Tuesday, 22 September 2015

Re: [wanabidii] Upatu, Deci, Babu Loliondo na sasa Edward Lowassa!

pole zake, R.I.P



On Tuesday, September 22, 2015 6:58 AM, fadhil fadhil <fadhil.fadhil96@gmail.com> wrote:


Innaillah wainnaillah rajuun. Kiwasila ikiwa ni kweli imefikia hatua hiyo ya kutokwa na haja ktk hadhara huo ni mtihani tena mkubwa. Yarrabi tunusuru waja wako na mrehemu huyu mzee kwa kumpa siha njema.
On Sep 22, 2015 12:41 AM, "Jovias Mwesiga" <ngonzy@gmail.com> wrote:
Huu utumwa wa mzungu ndo mwenye kuwaza sahihi mtoa Mada umenitoa hamu ya kusoma ulichotaka kuandika.
Utumwa wa fikra ni kitu kibaya basi katuletee wazungu watusaidie kutupa rais .
On Sep 21, 2015 9:57 AM, "fadhil fadhil" <fadhil.fadhil96@gmail.com> wrote:
Kiwasila
Wanakuelewa ila njaa wameitoa tumboni na kuipeleka kichwani wameharibu akiri
tukutane october 25
On Sep 21, 2015 1:35 PM, "'Hildegarda Kiwasila' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

Wampumzishe tu Lowasa. Kama ningekuwa nduguye-ningeomba UKAWA na Chadema wampumzishe alinde afya yake. Wanampa shinikizo la mwili  na akili wakati ni mgonjwa. Haya sasa Video zimezagaa mitandaoni jinsi mgombea alivyopata haja jukwaani akakimbizwa toilet kubadilishwa nguo. Mkewe yupo wapi asitetee huyu baba akapumzika. Stress wampayo ni kubwa wao mradi mkono uende tumboni-wachukue nchi. WaTZ ni nduma kuwili sisi. Si unaona wananchi wanavyouza majumba kariakoo, magomeni na maeneo mengi kwa mabilioni, kuvamia mabwawa ya kinyesi na maeneo hatarishi na wanatesa familia hasa watoto. Kutwa vijiweni na kutupa malundo ya uchafu katika mitaro ya wazi na kuingiza ndani ya mifereji waliyoiba mifuniko. Maji machafu ya kinyesi yanatoka majumbani kwao na kuzalisha mainzi na kipindupindu kinazidi kupamba moto. Tunalaumu serikali kwa uchafu huo tutupao mchana na usiku, kwa kukataza biashara ya vyakula maeneo machafu na katika hali ya uchafu. Tunakufa sisi na jamaa zetu
 lakini hatubadiliki tunalaumu third part kwa kipindupindu. huyo Sumaye hajitambui alisema nini huko nyuma na sasa anasema nini.Bila ya shaka wamempora mashamba aliyojilimbikizia alipokuwa kiongozi sasa hasira zake anaziweka kumuunga mkono yule aliyemshutumu zamani mradi tu aipinge serikali ya CCM. Inakuwa kama ile moja niliyoiona 1974 kijiji cha Mhenda Kilosa-mume alimpiga mke kisha akamvua nguo na kumpanua miguu pande mbili kumdhalilisha. Tuliokuwepo tulishangaa na kusikitisha sana lakini wakati ule mambo ya haki za wanawake, jinsia na deski maalum hayakuwepo. Mila na ujamaa ulishika hatamu. Cha kushangaza-kesho yake tuliwaona wakiwa wameongozana kama mume na mke baada ya kumfedhehesha vile mpaka watu kumuona utupu wake mke. Leo katika siasa ndio hii. Ulimtukana au kumkashifu ila ili uishi (survival) unamkubatia. Ni kama wafanyavyo ISIS na Al gaeda-Choma makanisa, kata vichwa wakistru na wasiokuunga mkono kisha unapokuwa umezidiwa nawe nyoa madevu,
 vibadili mavazi-kimbilia Itali na Roma kwa Papa, Greece, Australia, Hungary, Ujerumani for survival!!-Huko kuna bendera na katiba zenye misalaba. Lakini wanasema- We want goodlife, education, peace!!-Survival!! Hapa ni survival tu Ukawa iwe na liwe. jamaa wanamtesa. Muoneenu huruma akina Mollel huyo EDO.
--------------------------------------------
On Mon, 21/9/15, 'Mpambo R.' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

 Subject: Re: [wanabidii] Upatu, Deci, Babu Loliondo na sasa Edward Lowassa!
 To: "wanabidii@googlegroups com" <wanabidii@googlegroups.com>, "wanabidii@googlegroups com" <wanabidii@googlegroups.com>
 Date: Monday, 21 September, 2015, 12:34



 Sent
 from Yahoo Mail on Android  From:"'mpombe
 mtalika' via Wanabidii"
 <wanabidii@googlegroups.com>
 Date:Mon, Sep 21, 2015 at 12:30
 Subject:[wanabidii] Upatu, Deci, Babu
 Loliondo na sasa Edward Lowassa!



 Upatu, Deci, Babu
 Loliondo na sasa Edward Lowassa!


 Johnson
 Mbwambo

   

 Kwa nini nisiamini
 tuwavivu wa kufikiri?


 NIANZE kwa
 kuomba radhi wasomaji wangu kwamba katika sehemu
 ya mwisho ya makala yangu ya toleo lililopita nilifanya kosa
 la kiufundi kwa
 kukitaja chama cha Zitto Kabwe kuwa ni ADC Wazalendo.
 Nilichomaanisha ni ACT
 Wazalendo. Nakiomba pia radhi chama hicho kwa kosa
 hilo.


 Mengine yote
 niliyozungumza kuhusu chama hicho kipya kwamba
 kama hakitatetereka kimwelekeo miaka si mingi kitakuwa chama
 mbadala wa Chadema
 katika siasa za Tanzania, yanabaki kama yalivyo.


 Hayo pembeni,
 naomba leo nirejee makala niliyopata kuandika
 huko nyuma kuhusu utafiti uliowahi kufanywa ulioonyesha ya
 kuwa Tanzania ni
 miongoni mwa nchi duniani ambazo watu wake wana bongo zenye
 uwezo mdogo wa
 kufikiri (IQ).


 Nakumbuka
 makala ile iliibua mjadala mkubwa mitandaoni; huku
 baadhi wakinitumia sms za matusi na kejeli kana kwamba mimi
 ndiye niliyefanya
 utafiti huo. Nilichokieleza wakati huo, na ninachotaka
 kukirudia leo ni kwamba,
 kwa namna Watanzania tunavyoenenda, yawezekana Wazungu
 waliofanya tafiti hizo
 hawakuwa mbali sana na ukweli!


 Hebu tafakari
 yafuatayo: Miezi miwili na ushee iliyopita
 Edward Lowassa aliulizwa na wahariri wa magazeti iwapo
 ataihama CCM kama
 haitamchagua kugombea urais mwaka huu. Jibu lake lilikuwa
 kwamba hatahama CCM
 kamwe kwa sababu ilimlea, na kwamba huyo ambaye hamtaki
 ndani ya CCM ndiye
 akihame chama hicho!


 Hata hivyo,
 kabla hata mwezi haujakatika Lowassa akakihama
 chama hicho na kujiunga na chama cha Upinzani cha Chadema,
 na kikamteua
 kugombea urais, na sasa maelfu ya vijana wanamshabikia!
 Kimsingi, Lowassa
 aliongopa katika jibu lake lile na taswira aliyojijengea ni
 ya mtu asiyeaminika
 katika anayosema na ambaye ni kigeugeu.


 Ingekuwa ni
 Wazungu au ingekuwa sisi ni watu wenye kufikiri
 sawasawa, tusingemshabikia Lowassa kwa maelfu katika mbio
 zake za urais kwa
 sababu ni mtu mwongo, kigeugeu na asiyeaminika – mtu
 asiyeweza kusimamia maneno
 yake mwenyewe.


 Lakini kwa
 uwezo wetu mdogo wa kufikiri, baadhi yetu
 Watanzania 'tunamzawadia' mtu huyo kwa kumuunga mkono
 kwenye kampeni yake ya
 kuusaka urais kwa udi na uvumba!


 Uongo na
 ukigeugeu kama huo pengine ungevumilika kama nafasi
 yenyewe anayowania si urais. Lakini urais ni kazi yenye
 heshima, utukufu,
 uadilifu nk. Ni kazi ambayo haimfai mtu mwongo na
 asiyesimamia maneno yake
 mwenyewe.


 Lakini kwa
 hapa Tanzania hilo halionekani kuwa ni upungufu
 nyeti kwa mtu anayewania kuingia Ikulu. Vijana wetu
 hawajiulizi: Kama huyu
 alidiriki kutudanganya jana, kwa nini asiendelee
 kutudanganya hata leo au hata
 baada ya kuingia Ikulu. Tutamwini vipi katika hayo anayodai
 kuwa atatutendea
 akiingia Ikulu kama huko nyuma aliwahi kutudanganya kwa
 kushindwa kusimamia
 maneno yake mwenyewe?


 Kule Uingereza
 kuna waziri mmoja wa zamani (simkumbuki jina)
 alishinikizwa na umma kujiuzulu uwaziri kwa kutokuaminika.
 Waziri huyo alikuwa
 akiusifia mno mfumo wa elimu wa shule za umma za Uingereza
 uliokuwa ukikosolewa
 na wananchi, lakini baadaye ikagundulika kwamba licha ya
 kuusifia sana, wanawe
 walikuwa wakisoma kwenye shule binafsi (private school).
 Ilibidi ajiuzulu.


 Lakini hapa
 kwetu Tanzania hali ni tofauti kabisa. Mtu
 (Lowassa) anadanganya waziwazi na anaonyesha si mtu wa
 kusimamia maneno yake
 mwenyewe, lakini maelfu ya Watanzania wanamuona kuwa ndiye
 anayefaa kuwa rais
 wao! Bado wanaamini maneno yake kuwa atawaondolea umaskini!
 Kama huo sio uwezo
 mdogo wa kufikiri wa Watanzania, ni nini?


 Katika hilo,
 Lowassa anao 'wasanii' wengine wawili wa
 kisiasa wanaokamilisha ile listi ninayoweza kuiita The Three
 Musketeers –
 nawamaanisha Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Waziri
 Mkuu mstaafu,
 Frederick Sumaye.


 Nianze na
 Mbowe. Mbowe huyu ni miongoni mwa viongozi wa
 Chadema ambao walizunguka nchi nzima wakimtuhumu Lowassa
 kuwa ni fisadi mkubwa.
 Mara ya mwisho Mbowe kufanya hivyo ilikuwa wakati Lowassa
 akitafuta saini za
 kuungwa mkono ili CCM imteue kugombea urais. Mbowe akasema
 Lowassa ni fisadi na
 wananchi hawastahili kumchagua kuwa
 rais wao!


 Leo hii, Mbowe
 huyo huyo anapita mikoani akiwa na Lowassa
 akiwahamasisha
 Watanzania wamchague Lowassa kuwa rais
 mpya wa nchi. Tena
 anamkampenia bila soni wala kupepesa macho - anajitia
 hayakumbuki maneno yake
 hasi aliyoyahubiri huko nyuma dhidi ya Lowassa.


 Na Watanzania,
 kwa uwezo wetu mdogo wa kufikiri,
 tunamshangilia huyo Mbowe bila hata kujali kuwa ni mtu
 mwongo, laghai wa
 kisiasa asiyeweza kusimamia maneno yake mwenyewe
 anayoyatamka! Na wala
 hatujiulizi: Kama alitudanganya jana kuhusu Lowassa, kwa
 nini tusiamini kuwa
 hata leo anatudanganya pia kuhusu huyo huyo Lowassa?


 Hadithi ni
 hiyo hiyo kwa Frederick Sumaye. Miezi kadhaa
 iliyopita aliuambia umma wa Watanzania kwamba kama Lowassa
 (aliyemwita fisadi)
 atapitishwa na CCM kuwania urais, yeye Sumaye ataondoka CCM.
 Sasa, ni kweli
 aliondoka CCM lakini mbona sasa anampigia kampeni Lowassa;
 ilhali alimwita
 fisadi asiyestahili kupitishwa na CCM kugombea urais?


 Na sisi
 wananchi katika uzuzu wetu na IQ zetu ndogo
 tunampigia makofi Frederick
 Sumaye wakati akimnadi Lowassa; ilhali
 tunajua yeye
 Sumaye ni mtu aliyetuongopea kuhusu Lowassa. Badala ya
 kumkasirikia na kumzomea
 kwa ulaghai wake wa kisiasa, tunamshangilia kama vile ni
 shujaa eti tu kwa
 sababu kahama CCM!


 Jamani, si
 Sumaye huyo huyo ambaye alipokuwa waziri mkuu
 aliwaambia wafanyabiashara wa Moshi kama wanataka mambo yao
 yawanyookee wahamie
 CCM! Leo Sumaye kama atakwenda Moshi kumkampenia Lowassa,
 safari hii atawaambia
 nini tena wafanyabiashara wale wa Moshi? Atajipa ujasiri wa
 kuwaambia kwamba
 wakitaka mambo yao yawanyookee wahamie Chadema?! Na
 wanapaswa wamwamini kama
 alishawadanganya mwanzoni?


 Ndugu zangu,
 ninachojaribu kueleza hapa ni kwamba 'The Three
 Musketeers' – Lowassa, Mbowe na Sumaye ni watu waongo na
 wasioaminika katika
 wasemayo, na kwa mujibu wa Rais wa zamani wa Marekani,
 Dwight Eisenhower,
 hawastahili kuongoza hata genge la wahuni.


 Eisenhower
 alipata kutamka hivi: The supreme quality for
 leadership is unquestionably integrity. Without it, no real
 success is possible
 whether it is on a section gang, a football field, in an
 army or in an office
 (sifa kuu ya uongozi ni uadilifu, unyoofu na usema kweli
 usio na shaka. Bila
 hivyo hakuna mafanikio yoyote ya maana yanayoweza kupatikana
 iwe ni katika
 genge la wahuni, viwanja vya michezo, jeshini au
 ofisini.)


 Kwa mujibu wa
 Eisenhower, hata genge la wahuni linamhitaji
 kiongozi mkweli anayesimama katika maneno yake mwenyewe
 anayoyatamka! Sasa,
 kama hata genge la wahuni halimhitaji kiongozi mwenye
 udhaifu huo, sembuse
 Ikulu yetu? Ndo maana naamini uwezo wetu wa kufikiri una
 walakini.


 Lakini si
 hivyo tu. Lowassa na Sumaye tunawashangilia pia
 wakisema kwamba wataleta mabadiliko Tanzania. Ni kwa sababu
 ya uvivu wetu wa
 kufikiria tunasahau ya kuwa wote wawili walikuwa na nyadhifa
 za juu serikalini
 kwa zaidi ya miaka 20 ikiwa ni pamoja na kuwa mawaziri
 wakuu, na hakuna
 mabadiliko yoyote waliyoyapigania wakiwa madarakani.


 Katika miaka
 yote hiyo zaidi ya 20 ya utendaji kazi wao
 serikalini (walianza wakiwa vijana mpaka wakazeekea humo
 humo serikalini)
 hakuna mabadiliko yoyote waliyoyapigania na wakakwamishwa,
 lakini leo
 wameshazeeka na wameshaondoka serikalini baada ya
 kujitajirisha, na ndiyo
 wanaahidi kuwa wataleta mabadiliko, na sisi
 tunawaamini!


 Kama ni uozo
 wa CCM na serikali yake mbona nao kwa zaidi ya
 miaka 20 walikuwa sehemu ya uozo huo walipokuwa viongozi
 waandamizi serikalini?
 Kwa nini leo baada ya juhudi zao za kuutaka urais kugonga
 mwamba ndio
 wanakumbuka kwamba kuna mabadiliko yanahitajika kuletwa
 Tanzania? Walikuwa wapi
 miaka yote hiyo? Kwa nini hatuuoni ulaghai ndani ya ahadi
 zao hizo za kuleta
 mabadiliko nchini!?


 Kwa hakika,
 hili la Lowassa ndilo linalonitia shaka zaidi
 kuhusu viwango vya IQ zetu. Baadhi yetu tumejitahidi mno
 kuwaelemisha vijana wa
 nchi hii juu ya nakisi kubwa ya uadilifu ya Lowassa
 inayomfanya asistahili kuwa
 rais wetu, lakini vijana badala ya kuzipembua hoja hizo wao
 hukimbilia kwenye
 kutukana tu na kudai kuwa tumehongwa na CCM.


 Dk. Slaa, kwa
 mfano, amejaribu mno kuanika hadharani kila
 kitu (tena kwa data na ushahidi kibao) kuhusu tuhuma za
 ufisadi wa Lowassa
 ikiwa ni pamoja na kuidanganya Tume ya Maadili ya Viongozi
 kuhusu mali anazomiliki,
 lakini vijana wetu kwa IQ zao ndogo, hawana hata muda wa
 kupembua na kutafuta
 ukweli juu ya hoja za Slaa. Badala yake wanachokimbilia wao
 ni matusi na kudai
 eti kahongwa na CCM!


 Kwa miaka
 kadhaa sasa Lowassa ameandamwa na kashfa ya
 mkataba wa Richmond ambao unailazimisha Serikali kuilipa
 Dowans (kampuni hewa)
 kiasi sha Shilingi takriban bilioni 93 – fedha za
 walipakodi.


 Utetezi wake
 ni kwamba alijua kuwa huo ni mkataba wa
 kifisadi lakini aliutia saini eti kwa kulazimishwa na
 mamlaka za juu (bila
 shaka akimaanisha Rais Kikwete). Kama hivyo ni kweli, mbona
 hakukataa kuusaini,
 na kisha kujiuzulu nafasi yake ya uwaziri mkuu?




 Angeweza
 kumwambia Rais hivi: "Mheshimiwa Rais, huu ni
 mkataba wa kifisadi utakaowaumiza Watanzania, na kama
 unanilazimisha kuutia
 saini, mimi najiuzulu uwaziri mkuu, na hivyo teua waziri
 mkuu mwingine
 atakayetia saini mkataba huu wa kifisadi."


 Kama Lowassa
 angefanya hivyo, hadithi leo ingekuwa tofauti;
 maana angelionekana kama shujaa aliyekubali "kufa
 kidogo" kutetea maslahi ya
 Watanzania. Lakini sivyo alivyofanya; kwani aliusaini na
 akaendelea na uwaziri
 mkuu wake. Ni hivi karibuni tu baada ya kutemwa na CCM
 kugombea urais ndipo
 alipoanza kudai eti alilazimishwa na Kikwete kuusaini! Uongo
 mtupu!


 Ni Watanzania
 wenye IQ ndogo ndiyo wanaouamini utetezi wake
 huo, lakini wasio wavivu wa kufikiri wanajiuliza: mbona
 hakujiuzulu uwaziri
 mkuu wakati huo kama ni kweli alilazimishwa na Rais Kikwete
 kutia saini mkataba
 huo wa Richmond?


 Historia ya
 chama alichojiunga nacho cha Chadema inaonyesha
 kuwa mwasisi wake, Edwin Mtei alijiuzulu uwaziri wa fedha
 wakati Mwalimu
 Nyerere alipomshurutisha ayakatae mapendekezo ya Benki ya
 Dunia ya kurekebisha
 uchumi wa Tanzania.


 Mbona Lowassa
 hakufuata nyayo za Mtei kwa kujiuzulu uwaziri
 mkuu siku alipolazimishwa na Kikwete kusaini mkataba wa
 Richmond? Hivi kweli
 vijana wetu hawauoni ulaghai uliomo kwenye utetezi huo wa
 Lowassa kuhusu kashfa
 hiyo ya ufisadi ya Richmond?


 Kuna hili
 suala jingine analowadanganya maelfu ya vijana
 wanaomshabikia kwamba eti akiwa rais ataendesha
 'mchakamchaka' wa maendeleo
 nchini. Hivi hao vijana hawaoni (hata kwenye TV) kuwa
 Lowassa ana matatizo ya
 kiafya kiasi kwamba hawezi kuhutubia mkutano wa kampeni kwa
 muda mrefu, na hata
 kushika tu kipaza sauti kwake ni tatizo?


 Hivi mtu
 mwenye umri mkubwa na mwenye matatizo ya afya ya
 kiasi hicho anawezaje kuahidi 'mchakamchaka' wa
 maendeleo? Mbona huo
 'mchakamchaka' hatukuuona katika miaka zaidi ya 20 ya
 utumishi wake serikalini
 hasa alipokuwa kijana na mwenye afya nzuri? Mbona hata kule
 Monduli alikokuwa
 mbunge kwa miaka 20 hatujaona 'mchakamchaka' wa
 maendeleo alioufanya? Hivi hata
 hilo vijana wetu hawalioni?


 Sumaye naye ni
 hivyo hivyo. Anasimama majukwaani na
 kuzungumza lugha ya
 Chadema na ya Ukawa ya
 'kuwakomboa' vijana kiuchumi. Hivi
 hawa vijana wetu hawajui kwamba Sumaye anamiliki hekta
 40,000 za ardhi kule
 Mvomero alizozitwaa akiwa waziri mkuu na mpaka leo
 hajaziendeleza; ilhali
 vijana wa Mvomera hawana mashamba?


 Kama kweli
 dhamira yake ni ya kweli, mbona haanzi kwa
 kutangaza kwamba anazitoa hizo hekta 40,000 za ardhi
 anazozimiliki ili
 zigawanywe kwa vijana wasio na ajira nchini na wanaotafuta
 maeneo ya kulima?
 Angeanza na hilo, tungemuamini; maana angekuwa amekubali
 "kufa kidogo" kwa
 ajili ya vijana wa Tanzania! Kinyume cha hicho, anachofanya
 ni usanii mtupu, na
 ni wavivu tu wa kufikiri ndiyo wanaoweza kumwamini.


 Hivi taifa
 hili la kesho (tunaambiwa vijana ni taifa la
 kesho) litakuwa taifa la namna gani kama lina vijana wenye
 IQ ndogo kiasi hicho
 cha kutouona ulaghai wa watu kama hao? Yaani hatuna vijana
 ambao hawana uwezo
 wa kuchanganya akili za kuambiwa na akili zao wenyewe na
 kuung'amua ulaghai
 uliomo katika ugombea urais wa Lowassa?


 Kwa ufupi
 ndugu zangu, japo si jambo jema kulisema lakini ni
 lazima lisemwe. Jambo hilo ni kwamba sisi Watanzania ni
 wavivu wa kufikiri, na
 tunapenda kufuata mambo kwa pupa na kwa mkumbo bila
 kufikiri, na mwisho wake
 mara nyingi hauwi mwema kwetu.


 Kinachosikitisha na kukatisha tamaa ni
 kwamba hata wenzetu
 wengine wanapojaribu kuchokonoa bongo zetu na kutushawishi
 tufikirie kidogo
 kabla ya kuchukua maamuzi, tunawapuuza na kuwakejeli lakini
 mwishowe hatima
 inakuwa ni wao "kulizwa".


 Labda msomaji
 nikukumbushe mambo mawili au matatu hivi
 kuthibitisha hicho ninachokisema. La kwanza ni lile suala la
 moto wa Upatu (pyramid
 scheme) uliowaka Tanzania mwaka 1992. Mtakumbuka kuwa baadhi
 ya Watanzania
 wachache waliona mapema ulaghai ndani ya mpango huo na
 walijaribu kuwaelemisha
 wananchi kuwa watapoteza pesa zao.


 Nini
 kilitokea? Kilichotokea ni kwamba wananchi walikataa kupima
 hoja zilizotolewa, na badala yake wakamiminika kwa maelfu
 kuwekeza pesa za
 akiba zao za maisha katika Upatu ule. Na mwisho wa yote
 mpango huo uliporomoka
 kama ilivyobashiriwa, na maelfu ya Watanzania wakapoteza
 fedha zao hizo!


 Katika hali ya
 kawaida ya wananchi wenye IQ nzuri,
 usingelitaraji ulaghai kama huo ujitokeze tena baadaye na
 kushabikiwa tena na
 maelfu ya watu. Lakini ndivyo ilivyotokea tena hapa Tanzania
 kwani mwaka 2012
 'upatu mpya' kwa jina la DECI uliibuka, na Watanzania
 kwa maelfu wakawekeza
 tena fedha zao licha ya kuonywa tena na wachambuzi walioona
 ulaghai wa mpango
 huo sawa na ule wa upatu wa mwanzo.


 Nini
 kilitokea? Maelfu ya Watanzania 'wakalizwa' tena kwa
 kuibiwa pesa zao chini ya upatu huo mpya kwa jina la DECI.
 Yaani Watanzania wale
 wale 'waliolizwa' kwa kupoteza fedha zao kwenye Upatu
 'wakalizwa' tena fedha
 zao kwenye DECI. Ni kwa nini tusihoji kwanza mambo, na
 badala yake tukimbilie
 kwa maelfu kwa kufuata mkumbo tu? Kama sababu si IQ zetu
 kuwa ndogo, ni nini?


 Mfano wa tatu
 ni suala lile la Kikombe cha Babu wa Loliondo
 mwaka 2011. Binafsi nilijitahidi sana, kupitia safu hii,
 kuwatahadharisha
 Watanzania juu ya ulaghai uliokuwemo katika 'tiba' ya
 kikombe hicho cha Babu wa
 Loliondo aliyedai kaoteshwa na Mungu.


 Juhudi zangu
 hizo zilipokewa na matusi na kejeli kama
 ninayoyapokea hivi sasa ninapojaribu kuwatahadharisha
 Watanzania juu ya urais
 wa Edward Lowassa. Maelfu kwa maelfu ya Watanzania, wakiwemo
 viongozi, wakaenda
 Loliondo kufuata kikombe cha Babu.


 Nini kilitokea
 baadaye? Kilichotokea baadaye ni kwamba
 maelfu ya wagonjwa wa sukari na ukimwi walipoteza maisha yao
 kwa kuacha sindano
 za insulin na vidonge vya ARVs baada ya kunywa kikombe cha
 Babu. Baadaye,
 ikadhihirika kwamba kumbe Kikombe cha Babu kilikuwa ulaghai
 mtupu! Wale walionikejeli
 na kunitukana mpaka leo wanaona haya nikikutana nao!


 Kwa ufupi,
 kama Watanzania wasingekuwa wavivu wa kufikiri
 wangelizichambua hoja zilizotolewa na Watanzania wenzao
 dhidi ya pyramid
 schemes za Upatu na DECI na pia tiba ya kikombe cha Babu wa
 Loliondo. Na kama
 wangefanya hivyo, wangeliona ulaghai uliomo ndani yake na
 "wasingelizwa" kwa
 maelfu kama "walivyolizwa".


 Sasa, nakiona
 kile kilichotokea kwenye Upatu, DECI na
 Kikombe cha Babu wa Loliondo – yaani kufuata mambo kwa
 mkumbo bila kutafakari
 kikitokea pia katika suala hili la mbio za urais za Edward
 Lowassa. Maelfu
 wanamfuata bila kujihoji na kujitambua.


 Yaani, pamoja
 na juhudi zote za kina Slaa na kina sisi
 (ambao wala si wana CCM) kujaribu kuwatahadharisha
 Watanzania kuhusu hatari ya
 urais wa Lowassa, bado maelfu ya vijana wanamfuata kwa
 maelfu ki- mkumbo bila
 kwanza kufikiri, kutafiti au kuusaka ukweli wa hoja
 zinazotolewa dhidi yake.


 Kuanzia Upatu,
 DECI, kikombe cha Babu wa Loliondo, na sasa
 Lowassa, Watanzania tunadhihirisha kwamba sisi ni watu wa
 kufanya mambo kwa
 kufuata mkumbo, na hatima ya watu wanaofuata mkumbo bila
 kwanza kutafakari ni
 "kulizwa" . Je, hiyo inathibitisha kwamba IQ zetu
 Watanzania ni ndogo kama
 tafiti za Wazungu zinavyodai?


 Rais mstaafu
 Benjamin Mkapa aliwahi kutamka maneno
 yaliyowaudhi Watanzania wengi ambayo leo nikiyatafakari
 naona yalikuwa na
 ukweli wa kiasi fulani ndani yake. Alisema sisi Watanzania
 ni wavivu wa
 kufikiri. Rais Kikwete alikuja baadaye kuiboresha kauli hiyo
 ya Mkapa kwa
 kutupa changamoto hii: "Akili za kuambiwa changanya na
 zako za kuzaliwa ndipo
 ufanye maamuzi."


 Mimi
 nimechanganya akili za kuambiwa na akili zangu
 mwenyewe, na ndiyo maana nilikataa na nitaendelea kukataa
 kuifuata sauti ya
 mlio wa mpiga filimbi wa Hamelin (Lowassa), kwa sababu sina
 hakika na
 anakotupeleka Watanzania.


 Kwa akili za
 kuambiwa na nikichanganya na za kwangu za
 kuzaliwa, nauona wazi ulaghai na uongo unaoenezwa na hawa
 Three Musketeers –
 Mbowe, Sumaye na Lowassa. Ndugu zangu, tusiifanyie Ikulu
 yetu upatu – ni mahali
 patakatifu! Tafakari.


 Chanzo Raia
 Mwema





 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya
 kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and
 Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


0 comments:

Post a Comment