Sunday 31 August 2014

[wanabidii] UTAFITI WAIBUA MAKUBWA NGONO ZA UTOTONI DAR

Habari za asubuhi,

Tafadhali pokea CODES, nikutakie siku njema



<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/08/DSC_01401.jpg"><span style="color: #000080;"><img class="aligncenter size-full wp-image-115519" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/08/DSC_01401.jpg" alt="DSC_0140" width="640" height="427" /></span></a></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Mratibu wa mradi wa PREPARE ambaye pia ni Mwanasaikolojia wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi shirikishi cha Muhimbili, Kitengo cha magonjwa na afya ya akili, Lusajo Kajula (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukamilisha SAMPULI tathmini ya matokeo ya mradi wa PREPARE uliokuwa na lengo la kuangalia uwezekano wa vijana kupunguza ngono mwishoni mwa wiki kwenye kituo cha maelezo ya afya Muhimbili katika idara ya magonjwa ya akili. Kulia ni Mtathmini kiongozi wa mradi huo, Mrema Kilonzo.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Na Mwandishi wetu</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>SAMPULI tathmini ya matokeo ya mradi wa PREPARE uliokuwa na lengo la kuangalia uwezekano wa vijana kupunguza ngono, imebainisha haja ya elimu ya afya ya uzazi kukabili hali ya sasa ya tabia hatarishi zinazowakabili vijana wadogo.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Matokeo ya awali ya mradi yalionesha kuwa asilimia 10 ya vijana wenye umri wa miaka 12 mpaka 14 ambao ni darasa la tano na sita waliofanyiwa utafiti walikuwa wameshawahi kufanya ngono na asilimia kubwa ikiwa ni kwa kutumia njia ya haja kubwa.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Kauli hiyo imetolewa na mmoja wa watafiti wa Chuo Kikuu cha Afya na Sayansi shirikishi cha Muhimbili,Kitengo cha magonjwa na afya ya akili, Lusajo Kajula.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>"Vijana wengi walionekana wakifanya ngono ya uke na ya mdomo ikifuatiwa na ngono ya njia ya haja kubwa Kwa wale ambao wameshawahi kufanya ngono, asilimia 6.3 wamefanya ngono ya njia ya haja kubwa wakati asilimia 93.7 hawajawahi."</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Aidha alisema utumiaji wa kondomu ulionekana kuwa mdogo kwa vijana wadogo ambao wameanza kufanya ngono.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>"Asilimia 68 ya wale walioanza kufanya ngono hawajawai kutumia kondomu kabisa wakati asilimia 32 wamewahi kutumia kondomu."</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alisema utafiti huo ni sehemu ya utafiti wa miaka minne ulioshirikisha Vyuo Vikuu vya Makerere cha Uganda, Cape Town na Limpopo vya Afrika Kusini, Bergen na Oslo vya Norway, Maastricht cha Uholanzi na Sussex cha  nchini Uingereza.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/08/DSC_0154.jpg"><span style="color: #000080;"><img class="aligncenter size-full wp-image-115520" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/08/DSC_0154.jpg" alt="DSC_0154" width="640" height="427" /></span></a></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Mtathmini kiongozi wa mradi huo, Mrema Kilonzo akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) uliofanyika jijini Dar es Salaam.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Alisema utafiti umeonesha haja ya kutolewa elimu ya afya ya uzazi kwa vijana wadogo ambao bado hawajaanza ngono ili kuchelewesha kuanza ngono kwa mfumo wa kisaikolojia ili waweze kujitambua na kuacha kufuata nadharia za kisayansi pekee ambazo ndizo zinazotumika katika shule mbalimbali kuwaeleza mabadiliko ya miili yao.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Katika utekelezaji wa utafiti huo idadi ya wanafunzi 5,099 walichaguliwa mwanzoni mwa mradi kufanyiwa utafiti huo ambapo wanafunzi 4783 (asilimia 93.9) walifuatiliwa kwa miezi 6 na wengine 4370 (asilimia 85.8) walifuatiliwa kwa miezi 12.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Utafiti ulionesha elimu inayojishughulisha na masuala ya ujinsia na afya ya uzazi kwa vijana wadogo itumie mtazamo mpana utakaoleta mabadiliko ya msingi kwenye misingi ya virekebisho vya mabadiliko ya tabia.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Mradi huo wa PREPARE ulitekelezwa kwenye shule 38 kutoka manispaa ya Kinondoni zilizochaguliwa kwa kutumia taratibu sampuli mtawanyiko zilizopangwa katika makundi mawili ya shule za mwingilio yaani ilikotolewa elimu hiyo zilizokuwa 19 na za kulinganisha  zilizokuwa 19.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Ili kuweza kupata matokeo yaliyokusudiwa mradi ulitoa mafunzo kwa walimu watano wakufunzi wa wakufunzi; ulitoa mafunzo kwa walimu watekelezaji 76,  na waelimishaji rika wanafunzi 132 na kuelekeza watoa huduma 8 wa afya katika kliniki za huduma rafiki kwa vijana ili kutekeleza muingiliano.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Tathmini iliyotoa majibu ya jinsi utendaji unavyoendelea na ya matokeo ilihusisha shule zote na wanafunzi zaidi ya 6,000 waliowekwa kwenye muingiliano, huku uchambuzi wa tathmini ukihusisha wanafunzi wenye umri wa miaka 12-14, wenye kujua kusoma na kuandika.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Matokeo yaliyotathminiwa ni Mabadiliko katika masuala ya ngono (kuanza ngono) na Kutumia kondomu wakati wa  kujamiiana kwa wale waliokwisha anza ngono.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Kwa wastani mradi uliona kwamba mwingilio wa PREPARE ulipunguza uwezekano wa vijana wadogo (wavulana  na wasichana) kuanza ngono na kuongeza uwezekanao wa kutumia kondomu kwa wale walioanza.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong><a href="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/08/DSC_01482.jpg"><span style="color: #000080;"><img class="aligncenter size-full wp-image-115521" src="http://dewjiblog.com/wp-content/uploads/2014/08/DSC_01482.jpg" alt="DSC_0148" width="640" height="427" /></span></a></strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000080;"><em><strong>Baadhi ya waandishi wa habari waliohudhuria mkutano huo. Kushoto ni mwandishi wa habari wa gazeti la Mwananchi, Vicky Kimaro akiuliza swali kwenye mkutano huo.</strong></em></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Hata hivyo, katika utekelezaji wa mradi mabadiliko katika uchukuaji wa hatua yalionekana zaidi miongoni mwa wasichana waliopata mwingilio ukilinganisha na wale ambao hawakupata mwingilio.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Uchukuaji wa hatua ulisababisha tabia ya kutumia kondomu miongoni mwa wanafunzi wa kiume lakini siyo miongoni mwa wanafunzi wa kike.</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>"Kimsingi tunataka kuwaambia wanahabari kuwa miongoni mwa  mafanikio makubwa ya mradi wa PREPARE  ni kuchelewesha kuanza ngono miongoni mwa wanafunzi wa kiume na wa kike wenye umri wa miaka 12-14 katika mkoa wa Dar es Salaam, Tanzania;</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>"Kuongeza uchukuaji wa hatua ulio chanya katika kutumia kondomu kwa jinsia zote na taarifa za ongezeko la utumiaji wa kondomu miongoni mwa vijana wa kiume. "</strong></span></p>
<p style="text-align: center;"><span style="color: #000000;"><strong>Mradi huu uliofadhiliwa na Umoja wa Nchi za Ulaya, Programu ya utafiti wa afya umelenga kuangalia mwingilio ulio katika misingi ya utamaduni na jinsia, endelevu, kijamii ili kukuza ujinsia na afya ya uzazi miongoni mwa vijana wenye umri kati ya miaka 12-14 kwa kutumia shule kama njia ya kufundishia.</strong></span></p>

--
Zainul A. Mzige,
Operation Manager,
MO BLOG,
+255714940992.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment