Tuesday, 1 September 2015

Re: [wanabidii] Hotuba ya Dr. Slaa kwa Watanzania toka Hoteli ya Serena - Tarehe 1 Septemba, 2015

Kumbe ni huyu aliyekuwa akitwambia tule marimao kumbe alikuwa na kitu nyuma ya pazia.

Sasa ni zamu yake kula marimao

On Sep 2, 2015 5:54 AM, "fatma_elia via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com> wrote:
Elisa

Hebu tusubiri kwa vile Gwajima yupo huenda nae akatueleza kwa upande wake. Huu ni upande mmoja tu wa habari

Fatma
Sent from my BlackBerry® smartphone provided by Airtel Tanzania.

-----Original Message-----
From: "'ELISA MUHINGO' via Wanabidii" <wanabidii@googlegroups.com>
Sender: wanabidii@googlegroups.com
Date: Tue, 1 Sep 2015 14:09:47
To: <wanabidii@googlegroups.com>
Reply-To: wanabidii@googlegroups.com
Subject: Re: [wanabidii] Hotuba ya Dr. Slaa kwa Watanzania toka Hoteli ya
 Serena - Tarehe 1 Septemba, 2015

Hii ndiyo hatari ya kukariri kapengele kamoja au mstari mmoja. ukitaka kuelewa unasoma paragraph . Swala la maaskofu alikuwa anaeleza alichoambiwa na Gwasma hivyo mashehe hawaingii
--------------------------------------------
On Wed, 9/2/15, Neatness Msemo <nmuzeh@gmail.com> wrote:

 Subject: Re: [wanabidii] Hotuba ya Dr. Slaa kwa Watanzania toka Hoteli ya Serena - Tarehe 1 Septemba, 2015
 To: wanabidii@googlegroups.com
 Date: Wednesday, September 2, 2015, 12:06 AM

 Ameonyesha udini
 kuchochea kuwa maaskofu wamehongwa anataka waislam wajione
 kuwa lowasa ni wakristo hii ni mbaya ametumwa tunamsamehe
 bure yaani hasira imezidi
 On Sep 1, 2015 11:49
 PM, "Neatness Msemo" <nmuzeh@gmail.com>
 wrote:
 Nadhani ni vema sana kuangalia kwa makini kwani
 pamoja na ukweli au uongo wa anayezungumza  je chanzo cha
 haya yote source yake ni hasita au kukosa au nia yake ni
 kumwaga mboga lakini watanzania wamechoka kwani hakuna
 msafi
 On Sep 1, 2015 11:01
 PM, "'mpombe mtalika' via Wanabidii"
 <wanabidii@googlegroups.com>
 wrote:
 Slaa:
 Watanzania wana kiu ya kujua kwanini amekuwa kimya kwa muda
 mrefu sasa licha ya
 harakati za kisiasa kuendelea.



 Muda utakaotumika ni saa moja, hakuna muda mrefu sana.

 Ameamua kufanya hayo kwa kuwa imefika mahali ukweli lazima
 usemwe na
 upotoshwaji ukomeshwa. Namna pekee ya kufanya hivyo ni
 kutoka hadharani na
 kuusema ukweli.





 Sote
 tunafahamu kuwa hana tabia ya kuchenga mambo, mengi
 yamesemwa na watu tofauti,
 kwenye mitandao, magazeti na viongozi wake! Hana ugomvi na
 kiongozi yoyote, kwa
 kuwa siasa sio ugomvi. Kama binadamu wa kawaida hana chuki
 wala hasira na
 binadamu mwingine yoyote!



 Iwe wazi kuwa katika Taifa kuna misingi ambayo inaongoza
 taifa. Inapofika
 mahali taifa linaongozwa kwa msingi ya propaganda na
 upotoshwaji matokeo yake
 ni vurugu kubwa katika taifa. Yeye amekataa hayo yote!



 Anasema kuwa YEYE hakuwa likizo kama inavyosemwa na viongozi
 wake! Atafafanua
 kwa kifupi! Kilichotokea ni kuwa aliamua kuachana na siasa,
 tarehe 28 Julai
 2015, majira ya saa tatu usiku, baada ya kuona yanayofanyika
 ndani ya chama
 chake hayamridhishi.



 Kinachosemwa ni kuwa Dr. Slaa alishiriki tangu mwanzo kwenye
 mchakato. Anasema
 ni kweli alishirii kwenye majadiliano, akaweka msingi na
 msimamo wako. Kuna
 wakati wengi wanashinda kutokana na wingi wao, wewe
 unayeamini katika misingi
 inabidi uachie ngazi.



 Baada ya Edward Lowassa kukatwa na CCM Dodoma, Mshenga wake
 alimpigia simu na
 kuuliza nini kifuate baada ya tukio la dodoma. Akamuambia
 wawasiliane na
 mwenyekiti Freeman Mbowe, Gwajima nae akafika kwenye kikao
 hicho.



 Msimamo wa Slaa ni kuwa ni lazima kumsikiliza mtu kabla ya
 kuamua nini cha
 kufanya. chadema ni cham cha siasa na hakiwezi kumkataa mtu
 yeyote kujiunga na
 chama.Wakaweka vijana kuchunguza nini wanataka hao wanaotaka
 kujiunga na chama!



 Slaa akataka kwanza Lowassa atangaze kutoka kwenye chama
 chake alichopo, kisha
 atangaze anakwenda kwenye chama gani. Atumie nafasi hiyo ya
 mkutano huo
 ajisafishe na tuhuma zote ambazo amekuwa akituhumiwa na
 watu.



 Chadema ni cham ambacho kwa muda mrefu kimejijenga kwa
 msingi, na ni lazima
 wapokee mtu ambaye hawezi kukichafua chama chao. Lowassa
 hakutangaza kujitoa,
 wala kujisafisha hadi kwenye mkutano ambao uliandaliwa na
 chadema. Slaa
 hakuhudhuria ule mkutano.



 Kwenye kila jambo kuna jambo la kuzingatia. Mtu anayejiunga
 popote anakuja kama
 mtaji au kama mzigo? Lowassa anakuja chadema kama asset au
 liability? Ijulikane,
 suala sio urais! Mpaka siku hiyo Slaa hakuwa amechukua fomu
 ya Urais kwenye
 chama chake. Slaa hakuwa anamzuia Lowassa kugombea urais
 chadema. Alitaka
 mgombea mwenye sifa na uwezo wa kukitoa Chama cha
 Mapinduzi.



 Hakutamka popote kuwa anataka kugombea, hata 2010
 hakugombea, aliombwa
 kugombea! Urais wake binafsi hauwezi kuikomboa nchi bila
 mchango wa jamii
 nzima.





 Mwafrika,
 [01.09.15 15:45]

 Suala la adha Lowaasa ni msizo au mtaji halikujibiwa hadi
 siku ya mkutano
 tajwa. Wakataka kujua anapokuja anakuja na akina nani, ni
 wafuasi wa aina gani;
 vijana wa bodaboda, vijana wasio na ajira au watu
 waliosombwa tu, au wanakuja
 kwenye mapambano?



 Jibu lilikuwa ni kuwa tungepata wabunge 50 na wenyeviti wa
 CCM mkoa wasiopungua
 22, wenyeviti wa CCM wilaya 88. Slaa akakiri kuwa kama ni
 hivyo kutakuwa na
 tetemeko (la kisiasa).



 Wakahitaji majina ya hao waliotajwa kwa kuwa walikuwa kwenye
 mchakato wa
 kupitisha majina kwenye chama. KAtibu mkuu makini huwezi
 kuchukuwa watu usiowajua.
 Hakuna jina nililopewa mpaka tarehe 25.



 Tarehe 25 wakamfata na kumuambia aitishe Kamati Kuu ya
 chama. Akakubali lakini
 akatahadjharisha kuwa hajapata majina na hajapata jibu kuwa
 Lowassa ni asset au
 liability. Lakini akaitisha kikao kwa kuwa ni jukumu la
 kikatiba la katiba.

 Mwenyekiti akapiga simu, anasikia kuwa hajaridhika. Tangu
 2004 Slaa hajawahi
 kugombana na mwenyekiti wake, isingekuwa sawa kama
 wangetofautiana kwenye kikao
 rasmi.



 Wakakutana na Mwenyekiti, Gwajima, Lissu na wakajadiliana
 mpaka saa 9 mchana.
 Maneno kuwa alikuwa anakubaliana na mpango huo tangu mwanzo
 SI KWELI!

 Mkutano ukashindikana. Wdau wakasema waende nyumbani kwa
 Lowassa, Slaa akakataa
 wakaenda Kamati kuu.



 Kikao kikafanyika hadi saa 12 jioni. Ikaundwa kamati ndogo
 ya kumshawishi Slaa.
 Akakataa! Akaandika barua ya kujiuzulu kwa kamati, Prof.
 Safari akaichana barua
 yake. Akaandika barua nyingine kwa Makamu-Zanzibar, makamu
 akamuambia kuwa haya
 mambo yamepangwa, asijisumbue!



 Wanasema siasa ni mchezo mchafu, yeye anaaamini kuwa siasa
 ni sayansi! Asubuhi
 ya kesho akaandika barua, wasichojua ni kuwa kujiuzulu
 hakuhitaji barua. Maneno
 yakazuka kuwa Slaa hajaandika barua! Upotoshwaji ukaendelea
 kuwa Slaa
 atazungumza na waandishi wa habari, wengine wakasema
 amefungiwa, amefungiwa na
 mkewe na kadhalika! Ukweli ni kuwa alikuwa na Lissu, Gwajima
 na Mbowe tangu
 asubuhi.



 Maamuzi aliyoyafanya yanatokana nadhamiri yake! Josephine
 nae ni mwanaharakati,
 ana sababu ya kuwa na uchungu. Alipigwa mwaka 2011 wakati
 wengine walijificha!
 Propaganda hizo tumeshazisoea!



 Kama kuna mwenye ushahidi wa propaganda hizi aje, audited
 report zipo!
 Josephine halipwi na chama! Watu wanasema kuwa Slaa analipwa
 mil. 7, yeye
 ameendelea kula mihogo na maharage kama walivyoahidi mwaka
 2010. Wana uchungu
 na harakati!



 Kikubwa katika harakati ni credibilty, jina la chama
 kilichojengwa kwa muda
 mrefu kisichafuliwe kwa namna yoyote! Mwanasiasa yoyote
 hataki kuchaguliwa, na
 Slaa nae hataki kuchaguliwa! Wanasema kuna maslahi mapana ya
 taifa, ni nani
 anayapima? Lazima kuwe na kipimo cha kuapima hayo maslahi
 badala ya kutegemea
 mtazamo wa mtu!



 Anafafanua suala la liability sasa!



 Wamekuwa waongo kwa kuwa hakuna kipengele hata kimoja cha
 madai ya Slaa
 kimetekelezwa. Alisema wabunge waje kabla ya kura ya maoni
 ya CCM, kuja baada
 ya hapo ni kutafuta kichaka cha kujificha!



 Watanzania wameijenga Chadema kwa damu yao, rasilimali zao!
 Watu hawawezi
 kukimbilia kirahisi wakati sio wasafi, akiwemo Sumaye na
 wengine. Nani hajua
 kama Sumaye ni fisadi? Kwa muda mrefu Slaa haongei na Sumaye
 kwa kuwa
 alimtuhumu kwa ufisaidi.



 Sumaye ni mtu ambaye wanahabari walidai kuwa Sumaye alisema
 kuwa atahama chama
 endapo Lowassa atateuliwa, leo akageuka! 
 Leo anamsafisha Lowaasa, dhambi haisafishwa kwa
 dhambi. Anakumbusha jina
 la Mr. Zero (jina la utani la Sumaye).  Chama
 kimepokea makapi, na katibu alitahadharisha kuwa chama
 hakipokei makapi! Hakuna
 ambaye alijitoa kwa hiari, wengi walikuja baada ya kukatwa.
 Wenyeviti wengi ni
 mzigo, akiwemo Msindai.



 Anangoja ajibu amlipue hadharani kwa kuwa alikuwa mwenyekiti
 wa kamati ya bunge
 hesabu za serikali z mitaa. Siku aliyoambiwa aitishe kamati
 kuu aliuliza
 majina, akaambiwa anakuja chizi! Chizi ni nani, hata nyie
 hamumjui! Anaitwa
 chizi kwa kuwa ni mwizi wa kura ndani ya CCM.



 Kuna haja gani ya kushindana kama tunampango wa kuiba kura
 pia. Wakamtaja
 Guninita, nani asiyemjua udhaifu wake? Hawezi kuandika hata
 ukurasa mmoja wa
 ripoti, amehama vyama mara kadhaa!



 Mwafrika, [01.09.15 15:45]

 Viongozi wa Chadema wamepata kigugumizi, waseme nani
 ameongeza thamani kwenye
 chama? Najua maneno ya kuwa ni lazima kuiondoa CCM kwanza
 hata ikibidi tuweke
 mkataba na shetani, mimi ni padre wa Kanisa Katoliki!
 Kuwaondoa CCM kwa namna
 yoyote hakuleti maendeleo. CCM itaondolewa kwa program
 siriaz, sio kutumia watu
 wale wale!



 Lazima tujue nini kilifanya Watanzania waamini chadema, kwa
 kuwa waliamini wana
 misingi isiyoyumba na uadilifu. Leo tunasimamia uadilifu?
 Wanasema mwenye
 ushahidi aende mahakamani. Kama tusingewatuhumu Mramba na
 Yona wasingefikishwa
 kizimbani. Chadema imefungwa mdomo kwa kisingizio cha
 ushahidi!



 Ni bora kukaa kimya kuliko kupotosha. Anasema nukuu ya
 biblia kuhusu
 wapotoshaji! Inapofika mahali unapoambiwa hakuna mwenye
 dhambi ni makosa,
 dhambi haisahihishwi kwa dhambi nyingine! CCM wamekuwa
 waoga, wamewalea watu
 hawa kwa muda mrefu!



 Kwa Wafrika choo ni neno baya, kwa wazungu choo ni rest
 room! Choo cha
 Kitanzania huwezi kukihamisha ndani ya chumba cha kulala na
 ukakiita choo,
 huwezi kulala kwa kuwa kitanuka, tena zaidi! Ufisadi ilikuwa
 ajenda iliyowapa
 umaarufu CHADEMA, leo wamewachukua. Waanweza kuwa na ujasiri
 wa kukemea
 ufisadi?



 Mwaka 2008 Slaa alikuwa bungeni wakati wa sakata la
 Richmond, anafahamu kwa
 uzuri anachokimaanisha. Bahati mbaya waandishi hawasomi
 makaratasi, na wabunge
 wa CCM pia.



 Lowassa hatuhumiwi kwa habari ya Richmond pekee! Lowassa
 aliambiwa na Slaa
 aache kulalamika, atangaze uhalali au uharamu wa Richmond,
 anamtaka aseme hao
 'wakubwa' ni akina nani? Ni afadhali sifa yake
 iharibike kuliko kusema uongo.



 Ni aheri kupotea kwenye siasa za dunia kuliko kusimamia
 uongo! Msingi wa kwanza
 wa Richmond: Ili uelewe ni lazima urudi kwenye taarifa ya
 Kamati ya Mwakyembe,
 Slaa alifuatwa asubuhi ya siku ile kupewa rushwa, anashuru
 Sitta na Mwakyembe
 wajitokeze!



 Akamuuliza mtoa rushwa kama anatoa m.500 kwa mbunge, atakuwa
 nazo ngapi?
 Aliwaambia Sumaye na Lowassa kuwa rushwa ni jambo
 linaloanzia kifuani kwanza.
 Mwanzo wa jambo hili ni taarifa ya Baraza la Mawaziri la
 10.2.2006. Kamati ya
 mwakyembe iliangalia faili la kikao kile kisha kuandika
 ripoti!



 Suala hili lilianzia wakati wa utawala wa mkapa kutokana na
 dharura ya umeme
 nchini, wakawasiliana na kampuni moja ya Amerika Kaskazini
 kwa suluhu ya muda
 mfupi ya umeme. Serikali ya Kikwete ikapokea lile suala.
 Wakaruhusu mpango uendelee,
 ila kwa kufuata sheria. Hiyo ilikuwa kauli ya Baraza la
 Mawaziri!



 Wakati auala lile linaamuliwa, Lowassa alikuwa Waziri Mkuu!
 Na ndie mwenye
 mandate ya maamuzi ya Serikali, iweje leo akane kuhusika?
 Taarifa ya Mwakyembe
 inapotoshwa! Taarifa ilitaka Waziri Mkuu ajipime, au bunge
 limjadili na
 kumchukulia hatua. Lowassa akakimbia kwa kuwa alijua Bunge
 lingemfukuza kazi!



 Waliioomba tenda walikuwa 26, waliorudisha walikuwa 8.
 Kamati ya Tathmini
 ikaona hakuna anayefaa hata mmoja! Waziri Msabaha akaagiza
 taarifa ile ifutwe
 na tathmini ifanyike upya, mara ya kwanza, ya pili, ya tatu
 na ya nne. Jeuri wa
 Msabaha ilitoka wapi? Baraza likaamua baadaye tenda
 iliyopewa kwa kampuni ya
 kwanza ifutwe! Lowassa alishiriki!



 TANESCO wakatoa ushauriwa wao, Mamlaka husika ikatafute
 internatonal tender ya
 kununua turbine! Lowassa akaingilia mchakato dakika za
 mwisho, akamuagiza
 katibu muhtasi wake!



 Kwanini Lowassa, kwa kuwa anagombea urais, rais asiyeaminika
 hawezi
 kuchaguliwa!

 Lowassa alishawahi kumuita Slaa kuhusu habari ya Meremeta,
 na kumuambia kuwa
 taarifa yake inaiaibisha Serikali! Kampuni ya jeshi imewahi
 kutengeneza gari,
 imehujumiwa na wahuni. Akamtaka Lowassa amuambie ni nani
 aliyehusika?



 Akamuita mwingine kwnye Speaker lounge. Slaa akamuambia kuwa
 yeye ni fisadi
 kichwani, rohoni mpaka...!



 Tunamsifia Lowassa kuwa an=taleta maji wakti jimbo la
 Lowassa halina maji na
 ufisadi mkubwa umefanyika kwneye jimbo hilo. Mnazungumzia
 shule za kata wakati
 wakati hamjua zimeanza wapi? Slaa anataja nafasi alizowahi
 kushika Afrika.
 Uamuzi wa kujenga shule za kata ulifikiwa mwaka 90 huko
 Thailand, mpango huo
 ukaitwa Education for All, sio MMES kama unavyoitwa leo!



 Mwafrika, [01.09.15 15:45]

 Anasoma barua ya Ibrahim Msabaha kwa Flugence Kazaura,
 mkurugenzi wa bodi wa
 TANESCO!



 Mpango ulikuwa kuondoa suala la umeme mikononi mwa tanesko
 kwa kuwa imeshindwa
 kutekeleza. Ugomvi wake na Masha ni kwa kuwa Lowassa
 alimlaumu Masha kuingilia
 mchakato wa serikali, akawekewa kinasa sauti chumbani.
 Waziri Mkuu haruhusiwi
 na sheria kuingilia mchakato wowote wa tenda.



 Kwenye kampuni nane zilizowasilisha maombi ya zabuni,
 Richmond ni kampuni
 iliyokuwa mbovu. Ilikuwa ni kampuni ya steshenari, sio
 umeme!Wakadai wana
 ushirikiano na kampuni nyingine ya umeme, kampuni hiyo
 ikakataa kujihusisha na
 Richmond, wala kuzalisha na majenereta!



 Bill Clinton aliwai kukutwa na kashfa, walitaka kumchukulia
 hatua si kwa sababu
 ya zinaa, bali kwa kuwa alifanya uongo! Kwa kuwa alidanganya
 umma! Hata sheria
 za Tanzania zinakataza kuongopa, hata kesi za uchaguzi za
 Slaa zimethibitisha
 hilo.



 Lowassa anadai yeye alisimamisha tenda, Slaa anaonesha
 uthibitisho wa hilo kwa
 barua za Lowassa kwenda kwa Msabaha zinazokanusha hilo,
 'Anaisoma'! Waziri Mkuu
 aliharakisha mchakato wa tenda, tofauti na sheria ya PPRA.
 Barua imeandikwa
 miezi mitatu baada ya mkataba kusainiwa, kwa maagizo ya
 Waziri Mkuu.



 Tanesko ikaagizwa kusaini mkataba ambao haikuhusika kwenye
 kuujadili! Anaona
 aishie hapo... Anaupigia chapuo mdahalo wa Sitta na
 Mwakyembe, anasema Lowaasa
 nae afike kuondoa utata na kusema ukweli!



 Chadema ni chama kilichotoa matumaini kwa vijana wengi!
 Isifike mahali tukawa
 washabiki kama 2005 ambapo watu waliahidiwa maisha bora,
 wakajikaanga kutokana
 na ushabiki! Anatoa ushahidi wa kitakwimu wa mfumuko wa
 bei...



 Slaa ana uchungu kuona chama alichokijenga, kikifikia hatua
 ya kusomba watu kwa
 mabasi na malori kisha mkasema mafuriko hayazuiliki! Hayuko
 tayari,... Anakataa
 kuwa ZEZETA! Ajenda ya Chadema ni nini, ilikuwa ni rushwa!
 Wananchi waliamini
 kwa kuwa msingi huo ndio unakijenga chama!



 Sehemu kubwa ya kilichosemwa Jangwani ni ilani ambayo
 ilishaandaliwa tayari,
 hakuna kipya kilichosemwa. Kinachomuuma ni chama makini kuwa
 kibovu zaidi ya
 Chama cha Mapinduzi! Hatuwezi kujenga maadili tukiwa na watu
 wachafu, anaishi
 na mwanamke bila kufunga ndoa kwa kuwa Serikali ya CCM
 haitaki afunge ndoa.
 Kesi yake ililetwa na mawaziri, waandishi wa habari na mtu
 kutoka IKULU. Ndoa
 inafungwa na Mungu!



 Scotland Yard iliamrisha Lowassa achunguzwe, inakuwaje leo
 tunamtetea? Huu ni
 ushabiki usio na vielelezo, Slaa ana ushahidi! Hakuna
 ulazima wa kwenda
 mahakamani kwa kuwa kesi ya rushwa ni jinai, ni kesi ya
 serikali! Slaa au
 mwingine hana locus ya kwenda mahakamani kwa kesi ya jinai!
 Mwakyembe alisema
 kesi ya jinai haina mwisho (kama zilizyo za madai). chadema
 iliahidi kusafisha
 nchi kwanza endapo itashika dola, huku maendeleo
 yakiendelea!



 Anasoma barua ya mchakato wa Richmond kuwa DOWANS. Kampuni
 imesajiliwa Costa
 Rica, na mwenyekiti asiye na anuani, simu wala jengo! Siku
 iliyosajiliwa,
 mmiliki alisajili makampuni mengine 99! Zaidi ya hayo ana
 makampuni mengine
 zaidi ya 50, DOWANS ni jina tu. Kampuni haipo! Dowans sio
 kampuni halisi huko
 Kosta Rika, nchi nzima hakuna kampuni yenye uwezo wa
 kuzalisha umeme kwa
 kiwango hicho!



 Leo Lowaassa anatuambia tufunge mdomo, huu ni udikteta!
 Anakumbusha sakata lake
 na Waziri Marmo... Mabilioni ya fedha yanalipwa kwa kampuni
 ambayo haipo!
 Tunapenda ushabiki... Acha sifa iharibike!



 Anasema hataki kuingia kwenye mambo ya Babu Seya! Vyuo vikuu
 vinatumia kesi ya
 Babu Seya kama case study. Mtoto mdogo hawezi kutoa ushahidi
 mahakamani, haki
 inapuuzwa kwa kuwa mtoto hawezi kutoa ushahidi!



 Kesi ya Ulawiti rais hana mamlaka nayo, anatoa wapi kiburi
 cha kusema kuwa
 atamtoa? Aliyeagiza polisi kuingia na polisi kuingia na mbwa
 msikiti wa
 mwembechai ni Sumaye, akiwa waziri mkubwa. Leo hii ni mpiga
 kampeni wa Lowassa!
 Leo tunataka kura kwa namna yoyote! Ni afadhali kutokuwa na
 rais wa aina ya mtu
 huyu! anayesaka kura kwa kusaka huruma za watu. Slaa hayuko
 tayari kuona hilo
 linatokea... Anahitimisha kwa kusema hajagusa chochote
 kuhusu ilani wala
 mkakati!



 Mwafrika, [01.09.15 15:45]

 Kama taifa tuna kazi kubwa ya kuchambua vitu nje ya
 shamrashamra, maneno
 matamu! Tumeshaumwa na nyoka, tusilaghaiwe na maneno ya watu
 hawa tena! Utendaji
 uliotukuka unapimwa kwa utafiti, sio kwa ukasuku na kunukuu
 maneno ya
 wanasiasa!



 Lowassa alipokuwa Waziri Mkuu, matatizo ya wakulima na
 wafugaji yalikuwepo,
 alifanya nini? Lowassa aliwahi kubadili mpaka wa Monduli na
 Karatu na
 kusababisha mgogoro! Mkampenia wake, Sumaye alisababisha
 matatizo ya ardhi
 Mvomero, akipora ardhi ambayo ilitakiwa yajengwe makao makuu
 ya Mvomero!
 Mengine ya Sumaye ameyaweka kiporo, hisa zake za kampuni
 aziweke wazi kama
 Sekretarieti ya Maadili inavyotaka!



 Kutotangaza mali kunatosha kumtoa mtu ubunge! Sembuse
 Urais?



 ============================== =========================



 Ukweli huwa una tabia ya kuegemea upande, anasemea
 speculation kuwa ameisema
 chadema peke yake. Anasema amestaafu siasa, hana chama
 lakini bado anabaki kuwa
 mtanzania, mtetezi wa wanyonge na atabaki hivyo! Ataendelea
 kuwatumikia
 watanzania kadiri ya Mungu alivyomjalia vipawa! Kama
 alivyoombwa kugombea urais
 2010!



 Anaweza kuwatumikia Watanzania bila kuwa na chama!



 Anasema kuwa hajapata vitisho kama alivyopata kipindi hiki,
 inazidi hata wakati
 alipotangaza List of Shame. Rostam ndiye anafadhili kampeni
 za urais wa
 Lowassa! Anamnukuu vitisho vyake! anakiri kuwa maaskofu
 wamehongwa, Rostam
 akiwa anaona, m60-m300! Anasema hatenda chama chochote,
 anasisitiza! Amejitoa
 rasmi siasa za vyama vya siasa... Ataendelea kuwa msimamiaji
 wa anachokiamini!



 Anawataka watu aliowataja watoke hadharani, anatoa baraka za
 KIMUNGU kwa nchi
 na watu wake!



 MASWALI!



 Swali: Unawammbia nini Watanzania kuelekea uchaguzi, ni rais
 yupi anafaa?

 Amesema hana chama, hampigii kampeni mtu yoyote! Amesema
 anafanya uchambuzi wa
 madhara ambayo taifa litapata endapo watamchagua Lowassa, na
 kwa kuwa na uzoefu
 nao kwa muda mrefu!



 Hataki kufanya kampeni yoyote. Anawaelimisha Watanzania
 kuacha ushabiki
 utakaowagharimu! Ni watu wachache wanoweza kumtaja mtu kwa
 majina, kuna tofauti
 ya wanaotaja ajenda tu na wanaotaja majina.



 Rostam alimuambia kuwa ana dakika 5 za kuishi, apige magoti
 na kusali! Aliweka
 roho yake rehani kwa ustawi wa taifa hili...Anakumbusha ya
 Mwembeyanga na namna
 Usalama wa Taifa walivyokuwa na tension. Magazeti mengi
 yaliogopa hata kuandika
 habari, isipokuwa MWanaHalisi!



 Swali: Siasa ingekuwa asset kama angekuja na wabunge kadhaa.
 Angekuja kama asset,
 mengine yangesafishika? Kulikuwa na vigezo viwili, ama asset
 na liability,
 yaani hayo madhambi yote aliyoyasema. Baada ya hayo
 wangefanya tathmini kama
 anapokelewa au hapokelewi. Anatoa mfano wa Shirikisho la
 Afrika Mashariki na
 nchi zinazotaka kujiunga!



 Swali: Waliopokelewa ni makapi. Je wewe ulikuwa kapi 95?



 Anauliza kama watu wanaamini yeye alikuwa kapi? Tupime
 vigezo... Makapi ni watu
 waliokataliwa na watu wao baada ya kuwa wabunge kwa muda
 mrefu. CCM wakasema
 kuwa hakuwa mwenzao: hakuwa anahonga, hakuwa anapokea rushwa
 na kadhalika! Kuingia
 kwa tiketi ya Chadema ulikuwa ukombozi kwake!



 Swali: Umetangaza kustaafu siasa, una kadi za vyama viwili.
 Unazirudisha au
 unakaa nazo?



 Watanzania tuelimika, kadi sio uanachama. Kadi ni mali ya
 mwanachama, unaweza
 kuichoma, kuweka kumbukumbu au vyovyote, sawa na kadi ya
 ndoa ambayo
 hairudishwi hata kama ndoa itavunjika. Tuulize maswali ya
 kujenga.



 Swali: Anaoneka baada ya kukosa urais anamshambulia
 Lowassa!



 Wapi Slaa alichukua fomu ya Urais, hakuwa na nia na urais
 wala hawezi
 kukasirika. Tuache ushabiki, tuwe na mtiririko na kuzingatia
 hoja! Mwandishi
 awe msikivu sana... Ameeleza tangu mwanzo, hana chuki wala
 ugomvi na mtu
 yoyote!



 Chama cha Mapinduzi kilishakuja kumpa ofa kadhaa kuachia
 jimbo la Karatu, akaweka
 sharti la mkataba wenye sahihi za watu watatu; Rais, Slaa na
 Yesu Kristo.



 Swali: Kama wewe uliweza kuhama, wengine nao hawawezi?



 Dr. Slaa hakuwa na uchafu wowote, tatizo halikuwa kuhama
 chama, tatizo ni watu
 wa aina gani wanahama chama?



 Swali: Unahamasisha uwazi, mbona wewe umemficha muovu mmoja?


 Silaha haziwekwi zote mezani, amewaomba anaowatuhumu
 wajitokeze!
 CHANZO kwa hisani
 ya jf






 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com
  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.






 --

 Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

  

 Kujiondoa Tuma Email kwenda

 wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya
 kudhibitisha ukishatuma

  

 Disclaimer:

 Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
 for any legal consequences of his or her postings, and hence
 statements and facts must be presented responsibly. Your
 continued membership signifies that you agree to this
 disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.

 ---

 You received this message because you are subscribed to the
 Google Groups "Wanabidii" group.

 To unsubscribe from this group and stop receiving emails
 from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

 For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment