Thursday, 10 September 2015

Re: [wanabidii] 2015: NI KURA YA MAAMUZI MAGUMU

Umasikini wa kujitakia. Watanzania pale tulipo hatujitumi ipasavyo. NGO zifanye kazi ya kuhamasisha hasa zikishirikiana na extension staff na kutumia sheria kama mtu hataki kubadilika mfano kutokujenga nyumba bora na resources zipo mpaka mashine za kutengeneza matofari ya kuchoma ya kuingiliana -interlocking blocks, soil cement block na maeneo mengine wana mawe ya gypsum; kulima na kufuga endelevu, mabwawa ya samaki; kuingia mkataba na mwekezaji wakufaidika na madini achimbe yeye kwa vifaa vya kisasa ili waepuke zinaa machimboni na ukimwi, kushika madini chafuzi ya viungo vya mwili wao hatumie mafao kufanya kujiajiri katika shughuli nyingine endelevu. Kulinda raslimali-ardhi, mito, maziwa, misitu ni muhimu. unapouza mali yako kama nyumba, ardhi tumia hela kiakili badala ya kujitafutia matatizo kimaisha. Ona yanayoonekana na badilika. Jipende na kupenda nchi yako. Jijue na ujitambue na uwe mwaminifu kona zote. Kama ni dereva-zingatia sheria za uendeshaji
salama, wacha kuweka maduka kando ya barabara, vilabu vya pombe, viti barabarani na kila baada ya nyumba 3 ni bar na vitu vya anasa-Tutafika? Mtumishi wa serikali wacha uroho na ubadhirifu timiza wajibu wako. Ogopa Mungu wacha kuibia raia wenzako.


--------------------------------------------
On Thu, 10/9/15, 'ananilea nkya' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

Subject: [wanabidii] 2015: NI KURA YA MAAMUZI MAGUMU
To: mabadilikotanzania@googlegroups.com
Cc: "WANA BIDII" <wanabidii@googlegroups.com>
Date: Thursday, 10 September, 2015, 12:23

UCHAGUZI 2015:  NI KURA YA
MAAMUZI KUHUSU UMASKINI WA WANANCHI
Na Ananilea Nkya
Tanzania  ni  moja  ya nchi  chache
barani Afrika ambazo zimejaliwa utajiri  mkubwa wa mali
asili yakiwepo  madini, ardhi yenye rutuba iliyosheeni
milima mabonde  na wanyama  lakini  mamilioni
ya wananchi ni masikini  wa kutisha ingawa 
nchi  ilipata uhuru  zaidi ya miaka  50
iliyopita.

Ili nchi iweze kuondokana na umasikini hata kama inazo
rasilimali nyingi   inapaswa kuwa na
rasilimali nyingine muhimu—rasilimali uongozi –uongozi
unaohakikisha kuwa  mali za nchi 
zinanufaisha  wananchi wote na siyo kikundi 
kidogo cha viongozi.

Uongozi  wa  nchi kwa kawaida hupatikana kupitia
vyama vya siasa. Hivyo  ni muhimu wanaotafuta 
fursa ya uongozi  katika uchaguzi  wa mwaka huu
2015, kutambua kuwa  mamilioni ya Watanzania  hivi
sasa ni maskini ili hali kikundi kidogo cha viongozi 
ni matajiri  sana.

Kibaya zaidi  mamilioni ya  Watanzania
wanaotaabika kwa umaskini  hivi sasa  wametambua
kuwa   umaskini   wao
unatokana na  uongozi  unaotoa fursa 
kwa  viongozi  kuwa matajiri wa kupindukia 
na  mamilioni ya wananchi  kubaki maskini.

Mamimioni hayo ya wananchi  wanateseka kwa
umaskini   mwaka huu  wanataka
mabadiliko ya uongozi wa nchi yao.

Wanataka mabadiliko hayo baada ya kutambua kuwa  mfumo
wa utawala (Katiba)  uliotengenezwa na serikali ya
CCM   ndio  unawezesha watawala
wachache  kuwa  matajiri wa kutupa kwa kulipana
fedha   nyingi  za  umma na
kujigawia rasilimali za nchi kujitajirisha wao wenyewe.

Kwa mfano  wananchi wanajua kuwa watawala 
walijiuzia kwa  bei  chee  nyumba za
umma  zilizojengwa kwa mabilioni ya fedha za  kodi
ya Watanzania  wanaoteseka kwa umaskini.
Kadhalika,  wananchi wanafahamu
kuwa   viongozi  wa serikali 
walijigawina fedha za umma zilizoibiwa kwenye akaunti
ya  Tegeta escrow mwaka jana 2014.

Vilevile  wananchi  wanajua  kuwa 
watawala  mfano wabunge
wanalipwa   mishahara mikubwa na kiinua
mgongo kikubwa katika muda wa miaka mitano tu huku watumishi
wengine wa umma  mfano walimu, wauguzi na madaktari
wakiwa  wanalipwa  mishahara midogo sana.
   
Kwa sasa, mtu ambaye haijamuingia akilini kwamba mamilioni
ya wananchi wamechoka na umaskini  ambao chanzo
chake  ni uongozi  mbovu  katika nchi 
yao—uongozi ambao   unatajirisha wachache
na hivyo wanataka mabadiliko ya uongozi wa nchi yao, 
mtu huyo  atakuwa anajidanganya.

Jambo jema ni kuwa  hata  baadhi ya wagombea
Urais  kwa mfano mgombea wa  CCM,  Dr
John  Magufuli na mgombea wa  CHADEMA, Edward
Lowassa   kwa  niaba ya vyama
vinavyounda UKAWA  wamekuwa wakizungumza wazi
kwenye  mikutano yao  ya
kampeni   kwamba  wananchi wanataka
mabadiliko ya uongozi.

Tena wagombea  hawa wanatambua wazi kuwa 
mabadiliko watayaleta  hao
Watanzania   wenyewe  wanaoteseka
kwa  umaskini kwa kutumia sanduku huru la kura hapo
tarehe 25 Oktoba  mwaka huu 2015. 
Kwa maneno mengine mamilioni ya wapiga kura maskini wanajua
kuwa uchaguzi wa mwaka huu 2015 kura yao ni  kura 
ya maamuzi  juu ya maisha yao. Ni kura muhimu  ya
KUAMUA   KUENDELEA KUWA MASKINI AU KUUKATAA
UMASKINI.
   
Ni kura ya kuamua iwapo  wanataka watawala
wachache  wanaotengenezwa na   serikali
ya CCM  waendelee kuwa matajiri wa kutisha na mamilioni
ya Watanzania waendelee kuumizwa na umaskini ili hali nchi
yetu ikiwa ni tajiri mkubwa wa rasilimali za asili za
kuwawezesha Watanzania wote kuwa matajiri na kuishi maisha
ya furaha na yenye hadhi.

Wananchi wenyewe wanajua kuwa  mabadiliko 
wanayoyataka yanawezekana ingawa  kumekuwa na njama za
kujaribu  kupunguza nguvu ya umma inayodai mabadiliko
kutumia baadhi ya viongozi wa ngazi za juu kwenye vyama vya
upinzani vinavyounda UKAWA (CUF, CHADEMA, NCCR Mageuzi na
NLD)--vyama vinavyoongoza wananchi katika kutafuta
mabadiliko.

Wananchi  wameshuhudia baadhi ya viongozi wa
upinzani  wakiamua ghafla kuondoka kwanye uongozi 
na kuungana na watawala  ambao mfumo wa uongozi
umewafanya kuwa matajiri wa kutisha huku wananchi wengi
wakiwa ni maskini wa kutupa.

Lakini  pamoja na viongozi   hao 
kuachia ngazi, mamilioni ya wananchi hawajabadilika,
hawajayumba,  msimamo wao uko pale pale na
wanasonga  mbele  hadi waweze kufanya 
mabadiliko wanayoyataka.
 
Ni kwa nini wananchi wanataka mabadiliko ya uongozi wa nchi
yao?
Wanataka nao  wawe matajiri  katika  kipindi
cha miaka mitano kama  ambavyo  wananchi wenyewe
wameshuhudia  wanaochaguliwa  kuwa viongozi 
wakitajirika ghafla  baada ya kuchaguliwa  kuwa
viongozi!

Wananchi   wamechoka kuwa mafukara katika
nchi yao  yenye utajiri mwingi wa asili  lakini
utajiri huo  unatajirisha  makundi mawili tu--
watawala wachache  na wawekezaji wa kigeni.

Tena baadhi ya mamilioni ya Watanzania  wanaotaka
mabadiliko wengi wao hawana vyama vya siasa wanavyofungamana
navyo maana hata  fedha za kununua kadi ya chama cha
siasa hawana.
Baadhi waliobahatika kuwa wanachama wa vyama vya siasa 
kikiwepo chama kinachotawala nchi kwa sasa CCM, lakini 
wengi wa  wanachama  hao ni mafukara wa kutupa pia
wanaohangaika kwa umaskini kama wananchi  wengine.

Kimsingi,  mamilioni  ya watu maskini (nguvu kubwa
ya umma) ambayo mfumo wa uongozi wa serikali ya CCM
umezalisha, mabadiliko wanayoyataka ya uongozi hayaepukiki
maana hakuna anayeweza kuizuia  nguvu ya umma inapoamua
kuleta mabadiliko.
 
Isitoshe, mamilioni ya wananchi   hawa
maskini,   ni kama bomu ambalo  serikali
ya CCM  imelitengeneza kwa kujua au kwa kutokujua 
kwa miaka kadhaa  sasa  na  hivi sasa 
linasubiri kulipuka lenyewe kwa  amani  kwenye
sanduku huru la kura  tarehe 25  Oktoba 
2015.

Jambo la kuzingatia ni kwamba , atakayejaribu kuzuia 
kwa mkono bomu hilo lisilipuke kwa amani kwenye sanduku huru
la kura---uwanja  wa wazi ambao  ndio pekee bomu
hilo linaweza  kulipuka bila kuleta madhara ya kuvuruga
amani ya nchi,  mtu huyo  historia  ya taifa
hili itamhukumu. Mungu ibariki Tanzania.

NOTE: Naridhia anayetaka kuichapisha au kusambaza makala hii
isomwe na Watanzania  wengi afanye hivyo.

Ananilea Nkya
 E-mail:ananilea_nkya@yahoo.com

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com 
Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the
Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit
https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment