Thursday 20 April 2017

[wanabidii] KWA VIJANA WENYE NDOTO YA KUJIUNGA JESHI

ANDIKO HILI LISIHUSISHWE NA CHOMBO CHOCHOTE CHA ULINZI NA USALAMA .

Jeshi ni mkusanyiko wa watu wenye fani , taaluma , uwezo na jinsia tofauti lakini wenye lengo moja kulinda maslahi na uhuru wa nchi . tofauti kati ya jeshi moja na lingine ni Mafunzo , majukumu na taratibu za kazi kulingana na katika tuliyonayo sasa .

Yale maonyesho unayoyaona uwanja wa taifa na karibuni dodoma ni sehemu ndogo ya majeshi mbalimbali ndani yake kuna watu wa fani karibu zote unazozijua na usizozijua .
Kwa wale waliomaliza kidato cha nne au sita na kupitia au kutokupitia JKT na kutaka kwenda Jeshi .

Tafadhali kama umefanikiwa kufika hatua hii ya elimu , tafuta fursa ujiendeleze kwenye fani nyingine mbalimbali kama ualimu , kilimo , uvuvi , udereva , ufundi wa vitu mbalimbali , ushauri nasaha , ufamasia , uuguzi , usimamizi , ujasiriamali na nyingine nyingi zilizopo .

Unapokuwa na fani angalau moja au zaidi inaweza kuwa rahisi Zaidi kwako kujiunga na chombo chochote kama nafasi zikitangazwa siku nyingine kama bado unania hiyo na kama ukikidhi vigezo vya umri , afya , elimu na mengine mbalimbali . Hata pale unapokosa basi fani unayo maisha yanaendelea na kazi mbalimbali utaendelea kufanya .

Usijiunge na vyombo hivi kwasababu unadhani unaweza unaweza kutoka kimaisha na ajira ni ya uhakika – humu pia kuna risk zake nyingi pale usipofuata maadili na taratibu zilizopo hasa pale unapokua huna nia ya dhati na uzalendo kwa nchi yako Zaidi ya tamaa za kimaisha .

Usimpe vyeti vyako mtu yoyote kwa kisingizio kwamba ataenda kukusaidia kukuingiza kwenye vyombo hivi - unaweza kushangaa cheti chako kikatumiwa na mtu mwingine kufanikisha mambo yake mengine ikiwemo kujiunga na vyuo au kupata fursa nyingine mbalimbali – Wewe fuata taratibu zilizopo , kama fursa zimetangazwa Omba fuata masharti na vigezo .

Angalia mienendo yako binafsi kwenye mitandao ya kijamii vile unavyopost , changia , share , marafiki na watu wengine wa karibu – msururu huu unaweza kuchangia kukukwamisha kwenye mengi sio jeshi tu .

Kumbuka kuna Jeshi la Polisi , Jeshi la wananchi wa Tanzania , Jeshi la Magereza , Jeshi la Zimamoto , Uhamiaji , Usalama wa Taifa .



--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment