Jamani sasa kama wamehongwa asiseme
On Sep 3, 2015 8:17 AM, "boniface magessa" <magessabm@gmail.com> wrote:
-- --Mtu kawaongelea mpk maaskofu eti wamehongwa...kajichafua sana. yaani ni zaidi ya kujipizia!
magessa, bm.
0767 940 494
0716 150 176
Dsm.
From: emmbaga
Sent: 03/09/2015 08:14
To: wanabidii@googlegroups.com
Subject: Re: [wanabidii] DR SLAA KAJICHAFUAMama Nkya wewe ndio unazidi kujichafua. yaani mtu aseme ukweli wake ndio anajichafua. kisa anaawaumbua!!... time will tellernest
Sent from Samsung mobile
Neatness Msemo <nmuzeh@gmail.com> wrote:
Unajua mtu akikosa anasema lolote sasa sungura alipokosa alisema sizitaki mbichi hizi lakini hata kama lowasa ni mchafu hakuna msafi lakini Mungu anaweza kumbadiliaha Lowasa awe msafi watakavyo sema watanzania wamechoka kwani CCM wanataka watawale milele
On Sep 3, 2015 6:10 AM, "fadhil fadhil" <fadhil.fadhil96@gmail.com> wrote:
Mama nkya kazi ya moyo ni kusukuma damu kupenda ni kiherere chako. Tunajuaa una mahaba mgombea wako lkn wakati mwingine kupenda sana ni ugonjwa.
On Sep 3, 2015 2:18 AM, "'ananilea nkya' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com> wrote:
Dk SLAA KAJICHAFUA
Na Ananilea Nkya
Nimeisikiliza hotuba Dr Slaa kwenye youtube--nimeungana na wananchi ambao wamesema Dr Slaa kwa kujua au kwa kutokujua amekubali kutumika kuyumbisha maelfu ya wananchi wanaotaka mabadiliko nchini na kwa hiyo amejichafua mbele ya Watanzania.
Dr Slaa anapaswa kujua kwamba mabadiliko ni lazima kwa sasa na hayazuiliki tena maana nchi ilipofikia sasa Septemba 2015, wenye ari kubwa ya kuleta mabadiliko ni wananchi wenyewe kupitia sanduku la kura hapo tarehe 25 Oktoba.
Pengine Dr Slaa hakujua kuwa wananchi wanaotaka mabadiliko ya uongozi nchini walikuwa wameshamsahau maana tangu alipoacha kuonekana hadharani hasa wakati wa kumtambulisha Edward Lowassa kama mgombea Urais wa UKAWA--muungano wa vyama vinavyopigania kuingia madarakani vikiwa na ajenda ya kuandika Katiba Mpya inayotokana na maoni ya wananchi, wengi walishajua kuwa Dr Slaa hayupo tena upande wa wananchi.
Alichokisema Dr Slaa kwenye hotuba yake ya kile alichokiita 'kuachana na siasa za vyama' ni kajichafua yeye mwenyewe na kuharibu heshima aliyojijengea kwenye jamii.
Kwa mfano Dr Slaa alisema eti aliweka msingi kwamba angemkubali Edward Lowassa kugombea Urais iwapo angeondoka CCM na mtaji wa wabunge 50 kuhamia UKAWA ili wagombee ubunge kwa tiketi ya CHADEMA, CUF, NCCR Mageuzi na NLD- vyama vinavyounda UKAWA.
Hivi Dr Slaa aliona vijana wanaochakarika kwenye vyama vinavyounda UKAWA wao hawataki kuwa wabunge? Hawastahili nao kufaidi mshahara wa shilingi milioni 10 kila mwezi na kiinua mgongo cha zaidi ya shilingi milioni 200 baada ya miaka mitano ?
Hebu fikiria wabunge wa CCM ambao wengi wamekuwa bungeni miaka kumi, ishirini wengine miaka thelathini na zaidi. Ni matajiri kiasi gani leo hii? Hivi watu wa aina hiyo kweli wanaweza kuondoka kwenye chama chao kwa wingi kiasi hicho na kuamua sasa kupigania kuondoa mfumo unaowatajirisha wao ili wananchi wengi masikini nao watajirike?
Watakuwa na shida gani wakati kwenye chama chao hata kama mtu umekosa kuteuliwa kugombea ubunge malofa wakishaichagua CCM serikali ya CCM inawagawia kazi za ulaji watu waliokosa ubunge? Kwani wewe hujamsikia Mgombea Urais wa CCM Dr Magufuli akiwatangazia wale walioanguka kwenye kuwa za maoni ubunge CCM kwamba wasijali anazo kazi tele za kuwapa akichaguliwa Rais?
Kwa mtazamo wangu--walioamua kuondoka CCM na kujiunga na UKAWA kama kweli dhamira yao ni kushirikina na UKAWA kupigania kuingiza serikali ya UKAWA madarakani ili kuandika Katiba Mpya ya wananchi--watu hao wanastahili pongezi maana watakuwa wamefanya maamuzi magumu na muhimu ya kuwezesha wananchi wengi kuondoka kwenye umaskini unaosababishwa na serikali ya CCM.
Hivi Dr Slaa kweli anadhani mabadiliko ya kuchagua serikali itakayoandika Katiba Mpya inayotokana na maoni ya wananchi yatatokea nchini kwa wabunge wengi wa CCM kuondoka CCM –kujiunga UKAWA--wabunge ambao waliizika Rasimu ya Katiba ya wananchi pale Dodoma 2014 huku wakiwa wanalipw akila mmoja shilingi laki tatu kila siku kwa takriban miezi mitatu?
Hivi Dr Slaa hajui kwamba wanaotaka mabadiliko ni mamilioni ya Watanzania wakiwepo wanachama wa CCM wanaoumizwa na umaskini ambao chimbuko lake ni mifumo iliyowekwa na serikali ya CCM--mifumo inayotajirisha watawala wachache huku mamilioni ya wananchi wakiwa mafukara?
Kwa mtazamo wangu, wananchi wengi wakitafakari hatua aliyochukua Dr Slaa na maneno aliyoyazungumza hadharani watabaini kuwa Dr Slaa amejidhihirisha kuwa ni mtu mbinafsi.
Zaidi watabaini kuwa Dr Slaa pengine aliingia kwenye upinzani akidhani siasa ni kama kazi nyingine. Kumbe siasa hasa kuwa kwenye chama cha upinzania ni kujitoa hata kama kuna kuumia kiasi gani –hadi lengo la ukombozi wa pili wa taifa hili--ukombozi wa kuondoa mifumo inayowafukarisha wananchi ing'olewe.
Kwa maoni yangu, kama Dr Slaa angekuwa ameingia kwenye siasa kupigania ukombozi wa wananchi--kamwe asingekubali kukaa pembeni sasa--tena baada ya yeye mwenyewe kukubali Lowassa aingie UKAWA mradi awe ni mtaji na si hasara. Kibaya zaidi asingekuwa upande wa watawala wanaofukarisha wananchi eti kwa sababu Lowassa alishindwa kuleta UKAWA mtaji wa watu wa kugombea ubunge.
Pengine Dr Slaa amekuwa na tafsiri finyu kuhusu mtaji wa siasa. Siamini kuwa vyama vinavyounda UKAWA vina uhaba wa watu wenye uwezo wa kuwa wabunge. Hivyo mtaji muhimu ambao Dr Slaa angeutaka kwa Lowassa ni wapiga kura. Angejiuliza je huyu Lowassa anakubalika kwa wapiga kura?
Jibu kama Lowassa anakubalika kwa wapiga kura au la Watanzania wenyewe wanalo jibu na hadanganyiki mtu hapo. Watanzania wanaomuona Lowassa anafaa kuongoza Tanzania mafuriko. Huyo mtaji wa wapiga kura ambao Lowassa ameongeza UKAWA ndicho kinachowasumbua watawala.
Tena Watanzania wanaomuunga mkono Lowassa hawajakosea maana hata Mwalimu Nyerere alitamka hadharani mwaka 1995 kwamba Lowassa ni mtu mwenye dhamira na uwezo wa kuiongoza Tanzania.
Isitoshe wananchi wanamuona Lowassa kuwa ni mtaji muhimu maana kwa kuhama CCM amehamasisha nguvu kubwa ya umma katika kuleta mabadiliko yenye manufaa kwa wananchi.
Dr Slaa alisema eti kwenye familia yake wanakula mhogo na maharage. Hivi familia inayokula mhogo na maharage (yaani kwa sababu ya umaskini wa kikwelikweli) inaweza kumruhusu baba ambaye alijibainisha kuwa ni kamanda wa mapambano ya wanyonge awageuke mamilioni ya Watanzania ambao hata mhogo na maharage hawapati na hivyo siku nyingine hulazimika kulala njaa?
Kama Lowassa angeingia CHADEMA na asigombee Urais badala yake CHADEMA na UKAWA wangemteua Dr Slaa kugombea Urais, je Dr Slaa angetamka maneno aliyoyatamka? Hata kama Dr Slaa angekuwa na uadilifu kama malaika angetoa kauli zinazofanana na zile wanazotoa watalawa wa CCM dhidi ya mamilioni ya Watanzania wanaotaabika kwa umaskini?
Hivi Dr Slaa ameamua kuungana na serikali ya CCM kudanganya wananchi kwamba tatizo la umaskini unaosumbua mamilioni ya Watanzania chanzo chake siyo serikali ya CCM bali ni Lowassa na hivyo Lowassa akiingia madarakani uma ufisadi utaongezeka nchini?
Kimsingi Watanzania wa leo HATUDANGANYIKI. Zaidi sana Mungu wa wanyonge ni mnyofu sana hatawaacha Watanzania mwaka huu—mwaka wa mabadiliko.
Ninawatia moyo Watanzania wote mkiwepo wana CCM mnaoumizwa na hali ya umaskini miongoni mwa wananchi wengi nchini kwetu msikate tamaa wala kuogopa kama akitokea kiongozi mwingine wa UKAWA akageuka wananchi kama Dr Slaa na Prof Lipumba kabla ya uchaguzi mkuu tarehe 25 Oktoba 2015 ninyi songeni mbele, mabadiliko yanawezekana.
Kimsingi ni kila mtu kutambua kuwa kuna njama nyingi zinazofanyika kwa lengo la kuvuruga wananchi ili waogope au wapuuze kufanya mabadiliko.
Sote tuwe macho, hakuna kuchoka, hakuna kuogopa .Mabadiliko ni lazima hayazuiliki. Mungu ibariki Tanzania.
Narudia kusema mimi sina chama chochote cha siasa ninachofungamana nacho. Ninachopigania ni maslahi ya mamilioni ya Watanzania masikini (malofa) kwa utawala mbovu wa serikali ya CCM.
Ninaruhusu mwenye kutaka kuchapisha makala hii afanye hivyo maana historia itatuhukumu mmoja mmoja na kama kundi linalopigania mabadiliko Tanzania.
Kwa maswali niandikie: ananilea_nkya@yahoo.com
Ananilea Nkya
E-mail:ananilea_nkya@yahoo.com
--------------------------------------------
On Wed, 9/2/15, 'mpombe mtalika' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:
Subject: [wanabidii] Mtikisiko
To: "ELISA MUHINGO' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com>
Date: Wednesday, September 2, 2015, 2:29 PM
Mtikisiko
Waandishi Wetu
ALIYEKUWA Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema),
Dk. Wilbrod Slaa, amevunja ukimya kwa kueleza kile
kilichomsukuma
kujiuzulu wadhifa huo, sambamba na kujivua uanachama wa
chama hicho.
Katika kuvunja kwake ukimya huo, Dk. Slaa aliweka hadharani
namna
viongozi wenzake ndani ya Chadema, akiwamo mwenyekiti wao,
Freeman
Mbowe, Makamu Mwenyekiti Profesa Abdallah Safari
walivyoyumbisha
kusimamia misingi ya namna ya kumpokea Waziri Mkuu
aliyejiuzulu kwa
kashfa ya kampuni tata ya kufua umeme ya Richmond, Edward
Lowassa.
Mbali na hayo, mengine aliyoweka wazi ni namna Lowassa
alivyoratibu
mipango yake ya kuhamia Chadema akiwa bado CCM, akifanya
hivyo kwa
kumtumia Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat
Gwajima.
Kwa mujibu wa Dk. Slaa, Gwajima ndiye "mshenga" wa
Lowassa kwa Chadema
na kati ya hoja alizozitumia kumshawishi Dk. Slaa kumkubali
Lowassa ni
kwamba, mwanasiasa huyo aliyeokosa urais CCM, anaungwa mkono
na Kanisa
la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) na ndani ya Kanisa
Katoliki,
maaskofu 30 kati ya 34, wamehongwa na wamemkubali
Lowassa.
Ilivyokuwa na Kama ambavyo wahenga wanasema kimya kingi
kina mshindo,
ndivyo ilivyokuwa kwa kimya cha Dk. Slaa. Mshindo wa kimya
hicho ulianza
kujidhihirisha mapema, katika Hoteli ya Serena, jijini Dar
es Salaam,
alikofanyia mkutano huo, ambapo mpaka saa saba mchana idadi
kubwa ya
waandishi wa habari walikuwa tayari wamefika katika eneo
hilo, kushiria
kuwa tukio hilo litakuwa na ukubwa wa aina yake.
Dk. Slaa aliyewasili ukumbi wa mkutano saa 8:05 mchana,
jana, Jumanne,
aliweka bayana uamuzi wake wa kuzungumza na waandishi wa
habari,
akisema, kwa kuwa ikifika mahali ukweli unatakiwa kusemwa ni
lazima
usemwe, kutokana na upotoshwaji uliofanywa na watu
mbalimbali wakiwamo
baadhi ya viongozi wakuu wa Chadema, kwamba alikuwa
amepumzishwa
(likizo) na viongozi wa chama hicho.
"Nataka nianze na kusema mimi sikuwa likizo, sikupewa na
mtu yeyote,
niliamua kuachana na siasa Julai 18, 2015 usiku saa tatu,
baada ya kuona
yanayofanyika ndani ya chama changu sikubaliani nayo,"
alisema Dk.
Slaa.
Alisema alishiriki katika majadiliano ya kumakribisha
Lowassa ndani ya
Chadema lakini kwa kuweka misingi ambayo chama kilitakiwa
kwanza
kuizingatia kabla ya kufikia uamuzi wa kumkaribisha, baada
ya kukatwa
katika mbio za kuwania urais kupitia Chama Cha Mapinduzi
(CCM).
"Baada ya tarehe 11 Julai, Lowassa alipokatwa mshenga wa
Lowassa,
Askofu Josephat Gwajima alinipigia simu kuniambia sasa kule
Dodoma mambo
yameisha, nikamwambia awasiliane na Mwenyekiti (Mbowe),
tukawasiliana
na naye baadaye tukakutana naye, nikawaeleza msimamo wangu
kwamba ni
lazima kusikia mtu ana nini, tukakutana na vijana wake ili
tujue ana
nini," alisema na kuongeza; "Nikasema msingi wa kwanza
ni lazima
atangaze kutoka CCM, akijiondoa aseme anakwenda chama gani,
na atumie
nafasi hiyo kujisafisha na tuhuma zote zinazomkabili katika
nchi hii,
kwa sababu Chadema kimeaminika, ukipokea mtu ambaye
hajajisafisha
unakuwa unapokea na uchafu wake. Hilo halikufanyika mpaka
alipopokewa
Julai 28. Siwezi kumsafisha mtu ninayekaa naye meza
moja."
Dk. Slaa anasema msingi wa pili aliokipa chama chake kabla
ya kumpokea
ni kupima kama Lowassa ni rasilimali (asset) au mzigo
(liability) kwa
chama hicho, kwa kuwa walikuwa wameambiwa kwamba angekuja na
viongozi
wengi kutoka CCM. "Nikawauliza anakuja na nani, yeye peke
yake au na
wafuasi, na kama wafuasi ni wa aina gani, vijana wa boda
boda
wanaoshabikia tu au ni viongozi serious (makini). Nikaambiwa
anakuja na
wabunge 50, wenyeviti wa CCM mikoa 22 na wenyeviti wa wilaya
88,
nikakiri hili litakuwa tetemeko, nikahitaji kupewa majina,
Katibu Mkuu
makini hawezi kupokea idadi tu, na tulikuwa tunakwenda
kwenye uchaguzi
wa kura za maoni, ilikuwa lazima nijue nani anagombea wapi,
vinginevyo
uta – destabilize (utayumbisha) chama," alisema na
kuongeza kwamba;
mpaka chama hicho kinampokea Lowassa hakuna hata moja kati
ya misingi
hiyo iliyotekelezwa.
Kuhusu ushiriki wake katika kikao cha kumpokea Lowassa,
alisema aliombwa
kuitisha kikao cha Kamati Kuu ya dharura, lakini akaeleza
msimamo wake
kwamba hajapata jibu la upembuzi kama Lowassa ni mtaji au
mzigo.
"Asubuhi ya Julai 27, Mwenyekiti alinipigia simu
kunieleza sijaridhika
akaomba tukutane asubuhi tuzungumze ili tusije
tukatofautiana na
Mwenyekiti, kwangu mimi tangu mwaka 2004 sijawahi
kutofautiana na
mwenyekiti, tulifika pale akiwepo Tundu Lissu, na mshenga
wake Gwajima,
tukabishana tangu saa 3 asubuhi mpaka saa 9 alasiri, wapo
hapa waseme
kweli, mimi sikukubaliana nao tangu mwanzo, nawaomba
viongozi wangu wawe
wanyoofu na wenye hofu ya Mungu," alisema.
Kwa mujibu wa Dk. Slaa, baadaye walitakiwa kwenda nyumbani
kwa Lowassa
lakini alikataa akisema hawezi kwenda nyumbani kwa mtu wa
CCM katika
mazingira ya u-Katibu Mkuu wa Chadema. Aliongeza kwamba
baada ya hapo,
iliundwa kamati ya watu wachache kumshawishi (Slaa), ambayo
ilikaa tangu
saa 9 mpaka saa 12 jioni lakini akawapa masharti yale
yale.
"Tuliporudi kwenye kikao taarifa ya kikao kile
haikutolewa. Nikaandika
barua ya kujiuzulu nikampa Makamu Mwenyekiti Profesa Safari
akaichana,
nikaandika nyingine nikampa Makamu Mwenyekiti Zanzibar,
akaniambia Dokta
usihangaike mambo haya yamepangwa," alisema.
Akizungumzia watu waliokuja Chadema, alisema wote wamekuja
wakiwa
makapi baada ya kuwa wameshindwa kwanza kwenye mchakato wa
awali wa CCM
(kura za maoni) na hata huko walikotoka si wasafi. "Watu
kama Sumaye
hawakuwa safi, mimi mwenyewe nilimwita fisadi bungeni,
alichukua Shamba
la Magereza Kibaigwa, na yeye mwenyewe alifikia hatua ya
kusema CCM
wakimteua Lowassa yeye atahama chama, sasa yuko naye, najua
dhambi
haihalalishiwi na dhambi nyingine, lakini maneno hayo
yalitamkwa na
nani, Watanzania walimwita Sumaye ziro," alisema.
Aliendelea kuwaponda wana CCM waliohamia kuwa ni kama makapi
ambao
hawataongeza thamani yoyote kwa chama hicho akiwataja Mgana
Msindai na
Matson Chizii kuwa ni sehemu ya makapi ambayo hayataongeza
thamani
yoyote kwa Chadema. "Kuna watu wanasema ondoa CCM kwanza
hata
ikiwezekana kuweka mkataba na shetani, mimi ni Padri
Mkatoliki, hata
kama nimestaafu, nikubali kuweka mkataba na shetani mradi tu
niondoe
CCM. Unaondoa CCM kwa program serious na watu makini au
unaondoa na watu
wale wale?" alihoja Dk. Slaa.
Chadema na tuhuma za ufisadi Mbali na kuhoji endapo
waliohamia Chadema
kutoka CCM wameongeza thamani yoyote kisiasa; Dk. Slaa
aliyesimama imara
akizungumza kwa saa 1.32 alisema; "Chadema iliaminika
miongoni mwa
Watanzania kwa kutoyumbishwa na kusimamia uadilifu. Sasa leo
Chadema
wanathubutu kusema etu usimtuhumu mtu? Upuuzi mtupu! Kama
tusingemtuhumu
[The entire original message is not included.]
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.
0 comments:
Post a Comment