Sunday 30 July 2017

[wanabidii] MAMA NAMAINGO ‘AWAFUNDA’ AKINAMAMA WA GREEN VOICES KILIMOBIASHARA NA UJASIRIAMALI

CODES:
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<b><i><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Mkurugenzi wa Namaingo, Biubwa Ibrahim</span></i></b></div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<b><i><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Mratibu wa Mradi wa Green Voices kutoka Hispania, Alicia Cedaba, akiwapa majukumu washiriki wa warsha hiyo.</span></i></b></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;"><br /></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">MKURUGENZI
Mtendaji wa kampuni ya Namaingo Business Agency, Biubwa Ibrahim, amewataka
akinamama wanatekeleza mradi wa Green Voices Tanzania kuwa wabunifu na kutokata
tamaa katika shughuli wanazozifanya.</span></span></div>
<!--more--><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;"><o:p></o:p></span><br />
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Akizungumza
wakati wa kufunga semina ya siku sita ya mafunzo yaliyowashirikisha akinamama
15, Biubwa alisema kwamba, ubunifu, jitihada na kutokata tamaa ndiyo silaha
kubwa katika mafanikio, huku akiwahimiza watafute fedha bila kuchoka.<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">"Lazima
muwe wabunifu, halafu ni dhambi kubwa kukata tamaa bali mnatakiwa kuongeza
jitihada katika mradi yenu," aliwahimiza.<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Aidha,
alisema kwamba, mafanikio yoyote hayawezi kuja kwa siku moja, hivyo wanapaswa
kuwa wavumilivu daima ili waweze kufanikiwa.<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Akinamama
hao wa Green Voices wanatekeleza miradi mbalimbali ya kilimo inayoendana na
mapambano dhidi ya uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabianchi, ambayo
inadhaminiwa na taasisi ya Women for Africa Foundation ya Hispania inayoongozwa
na makamu wa rais mstaafu wa nchi hiyo, Bi. Maria Tereza Fernandes de la Vega.<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Biubwa
alisema, wajasiriamali wengi wanaposhindwa kuona faida ya shughuli
wanazozifanya huvunjika moyo mapema, lakini hilo lisiwe kikwazo kwao kwani
wanapaswa kukaa chini na kutafakari njia mpya ya kuendesha biashara ama miradi
yao.<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">"Inabidi
kujiuliza wewe mwenyewe kama hapo ulipo ndipo mahali sahihi, vinginevyo usife
moyo unapoona mambo hayaendi, bali angalia wapi ulipokosea na ujipange upya
halafu utaona matokeo yake," alisema.<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Akaongeza:
"Mimi nilianza na mtaji wa shilingi elfu nne tu, nimepitia changamoto nyingi
ikiwemo kudhulumiwa fedha, lakini katu sikukata tamaa nimeendelea kupambana na
mpaka sasa kupitia kampuni yangu nimeweza kusajili wakulima 400,000 nchi
nzima."<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<i><b><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Mwanahabari mshiriki wa mradi wa Green Voices, Farida Hamisi, akipokea cheti kutoka kwa Alicia Cedaba, Mratibu wa Green Voices kutoka Hispania. Katikati ni muwezeshaji wa mafunzo hayo, Dkt. Olomi kutoka taasisi ya IMED.</span></b></i></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: 0.0001pt; text-align: center;">
<span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;"><br /></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Mradi wa
Green Voices unatekelezwa nchini Tanzania pekee, ambapo akinamama 10 kati ya 15
wanaendesha miradi mbalimbali ya kilimo, ufugaji wa nyuki, ukaushaji wa mboga
na matunda pamoja na utengenezaji wa majiko rafiki katika jitihada za kupambana
na mabadiliko ya tabianchi.<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Akinamama walioanzisha miradi hiyo – miradi na mikoa
watokayo vikiwa kwenye mabano –ni Regina Kamuli (Mkuranga, Pwani – <a href="https://www.jamiiforums.com/threads/dc-kihato-ni-aibu-mwanamke-kutoka-alfajiri-kutafuta-kuni-mume-amelala.1054634/">Majiko
Banifu</a>), Abiah Magembe (Kisarawe, Pwani – <a href="http://www.fikrapevu.com/kilimo-cha-muhogo-chawanufaisha-akinamama-kisarawe/">Usindikaji
wa Muhogo na Mtama</a>), Magdalena Bukuku (Kinondoni, Dar es Salaam – <a href="http://maendeleovijijini.blogspot.com/2016/07/kilimo-cha-uyoga-dar-chawavutia.html">Kilimo
cha Uyoga</a>), Mariam Bigambo (Dakawa, Morogoro – <a href="http://maendeleovijijini.blogspot.com/2016/07/dakawa-green-voices-wafuga-nyuki.html">Ufugaji
wa Nyuki</a>), na Esther Muffui (Morogoro – <a href="http://maendeleovijijini.blogspot.com/2016/07/akinamama-morogoro-waelimishwa-jinsi-ya.html">Ukaushaji
wa Mboga na Matunda</a>).<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Wengine ni Farida Makame (Kilimanjaro – <a href="http://maendeleovijijini.blogspot.com/2016/12/mradi-wa-green-voices-wafanikisha.html">Majiko
ya Umeme-Jua</a>), Leocadia Vedastus (Ukerewe, Mwanza – <a href="http://maendeleovijijini.blogspot.com/2016/07/dc-ukerewe-ashauri-wananchi-kulima.html">Kilimo
na Usindikaji wa Viazi Lishe</a>), Monica Kagya (Kisarawe, Pwani – <a href="http://maendeleovijijini.blogspot.com/2016/07/wanawake-wafuga-nyuki-kuokoa-misitu-ya.html">Ufugaji
wa Nyuki</a>), Dkt. Sophia Mlote (Kinyerezi, Dar es Salaam – <a href="https://www.jamiiforums.com/threads/dk-mlote-kilimo-hifadhi-kitanikomboa-hata-nikistaafu.1048022/">Kilimo
Hai cha Nyanya na Mbogamboga</a>), na Evelyn Kahembe (Uvinza, Kigoma – Kilimo
cha Matunda).<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span lang="ES" style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Mradi huu wa Green Voices ambao mwaka huu uko
katika awamu ya pili, ulizinduliwa Julai mwaka 2016 na Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan.<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span lang="ES" style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Katika awamu ya pili kinamama hawa
wameendelea kuboresha kilimo cha mazao yao kinachozingatia uhifadhi wa
mazingira na mabadiliko ya tabia nchi katika mikoa sita nchini. <o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span lang="ES" style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">"Pamoja na kilimo, Mradi wa Green Voices
umaeandaa mafunz mbalimbali ya kuongeza ujuzi katika kilimo (climate smart
agricultura) pamoja na mafunzo ya jinsi ya kuandaa mazao au bidhaa
wanazozalisha kupitia kilimo," alisema Mratibu wa Green Voices nchini Tanzania
Secelela Balisidya.<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span lang="ES" style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Katika kutekekelza hilo, Green Voices kupitia
mfadhili wake, Women for Africa Foundation, walishiriki katika mafunzo
mbalimbali ya Mbinu bora za kuweka nembo na kufungasha bidhaa za vyakula,
Viwango vya Ubora, na Kanuni za uchakataji wa vyakula.<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span lang="ES" style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Mafunzo hayo ambayo yalifanyika Julai 16 -22,
2017 yalizinduliwa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), Selemani
Jaffo, ambaye aliahidi kuwapa ushirikiano akina mama hao.<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<br /></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<b><span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Utengenezaji bidhaa na ufungashaji<o:p></o:p></span></span></b></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Kwa siku
sita baada ya kuzinduliwa kwa mafunzo, akinamama hao walijifunza kuhusu Mchango
wa kilimo katika mabadiliko ya tabianchi, Jinsi ya kuweka mazingira bora ya
umwagiliaji, Mikakati ya biashara katika ujasiriamali wa kilimo, Utafutaji wa
rasilimali na mkakati wa kuongeza mtaji, Ukuzaji wa mtaji kupitia Vicoba, na Mbinu
za uongozi.<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Akinamama
hao walipata fursa ya kutembelea Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Shirika la
Maendeleo ya Viwanda Vidogo (SIDO) ambapo ilikutana na wajasiriamali walio
katika hatua za juu za kufungasha na kuuza bidhaa zao, ambapo walipata nafasi ya
kubadilishana nao mawazo ili kuongeza ujuzi wao.<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Katika
mafunzo hayo, Linus Gedi ambaye ni mtaalam wa ubora wa chakula na viwango kabla
ya kuvipeleka sokoni, aliwaeleza washiriki kwamba ni muhimu kufungasha na
kuweka nembo kwani inasaidia kuhifadhi bidhaa na inarahisisha&nbsp; mteja kutambua hiyo ni bidhaa ya aina gani,
imetengenezwa wapi na ina mchanganyiko gani.<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<div class="separator" style="clear: both; text-align: center;">
<i><b><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Akinamama wanaotekeleza mradi wa Green Voices walipotembelea Ofisi za SIDO jijini Dar es Salaam.</span></b></i></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: 0.0001pt; text-align: center;">
<span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;"><br /></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">"Ni
muhimu sana kuhakikisha chakula hakisababishi maradhi, lakini pia kinafikia
malengo ya walaji, hii huepusha sumu kwenye chakula, mchanganyiko usiofaa,
upotevu wa chakula, kupoteza bidhaa na kuepukana na masuala ya kisheria,"
alisema Linus.<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Alisema
uzalishaji wa chakula unatakiwa kuzingatia mbinu bora za uzalishaji na pamoja
na usafi.<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Aidha,
aliwataka kuzingatia ubora, usafi na viwango vya chakula wanachozalisha ili
kifikia malengo ya walaji.<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Kwa upande
wake, Richard Jackson akielezea umhimu wa kunadi bidhaa, alisema ni lazima kuwa
na mikakati imara ya masoko ili kuhakikisha mjasiriamali anapata faida.</span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Alisema ni
vizuri kujua wateja maalum na wateja wa ujumla na nini hasa wanahitaji ikiwa ni
pamoja na namna ya kuwafikia.<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;"><span style="font-size: 14pt;">"Ni lazima
kujua kati ya wanaohitaji bidhaa zako, ni nani ambao siyo wateja wako walengwa
na kwa nini wateja wanunue bidhaa zako na siyo kwa washindani wako? </span><span lang="ES" style="font-size: 14pt;">Lazima ujue tabia zao na ukubwa wa soko lako," alisema Jackson.<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span lang="ES" style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Aidha, alisema ni muhimu kuwajua wateja wako ili kuelewa
mahitaji yao na kwa nini wananunua bidhaa wanazonunua pamoja na kutambua mambo
yanayowaudhi ili usiwakwaze.<o:p></o:p></span></span></div>
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<span lang="ES" style="font-size: 14pt;"><span style="font-family: Georgia, Times New Roman, serif;">Kwa upande wa uchangishaji fedha na kutafuta
mitaji kwa biashara na kilimo, Rais wa VICOBA Endelevu Tanzania, Devota
Likokola, alieleza jinsi mfumo wa VICOBA Endelevu unavyoweza kuwasaidia
kinamama wa Green Voices kupata mitaji ya kuendeleza miradi yao.<o:p></o:p></span></span></div>
<br />
<div class="MsoNormal" style="line-height: normal; margin-bottom: .0001pt; margin-bottom: 0in;">
<br /></div>


​KAWAIDA:

Mkurugenzi wa Namaingo, Biubwa Ibrahim

Mratibu wa Mradi wa Green Voices kutoka Hispania, Alicia Cedaba, akiwapa majukumu washiriki wa warsha hiyo.


MKURUGENZI Mtendaji wa kampuni ya Namaingo Business Agency, Biubwa Ibrahim, amewataka akinamama wanatekeleza mradi wa Green Voices Tanzania kuwa wabunifu na kutokata tamaa katika shughuli wanazozifanya.


Akizungumza wakati wa kufunga semina ya siku sita ya mafunzo yaliyowashirikisha akinamama 15, Biubwa alisema kwamba, ubunifu, jitihada na kutokata tamaa ndiyo silaha kubwa katika mafanikio, huku akiwahimiza watafute fedha bila kuchoka.

"Lazima muwe wabunifu, halafu ni dhambi kubwa kukata tamaa bali mnatakiwa kuongeza jitihada katika mradi yenu," aliwahimiza.

Aidha, alisema kwamba, mafanikio yoyote hayawezi kuja kwa siku moja, hivyo wanapaswa kuwa wavumilivu daima ili waweze kufanikiwa.

Akinamama hao wa Green Voices wanatekeleza miradi mbalimbali ya kilimo inayoendana na mapambano dhidi ya uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabianchi, ambayo inadhaminiwa na taasisi ya Women for Africa Foundation ya Hispania inayoongozwa na makamu wa rais mstaafu wa nchi hiyo, Bi. Maria Tereza Fernandes de la Vega.

Biubwa alisema, wajasiriamali wengi wanaposhindwa kuona faida ya shughuli wanazozifanya huvunjika moyo mapema, lakini hilo lisiwe kikwazo kwao kwani wanapaswa kukaa chini na kutafakari njia mpya ya kuendesha biashara ama miradi yao.

"Inabidi kujiuliza wewe mwenyewe kama hapo ulipo ndipo mahali sahihi, vinginevyo usife moyo unapoona mambo hayaendi, bali angalia wapi ulipokosea na ujipange upya halafu utaona matokeo yake," alisema.

Akaongeza: "Mimi nilianza na mtaji wa shilingi elfu nne tu, nimepitia changamoto nyingi ikiwemo kudhulumiwa fedha, lakini katu sikukata tamaa nimeendelea kupambana na mpaka sasa kupitia kampuni yangu nimeweza kusajili wakulima 400,000 nchi nzima."

Mwanahabari mshiriki wa mradi wa Green Voices, Farida Hamisi, akipokea cheti kutoka kwa Alicia Cedaba, Mratibu wa Green Voices kutoka Hispania. Katikati ni muwezeshaji wa mafunzo hayo, Dkt. Olomi kutoka taasisi ya IMED.


Mradi wa Green Voices unatekelezwa nchini Tanzania pekee, ambapo akinamama 10 kati ya 15 wanaendesha miradi mbalimbali ya kilimo, ufugaji wa nyuki, ukaushaji wa mboga na matunda pamoja na utengenezaji wa majiko rafiki katika jitihada za kupambana na mabadiliko ya tabianchi.

Akinamama walioanzisha miradi hiyo – miradi na mikoa watokayo vikiwa kwenye mabano –ni Regina Kamuli (Mkuranga, Pwani – Majiko Banifu), Abiah Magembe (Kisarawe, Pwani – Usindikaji wa Muhogo na Mtama), Magdalena Bukuku (Kinondoni, Dar es Salaam – Kilimo cha Uyoga), Mariam Bigambo (Dakawa, Morogoro – Ufugaji wa Nyuki), na Esther Muffui (Morogoro – Ukaushaji wa Mboga na Matunda).

Wengine ni Farida Makame (Kilimanjaro – Majiko ya Umeme-Jua), Leocadia Vedastus (Ukerewe, Mwanza – Kilimo na Usindikaji wa Viazi Lishe), Monica Kagya (Kisarawe, Pwani – Ufugaji wa Nyuki), Dkt. Sophia Mlote (Kinyerezi, Dar es Salaam – Kilimo Hai cha Nyanya na Mbogamboga), na Evelyn Kahembe (Uvinza, Kigoma – Kilimo cha Matunda).

Mradi huu wa Green Voices ambao mwaka huu uko katika awamu ya pili, ulizinduliwa Julai mwaka 2016 na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan.

Katika awamu ya pili kinamama hawa wameendelea kuboresha kilimo cha mazao yao kinachozingatia uhifadhi wa mazingira na mabadiliko ya tabia nchi katika mikoa sita nchini.

"Pamoja na kilimo, Mradi wa Green Voices umaeandaa mafunz mbalimbali ya kuongeza ujuzi katika kilimo (climate smart agricultura) pamoja na mafunzo ya jinsi ya kuandaa mazao au bidhaa wanazozalisha kupitia kilimo," alisema Mratibu wa Green Voices nchini Tanzania Secelela Balisidya.

Katika kutekekelza hilo, Green Voices kupitia mfadhili wake, Women for Africa Foundation, walishiriki katika mafunzo mbalimbali ya Mbinu bora za kuweka nembo na kufungasha bidhaa za vyakula, Viwango vya Ubora, na Kanuni za uchakataji wa vyakula.

Mafunzo hayo ambayo yalifanyika Julai 16 -22, 2017 yalizinduliwa na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), Selemani Jaffo, ambaye aliahidi kuwapa ushirikiano akina mama hao.

 

Utengenezaji bidhaa na ufungashaji

Kwa siku sita baada ya kuzinduliwa kwa mafunzo, akinamama hao walijifunza kuhusu Mchango wa kilimo katika mabadiliko ya tabianchi, Jinsi ya kuweka mazingira bora ya umwagiliaji, Mikakati ya biashara katika ujasiriamali wa kilimo, Utafutaji wa rasilimali na mkakati wa kuongeza mtaji, Ukuzaji wa mtaji kupitia Vicoba, na Mbinu za uongozi.

Akinamama hao walipata fursa ya kutembelea Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Shirika la Maendeleo ya Viwanda Vidogo (SIDO) ambapo ilikutana na wajasiriamali walio katika hatua za juu za kufungasha na kuuza bidhaa zao, ambapo walipata nafasi ya kubadilishana nao mawazo ili kuongeza ujuzi wao.

Katika mafunzo hayo, Linus Gedi ambaye ni mtaalam wa ubora wa chakula na viwango kabla ya kuvipeleka sokoni, aliwaeleza washiriki kwamba ni muhimu kufungasha na kuweka nembo kwani inasaidia kuhifadhi bidhaa na inarahisisha  mteja kutambua hiyo ni bidhaa ya aina gani, imetengenezwa wapi na ina mchanganyiko gani.

Akinamama wanaotekeleza mradi wa Green Voices walipotembelea Ofisi za SIDO jijini Dar es Salaam.


"Ni muhimu sana kuhakikisha chakula hakisababishi maradhi, lakini pia kinafikia malengo ya walaji, hii huepusha sumu kwenye chakula, mchanganyiko usiofaa, upotevu wa chakula, kupoteza bidhaa na kuepukana na masuala ya kisheria," alisema Linus.

Alisema uzalishaji wa chakula unatakiwa kuzingatia mbinu bora za uzalishaji na pamoja na usafi.

Aidha, aliwataka kuzingatia ubora, usafi na viwango vya chakula wanachozalisha ili kifikia malengo ya walaji.

Kwa upande wake, Richard Jackson akielezea umhimu wa kunadi bidhaa, alisema ni lazima kuwa na mikakati imara ya masoko ili kuhakikisha mjasiriamali anapata faida.

Alisema ni vizuri kujua wateja maalum na wateja wa ujumla na nini hasa wanahitaji ikiwa ni pamoja na namna ya kuwafikia.

"Ni lazima kujua kati ya wanaohitaji bidhaa zako, ni nani ambao siyo wateja wako walengwa na kwa nini wateja wanunue bidhaa zako na siyo kwa washindani wako? Lazima ujue tabia zao na ukubwa wa soko lako," alisema Jackson.

Aidha, alisema ni muhimu kuwajua wateja wako ili kuelewa mahitaji yao na kwa nini wananunua bidhaa wanazonunua pamoja na kutambua mambo yanayowaudhi ili usiwakwaze.

Kwa upande wa uchangishaji fedha na kutafuta mitaji kwa biashara na kilimo, Rais wa VICOBA Endelevu Tanzania, Devota Likokola, alieleza jinsi mfumo wa VICOBA Endelevu unavyoweza kuwasaidia kinamama wa Green Voices kupata mitaji ya kuendeleza miradi yao.

 

--
Brother Danny Blog (Kisima cha Hekima na Busara)
Cell: +255 - 715 - 070 109
Whatsapp: +255 - 656 - 331 974

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment