Saturday 30 August 2014

[wanabidii] UB ILIVYOPANIA KUINUA ELIMU YA BIASHARA,UWEKEZAJI KIMATAIFA

UB ILIVYOPANIA KUINUA ELIMU YA BIASHARA,UWEKEZAJI KIMATAIFA
Na Happiness Katabazi
AGOSTI 11- 22 mwaka huu, Chuo Kikuu cha Bagamoyo ( UB) kilichopo Mikocheni kwa Warioba Dar es Salaam, kiliandika historia mpya kwaniaba ya serikali Tanzania, kwa kuendesha Mafunzo ya siku 14 ya jinsi ya kujadili mikataba ya Biashara na Uwekezaji Kimataifa .

Mafunzo hayo ambayo yameshirikisha maofisa Biashara waandamizi toka serikali za nchi nane ikiwemo Tanzania na yalifadhiliwana na Taasisi ya Nordic Afrika ya Chuo Kikuu Cha Uppsalla , Sweeden ambayo Taasisi hiyo ili wakilishwa na Profesa Francis Matambalya na mtandao wa vyuo vikuu vitano ambapo UB ni mwanachama wa mtandao wa (TANUP/PUTAna serikali iliwakirishwa na Biashara toka Wizara ya Viwanda na Biashara na Ofisa Biashara wa Wizara hiyo Elia Mtweve.

Akizungumza Katika siku ya Kufunga Mafunzo hayo Ijumaa iliyopita Katika Hoteli ya Habour View Da Es Salaam, Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Bagamoyo(UB), Profesa Costa Rick Mahalu aliishukuru Taasisi ya Nordic Afrika ya Chuo Kikuu Cha Uppsalla, Sweedn kilichowasilishwa na Mtanzania ambaye ni mwadhiri wa Uchumi wa Chuo hiyo nchini Sweeden, Profesa Matambalya kukubali ombi la Chuo Kikuu Cha Bagamoyo la kufadhiliwa Mafunzo ya jinsi kuandaa majadaliano ya Biashara na uwekezaji kwa maofisa wa fani ya Biashara toka nchi nane ambapo Tanzania kupitia Chuo Kikuu Cha Bagamoyo.

Profesa Mahalu pia alisema anaishukuru serikali ya Tanzania kukubali Mafunzo hayo ambayo ya naenda kusababisha Chuo Kikuu Cha Bagamoyo Oktoba Mwaka huu kuanzisha shahada mpya ya jinsi ya kuanda mjadala ya Kibiashara na uwekezaji ambayo itakuwa ni shahada ya kwanza kuanza kutolewa Katika vyuo vikuu hapa nchini na nchi zilizoshiriki Katika Mafunzo hayo, yaendeshwe hapa nchini.

Profesa Mahalu alisema washiriki wa Mafunzo hayo walitokea nchi Tanzania ambayo ni Mwenyeji, Kenya, Uganda, Burundi, Rwanda, Lesotho, Kongo, Malawi, Ethiopia, Zambia na Madagascar.Na Baadhi wa washiriki ni maofisa wa juu wa serikali wa nchi wanazotoka na mmoja ni Mkurugenzi wa Taasisi za Sekta Binafsi nchini Lesotho, Thabo Quesi na wengine wanatoka Vyuo Vikuu Vya vya mataifa Yao.

' Kwa Kuwa Mafunzo haya yameletwa UB, Kwaniaba ya Chuo Kikuu Cha Bagamoyo, tunaahidi kufanya mradi wa Mafunzo haya ni endelevu na unakuwa kwa kasi Kwani Tayari tumeishaanzisha Taasisi mpya itakayokuwa chini ya Shule ya Biashara na Utawala ya UB inayoongozwa na Dk.Lenny Kasoga ambapo Taasisi hiyo itakuwa inatoa Mafunzo ya jinsi ya kuandaa majadiliano ya Kibiashara na uwekezaji :

" Nanaiomba serikali kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara iruhusu maofisa wake wa Biashara waje kusoma shahada hiyo Kwani shahada hiyo itakuwa ni mpya na itawasaida maofisa Biashara wetu kukabiliana na tatizo la kushindwa kufanya vizuri Katika eneo la majadiliano na Biashara ya Kimataifa na wananchi wengine Waje kusoma kozi hiyo" anasema Profesa Mahalu.

Profesa Mahalu Alisema Seneti ya UB Imefikia uamuzi wa kuwatunuku uprofesa kuwa maprofesa wa UB, wasomi wanne waliobobea Katika fani Biashara na kutokana na Seneti imejiridhisha Kuwa wasomi Hao wamefanya mambo Makubwa kupitia taaluma ya Biashara .

Aliwataja wasomi Hao Kuwa ni Dk.Dickson Yeboah ambaye ni Mfanyakazi wa Shirika la Biashara la Dunia (WTO) yenye makao yake makuu Geneva Uswiss, Dk.Francis Matambalya,Dk. Baoudoiun Michael na Mkurugenzi wa Mtangamano wa Biashara toka Wizara ya Viwanda na Biashara nchini, Lucas Saranga Kuwa maprofesa.Na kwamba kuanzia siku hiyo ya Agosti 22 Mwaka huu ,wasomi Hao wametunukiwa Kuwa ni maprofesa.

Aidha Balozi Mahalu anasema sherehe za ufungwaji wa Mafunzo Yale uliambatana na kuwatunuku uprofesa na pia kuzindua Mtandao wa vyuo vikuu vitano (TANUP/PUTA) ambavyo vyuo vikuu hivyo vi nafanyakazi Kwa kushirikiana ambapo ulizinduliwa Mtandao huo.

Mkuu wa Shule ya Biashara na Utawala ya Chuo Kikuu Cha Bagamoyo, Dk.Lenny Kasoga , Profesa Lucas Saranga, Profesa Yeboah ,Profesa Matambalya , Profesa Baoudoiun na Profesa Vale Karugaba ambao wote walikuwa ni wakufunzi katika mafunzo hayo kwa nyakati tofauti walisema waliweza kuwafundisha washiriki wa mafunzo hayo mambo makuu matano:

Moja, kiwango cha biashara na uwekezaji kilichofikiwa.Pili, misingi ya uwekezaji na mazingira ya biashara katika ngazi ya kimataifa, Tatu; Uchambuzi wa uwiano wa ushindani wa kibiashara na uwekezaji ngazi ya kimataifa. Nne; Nadharia ya majadiliano ya Biashara na uwekezaji kwa vitendo.Tano; kushiriki kwa majadiliano ya Biashara na uwekezaji.

Aidha Matambalya ambaye Taasisi yake ndiyo Imebadili Mafunzo hay ya kwanza kutolewa nchini anasema yeye ni Mtanzania na anafanyakazi Katika Taasisi hiyo ya kigeni ya Nordic ,Uppsalla,Uswiss ataakikisha huo mradi wa Mafunzo ambao wameupeleka UB, unakuwa endelevu na Taasisi yake itaendelea kufadhili ili Watanzania wengi waweza kusoma kozi hiyo ili mwisho wa siku taifa liweze kuondokana na tatizo la Kuwa na wataalamu wasiyobobea Katika eneo la majadiliano ya Biashara na uwekezaji na kuingia mikataba na wawekezaji .

Kwa upande wake Aliyekuwa mgeni rasmi katika kufunga mafunzo hayo ,Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Elimu ya Juu serikali imewataka washiriki wa mafunzo ya jinsi ya kujadili mikataba ya Biashara na uwekezaji kutumia taaluma hiyo waliyoipata kwaajili ya kuleta manufaa kwa mataifa Yao.

Dk. Mbwambo kwaniaba ya Waziri wa wizara hiyo, Dk.Shukuru Kawambwa anasema serikali inakipongeza Chuo Kikuu Cha Bagamoyo (UB), kwa kuandaa Mafunzo hayo ambayo yameshirikisha maofisa wajuu wa serikali mbalimbali Kwani kupitia Mafunzo Hao maofisa Hao wameweza kubadilishana uzoefu wa masuala ya nchi zao kuhusu Sekta ya masoko na uwekezaji.

Dk.Mwambo anasema kila kukicha baadhi ya nchi za Africa zimekiwa zikigundulika kuwa na utajiri mkubwa aridhini na mfano mzuri ni nchi ya Tanzainia ambayo imegundulika kuwa ina nishati ya gesi , madini hivyo kupitia mafunzo hayo kwa upande wa Tanzania Wizara ya Viwanda na Biashara iliwakirishwa na maofisa wake Wawili wameweza kupata ujuzi ambao utaki saidia serikali ya kuweza kufanya vizuri Katika uandaaji wa masoko na uwekezaji wafanyabiashara wa Kimataifa watakaokuwa wanakuja kuwekeza nchini.

' Nchi nyingi za Afrika ikiwemo Tanzania zimegundulika Kuwa na utajiri mfano Tanzania hivi sasa imegundulika Kuwa na nishati ya gesi hivyo Mafunzo hayo yataisidia nchi kuondokana na tatizo kuingia mikataba na wawekezaji wa kigeni ambayo italeta tija kwa mataifa ya nchi zinazoendelea.

Nao washiriki wa Mafunzo hayo Bifou Lufuma toka Serikali ya Kongo na Thabo Quesi (Lesotho) na Elia Mtweve kutoka Tanzania wanasema Mafunzo hayo yamewajengea uwezo na kwamba watakuwa mabalozi wazuri Katika maeneo Yao ya Kazi na kwamba wanaiopongeza UB kuendesha Mafunzo ambayo ni ya kwanza kutolewa hapa nchini.

Mwandishi wa makala hii ni:
Ofisa Habari wa Chuo Kikuu Cha Bagamoyo (UB)
0716 774494
Blog:www.katabazihappy.blogspot.com
Facebook: Happy Katabazi
Chanzo: Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi, Agosti 30 Mwaka 2014








Sent from my iPad

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment