Thursday, 3 September 2015

RE: [wanabidii] DR SLAA KAJICHAFUA

Jamani sasa kama wamehongwa asiseme

On Sep 3, 2015 8:17 AM, "boniface magessa" <magessabm@gmail.com> wrote:
Mtu kawaongelea mpk maaskofu eti wamehongwa...kajichafua sana. yaani ni zaidi ya kujipizia!

magessa, bm.
0767 940 494
0716 150 176
Dsm.

From: emmbaga
Sent: ‎03/‎09/‎2015 08:14
To: wanabidii@googlegroups.com
Subject: Re: [wanabidii] DR SLAA KAJICHAFUA

Mama Nkya wewe ndio unazidi kujichafua. yaani mtu aseme ukweli wake ndio anajichafua. kisa anaawaumbua!!... time will tell
ernest




Sent from Samsung mobile

Neatness Msemo <nmuzeh@gmail.com> wrote:

Unajua mtu akikosa anasema lolote sasa sungura alipokosa alisema sizitaki mbichi hizi lakini hata kama lowasa ni mchafu hakuna msafi lakini Mungu anaweza kumbadiliaha Lowasa awe msafi watakavyo sema watanzania wamechoka kwani CCM wanataka watawale milele

On Sep 3, 2015 6:10 AM, "fadhil fadhil" <fadhil.fadhil96@gmail.com> wrote:

Mama nkya kazi ya moyo ni kusukuma damu kupenda ni kiherere chako. Tunajuaa una mahaba mgombea wako lkn wakati mwingine kupenda sana ni ugonjwa.

On Sep 3, 2015 2:18 AM, "'ananilea nkya' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com> wrote:
Dk SLAA  KAJICHAFUA

Na Ananilea Nkya

Nimeisikiliza  hotuba Dr Slaa  kwenye youtube--nimeungana na wananchi ambao wamesema  Dr Slaa kwa kujua au kwa kutokujua amekubali  kutumika kuyumbisha maelfu ya wananchi wanaotaka  mabadiliko nchini na kwa hiyo amejichafua mbele ya Watanzania.

Dr Slaa anapaswa kujua kwamba mabadiliko ni lazima kwa sasa  na hayazuiliki tena maana  nchi ilipofikia  sasa  Septemba 2015,  wenye ari kubwa ya kuleta mabadiliko  ni wananchi wenyewe    kupitia sanduku la kura hapo tarehe 25 Oktoba.

Pengine Dr Slaa hakujua kuwa wananchi wanaotaka mabadiliko  ya uongozi nchini walikuwa wameshamsahau maana tangu alipoacha kuonekana hadharani  hasa wakati wa  kumtambulisha Edward Lowassa kama mgombea Urais wa UKAWA--muungano wa vyama vinavyopigania kuingia madarakani vikiwa na ajenda ya kuandika Katiba Mpya inayotokana na maoni ya wananchi, wengi walishajua kuwa  Dr Slaa  hayupo tena upande wa wananchi.

Alichokisema   Dr Slaa  kwenye hotuba yake  ya kile alichokiita 'kuachana na siasa za vyama' ni  kajichafua yeye mwenyewe na kuharibu heshima aliyojijengea  kwenye jamii.

Kwa mfano Dr Slaa alisema  eti aliweka msingi kwamba angemkubali Edward Lowassa kugombea  Urais iwapo angeondoka CCM  na mtaji wa  wabunge 50  kuhamia  UKAWA   ili wagombee ubunge  kwa tiketi ya CHADEMA, CUF, NCCR Mageuzi na NLD-  vyama vinavyounda   UKAWA.

Hivi Dr Slaa aliona vijana wanaochakarika kwenye vyama vinavyounda UKAWA  wao hawataki kuwa wabunge? Hawastahili nao  kufaidi  mshahara wa shilingi milioni 10 kila mwezi na kiinua mgongo cha zaidi ya shilingi milioni 200 baada ya miaka mitano ?

Hebu fikiria wabunge wa CCM ambao wengi wamekuwa bungeni miaka kumi, ishirini wengine  miaka thelathini na zaidi. Ni matajiri kiasi gani leo hii? Hivi watu  wa aina hiyo kweli wanaweza  kuondoka kwenye chama chao  kwa wingi kiasi hicho na kuamua  sasa kupigania  kuondoa mfumo unaowatajirisha wao ili  wananchi  wengi masikini nao watajirike?

Watakuwa na shida gani wakati kwenye chama chao hata kama mtu umekosa kuteuliwa kugombea ubunge malofa wakishaichagua CCM  serikali ya CCM  inawagawia kazi za ulaji watu waliokosa ubunge? Kwani wewe hujamsikia  Mgombea Urais wa CCM  Dr Magufuli akiwatangazia wale walioanguka kwenye kuwa za maoni  ubunge CCM  kwamba wasijali anazo kazi tele za kuwapa akichaguliwa Rais?

Kwa mtazamo wangu--walioamua kuondoka CCM na kujiunga na UKAWA  kama kweli dhamira yao  ni kushirikina na UKAWA kupigania kuingiza serikali ya UKAWA madarakani ili kuandika Katiba Mpya ya wananchi--watu hao wanastahili pongezi maana watakuwa wamefanya maamuzi magumu na muhimu ya kuwezesha wananchi wengi kuondoka kwenye umaskini unaosababishwa na serikali ya CCM.

Hivi Dr Slaa kweli anadhani mabadiliko ya  kuchagua  serikali  itakayoandika  Katiba Mpya inayotokana na maoni ya wananchi yatatokea nchini kwa wabunge wengi  wa CCM  kuondoka CCM –kujiunga   UKAWA--wabunge ambao waliizika Rasimu ya Katiba ya wananchi pale Dodoma 2014  huku wakiwa  wanalipw akila mmoja shilingi laki tatu kila siku kwa  takriban miezi mitatu?

Hivi Dr Slaa hajui kwamba wanaotaka mabadiliko ni mamilioni ya Watanzania  wakiwepo wanachama wa CCM wanaoumizwa na umaskini ambao chimbuko lake ni mifumo iliyowekwa na serikali ya CCM--mifumo  inayotajirisha watawala wachache huku mamilioni ya wananchi wakiwa mafukara?

Kwa mtazamo  wangu, wananchi wengi wakitafakari hatua aliyochukua Dr Slaa na maneno aliyoyazungumza hadharani watabaini kuwa  Dr Slaa amejidhihirisha kuwa ni  mtu  mbinafsi.
Zaidi watabaini kuwa Dr Slaa  pengine aliingia kwenye upinzani akidhani  siasa ni kama kazi nyingine. Kumbe  siasa  hasa kuwa kwenye chama cha upinzania  ni  kujitoa  hata kama kuna kuumia kiasi gani –hadi lengo  la ukombozi wa pili wa taifa hili--ukombozi wa kuondoa mifumo inayowafukarisha wananchi  ing'olewe.

Kwa maoni yangu, kama Dr Slaa angekuwa ameingia kwenye siasa kupigania ukombozi wa wananchi--kamwe asingekubali kukaa pembeni sasa--tena baada ya yeye mwenyewe kukubali Lowassa aingie UKAWA mradi awe ni mtaji na si hasara.   Kibaya zaidi asingekuwa upande wa watawala wanaofukarisha wananchi eti kwa sababu Lowassa  alishindwa kuleta UKAWA  mtaji  wa watu wa kugombea ubunge.

Pengine Dr Slaa amekuwa na tafsiri finyu kuhusu mtaji  wa siasa.  Siamini kuwa  vyama vinavyounda UKAWA  vina  uhaba wa  watu wenye uwezo wa kuwa wabunge. Hivyo  mtaji  muhimu  ambao Dr Slaa angeutaka kwa  Lowassa  ni  wapiga kura.  Angejiuliza je huyu Lowassa anakubalika kwa wapiga kura?

Jibu kama Lowassa  anakubalika kwa wapiga kura au la Watanzania wenyewe wanalo jibu na hadanganyiki mtu hapo.  Watanzania wanaomuona Lowassa  anafaa kuongoza Tanzania  mafuriko.  Huyo mtaji wa wapiga kura ambao  Lowassa  ameongeza UKAWA  ndicho kinachowasumbua watawala.

Tena Watanzania wanaomuunga mkono Lowassa  hawajakosea maana hata Mwalimu Nyerere  alitamka  hadharani mwaka 1995 kwamba Lowassa  ni mtu mwenye  dhamira  na uwezo  wa kuiongoza Tanzania.

Isitoshe  wananchi wanamuona Lowassa kuwa ni mtaji muhimu maana kwa kuhama CCM  amehamasisha nguvu kubwa ya umma  katika kuleta mabadiliko yenye manufaa kwa wananchi.

Dr Slaa alisema eti kwenye familia yake wanakula mhogo na maharage. Hivi familia  inayokula mhogo na maharage (yaani kwa sababu ya umaskini wa kikwelikweli) inaweza kumruhusu baba ambaye alijibainisha kuwa ni kamanda wa mapambano ya wanyonge awageuke mamilioni ya Watanzania ambao hata mhogo na maharage hawapati  na hivyo siku nyingine hulazimika kulala njaa?

Kama Lowassa angeingia CHADEMA na asigombee Urais badala yake  CHADEMA  na UKAWA wangemteua  Dr Slaa kugombea  Urais, je Dr Slaa angetamka maneno aliyoyatamka?  Hata kama Dr Slaa angekuwa na uadilifu kama malaika angetoa kauli zinazofanana na zile  wanazotoa  watalawa wa CCM dhidi ya   mamilioni ya Watanzania wanaotaabika kwa umaskini?

Hivi Dr Slaa ameamua kuungana na  serikali ya CCM kudanganya wananchi  kwamba tatizo la umaskini unaosumbua mamilioni ya  Watanzania  chanzo chake siyo serikali ya CCM bali  ni Lowassa na hivyo Lowassa akiingia madarakani uma ufisadi  utaongezeka nchini?

Kimsingi Watanzania wa leo HATUDANGANYIKI. Zaidi sana Mungu wa wanyonge ni mnyofu  sana  hatawaacha Watanzania   mwaka huu—mwaka wa mabadiliko.

Ninawatia moyo Watanzania wote mkiwepo wana CCM  mnaoumizwa  na hali  ya umaskini miongoni mwa  wananchi wengi nchini kwetu  msikate tamaa  wala kuogopa kama akitokea  kiongozi mwingine wa   UKAWA  akageuka wananchi kama   Dr Slaa na  Prof Lipumba kabla ya uchaguzi mkuu tarehe 25 Oktoba 2015 ninyi songeni mbele, mabadiliko yanawezekana.

Kimsingi ni  kila mtu kutambua kuwa kuna njama nyingi   zinazofanyika kwa lengo  la kuvuruga  wananchi  ili waogope au wapuuze  kufanya mabadiliko.

Sote tuwe macho, hakuna  kuchoka, hakuna kuogopa .Mabadiliko ni lazima hayazuiliki.   Mungu ibariki Tanzania.

Narudia kusema mimi sina chama chochote cha siasa ninachofungamana nacho. Ninachopigania  ni maslahi ya  mamilioni ya Watanzania masikini (malofa)  kwa utawala mbovu wa  serikali ya CCM.

Ninaruhusu mwenye kutaka kuchapisha makala hii  afanye hivyo maana historia itatuhukumu mmoja mmoja na kama kundi linalopigania mabadiliko Tanzania.

Kwa maswali  niandikie: ananilea_nkya@yahoo.com



Ananilea Nkya
 E-mail:ananilea_nkya@yahoo.com

--------------------------------------------
On Wed, 9/2/15, 'mpombe mtalika' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

 Subject: [wanabidii] Mtikisiko
 To: "ELISA MUHINGO' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com>
 Date: Wednesday, September 2, 2015, 2:29 PM

 Mtikisiko







                                        Waandishi Wetu



 ALIYEKUWA Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo
 (Chadema),
 Dk. Wilbrod Slaa, amevunja ukimya kwa kueleza kile
 kilichomsukuma
 kujiuzulu wadhifa huo, sambamba na kujivua uanachama wa
 chama hicho.
 Katika kuvunja kwake ukimya huo, Dk. Slaa aliweka hadharani
 namna
 viongozi wenzake ndani ya Chadema, akiwamo mwenyekiti wao,
 Freeman
 Mbowe, Makamu Mwenyekiti Profesa Abdallah Safari
 walivyoyumbisha
 kusimamia misingi ya namna ya kumpokea Waziri Mkuu
 aliyejiuzulu kwa
 kashfa ya kampuni tata ya kufua umeme ya Richmond, Edward
 Lowassa.



   Mbali na hayo, mengine aliyoweka wazi ni namna Lowassa
 alivyoratibu
 mipango yake ya kuhamia Chadema akiwa bado CCM, akifanya
 hivyo kwa
 kumtumia Askofu wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat
 Gwajima.



   Kwa mujibu wa Dk. Slaa, Gwajima ndiye "mshenga" wa
 Lowassa kwa Chadema
  na kati ya hoja alizozitumia kumshawishi Dk. Slaa kumkubali
 Lowassa ni
 kwamba, mwanasiasa huyo aliyeokosa urais CCM, anaungwa mkono
 na Kanisa
 la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) na ndani ya Kanisa
 Katoliki,
 maaskofu 30 kati ya 34, wamehongwa na wamemkubali
 Lowassa.



   Ilivyokuwa na Kama ambavyo wahenga wanasema kimya kingi
 kina mshindo,
 ndivyo ilivyokuwa kwa kimya cha Dk. Slaa. Mshindo wa kimya
 hicho ulianza
  kujidhihirisha mapema, katika Hoteli ya Serena, jijini Dar
 es Salaam,
 alikofanyia mkutano huo, ambapo mpaka saa saba mchana idadi
 kubwa ya
 waandishi wa habari walikuwa tayari wamefika katika eneo
 hilo, kushiria
 kuwa tukio hilo litakuwa na ukubwa wa aina yake.



 Dk. Slaa aliyewasili ukumbi wa mkutano saa 8:05 mchana,
 jana, Jumanne,
 aliweka bayana uamuzi wake wa kuzungumza na waandishi wa
 habari,
 akisema, kwa kuwa ikifika mahali ukweli unatakiwa kusemwa ni
 lazima
 usemwe, kutokana na upotoshwaji uliofanywa na watu
 mbalimbali wakiwamo
 baadhi ya viongozi wakuu wa Chadema, kwamba alikuwa
 amepumzishwa
 (likizo) na viongozi wa chama hicho.



   "Nataka nianze na kusema mimi sikuwa likizo, sikupewa na
 mtu yeyote,
 niliamua kuachana na siasa Julai 18, 2015 usiku saa tatu,
 baada ya kuona
  yanayofanyika ndani ya chama changu sikubaliani nayo,"
 alisema Dk.
 Slaa.



   Alisema alishiriki katika majadiliano ya kumakribisha
 Lowassa ndani ya
  Chadema lakini kwa kuweka misingi ambayo chama kilitakiwa
 kwanza
 kuizingatia kabla ya kufikia uamuzi wa kumkaribisha, baada
 ya kukatwa
 katika mbio za kuwania urais kupitia Chama Cha Mapinduzi
 (CCM).



   "Baada ya tarehe 11 Julai, Lowassa alipokatwa mshenga wa
 Lowassa,
 Askofu Josephat Gwajima alinipigia simu kuniambia sasa kule
 Dodoma mambo
  yameisha, nikamwambia awasiliane na Mwenyekiti (Mbowe),
 tukawasiliana
 na naye baadaye tukakutana naye, nikawaeleza msimamo wangu
 kwamba ni
 lazima kusikia mtu ana nini, tukakutana na vijana wake ili
 tujue ana
 nini," alisema na kuongeza; "Nikasema msingi wa kwanza
 ni lazima
 atangaze kutoka CCM, akijiondoa aseme anakwenda chama gani,
 na atumie
 nafasi hiyo kujisafisha na tuhuma zote zinazomkabili katika
 nchi hii,
 kwa sababu Chadema kimeaminika, ukipokea mtu ambaye
 hajajisafisha
 unakuwa unapokea na uchafu wake. Hilo halikufanyika mpaka
 alipopokewa
 Julai 28. Siwezi kumsafisha mtu ninayekaa naye meza
 moja."



   Dk. Slaa anasema msingi wa pili aliokipa chama chake kabla
 ya kumpokea
  ni kupima kama Lowassa ni rasilimali (asset) au mzigo
 (liability) kwa
 chama hicho, kwa kuwa walikuwa wameambiwa kwamba angekuja na
 viongozi
 wengi kutoka CCM. "Nikawauliza anakuja na nani, yeye peke
 yake au na
 wafuasi, na kama wafuasi ni wa aina gani, vijana wa boda
 boda
 wanaoshabikia tu au ni viongozi serious (makini). Nikaambiwa
 anakuja na
 wabunge 50, wenyeviti wa CCM mikoa 22 na wenyeviti wa wilaya
 88,
 nikakiri hili litakuwa tetemeko, nikahitaji kupewa majina,
 Katibu Mkuu
 makini hawezi kupokea idadi tu, na tulikuwa tunakwenda
 kwenye uchaguzi
 wa kura za maoni, ilikuwa lazima nijue nani anagombea wapi,
 vinginevyo
 uta – destabilize (utayumbisha) chama," alisema na
 kuongeza kwamba;
 mpaka chama hicho kinampokea Lowassa hakuna hata moja kati
 ya misingi
 hiyo iliyotekelezwa.



 Kuhusu ushiriki wake katika kikao cha kumpokea Lowassa,
 alisema aliombwa
  kuitisha kikao cha Kamati Kuu ya dharura, lakini akaeleza
 msimamo wake
 kwamba hajapata jibu la upembuzi kama Lowassa ni mtaji au
 mzigo.



   "Asubuhi ya Julai 27, Mwenyekiti alinipigia simu
 kunieleza sijaridhika
  akaomba tukutane asubuhi tuzungumze ili tusije
 tukatofautiana na
 Mwenyekiti, kwangu mimi tangu mwaka 2004 sijawahi
 kutofautiana na
 mwenyekiti, tulifika pale akiwepo Tundu Lissu, na mshenga
 wake Gwajima,
 tukabishana tangu saa 3 asubuhi mpaka saa 9 alasiri, wapo
 hapa waseme
 kweli, mimi sikukubaliana nao tangu mwanzo, nawaomba
 viongozi wangu wawe
  wanyoofu na wenye hofu ya Mungu," alisema.



 Kwa mujibu wa Dk. Slaa, baadaye walitakiwa kwenda nyumbani
 kwa Lowassa
 lakini alikataa akisema hawezi kwenda nyumbani kwa mtu wa
 CCM katika
 mazingira ya u-Katibu Mkuu wa Chadema. Aliongeza kwamba
 baada ya hapo,
 iliundwa kamati ya watu wachache kumshawishi (Slaa), ambayo
 ilikaa tangu
  saa 9 mpaka saa 12 jioni lakini akawapa masharti yale
 yale.



   "Tuliporudi kwenye kikao taarifa ya kikao kile
 haikutolewa. Nikaandika
  barua ya kujiuzulu nikampa Makamu Mwenyekiti Profesa Safari
 akaichana,
 nikaandika nyingine nikampa Makamu Mwenyekiti Zanzibar,
 akaniambia Dokta
  usihangaike mambo haya yamepangwa," alisema.



   Akizungumzia watu waliokuja Chadema, alisema wote wamekuja
 wakiwa
 makapi baada ya kuwa wameshindwa kwanza kwenye mchakato wa
 awali wa CCM
 (kura za maoni) na hata huko walikotoka si wasafi. "Watu
 kama Sumaye
 hawakuwa safi, mimi mwenyewe nilimwita fisadi bungeni,
 alichukua Shamba
 la Magereza Kibaigwa, na yeye mwenyewe alifikia hatua ya
 kusema CCM
 wakimteua Lowassa yeye atahama chama, sasa yuko naye, najua
 dhambi
 haihalalishiwi na dhambi nyingine, lakini maneno hayo
 yalitamkwa na
 nani, Watanzania walimwita Sumaye ziro," alisema.



 Aliendelea kuwaponda wana CCM waliohamia kuwa ni kama makapi
 ambao
 hawataongeza thamani yoyote kwa chama hicho akiwataja Mgana
 Msindai na
 Matson Chizii kuwa ni sehemu ya makapi ambayo hayataongeza
 thamani
 yoyote kwa Chadema. "Kuna watu wanasema ondoa CCM kwanza
 hata
 ikiwezekana kuweka mkataba na shetani, mimi ni Padri
 Mkatoliki, hata
 kama nimestaafu, nikubali kuweka mkataba na shetani mradi tu
 niondoe
 CCM. Unaondoa CCM kwa program serious na watu makini au
 unaondoa na watu
  wale wale?" alihoja Dk. Slaa.



 Chadema na tuhuma za ufisadi Mbali na kuhoji endapo
 waliohamia Chadema
 kutoka CCM wameongeza thamani yoyote kisiasa; Dk. Slaa
 aliyesimama imara
  akizungumza kwa saa 1.32 alisema; "Chadema iliaminika
 miongoni mwa
 Watanzania kwa kutoyumbishwa na kusimamia uadilifu. Sasa leo
 Chadema
 wanathubutu kusema etu usimtuhumu mtu? Upuuzi mtupu! Kama
 tusingemtuhumu
 

[The entire original message is not included.]

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment