawi wa utamaduni wa vyama vingi.

Alisema pia kuna haja ya kuimarishwa kwa taasisi zinazosaidia utamaduni huo kama Tume huru ya Uchaguzi, Bunge na hata mfumo wa utawala ambapo wakuu wa mikoa na wilaya wasiwe katika hali ya kikada bali wale wanaoweza kutekeleza majukumu yanayostahili katika maeneo yao.

jaji Mutungi akiwa na Mkurugenzi UNDP Poinsot

Jaji Mutungi akiteta jambo na Mkurugenzi UNDP, Bw. Poinsot.

Aidha alisema kwamba vyama vingi vya siasa vinafanyakazi ya uanaharakati badala ya kuwa na itikadi ya kuifuata .

Alizungumzia pia haja ya vyama vya upinzani kujivunja na kuanzisha chama kimoja na kutengeneza mkakati wa kutwaa dola huku akisema muungano wa Ukawa kwa sasa una mushkeri zaidi badala ya kusaidia kujiandaa kutwaa dola.

Katika mdahalo huo ambao ulielezwa na Msajili wa vyama vya Siasa jaji  Francis Mutungi, si mkusanyiko wa kufanya kampeni ya uchaguzi bali jukumu la ofisi ya msajili hasa kuelekea uchaguzi mkuu, washiriki wake pia walielezwa changamoto za siasa za vyama vingi.

Profesa Rugumamu alisema kwamba katika tafiti aliyoifanya yeye na wenzake katika nchi 15 za bara la Afrika wamekumbana na changamoto  takribani saba ambazo ni kikwazo katika kupata na kukuza utamaduni wa demokrasia ya vyama vingi.

IMG_4917

Jopo la wanazuoni kuanzia kulia Dk Bana, Profesa Meena, Profesa Rugumamu na mwishoni ni msimamizi wa mdahalo Prof Bernadetta Killian.

Miongoni mwa changamoto hizo ni vyama vikongwe na utamaduni wake kushindwa kuainisha kati ya mamlaka ya dola na vyama vyenyewe, kuwepo kwa vyama vya kikanda na kidini katika  kipindi cha mpito katika demokrasia ya vyama vingi, wanasiasa kubadili katiba waendelee kutawala, vyama na wanachama kutojua haki na wajibu wao kutokana na kutofundishwa uraia tangu awali.

Pia alizungumza uadui unaojijenga kwa nchi ambazo zimetoka vitani na uanzishaji wa makundi ya ulinzi ya vyama ambavyo husababisha mitafaruku wakati wa uchaguzi au kwenye uchaguzi na matumizi ya fedha yasiyojulikana kwa ama kukosa sheria au sheria kuwapo na watu kutoizingatia.

Alisema dosari zote hizo zinatikisa ujenzi wa utamaduni wa demokrasia ya vyama vingi.

Awali akimkaribisha Jaji Mutungi kufungua mkutano huo Mkurugenzi wa UNDP nchini, Philippe Poinsot alisema Umoja wa mataifa  umefurahishwa kwa wadau wa siasa nchini Tanzania kuwa na mazungumzo yenye lengo la kustawisha amani  kuelekea uchaguzi na kutengeneza mfumo wa majadiliano kama kukiwepo na kutokuelewana.

Alisema mkutano huo walioufadhili ni sehemu ya makubaliano ya Ofisi ya Msajili na UNDP kupitia mradi wake wa kuimarisha demokrasia (DEP) yenye kulenga kujenga uwezo na kuimarisha demokrasia ya vyama vingi na kuleta maelewano ndani ya vyama na kitaifa wakati nchi inaelekea katika uchaguzi mkuu.

IMsimamizi wa mdahalo Prof Bernadetta Killian

Msimamizi wa mdahalo Prof Bernadetta Killian.

Alisema ni matumaini yake kwamba mkutano huo utatengeneza mustakabari bora wa Tanzania kuwa na uchaguzi huru na  wa amani.

Alisema kutokana na ushindani, uchaguzi unaweza kuleta matata kwa hiyo ni vyema kama wadau wataliangalia hilo na kuona namna ya kutanzua matata ili taifa libaki  na amani na kusonga mbele katika maeneo yote ya jamii.

Naye Jaji Mutungi aliwaasa washiriki kutambua kwamba hakuna sababu ya kukamiana  na kukomoana miongoni mwa vyama vya siasa kwani wote wanajenga nyumba moja na kimsingi hawana sababu ya kugombania fito.

Alitaka wadau kucheza mchezo wa siasa kwa maridhiano ili wasibomoe misingi ya amani ya taifa na mafanikio yake.

Alisema lengo la mkutano huo ni kuweka sawa dhana ya demokrasia ya vyama vingi na kutafuta majibu ya changamoto zinazokabili pasipo kuvunja amani ya nchi.

Profesa Ruth Meena akizungumzia ushiriki wa kijinsia katika demokrasia ya vyama vingi

Profesa Ruth Meena akizungumzia ushiriki wa kijinsia katika demokrasia ya vyama vingi.

Profesa Rugumamu akizungumza

Profesa Rugumamu akizungumza.

IMG_4861

Baadhi ya washiriki wakijadiliana.

IMG_4879

Washiriki wa mkutano wakijadiliana.

wanamdahalo wakiwa makini

Wanamdahalo wakiwa makini.


--
Zainul A. Mzige,
Operation Manager,
MO BLOG,
+255714940992.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment