Thursday 30 April 2015

Re: [wanabidii] OIC na AZIMIO LA ABUJA LINAPOPOTOSHWA KUENEZA CHUKI BAINA YA WATANZANIA

ndugu mbona hata kanisani kwa padre mapunda pale ukombozi manzese wanacheza karate kucheza karate kwa miaka kadhaa sasa

2015-04-30 17:11 GMT+03:00 'ELISA MUHINGO' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>:
ambo haya magumu sana kuyaelewa na kuyajadili. Padri Mapunda amesema ambacho kinaonwa na wengi na mimi nikiwemo. Taabu sana ni jinsi ya kukisemea.
Ukweli ni huu kwamba mambo yanayosemekana kuwemo ndani ya azimio la abuja hayawezi kutekelezwa kama ambavyo tunatekeleza ilani ya chama. Nikama yanatekelezwa kwa siri na ni rahisi kuyakana. Fadhiri hapa ndipo penye shida. Kunamambo yanaeda kichinichini na ni rahisi wanaohusika kuyakana. Tutaibukia kwenye shida kwa sababu tulikosa watu kama mapunda kuyasemea.
Vituko vya kukuta watoto wamefungiwa wanapata mafunzo fulani huko Mosho ni utekelezaji wa azimio la Abuja.
Sehemu mbalimbali tunaona mashule ambayo kuna tetesi kuwa usiku kunafundishwa judo nakadhalika. haijulikani kama ndio mwanzao wa kuimafrisha dola la kiislamu. Uchinjaji wa wakristo huko Libya na Syria. ni utekelezaji wa mikakati hiyo.
Twaweza kusema tunaishi kwa kuchekeana kumbe wengine wanalo wanalolisubiri. Huenda kuyasema yakajadiliwa ndipo tunaweza kusema -ahaa hebu tujipekue.
fadhili usikanushe kila kilichoandikwa na Padri mapunda, labda kama una siri fulani. amesema ukweli na ni vizuri tukashirikiana kurekebisha mambo.
Niliwahi kusikia kuwa katika mkutano wa abuja Tanzania iliwakirishwa na waziri wa mambo ya nje wa wakati huo sikumbuki alikuwa nani. nakumbuka kuandika makala nikitaka serikali ikane haikuwahi kukana.
Hatasasa haitakana.
--------------------------------------------
On Thu, 4/30/15, fadhil fadhil <fadhil.fadhil96@gmail.com> wrote:

 Subject: [wanabidii] OIC na AZIMIO LA ABUJA LINAPOPOTOSHWA KUENEZA CHUKI BAINA YA WATANZANIA
 To: "'Hildegarda Kiwasila' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com>
 Date: Thursday, April 30, 2015, 4:41 PM



 Nikiwa 
 mpenzi wa "ukweli usiyotiliwa shaka",
 nimeshawishika katika kuonyesha upungufu yaliyomo kwenye
 makala  ya Padri Baptiste Mapunda
 iliyochapishwa
 kwenye Toleo Na. 230 la Machi 14 hadi 20, 2012, ukurasa wa
 5, Raia Mwema (ISSN
 1821 – 6250)  yenye kichwa,
 "TANZANIA NA
 OIC: ambapo leo hii kila mwenye ajenda ya siri na OIC
 anaitumia makala hiyo ktk
 uchambuzi wake.

  

  Lijue lengo
 kuu la Azimio la Abuja" kama
 ilivyoandikwa na Padri Baptiste Mapunda (wa Kanisa
 Katoliki).Padri Mapunda
 ameanza kwa utangulizi
 wenye kulielezea tamko (linaloitwa
 Abuja Declaration) na taathira ya tamko hilo kwa

 Tanzania! Ili kupata matini ya
 dhamira ya utangulizi wake tutazame ushahidi huu:

  

  "Baada ya
 kulisoma, nikaridhika na
 nikaunganisha yanayotokea katika nchi yetu ya Tanzania, juu ya harakati
 za
 wenzetu Waislamu ikiwa ni utekelezaji wa tamko hilo muhimu
 la Abuja." Bila ya
 kuonyesha harakati za Waislamu wa Tanzania na taathira ya
 moja kwa moja ya
 tamko hilo (kama limeridhiwa na Waislamu wa Tanzania au la),
 Padri Mapunda ameridhika
 na kuunganisha na kutoa hukumu ya moja kwa moja.

  

 Hapa kuna hoja mbili muhimu ambazo
 Padri Mapunda alihitajika (kwa mujibu wa uchunguzi na
 mantiki inayoufanya
 utafiti uwe wa kisayansi). Kwanza, kwa kuwa tamko la Abuja
 (Abuja Declaration)
 lililotolewa tarehe 28, Novemba 1989

 nchini Nigeria limekuwapo kwa
 takriban miaka 22 sasa; na kwa kuwa (kama anavyodai Padri
 Mapunda) lengo lake
 lilikuwa kuzifuta imani nyingine zisizokuwa

 Uislamu;

  

  nadhani
 ilikuwa vema aonyeshe jinsi tamko hilo
 lilivyoathiri Ukristo katika Tanzania na au hata aonyeshe jinsi
 lilivyotafsiriwa na kufanyiwa kazi na Waislamu wa Tanzania.
 Pili, (Waislamu wa)
 Tanzania si miongoni mwa nchi zilizoshiriki na au hata
 kuridhia tamko hilo; kwa jinsi hiyo,
 Padri Mapunda alitakiwa aoneshe kisayansi jinsi tamko hilo
 lilivyowaathiri
 Waislamu wa Tanzania hata yeye (Padri Mapunda)
 kufikia hatua ya
 kuunganisha yale aliyoyaita
 matukio yanayotokea Tanzania na "tamko la
 Abuja.".

  

 Padri Mapunda, katika kusisitiza
 dhamira ya uandishi wa makala yake, anaandika hivi:
 "Inadaiwa kwamba katika
 yote hayo lengo kuu la OIC na hasa kupitia Azimio la Abuja
 ni kuona kwamba Bara
 lote la Afrika linakuwa la Kiislamu."

 Nilistushwa sana na maelezo haya kwa vile
 mantiki inaonesha kwamba mwandishi (Padri Mapunda) anaandika
 hapa kwamba,
 "inasadikiwa" kana kwamba yeye aidha

 hajasoma malengo ya OIC au ameamua
 kwa makusudi kuwapotosha wasomaji wasielewe dhana hizi
 mbili; yaani OIC na
 tamko (Azimio) la Abuja."

  

 Katika hali hii imenifanya kufanya
 upitizi kwa mara nyingine ili nijiridhishe juu ya malengo ya OIC; kwa ujumla,
 malengo ya OIC kwa mujibu wa Hati Idhini (OIC Charter)
 hayajabadilika tangu
 yalipoidhinishwa na wanachama wake.

  

 Akitumia uandishi wa "ujanja wa
 mbuni kuficha kichwa mchangani ilhali mwili wake uko nje", Padri
 Mapunda
 anaandika hivi: "Huu ndio ukweli wa mambo wala si
 uchochezi wala si
 propaganda ukitaka ukweli nenda tu kwenye internet utaupata
 najisomee maandishi
 mbalimbali juu ya umoja huo wa nchi za Kiislamu, yaani
 OIC."

  

  Nadhani
 mwandishi huyu alijua kwamba
 alichoandika ni"uchochezi" kwa kuwa suala la Tanzania kujiunga na OIC
 limekuwa likipigwa danadana na serikali yaTanzania kwa
 shinikizo la Kanisa
 Katoliki (hili linafahamika). Na vilevile Padri Mapunda
 anafahamu kwamba
 alichoandika ni "propaganda;" yaani, uongo uliokolezwa
 chumvi nyingi dhidi ya
 OIC!Kwa kujaribu kumuweka sawa Padri Mapunda na "uchochezi" na
 "propaganda" zake naomba hapa nichore mifano michache ya
 nchi wanachama wa OIC
 na demografia yake kidini.

  

 OIC (kwa mujibu wa takwimu za
 karibuni) ina nchi wanachama zinazokadiriwa kufikia 57 na
 miongoni mwa nchi
 hizo ni: Msumbiji (Mozambique); Togo; Lebanon; Uganda; Burkina Faso;
 Cameron; na Nigeria.

  

 Kwa nchi zilizotajwa tujaribu
 kuangalia nchi nne (4) kwa uwiano wa kidini kwakurahisha
 ufafanuzi. Msumbiji
 ilijiunga mwaka 1994 ina Wakristo asilimia 56.1(%), Waislamu
 asilimia 17.9 (%)
 na dini nyingine asimilia 26 (%). Kwa maana hiyo Msumbiji ni
 nchi yenye
 Wakristo wengi na iliamua kujiunga na OIC, siyo?

  

  Togo
 ilijiunga na OIC mwaka 1997 ina dini za
 kienyeji asilimia 51 (%), Wakristo asimilia 29 (%) ilhali
 Waislamu asilimia 20
 (%). Hii ina maana kwamba, Togo si nchi ya Kiislamu lakini
 ni mwanachama wa
 OIC! Na kielelezo kingine ni Cameroniliyojiunga mwaka 1975
 ina Wakristo asilimia
 69 (%), Waislamu asilimia 21 (%) na dini nyingine asilimia
 10 (%). Kwa udondozi
 huu Cameron ni nchi yenye Wakristo wengi kuliko dini
 nyingine na ni mwanachama
 wa OIC.

  

 Tumalizie kwa mfano kutoka Afrika ya
 Mashariki; Uganda ilijiunga mwaka 1974 (inawezekana hoja ikawa kwamba
 wakati huo ilikuwa ikitawaliwa na Idd Amin Dada ambaye
 alikuwa
 Muislamu) ina Wakristo asilimia 84 (%) na Waislamu wakiwa
 asilimia 12 (%).
 Uganda ni nchi yenye Wakristo wa madhehebu ya Roman Katoliki
 kama asilimia 41.9
 (%) na kwa kujiunga kwake tangu 1974 hadi leo (ni mwanachama) na hatujasikia
 nchi hiyo imekuwa ya Kiislamu kama

 anavyodai Padri Mapunda!



 Nadhani kungekuwa na hoja nyingine
 juu ya "Islamization of Africa"lakini kwa kutumia uandishi wa
 uchochezi na au propaganda zilizopitwa na wakati kwa kutumia
 ukweli "ghushi"
 unaotengenezwa na mashine za propaganda

 kama "The
 Ministry."
 Katika kuweka
 dhana na kuthibitisha falsafa ya

 uchochezi na propaganda dhidi ya
 Waislamu na Uislamu, Padri Mapunda anaandika hivi, "Sehemu ya
 madhumuni
 ya OIC, kupitia tamko la Abuja ni kufuta katika hali zote
 imani ya
 dini isiyo ya Kiislamu katika nchi wanachama.

  

  Na imani
 ambazo zitabidi zifutwe ni dini ya
 Kikristo, na nyinginezo ambazo hazikubaliani na imani ya
 Kiislamu." Haya ni
 madai mazito sana kuandikwa na mtu anayedhaniwa kwamba ni
 "kiongozi wa kiroho" na padri wa Kanisa

 Katoliki linaloamini juu ya makosa
 dhidi ya kweli kama inavyobainishwa kwenye fungu la 2475 la
 Katekisimu ya
 Kanisa Katoliki!Kwa ujumla, Uislamu unakataza kumlazimisha
 mtu yoyote kuingia
 kwenye Uislamu kwa nguvu (tazama Qur'an 2:
 256).

  

  Kwa katazo
 hilo, vilevile Uislamu umeweka wazi
 juu ya dhana ya kila mtu kuwa na dini yake (tazama Qur'an
 109: 1 – 6) kwa
 falsafa na matini ya aya hizo sidhani kama alichonukuu Padri
 Mapunda ndio
 ufafanuzi wa kweli na haki juu ya malengo ya OIC, kama
 inavyodai makala yake.

  

 Padri Mapunda amejaribu kuonyesha
 vurugu na sintofahamu zinazotokea Nigeria na lile analoliita Azimio
 la
 Abuja! Nadhani hapa pana hoja chaparare inayohitaji (hata
 hivyo) kujibiwa; kama
 tamko la Abuja (Abuja Declaration)

 liliasisiwa miaka 22
 iliyopita,

  

  Boko Haram
 iemanzishwa na tamko hilo?Je, kwa
 kila vurugu za kidini na au sintofahamu na mauwaji ya kidini
 chanzo chake ni
 tamko la Abuja? Nadhani hii haitakuwa sahihi kwa kuwa suala
 la vurugu,
 sintofahamu, songombingo na hata

 mauwaji ya kidini yamekuwa yakitokea
 duniani kutokana na sababu za kibinafsi zaidi

 kuliko za dini yenyewe.

  

 Tuchukuwe mfano wa vita vya kidini
 ndani ya dini moja moja na kwa madhehebu tofauti, kama
 mfano! Waislamu wa
 madhehebu ya Sunni na wa madhehebu ya Shia wamekuwa
 wakipigana na hata kuuwana
 sehemu tofauti za dunia ya Waislamu; kama wanavyouwana waamini wa
 madhehebu ya Kikristo (rejea mauwaji yaliyokuwa yakitokea
 Ireland ya Kaskazini
 kati ya Wakatoliki na Waprotestant); na hapa napo
 tusemeje?

  

  Cha kusikitisha sana Padri Mapunda
 anaandika kwa uangalifu mkubwa sana kwamba:

 "Ukichunguza kwa kina unaweza
 kubaini kwamba utekelezaji wa Azimio la Abuja unakuja
 polepole, hauna haraka.

  

 Na ninasema wazi kwamba katika
 uchunguzi wangu nchini Tanzania, mipango hii pia imeanza
 kutekelezwa kimya
 kimya na kwa uangalifu mkubwa sana." Hapa inaonyesha
 kwamba Padri Mapunda
 amefanya utafiti wa kina na wa kutosha na anazo data (na taarifa) rasmi juu ya
 matokeo ya taathira ya lile analodai ni Azimio la
 Abuja.

  

 Padri Mapunda, kama muamini na
 kiongozi (kwa ngazi ya upadri) anapaswa kufuata vema na kwa
 makini fungu la
 2478 la Katekisimu ya Kanisa Katoliki
 linalotamka kwamba: Ili
 kuzuia hukumu ya haraka,
 kila mmoja awe mwangalifu kadiri inavyowezekana kutafsiri
 mawazo, maneno, na
 matendo ya jirani yake kwa namna nzuri.

  

 Hapa naomba nieleweke kwamba jirani
 ya Wakristo katika Tanzania ni Waislamu (tunaishi ndani ya
 paa moja la Tanzania) kwa hiyo ni vema na hakitukiheshimiana
 kwa tofauti za dini zetu,
 tukipendana kama watoto wa Baba Mmoja (Adam) na tukiabudu
 kwa kila mmoja na
 dini yake ilhali wote tunamuelekea Mungu Mmoja kwa imani
 tofauti.

  

  Uislamu,
 kama mfumo maisha, hauwezi kumlazimisha yoyote kuingia
 kwenye dini (Qur'an
 2: 256) na dini inayotumia
 zaidi hekima na mawaidha mema (Qur'an 16:125)

  

  





 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya
 kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment