Tuesday, 10 November 2015

Re: [wanabidii] KIKWETE KAULI HATARI UCHAGUZI

Unalindaje KURA wakati kuna Mawakala ambao wanacheki jina la kila anayeingia kupiga kura. Watu zaidi ya kumi wajae hapo na kusoma majina kila anayeingia na kutoka na kila kura iliyopigwa? Hata hivyo-kila mgombea anajiaminisha ni yeye mshindi kutokana na wananchi wadanganyika na wadanganya wafanyavyo kwa wagombea. Unamkuta mgombea ana watu 100 ktk mtutano hao 100 wanamuimbia...Rais! Raisi! Raisi!! Anakuja Lowasa wanajaa milioni 2 na Mangufuri milioni 2 na sare zao wanaimba hivyo hivyo. Anakuja Mghwila ni idadi hiyo na wanaimba Mama Raisi! mama Raisi huyoo!. Ukija kwenye Kura waliomuaminisha kuwa anapendwa na atashinda mfano Rungwer jimbo hilo anakura 100, wenzake millioni 3 hadi 5 mwingine Chief fulani anazo 30 tu. Halafu kila mmoja ana amini kuwa ameibiwa kura kwa vile walisema wanampenda waliimba Raisi Raisi!! Kwa hiyo kura za Chama chao zimeibiwa. Wakala amesaini walipohesabu-unalindaje ukiwa nje? kama mji au jimbo lina watu laki 5 na hao laki tano walivaa sare za vyama mbali mbali wakishakilia hivyo hivyo. Huoni kuwa ni changa la macho kudai umeibiwa? Ni hao hao tu vi T-shirt, hela ya mafuta na madela wanaserebura pande hii anapata hiki pande ile hiki anaweka sandukunu. Wewe umeliwa, wanampigia wamtakae au aliyeyetoa hela nyingi kwao kwa faida binafsi. Sijui kama kusingekuwa na mawakala mpambano wa kuvamia vituo na wasimamizi ungekuaje!

Kama si jeshi kupewa vifaa na kuzagaa kila kona-kweli uchaguzi wa mwaka huu ungekuwa vita vingeanzishwa na wapenda madaraka. Fikiria kura imepiwa kilometa 120 lakini wanatoka hapo kwenda kuchoma nyumba ya mgombea aliyeshinda kilometa hizo 120 mbali sana. Wengine wakifahamu kuwa kufika vijiji vya milimani huko Njombe, Morogoro si mchezo na usafiri ni miguu mpaka ufike pale pikipiki zinapoishia. Wanaona wanachelewesha kupewa matokeo nafanika kuchoma kituo cha kata, polisi na nyumba ya chama fulani-tawala. Wakati yeye hata kutembelea nduguze milimani huko mbali mpaka kuwe na kilio labda kutokana na umbali na njia mbaya. Ila wakusanya matokeo ndi wajinga labda watafute kitunga waruke nacho juu raia hawana subira kusubiri 2 days. Na wanapochoma ofisi ya Kata, kituo cha polisi-wanachoma mafaili ya ndugu zao, jirani zao kama si yao wenye kesi mbalimbali na vidhibiti humo. Huu si ukichaa chini ya kisingizio cha haki ya binadamu ya Kura?

Ukiangalia police wa Marekani au UK na vivalo vyao-huwezi kuamini na utawaona wanavyotwangana na wananchi wanaoandamana na kuvunja sheria wengine kuvunja maduka na kupora. Police wanapigwa, wanauawa nao kuvunja watu na kuua. Ila polisi wa TZ wawaache wananchi wafanye watakavyo, kuvunja sheria under the mwamvuli wa demokrasia? Mbona huko demokrasia ilikoiva makari ya washawasha yanatumika na ndio wao wanatengeneza, wanatumia na wanatuuzia? Na kisha pamoja na kuwa na demokrasia kuna Camera barabara zote, kwenye majumba ya biashara na ya serikali, bank, mataa ya barabarani, nyumba za kuishi mwenye uwezo na vyuoni. Likitokea la kutokea ni police kukusanya vifaa vya camera tukio nilipotokea na kuwafuatilia wahusika. Sisi hapa watu watarusha mitandaoni tukio la kumchoma mtu moto, mwanamke kupigwa uchi au watu wamefumaniwa wanatembezwa bila nguo na watu kuwarushia mawe-hakuna linalofanyika kuwakamata wale na yule mume aliyemtembeza mke uchi na kumweka ndani, kumshitaki, kumwadhibu. Hata NGO huoni zikaandamana kuwa yume mtembeza mfumaniwa wake (me) na mkewe akamatwe na kumfuatilia mpaka ofisini/nyumbani kwake. Hapa demokrasia ipo ila ya Kura tu na mawakala wamesaini-HAIPO. Excuse me! Kuna lililotakiwa litokee la machafuko kama kisingizio lakini halikuwezekana kwa kiwango kilichotakiwa. MTAJI UMEINGIA NUKSI, KIKWETE ALIJIANDAA ILA KWA MANUFAA YETU WOTE. Tunapo pa kukimbilia? Mifano nchi za wenzetu hatuioni? Kura zimepita-tujenge nchi kwa upendo na Amani. Mtaji wa Vurugu ilele ulaji utarudi tena 2020.



--------------------------------------------
On Tue, 10/11/15, 'dani killo' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

Subject: Re: [wanabidii] KIKWETE KAULI HATARI UCHAGUZI
To: "wanabidii@googlegroups.com" <wanabidii@googlegroups.com>, "mabadilikotanzania@googlegroups.com" <mabadilikotanzania@googlegroups.com>
Cc: "Wanazuoni - Informal Network of Tanzanian Intellectuals" <wanazuoni@yahoogroups.com>
Date: Tuesday, 10 November, 2015, 9:42

Hii
ndo nchi ya demokrasia? nina
makengeza God created men in LOVE ,let us live with
LOVE



On Saturday, October
17, 2015 4:50 PM, 'ELISA MUHINGO' via Wanabidii
<wanabidii@googlegroups.com> wrote:



Ni haki kwa watanzania
kubaki vituoni kusubiri matokeo. Lengo ni kujua matokeo na
kujua kiongozi wako ngazi fulani na kujua mwelekeo wa
kiongozi ambaye kura zake zinahitaji jumba toka sehemu
nyingine.
Huko nyuma tumeshuhudia hayo. mara
kadha nimekuwa nawapigia vijana wangu waliolala vituoni
kutaka kujua nani kashinda.
Siku hizo
makundi yote yalisimama na kusubiri matokeo. Aliposhinda wa
chama fulani wote na wa chama kingine waliungana
kushngilia.
Mwaka huu ni tofauti.
Kuna vyama vimetamka wazi kuwa hsi kwamba
wanaenda kusubiri matokeo bali wanakwenda kulinda kura.
Wanasema kama matokeo yataonesha chama chao kimeshindwa basi
kura zao zimeibiwa. Hapa ndio Rais anasema hakuna kulinda
kura. Maana yake kuna chama kikitangazwa kushindwa wakati
wananchama walioshinda wamesimama pembeni basi hapo ngumi na
mateke vinaanza. Wote tunajua kuwa rais anaendesha nchi kwa
vyombo vya dola. Ni uelewa gani tena kuwa rais anatishiwa
kushitakiwa ICC kwa sababu ya kutumia vyombo vyake vya dola.
Kuna kila dalili kuwa kuna watanzania hawathamini tena nchi
yao; uongozi wa nchi kwa kudhani kuwa watakwenda kulalamika
ICC. WATU HAO WAMECHELEWA. hakuna kugombana. Hakuna
kupigana. Wala hakuna kwenda ICC. Kama mtu anafikiri
atawapiga mawe Polisi na wasifanywe lolote. HUU NAO NI
UPUMBAVU MPYA.
--------------------------------------------
On Fri, 10/16/15, 'ananilea nkya' via
Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>
wrote:

Subject:
[wanabidii] KIKWETE KAULI HATARI UCHAGUZI

To: mabadilikotanzania@googlegroups.com,
"WANA BIDII" <wanabidii@googlegroups.com>
Cc: "Wanazuoni - Informal Network of
Tanzanian Intellectuals" <wanazuoni@yahoogroups.com>
Date: Friday, October 16, 2015, 11:42 AM

RAIS KIKWETE WANANCHI
KULINDA KURA
UTAEPUKA KUSHTAKIWA
 
Na Ananilea Nkya

Uchaguzi mkuu utakaofanyika
Jumapili tarehe 25 Oktoba mwaka
huu 2015
huenda vyombo vya dola vikatumika kifisadi kupora
mamlaka ya wananchi   kuchagua kiongozi
wanayemtaka katika ngazi ya Urais, ubunge na
udiwani.

Hii ni kwa
sababu Rais Kikwete   siku
alipozima
mwenge wa Uhuru huko Dodoma alitoa kauli 

hatari kwamba   vyombo vya dola

vitawashughulikia wananchi ambao watakuwa wako karibu na
vituo vya  kura  kulinda kura zao na
kushuhudia
kuwa atakayeshinda  atakuwa 
ameshinda kihalali na
siyo kwa  'goli la
mkono' (wizi).


Kinachoshangaza  Rais Kikwete ambaye pia ni mwenyekiti
wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)   ametoa 
kauli hii  huku akijua wazi kuwa  sheria
ya
uchaguzi  inawaruhusu wananchi kukaa
mita 200 kutoka
kituo cha kupigia kura kwa
lengo la kushuhudia upigaji
kura, 
kuhesabu kura na kutanga matokeo.
 
Vyama vya upinzani  vikiwepo  vinavyounda
Umoja wa
Katiba ya Wananchi (UKAWA)
–CHADEMA, CUF, NCCR-
Mageuzi  na NLD 
ambavyo  vimeamua
kusimamisha mgombea
mmoja mmoja kwenye nafasi ya urais,
ubunge
na  udiwani   vimekuwa 
vikiwahimiza 
wananchi  kulinda kura.


Kufuatia kauli hiyo ya Rais Kikwete wananchi
wanauliza:  Rais ambaye anapaswa kuwa mlinzi
namba moja
wa sheria za nchi inakuwaje
ametoa kauli inayoashiria kuwa

anakusudia   kuvunja sheria ya uchaguzi?


Wananchi wanauliza swali hili kwa sababu 
Rais
kutumia  vyombo  vya umma
vinavyopaswa
kulinda  usalama  wa
wananchi  kama 
vile  jeshi la  polisi
au 
jeshi   la wananchi kunyanyasa
wananchi 
siku ya kupiga kura  kinyume na
sheria  ya
uchaguzi  ni  sawa na 
kufanya ufisadi katika
mchakato
wa   kupata viongozi wa  nchi.

Kufanya ufisadi huo   siyo tu
ni   kuvuruga amani na  demokrasia ya
uchaguzi unaohusisha vyama vingi vya
siasa   bali pia  ni  kukwamisha
juhudi za kukomesha umaskini unaowatafuna
wananchi wengi
kutokana ambao chanzo
chake  ni ufisadi.

Rais
Kikwete  kutumia vibaya  nguvu ya

kimamlaka   aliyopewa na

umma   kwa 
kuagiza   vyombo
vya 
dola   kunyima wananchi kulinda
kura
zao   ni kutaka    viongozi 
wan chi yetu wapatikane kwa njia za ufisadi na
wizi wa kura
na hivyo wakiingia 
madarakani  wataendelea
ufisadi huo huo 
katika  chaguzi zijazo.


Hii ni hatari kubwa kwa taifa kwa sababu madhara yake 
ni makubwa  kwa  maendeleo ya  nchi
yetu  kudumu kwa  amani  ya kweli
inayotokana
na haki  kutendeka kwenye
uchaguzi.

Ndiyo sababu
wananchi  wanauliza   lengo
la Rais
Kikwete  lilikuwa ni nini  kutaka

kuvunja  sheria ya uchaguzi kama siyo  anafanya
hivyo  kuandaa mazingira ya kutekeleza 
azma
ya   chama chake ---Chama cha
Mapinduzi 
(CCM)  kutumia 'goli la
mkono' kupata ushindi 
kwa gharama
yoyote kama wanavyozungumza kwenye majukwaa ya
kampeni?
 

Maswali haya ya wananchi  yanatokana na ukweli
kwamba   kauli  ya Rais 

Kikwete  kuzuia wananchi  kuwa  karibu na
vituo vya kupiga kura kinyume na sheria ya
uchaguzi   ilianza kutolewa  kwa
msisitizo  na  Mwenyekiti wa Tume ya Taifa
ya
Uchaguzi (NEC) Jaji  mstaafu Damian
Lubuva.

Lubuva
alinukuliwa akihoji:  "Tume inashangaa kwa
nini vyama vinang'ang'ania kubaki katika
vituo vya
kupigia kura''.

Kadhalika, jambo
linaloshangaza wananchi ni
kwamba   hata
Msajili wa vyama vya siasa ,
Jaji Francis
Mutungi naye ameunga mkono uvunjaji huo wa

sheria ya uchaguzi  kwa sababu  badala ya

kumshauri Rais  kufuta kauli yake hiyo , ameuunga
mkono.

Jaji
Mutungu amenukuliwa akisema ''ni kweli sheria
imeruhusu wananchi kubaki katika kituo cha
kupiga kura kwa
umbali wa mita 200, lakini
sheria hiyo ina upungufu ambao
wameuona
ndio maana Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), imetoa
kauli hiyo ya kuwezesha uchaguzi kufanyika
katika mazingira
ya amani''

Wananchi wanauliza kama 
sheria ya uchaguzi 
ilikuwa na mapungufu
ni kwa nini serikali haikuipeleka
Bungeni
iweze kufanyiwa marekebisho kabla ya uchaguzi 
wakati uchaguzi  halikuwa  jambo 
ghafla?

Kadhalika 
wananchi wanauliza:  Rais Kikwete 
pamoja
na Jaji Lubuva na Jaji Mutungi  wamepatwa na
nini gafla  kiasi kwamba  wameamua 
kushabikia uvunjifu wa Katiba ya nchi na 
sheria ya
uchaguzi  kunakoweka  rehani
amani, usalama na
heshima kubwa ambayo
Tanzania imejijengea mbele ya mataifa?
 

Pengine kinachowafanya  wananchi kuamini
kuwa 
huenda   Rais 

Kikwete   na na CCM yake  wanakusudia

kutumia  'goli la mkono'  kupata viongozi wa
nchi yetu kwa kutumia ufisadi wa kura  ni
kwamba 
Jaji  Lubuva na  Jaji Mutungi 
wote ni 
mwanasheria   waliobobea na
kwa nyadhifa
zao  wanapaswa  kuitiii
Jamhuri ya Muungano 
kama  walivyoapa
siku walipoteuliwa  kushika
nyadhifa hizo
na siyo vinginevyo.


Kutii  Jamhuri maana yake  siyo  kusema ndiyo
kwa kila analosema, kuagiza au analotaka Rais
wa Jamhuri
yetu,  bali  ni kutumia 
busara  na
kuheshimu  kiapo cha utii 
kwa Jamhuri 
kumshauri  Rais  kuepuka 
kutoa 
kauli  au  kupanga  mambo
maovu
yanayoweza  kufanya uchaguzi
kultumbukiza nchi yetu
kwenye machafuko.

Hebu jiulize ni wanawake
wangapi, watoto wangapi, wazee
wangapi na
vijana wangapi wataathirika ikitokea hii kauli
hatari ya Rais Kikwete ikitekelezwa na nchi
yetu ikakumbwa
na machafuko kwenye uchaguzi
mwaka huu?

Rais Kikwete
ajue kwamba kwa kauli alioyoitoa  kama

atatekeleza hiyo azma yake ni lazima katika uchaguzi wa
mwaka huu kutokee umwagaji mkubwa wa damu kwa
sababu kauli
yake  imewafanya wananchi
kuamini kuwa haki yao ya
kulinda kura
inapokonywa na Rais kwa kuamua kuivunja sheria
ya uchaguzi.

Muhimu, wananchi  hasa katika  wakati
huu 
nchi inaelekea kwenye siku ya
uchaguzi mkuu  tarehe
25, 
wanategemea   Jaji Lubuva kuonyesha

hekima, busara na ujasiri wa hali ya kuu kuhakikisha NEC
inasimamia na kutenda    ili  wananchi 
waridhike kwa dhati kabisa kwamba haki
imetendeka kwenye
uchaguzi maana bila haki
kutendeka hakuna amani ya kweli nay
a
kudumu Tanzania.
 

Aidha  wananchi  wanatarajia pia  kuwa 

wadau  wakubwa wa amani vikiwepo vyombo vya habari na
hususan wahariri ,  viongozi wa dini zote, 
wakuu
wa vyombo vya  usalama  hususana
jeshi la polisi
na jeshi la wananchi, 
viongozi wa vyama vya siasa,
mashirika ya
kiraia NGOs mfano TAMWA, TGNP na LHRC 

wasomi,  wahanahakati na kila mtu mwenye nia njema na
Tanzania anachukua hatua bila 
woga   kumtahadharisha Rais  Kikwete
kwamba  kuvunja sheria ya uchaguzi kwa
kuwazuia
wananchi kulinda kura zao ni
ufisadi  mbaya
utakaoigharimu nchi yetu
.

Bila  kumtaadharisha
Rais Kikwete,  ikitokea
vyombo vya dola
vikapambana na wananchi walioamua kutumia

haki yao ya kisheria  kulinda kura,  Jaji 
Lubuva na  Mutungi hawatakwepa  mkono wa
sheria za
kimataifa  kwa  kushiriki 
jinai 
ya  kufisadi uchaguzi  wa mwaka
huu 
kwa  kuamua  kuwasaidia 
watawala  wa
CCM wanaotaka chama chao 
kung'ang'ania madaraka
kwa gharama
yoyote  hata kama kitakuwa
kimekataliwa 
na wananchi.

Tukumbuke
kuwa kauli ya kwamba CCM itashinda kwa gharama
yoyote imekuwa ikitolewa na viongozi mbali
mbali waandamizi
wa CCM akiwepo Katibu Mkuu
wao, Abrahamani Kinana.


Hivi sasa  baada ya  Jaji Lubuva na Jaji

Mutungi  kuungana na Rais Kikwete kutaka 

kuvunja  Katiba ya  nchi yetu na

kukiuka   sheria ya uchaguzi  ili

kuwanyima  wananchi haki ya  kukaa karibu na 
vituo vyao vya kura  hadi  mwisho kujua
hatma ya
kura yao   kumewafanya wananchi
kuuliza :

Hivi Tanzania 
imebinafsishwa
lini   na 
lini   na
kugeuzwa kuwa   mali
binafsi ya 
Rais  Kikwete   na
watawala wachache wa
CCM  kiasi  kwamba
wanaweza  kufanya lolote
na Watanzania
wengine wote hawana  tena mamlaka juu ya

nchi yao?

Hivi Tanzania 
imebinafsishwa   kwa
hivyo hivi
sasa   nchi hii  ni
mali   binafsi
ya  Rais KIkwete na
watawala wachache wa 
CCM kwa hivyo wanaweza 
kufanya watakavyo
na wananchi hawana  tena mamlaka juu
ya
nchi yao?

Wananchi 
wanauliza  kama  Tanzania

haijabinafsishwa kifisadi  Rais Kikwete, Jaji Lubuva na
Jaji Mutungi  wanapata  wapi  kile 
Dakta Harrison  Mwakyembe alichokiita
'jeuri ya
kifisadi'  ya kutaka
kuvunja  sheria za
uchaguzi  kuruhusu
vyombo vya dola  kunyanyasa
wananchi siku
ya uchaguzi ili sauti ya umma inayotaka

mabadiliko ya uongozi  isisikike kupitia sanduku huru
la kura?


Wananchi wanauliza maswali haya kwa sababu wanaona kauli
iliyotolewa na Rais Kikwete kwamba ataamuru 
vyombo vya
dola kushughulikia wananchi
watakaokuwa karibu na vituo vya
kupigia
kura na kisha kauli hiyo kushabikiwa na Jaji Lubuva
na Jaji Mutungi  kunaashiria  wanataka
Tanzania
iingie kwenye balaa
zililozikumba 
nchi   kadhaa  za
Afrika ikiwepo nchi
jirani ya Burundi.

Kwa Rais Kikwete kutaka
kuivunja  sheria ya uchaguzi
juu ya haki
ya wananchi, tafsiri yake ni

kwamba   anataka kuweka historia mbaya 

ya  kuingiza Tanzania kwenye  machafuko  kwa
kulaka kulazimisha  CCM kubaki madarakani 
kwa
'goli la mkono'  ambalo  ni
sawa  ni sawa
na uhaini.


Je  kwa  Rais Kikwete  kwa kutaka 
kuvunja sheria ya uchaguzi inayoruhusu
wananchi  kukaa
mita  200  kutoka kituo
cha uchaguzi  anataka
kuwaambia Watanzania
kuwa   tarehe 25 Oktoba
2015 
amejiandaa   kutumia  vyombo
vya dola 
kuwapora wananchi Watanzania  mamlaka ya

kuamua  nani awe kiongozi wao?

Kama Kikwete ndivyo anataka ni vema ajiandae
kushtakiwa
kwenye mahakama ya
Kimataifa   ya makosa ya
jinai.

Akiamua kutekeleza jinai
hiyo  siyo tu atakuwa
amejidhalilisha
mwenyewe na CCM yake bali pia Wanzania

wote  na  Tanzania ambayo  inaheshimika

duniani kote kutokana na  misingi ya haki na 
kuheshimu  wananchi kulikojengwa na muasisi
wa taifa
hili Juliua Nyerere.

Lakini zaidi itakuwa ni aibu
kwa CCM ambayo imeongoza
nchi  hii 
miongo mitano  kuonekana kuwa
serikali
yake  haikuanzisha vyama vingi  kwa nia

ya dhali kuleta ushindani wa kisiasa kukomesha umaskini
unaotafuna mamilioni  ya Watanzania.
   
Hii ni kwa sababu Rais
wa serikali  ya CCM kujaribu
kuvunja
sheria  ya  uchaguzi  kulazimisha
CCM 
kubaki madarakani ni kukataa mfumo wa vyama vingi
usifanye kazi   kuondoa umaskini.

Huku ni kukataa mabadiliko
wakati  mmoja wa 
waasisi mashuhuri wa
CCM, Mzee   Kingunge
Ngombale Mwiru 
ambaye  ameamua kuondoka CCM kwa
tuhuma za
kukiukwa kwa  Kanuni na Katiba ya chama hicho
wakati wa mchakato wa kumpata mgombea urais,
amekiri
hatadhani kuwa chama hicho sasa
kimechoka, kimekosa
pumzi,  uchumi wa 
nchi umekwama, kinakodisha
mavuvuzela
kutukana watu , hivyo  madadiliko ni 

lazima mwaka huu 2015.


Lakini zaidi Rais Kikwete  asipoacha kutekeleza kauli
yake  atakuwa  ameuthibitishia
ulimwengu 
kwamba Tanzania  ni miongoni
mwa  nchi
ambazo  wanazuoni Daron
Acemoglu and James Robinson
kwenye kitabu
chao ''Why Nations Fail '' 
 
wanadai kwamba   chanzo  kundi
kubwa la
wananchi kubaki maskini na kikundi kidogo cha
watawala kujajirika kufuru ni  chama
kinapokuwa
madarakani serikali  kukataa
mabadiliko ya
uongozi   hivyo kutumia 
vibaya vyombo
vya dola  kung'ang'ania
madaraka.
 
Hii itakuwa
ni aibu kwa CCM iliyoongoza  Tanzania 

miongo mitano  kuonekana kuwa serikali yake 
haikuanzisha vyama vingi   vya siasa 
kwa nia ya dhati  ya kuleta ushindani wa
kisiasa
kukomesha umaskini unaotafuna
mamilioni  ya Watanzania.
Mungu ibariki
Tanzania.
 
Note:
Nimeridhia yeyote anayetaka kuchapisha au kusambaza
andiko hili afanye hivyo.  Tuwasiliane: ananilea_nkya@yahoo.com

Ananilea Nkya
 E-mail:ananilea_nkya@yahoo.com

--
Send
Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda

wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com 
Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:

Everyone posting to this Forum bears the sole
responsibility
for any legal consequences
of his or her postings, and hence

statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree
to this
disclaimer and pledge to abide by
our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are
subscribed to the
Google Groups
"Wanabidii" group.
To unsubscribe
from this group and stop receiving emails

from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit

https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda

wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com 
Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to
this Forum bears the sole responsibility for any legal
consequences of his or her postings, and hence statements
and facts must be presented responsibly. Your continued
membership signifies that you agree to this disclaimer and
pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message
because you are subscribed to the Google Groups
"Wanabidii" group.
To unsubscribe
from this group and stop receiving emails from it, send an
email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit
https://groups.google.com/d/optout.




--

Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

 

Kujiondoa Tuma Email kwenda

wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya
kudhibitisha ukishatuma

 

Disclaimer:

Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and
Guidelines.

---

You received this message because you are subscribed to the
Google Groups "Wanabidii" group.

To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment