Tuesday, 22 September 2015

Re: [wanabidii] CCM WANAJIDANGANYA

Kuna mtu alisema maswali haya hayatajibiwa. nimeamini ukweli huo. Nimemkumbuka marehemu Horace Kolimba. Alikuwa akiulizwa sawali akianza kujibu anatumia maneno mengi kutojibu swali.
--------------------------------------------
On Tue, 9/22/15, 'ananilea nkya' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

Subject: Re: [wanabidii] CCM WANAJIDANGANYA
To: wanabidii@googlegroups.com
Cc: "mabadilikotanzania@googlegroups.com" <mabadilikotanzania@googlegroups.com>
Date: Tuesday, September 22, 2015, 1:09 AM

Mwalimu Malata 
Nianze  kwa kukushukuru  kwa kusoma makala zangu
ninazoweka   kwenye jukwaa hili la
mabadiliko.  Niwashukuru pia  wengine wote 
kwa kusoma na kuchangia hoja niliyoandika kuhusu CCM
kujidanganya.

Mwalimu Malata nashukuru  kwa  maandishi
yako  ambayo  uliyosema   ni
maswali. Lakini  nilipoyapitia  mengi 
hayakuwa ni maswali  kwa 
sababu   kama umekuwa ukisoma 
hoja  ambazo nimekuwa nikiandika humu jukwaani tangu
kampeni za uchaguzi zianze,   usingeuliza
maswali haya. Hata hivyo sikulaumu sana  hii ndiyo
shida ya  bora elimu ambayo   Watanzania
wamekuwa wakiipata.

Ninachokushauri, hata kama wewe ni mwanachama wa CCM au
chama kingine cha siasa, ni vema  ukasoma na kutafakari
kwa kina  hoja zinazoandikwa na watu mbali mbali
humu  jukwaani  maana zitakusaidia kupata upeo
kama kweli wewe ni mwalimu  na kama unaamini kwamba
Tanzania inahitaji  mabadiliko  ya 
uongozi   vinginevyo haya mafuriko ya
wananchi maskini  yaliyotengenezwa na serikali ya CCM
yakiachiwa  kuendelea kuzalishwa  kutahatarisha
amani ya nchi yetu  tuendako. 
Nimejibu  kama ifuatavyo:

(A) Umesema "…Chama cha Mapinduzi (CCM) na 
serikali yake  wanapaswa  wasijidanganye 
kwamba kwa kumteua Dr John Magufuli kuwa mgombea  wa
Urais  chama hicho kimekuwa kisafi..."
1.      Je, usafi na AU uchafu wa chama
unatokana na nini?
      Jibu:   Usafi au uchafu
wa chama cha siasa unatokana na misingi ambayo chama
kinakuwa kimejiwekea.  Kwa mfano CCM  zama za
Mwalimu Julius Nyerere iliweka Azimio la Arusha kama msingi
wa kujenga usafi  wa wanachama na viongozi . 
Lakini  baada ya Mwalimu  kuondoka
madarakani  CCM ilizika  Azimio la Arusha na hivyo
kiliagana na  usafi kikaanza kukumbatia uchafu. 
CCM ya leo haiamini tena katika usafi uwe ni wa wanachama
wake mmoja mmoja  au chama kizima. Tangu CCM
kilipozika   azimio la Arusha --kilizika
misingi yake ya usafi na kikaasisi misingi ya
uchafu—ufisisadi, rushwa na ubabe na ndiyo sababu 
kwa kuwa ndicho kimekuwa kikiongoza serikali  nchi
nzima sasa inanuka uchafu wa ufisadi na
rushwa.   Kibaya zaidi  CCM iliondoa
Azimio la Arusha  bila kuweka  kitu kingine badala
yake. Hata  wananchi walipoamua  kuandika Katiba
Mpya inayotokana na maoni yao kama mbadala wa  Azimio
la Arusha serikali ya  CCM  imekataa hiyo 
Rasimu ya Katiba na iliizika
rasmi pale Dodoma mwaka jana 2014 tena  kwa kufanya
ufisadi mchana kweupe kwa  kuwalipa wanaCCM wajumbe wa
Bunge la   kila mmoja shilingi laki tatu kwa
siku   kwa siku karibu mia moja. 
Tangu   kuzikwa Azimio la Arusha, kila 
wakati CCM ilipochaguliwa kuingia madarakani serikali yake
imekuwa inafanya ufisadi kwa sasabu CCM na serikali yake
ndiye mnufaika wa ufisadi.  Kumbuka  mfano ufisadi
wa EPA,Meremeta, Richmond na Tegeta escrow.   
Kadhalika tangu kuzikwa kwa azimio la
Arusha   kulikoiondoa CCM kwenye usafi na
kukipeleka kwenye uchafu,  wananchi wengi ambao wanajua
shughuli zao  siyo safi vya
kutosha   wanaingia  CCM. Mtu ukiwa ni
mwanachama wa CCM hata kama unapata fedha kwa njia chafu
wewe uko salama-utalijwa na hakuna mashtaka yatakufika hata
kama umehusika kwenye ufisadi.  Kama huamini 
angalia  mawaziri waliohusika na Tegeta escrow kwa
ushahidi kabisa mwaka huu wanateuliwa kugombea ubunge
CCM  na wananadiwa kama vile hawajawahi kuhusika na
ufisadi.
Lakini  hata kama una tuhuma tu  za
kupakaziwa  kama vile Edward Lowassa ukithubutu
kujiunga na chama cha upinzani  utaiona jehanamu ya
moto.  Hivyo watu wengi wako CCM kimaslahi zaidi si kwa
vile chama hicho ni chama kisafi makini kinachotetea maslahi
ya mamilioni ya Watanzania.   Watu wengi
wako  CCM  wasitiwe misukosuko hasa kama wanataka
kupata   utajiri wa haraka  iwe 
ni  kupata tenda  za miradi  kutoka serikali
ya CCM  au uongozi ili  kujitajirisha  huku
mamilioni ya wananchi wakibaki maskini. Lakini subiri baada
ya tarehe 25 Oktoba, kama  mamilioni ya
Watanzania  maskini ambao  serikali ya CCM 
imewazalisha baada ya  kuacha misingi ya  kuongoza
nchi kwa usafi  wataamua   kuiondoa
CCM  madarakani—utaona jinsi CCM itakavyokufa 
kutokana na kukimbiwa na wanachama maslahi.
2.      Kwa mtazamo wako CCM si kisafi?
Ulitegemea CCM wafanye nini ili kuwa safi katika kipindi
hiki kuelekea uchaguzi mkuu?    Jibu: soma majibu
ya swali No 1.
3.      Je, Unaamini katika
"KUJISAHIHISHA"?   Jibu: soma majibu
swali No  1.

(B)        Umesema "…Hivyo hakuna
mamtiki yoyote kwa CCM kutumia propaganda kwamba  kwa
mgombea wake wa Urais  kupata watu kwenye mikutano
ya  kampeni basi  tayari kimeshinda kwa asilimia
69.3…… Kama  umati wa watu  ndicho
kigezo  cha ushindi  wa  CCM ….".
1.      Bila shaka ni wazi kuwa unatambua
kuwa CCM ni taasisi na si kijiwe cha wahuni. Kwa maendeleo
endelevu ya Taasisi yoyote ni budi iwe na idara/kitengo
maalumu kwa ajili ya M & E. N a kama taasisi bila shaka
CCM ina "policy kuhusu namna ya kutathimini mwelekeo
wake.   
2.      Je ni dhambi kwa taasisi kufanya
tathmini na kutoa matokeo kwa umma?
Jibu: Kujitathmini siyo dhambi. Dhambi ni kujitathmini bila
kutumia vigezo vya kutoa tathmini ya ukweli. 
Watanzania  wanaojua  hali halisi  ya
umaskini unaowakabili  mamilioni ya Watanzania 
wanajua  hiyo  asilimia
69.3   ambayo CCM imejinasibu  kuwa
itapata  kwenye uchaguzi wa mwaka huu  2015 
haiwezekani  katika Tanzania ya leo  kama
uchaguzi  utakuwa  huru.   Kama
hiyo tathmini  ni ya kweli  leo  CCM 
katika kampeni zake  isingekuwa inatoa kauli
za   kutisha wananchi 
kwamba   vyama vya upinzani hasa
CHADEMA  ndani ya 
UKAWA   vikichaguliwa nchi  itaingia
kwenye machafuko. Au kauli  za kuweweseka
zinazotolewa  na baadhi  ya   na
viongozi waandamizi wa CCM  wanaposimama kwenye
majukwa   mchana kweupe   na
kusema  kwamba  katika jambo lolote ambalo CCM
haiwezi kufanya ni kuwapa wapinzani  nchi
waongoze.   Jiulize je nchi hii ni mali ya
CCM?   Ni kwa nini viongozi  wa
CCM  wanang'ang'ania madaraka  kama siyo 
madaraka hayo yananufaisha viongozi
wachache na kufukarisha wananchi?   Muhimu
zaidi jiuliza hivi chama cha siasa ambacho kimefanya utafiti
na kikabaini kweli kwamba  kuna kila dalili  ya
kushinda kwa asilimia 69.3  ni kwa nini basi kiwe na
wasiwasi  na kutoa kauli  za uvunjivu wa amani
na  kutaka kuvuruga uchaguzi? 
Kwa mwenye akili yake  ya kufanya uchambuzi 
atabaini kuwa  hizo data  ni propaganda 
na   pengine ni mbaya  kwa  chama
hicho  pengine kuliko 2010 ilipochakachua  kura za
Rais kwa zaidi ya wiki mbili. Hivyo inachokifanya sasa ni
ufisadi wa maneno kutisha
wananchi   wasijitokeze kupiga kura. Lakini
CCM wanajidanganya maana Watanzania wengi wa leo
HAWADANGANYIKI   kama  wameamua kufanya
mabadiliko ya uongozi wan chi yao hapo tarehe 25 Oktoba
mwaka huu 2015.  Watavaa kanga, kofia, fulana, watakula
na kunywa, watapokea fedha n a hata  fedha za 
ufisadi wa Tegeta escrow zilizochotwa kwa tandarusi na
magunia  zikitumika kuwalipa  gharama za
kusafiri  kwenda  kuhudhuria mikutano ya kampeni
mikoa mingine  kujaza uwanja kutengeneza taswira 
ya kupendwa  watafanya hivyo, lakini tarehe 25 
watafanya maamuzi  --kubadilisha uongozi unaofukarisha
mamilioni na kutajirisha mamia kadhaa tu ya watawala.
3.      Una ushahidi gani wa kutuaminisha
kuwa CCM wametumia kigezo cha wingi wa watu katika kampeni
kutoa tathimini yao?  Jibu: soma hiyo taarifa ya CCM.
4.      Je  propaganda  ni nini na
kwa nini?  Jibu:  Ni kujifurahisha na kujihami)
5.      Je, unachokifanya ni sehemu ya hizo
propaganda au?   JIbu: Utakavyoona wewe . Una
haki ya kuwa na mtazamo na maoni yako sikuzuii)

(C)  Umesema "…Rais  Jakaya Kikwete katika
kipindi ccha utawala wake  amesafiri nje ya nchi mara
409  na safari hizo ziligharimu  shilingi 
trilioni 4.5……Maana yake angalao kila mwaka Rais
alisafiri nje ya nchi mara  40 akipoteza siyo tu fedha
alizotumia kwa safari hizo bali pia muda  mwingi wa
kuwatumikia Watanzania…."
1.      Katika maelezo yako hayo hapo juu,je
unaweza kutuainishia bajeti ya serikali kwa Idara ya Itifaki
kwa mwaka kuanzia mwaka 2005 hadi sasa?  Jibu: 
Kama una tofauti na hiki nilichoandika hapa  ni wajibu
wako kutuwekea hapa. Kama huna kaa kimya)
2.      Kama hujakurupuka na kumeza matango
poli kasha kuwatapikia watanzania kuhusu jambo hilo, Je
unaweza kutuaninishia  kutuainishia safari hizo na
bajeti yake kwa kila safari ili tujiridhishe na tarakimu
uliyotaja hapo? 
Jibu:   Soma   majibu No 
1 hapo juu. Kadhalika niongeze hapa kwamba  kwa wewe
mwenyewe  kutumia lugha chafu hapa unaendelea
kutuaminisha kuwa  hiyo tathmini ni ya 
kujidanganya  na kujenga saikolojia ya goli la mkono au
ufisadi wa maneno ili kuvuruga uchaguzi)
3.      Unaposema alipoteza muda wa
kuwatumikia watanzania kwa hizo safari, Je zilikuwa safari
zake binafsi [I mean was it for the personal issues/family
matter or for the sake of our
country?   Jibu:  Alipoteza muda wa umma
kwenda kuomba net  na kuchukua digrii za heshima ili
hali nchi yetu inawalipa mabalozi mishahara kufanya kazi
hizo.
4.      Ikiwa unaamini, kama mimi ninvyoamini
kuwa zilikuwa safari za kikazi; Je unaweza kuueleza umma wa
Tanzania Impact ya kila safari ya Mh.Raisi with reference to
matumizi kwa kila safari?  Jibu:  Madhara ya hizo
safari  ni  kutengenezwa kwa mamilioni ya
Watanzania maskini ambao ndio wamejiandaa kuing'oa CCM
madarakani hapo tarehe 25 Oktoba mwaka huu 2015.

(D) Umesema "…Je CCM  na  serikali ya CCM
yake  mwaka huu  2015  watatumia kwa 'goli
la mkono' kuzuia maamuzi  ambayo wananchi wa
Tanzania  watakuwa wamefanya  kupitia sanduku huru
la kura kuhusu hatma ya uongozi wa nchi yao …?"

1.      Napata shida kuitafakari kauri
(sahihisho hili neno linaandikwa kauli)  hii,Je
umetumia kigezo gani  kusema " ..watanzania watakuwa
wamefanya kupia sanduku huru.." Je tayari una majibu ya
jambo ambalo hatujalifanya? Kama hivyo ndivyo ni hatari sana
kwa kuwa ni sawa na mtu anayeingia uwanjani akiwa na matokeo
mkononi.Nini kitatokea ikiwa
atashindwa?   Jibu:  Inaelekea
hufuatilii kwa makini  kampeni za  chama chako
CCM  kusikia na kuelewa
wanachokisema.   Kama hukumbuki ni nani
aliyesema CCM itashinda kwa goli la mkono basi siyo kazi
yangu kukuelimisha hilo.
2.      Ikiwa na wengine watakuwa na mawazo
kama yako,huoni kama ni hatari kwa kuwa hamtakuwa tayari
kupokea matokeo kwa kuwa tu mnaamini kuwa "mtaibiwa
kura" na ccm hata kama haitakuwa hivyo?    Jibu
:   Kuiba kura ni ufisadi.  Wenye
historia ya ufisadi 
wanaotegemewa   kufanya kila giliba iwe
ni  kutumia  maneno machafu nay a vitisho,
kuteneneza  wenyewe  au kutumia 
taasisi   za wasomi uchwara  kufanya
tafiti uchwara   kuonyesha wanashinda. Lakini
ukweli utabaki pale pal—maamuzi ya mamilioni ya Watanzania
maskini ambao wamefukarishwa na utawala wa serikali ya CCM
ni tarehe 25 Oktoba 2015. Tusubiri.

Nitashukuru ikiwa maswali  haya yatapatiwa majibu.

Asante

______________________________
Without "Ethical Culture" there is No Salvation for Humanity

______________________________
A D D R E S S
John J. Malata
Tutor. Vikindu TC
P.O  Box 16268
DAR ES SALAAM
TANZANIA 
Mobile:    +255 782366090
Blog:http://pengotz.blogspot.com/

Ananilea Nkya
 E-mail:ananilea_nkya@yahoo.com

--------------------------------------------
On Sat, 9/19/15, 'Malata.' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>
wrote:

Subject: Re: [wanabidii] CCM WANAJIDANGANYA
To: "wanabidii@googlegroups.com"
<wanabidii@googlegroups.com>
Cc: "mabadilikotanzania@googlegroups.com"
<mabadilikotanzania@googlegroups.com>
Date: Saturday, September 19, 2015, 11:47 AM

Kwako Mama
Nkya

 

Salaam!!

Kwa muda mrefu
nimekuwa nikifatilia mwenendo wa mijadala unayochangia
katika majukwaa
mbalimbali. Wewe ni mmoja wa watu/wanaharakati
mliojipambambanua mbele ya jamii
kwa muda mrefu na kutuaminisha kuwa ninyi watu wa aina
gani.

 

Nimesoma kwa
umakini sana makala yako uliyoipa jina "CCM
WANAJIDANGANYA", kimsingi ni makala nzuri japo sio
bora kama ambavyo
nilitegemea kitu bora kutoka kwa mtu wa kariba
yako.

 

Napenda
kujadili sana mada hiyo ila tafadhali naomba nisaidie
majibu
ya maswali yangu
yafuatayo yanayotokana na mkanganyiko nilioupata kwa
maneno
yak ohayo.

 

(A) Umesema
"…Chama cha Mapinduzi (CCM) na 
serikali yake  wanapaswa  wasijidanganye  kwamba kwa
kumteua Dr
John Magufuli kuwa mgombea  wa Urais  chama hicho
kimekuwa
kisafi..."

1.      Je,
usafi na AU uchafu wa chama unatokana na nini?

2.      Kwa  mtazamo wako CCM si kisafi? Ulitegemea
CCM
wafanye nini ili kuwa safi katika kipindi hiki kuelekea
uchaguzi mkuu?

3.      Je,
Unaamini katika "KUJISAHIHISHA"?

 

(B)       
Umesema "…Hivyo hakuna mamtiki yoyote kwa CCM kutumia
propaganda kwamba  kwa
mgombea wake wa Urais  kupata watu kwenye mikutano ya 
kampeni
basi  tayari kimeshinda kwa asilimia 69.3…… Kama 
umati wa watu 
ndicho kigezo  cha ushindi  wa 
CCM ….".

1.      Bila
shaka ni wazi kuwa unatambua kuwa CCM ni taasisi na si
kijiwe cha wahuni. Kwa
maendeleo endelevu ya Taasisi yoyote ni budi iwe na
idara/kitengo maalumu kwa
ajili ya M & E. N a kama taasisi bila shaka CCM ina
"policy kuhusu namna ya
kutathimini mwelekeo wake.

2.      Je
ni dhambi kwa taasisi kufanya tathmini na kutoa matokeo
kwa
umma?

3.      Una
ushahidi gani wa kutuaminisha kuwa CCM wametumia kigezo
cha
wingi wa watu
katika kampeni kutoa tathimini yao?

4.      Je
 propaganda  ni nini na kwa nini?

5.      Je,
unachokifanya ni sehemu ya hizo propaganda au?

 

(C)  Umesema
"…Rais  Jakaya Kikwete katika kipindi
ccha utawala wake  amesafiri nje ya nchi mara 409  na
safari hizo
ziligharimu  shilingi  trilioni 4.5……Maana yake
angalao kila mwaka
Rais alisafiri nje ya nchi mara  40 akipoteza siyo tu
fedha
alizotumia kwa
safari hizo bali pia muda  mwingi wa kuwatumikia
Watanzania…."

1.      Katika
maelezo yako hayo hapo juu,je unaweza kutuainishia bajeti
ya
serikali kwa Idara
ya Itifaki kwa mwaka kuanzia mwaka 2005 hadi
sasa?

2.      Kama
hujakurupuka na kumeza matango poli kasha kuwatapikia
watanzania kuhusu jambo
hilo, Je unaweza kutuaninishia  kutuainishia safari hizo
na bajeti yake
kwa
kila safari ili tujiridhishe na tarakimu uliyotaja
hapo?

3.      Unaposema
alipoteza muda wa kuwatumikia watanzania kwa hizo safari,
Je
zilikuwa safari
zake binafsi [I mean was it for the personal issues/family
matter or for the
sake of our country?

4.      Ikiwa
unaamini, kama mimi ninvyoamini kuwa zilikuwa safari za
kikazi; Je unaweza
kuueleza umma wa Tanzania Impact ya kila safari ya
Mh.Raisi
with reference to
matumizi kwa kila safari?

 

(D) Umesema
"…Je CCM  na  serikali ya CCM
yake  mwaka huu  2015  watatumia kwa 'goli la
mkono'
kuzuia
maamuzi  ambayo wananchi wa Tanzania  watakuwa
wamefanya 
kupitia sanduku huru la kura kuhusu hatma ya uongozi wa
nchi
yao …?"

 

1.      Napata
shida kuitafakari kauri hii,Je umetumia kigezo gani
 kusema " ..watanzania watakuwa wamefanya
kupia
sanduku huru.." Je tayari una majibu ya jambo ambalo
hatujalifanya? Kama hivyo
ndivyo ni hatari sana kwa kuwa ni sawa na mtu anayeingia
uwanjani akiwa na
matokeo mkononi.Nini kitatokea ikiwa
atashindwa?

2.      Ikiwa
na wengine watakuwa na mawazo kama yako,huoni kama ni
hatari
kwa kuwa hamtakuwa
tayari kupokea matokeo kwa kuwa tu mnaamini kuwa
"mtaibiwa
kura" na ccm hata
kama haitakuwa hivyo?

 

Nitashukuru ikiwa
maswali  haya yatapatiwa majibu.
Asante


 ______________________________
Without
"Ethical Culture" there is No Salvation for
Humanity
______________________________
A D D R E S
S
John J.
Malata
Tutor.
Vikindu TC
P.O  Box
16268
DAR ES
SALAAM
TANZANIA 

Mobile:   
+255 782366090
Blog:http://pengotz.blogspot.com/




     On Friday, September
18, 2015 10:54 PM, 'Leonard Elias' via Wanabidii
<wanabidii@googlegroups.com>
wrote:

   

  Kaz nzuri sana mama
Inkya
Nadhan mkapa anaigiwa na hofu na ccm
ikianguka igakuaje kuhusu yy na mali zake ndo maana ana
weweseka

Sent from my
iPhone

> On Sep 18,
2015, at 19:26, 'ananilea nkya' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>
wrote:
>
> CCM
WANAJIDANGANYA
>
>
Na Ananilea Nkya
>
>
Chama cha Mapinduzi (CCM) na  serikali yake  wanapaswa 
wasijidanganye  kwamba kwa kumteua Dr John Magufuli kuwa
mgombea  wa Urais  chama hicho kimekuwa kisafi na na
hivyo
kinaweza kuwatumikia wananchi na kuondoa umaskini
unaoumiza
mamilioni ya wananchi nchini hivi sasa.
>

> Hakuna chama chochote cha siasa
duniani kimeweza kujisafisha kikiwa madarakani.
>
> Zaidi siyo dhambi
wala aibu  kwa chama cha siasa kushindwa uchaguzi. Ni
jambo
la kawaida na ni heshima pia kama chama cha siasa
kinakubali
kushindwa uchaguzi ikiwa imetokea hivyo.
>
> Chama cha siasa
kinaposhindwa uchaguzi na kukubali kushindwa kinastahili
kupongezwa na kuheshimiwa.
>
> Hivyo hakuna mamtiki yoyote kwa CCM
kutumia propaganda kwamba  kwa mgombea wake wa Urais 
kupata watu kwenye mikutano ya  kampeni basi  tayari
kimeshinda kwa asilimia 69.3. Huku ni kujidanganya na
kudanganya umma.
>
>
Kama  umati wa watu  ndicho kigezo  cha ushindi  wa 
CCM  takwimu hizi zinapingana  na hiki kigezo  kwa
sababu  viko vyama vingine pia ambavyo vimekuwa vikipata
umati mkubwa wa watu kwenye mikutano—tena wanaokwenda
kwa
hiari na gharama zao.
>
> Je vyama hivi na vyenyewe vikifanya
propaganda na kutangaza kwamba kutokana na wingi wa watu
wanaohudhuria  mikutano yao vinaweza kushinda kwa
asilimia
80 nchi itakuwa imewekwa katika hatari  kiasi gani 
baada
ya uchaguzi ?
>
>
CCM na serikali yake  inapaswa kutambua kuwa   siasa
za
ushindani  katika nchi zikiendeshwa  vema bila chama
chochote kuendesha propaganda kwa lengo la kubaki
madarakani
hata  wakati kimekataliwa  na umma  ni kuvuruga amani
na
kuongeza umaskini katika nchi.
>
> Imetokea katika nchi kadhaa duniani 
vyama  vilivyotawala muda mrefu vimeondoka madarakani na
nchi  hizo zikabaki salama na kupiga hatua kubwa ya
kimaendeleo.
>
>
Mfano nchi jirani za  Kenya na Zambia  vyama  vikongwe
vimeshindwa  na  vyama vingine vimepewa ridhaa na
wananchi
wan chi hizo na  vimeendesha nchi bila matatizo yoyote na
maisha ya wananchi yanasonga mbele.
>
> Vyama vingi vinawezesha chama kinachopewa
ridhaa  kikishindwa kutekeleza ahadi zake kupunzishwa 
kwa
muda ili kujipanga  upya nan a kwa kufanya hivyo
kinalazimika  kuacha jeuri dhidi ya wananchi, uzembe ,
ufisadi na rushwa.
> Chama cha siasa 
kikishapunzishwa  kwa muda na kujisafisha, hulazimika
kubuni  sera nzuri za maendeleo na  mikakati ya
kuzitekeleza  na chaguzi zinazofuata kikiomba tena ridhaa
kwa wananchi na kinakubaliwa.
>
> Hapa ndipo mfumo wa vyama vingi unakuwa na
manufaa kwa  nchi  husika.  Kuondoa umaskini miongoni
mwa
wengi na kuiletea nchi maendeleo.
>
> Vinginevyo rasilimali za nchi zinabaki
kunufaisha watawala wachache na wawekezaji wa nje katika
zama hizi za utandawazi wizi, soko holela na
utandawaziwizi
wa zama  za ukoloni mpya kibepari   duniani 
unaofukarisha  mafukara mamilioni ya wananchi.
>
> Wanaoitetea  CCM
ibaki madarakani wanapaswa kujiuliza :  Ni kwa  nini 
CCM
ing'ang'anie madaraka  na isipewe muda wa
kupunzika, kujitafakari, kujisafisha na kupata nguvu  na
maono na sera  ya mapya za  kuongoza nchi yetu ili
Tanzania ipae kimaendeleo?
>
> Ni kwa nini nchi yetu iendelee kuongozwa
na  CCM  ilichochoka kiasi kwamba sera zake kila uchao
zinazaa mamilioni ya wananchi maskini wa kutisha 
wakiwepo
wanachama wengi wa CCM  na  huku viongozi wakiwa
matajiri
wa kutishwa kutokana na ufisadi, rushwa, uzembe, uvivu na
watawala kutafuna fedha za wananchi  kwenye miradi ya
umma  na kujipangia safari za nje ya nchi tena kwa
kupanda
ndege daraja la kwanza kwenda kuomba  misaaada  kama
neti
za mbu au kuchukua digrii ya heshima?
>

> Hebu fikiria  kwa mfano  Mwenyekiti
mwenza wa UKAWA,  James  Mbatia  ameweka bayana kwamba 

Rais  Jakaya Kikwete katika kipindi ccha utawala wake 
amesafiri nje ya nchi mara 409  na safari hizo
ziligharimu  shilingi  trilioni 4.5.
>

> Maana yake angalao kila mwaka Rais
alisafiri nje ya nchi mara  40 akipoteza siyo tu fedha
alizotumia kwa safari hizo bali pia muda  mwingi wa
kuwatumikia Watanzania.
>
> Mbatia alisema  safari hizo za nje
zingepunguzwa kwa asilimia 80 zingepatikana  fedha 
ambazo  zingetosha  kujenga  vyuo vikuu 80 nchini 
kila
chuo kikigharimu shilingi bilioni 50.
>

> Aidha fedha  hizo  zingeweza
kujenga  vyuo  vya ufundi 200 nchi nzima kila chuo
kikigharimu bilioni 20. Kadhalika  fedha hizi zineweza
kujenga hospitali 100  na kila hospitali  ikigharimu
bilioni 30.
>
> Je
kwa hali hii kuna   Mtanzania hata awe mwana CCM 
mwenye
akili  timamu  na anayeipenda Tanzania kwa dhati kabisa
na  anayeweka  mbele maendeleo  ya nchi yetu na 
mamilioni ya watu wake  ambaye  atatelea  CCM
iendelee 
kuongoza nchi yetu miaka mingine mitano kuanzia tarehe 25
Oktoba mwaka huu 2015?
>
> Ni mwanaCCM  wa aina gani asiye na
huruma  na mamilioni ya Watanzania wanaoteseka kwa
umaskini  ambaye atataka  CCM iendelee kuwa madarakani 
huku watawala  wakijinufaisha  kwa kusafiri nje ya nchi
kwa fedha ambazo zingeweza  kutoa  elimu bora  hadi
chuo
kikuu, huduma bora za afya maji safi na salama au kujenga
barabara au viwanda vya kutoa ajira ?
>

> Mbona hata CCM wenyewe wanajua kuwa 
sera za  chama chao hakiuziki  katika uchaguzi wa 
mwaka
huu  na ndiyo sababu badala ya kuuza chama na sera zake 
wanauza mgombea wao wa urais Dr John Magufuli?
>
> Hata hivyo 
wananchi wanafahamu kuwa  makubaliano ya uongozi wa 
nchi
ni kati ya chama/vyama vinavyoomba uongozi  wa  nchi 
na
wananchi na siyo kati ya mgombea  Urais wa chama  fulani
na wananchi.
>
> Hii
ina maana kuwa  mwisho mwa siku ni chama/vyama husika
vinavyoomba ridhaa ya kuongoza nchi  ndivyo
vitawajibika 
kutekeleza ahadi zake kwa wananchi. Ahadi
zisipotekelezaka 
uchaguzi unaofuata wananchi wanachukua maamuzi sahihi
kupitia sanduku huru la kura.
>
> CCM isijidanganye  kuwa  Dr Magufuli 
ndiye  CCM maana CCM ni taasisi ni chama cha siasa na kwa
taratibu za uchaguzi  makubaliano ya kuongoza nchi 
hufanyika  baina ya vyama vya siasa  na wananchi na siyo
baina ya mgombea  Urais na wananchi.
>

> Makubaliano ya kuongoza nchi 
yanakuwa ni kati ya vyama  vya siasa na wananchi kwa
sababu
mgombea   kama binadamau anaweza kuondoka  katika
chama 
kwa sababu mbali mbali lakini chama cha siasa kama taasisi
kinabaki,  hakiondoki na hivyo  kitakuwa kitadaiwa 
utekelezaji wa  ahadi zake  kwa wananchi.
>
> Hebu fikiria kama 
vyama  vinavyounda  UKAWA vingekuwa vimeingia 
makubaliano na  mtu  mmoja  mmoja mfano CUF  
(Prof
Ibrahim Lipumba) au  CHADEMA (Dr  Wilbroad Slaa).  Je
leo
hii  UKAWA ingekuwa ipo  na kuendelea kufanya kazi nzuri
ya kisiasa  kwa  maendeleo ya nchi yetu kama ambavyo
imekuwa ikifanya hadi sasa?
>
> Kwa  hiyo ni  vema  wanaCCM na viongozi
wa CCM  katika uchaguzi wa mwaka huu 2015  wakaanza
kujiandaa kisaikolojia kwamba CCM inaweza  ikashindwa au
ikashinda kwenye uchaguzi  badala  ya  kufanya
propaganda
zinazoashiria kuwa  hakiko tayari kuondoka madarakani
hata
kama kitakuwa kimekataliwa na wananchi kwenye sanduku huru
la kura.
>
> Aidha
ni muhimu hasa viongozi waandamini ndani ya CCM na
serikali
yake   kutambua kuwa  katika siasa za vyama vingi 

maendeleo ya nchi yanapatikana kwa haraka zaidi   na
umaskini miongoni mwa wananchi walio wengi unapungua kwa
kasi endapo uchaguzi unafanyika kwa uhuru na haki.
>
> Kadhalika  watambue
kuwa ni kawaida  na ni afya kwa nchi kama chama
kilichokaa
madarakani muda mrefu kikishindwa  kukubali  kushindwa
bila kulazimisha ushindi kwa goli la mkono.
>
> Vile vile  watambue
kuwa kitendo chochote  cha CCM na  watawala  wa
serikali
ya CCM kuzuia  chama  kingine cha siasa  kisiongoze 
nchi yetu  katika kipindi cha miaka mitano ijayo,  hata
pale wananchi watakapokuwa wameamua hivyo  ni sawa  na 
kukwamisha maendeleo ya Tanzania   na  kutaka
mamilioni ya
Watanzania wanaoishi kwa umaskini waendelee  na umaskini
wao   kwa miaka mingine mitano.
>
> Hiyo haitakubalika. Itakuwa ni sawa na 
kuanzisha vurugu zenye lengo la  kuitumbukiza nchi yetu
katika  vitendo vya kusababisha  kuvunjika kwa amani.
> Ni pale tu demokrasia ya vyama vingi
inapofanya kazi bila hila kwa Tume ya Uchaguzi kufanya
kazi
kikamilifu, ubunifu bila upendeleo,  chama kilichopo
madarakani  kuacha kuendesha kampeni  kwa kutumia lugha
za
vitisho, dharau kwa  vyama vingine, giliba, rushwa,
uchakachuaji na  ubabe ndipo wananchi    na nchi 
inaponufaika  na mfumo wa vyama vingi vya siasa kwa
kutokomeza umaskini.
>
> Mwaka 2011, Rais Kikwete aliwahi
kuulizwa  na mwanahabari mmoja kutoka  nje ya Tanzania
kuwa ni kwa nini Tanzania  ni maskini ili hali ina
rasilimali nyingi za asili zinawezeza kutumika kutajirisha
Watanzania wote  na alimjibu kuwa hajui.
>
> Hata hivyo,  Rais
Kikwete anapaswa kutambua kuwa moja ya sababu
zinazochangia
umaskini  kuitafuna Tanzania  ni  CCM  kutokukubali 
kwa dhati  mfumo wa vyama vingi   vya siasa 
ufanye
kazi  inavyotakiwaili hali chama hicho  kimeshaacha 
falsafa ya Ujamaa iliyoendana na mfumo wa chama kimoja
nabadala yake imebeda falsafa ya ubepari inayoendeana na
mfumo wa vyama vingi.
>
> Kuthibitisha kuwa CCM bado haijakubali
mfumo wa vyama vingi ufanye kazi, Rais mstaafu 
Benjamini  Mkapa  akipiga Kampeni  kule Bukoba 
katika 
uchaguzi wa mwaka huu 2015 alikaririwa na baadhi ya vyombo
vya habari akisema kuwa  vyama vya upinzani  havistahili
kupewa  dhamana ya kuongoza  mpaka vifikishe umri wa 
miaka 50.
>
>
Wananchi wanajiuliza ni  kwa nini  CCM isubiri hadi
vyama
vya upinzani  vizeeke  ndipo vipewa ridhaa ya kuongoza
nchi?
>
> Hii
kauli  ya  Mkapa inatukumbusha Watanzania zama za ASP na
TANU vilipokuwa vinapigania uhuru kutoka  kwa  wakoloni 

mbapo  mwishoni mwa miaka ya 50 ambapo wakoloni  kama
anavyofanya Mkapa walikuwa wanadai kuwa  ASP na TANU 
vilikuwa bado ni vyama  vichanga hivyo havikustahili 
kupewa  ridhaa  ya kuongoza Tanzania (Zanzibar na
Tanganyika).
>
>
Lengo la wakoloni   lilikuwa ni kuchelewesha uhuru.
Hata
hivyo TANU NA ASP vilikaza buti  na  viliwapuuza 
wakoloni na uhuru   wa nchi yetu ulipatikana bila
kuchelewa
kama walivyotaka wakoloni.
>
> Hivyo  watawala wa CCM wanaotaka CCM 
iendelee kuongoza nchi  wanapaswa kujiuliza  ni kwa
nini 
Watanzania wakubali  kuacha mali za  nchi  yao zikiwa
zinatajirisha  watawala wachache na wawekezaji  
kutoka 
nje ya nchi  ili hali mamilioni ya Watanzania  wakiwepo
wanachama wa  CCM  wengi wakiendelea kubaki maskini na
mafukara?
>
> Ni kwa
nini CCM isipumzishwe kwa miaka mitano kiweze kujitafakari
na kujipanga upya kama kweli kimekubali mfumo wa vyama
vingi
kwa dhati kabisa na kwa kutambua kuwa  siasa za vyama
vingi
zikiendeshwa kwa uhuru ndipo  nchi yetu itaweza
kukomesha 
uzalishaji wa mafuriko ya wananchi maskini katika nchi
yetu
ili hali nchi yetu ni tajiri wa mali asili—madini, gesi,
maji, misitu an ardhi yenye rutuba?
>
> Nadhani Rais mstaafu  Mkapa  alitoa
kauli hiyo au kwa vile hajatafakari vema manufaa ya siasa
za
vyama vingi  na umuhimu CCM  kukubali kushindwa uchaguzi
kwa uhuru na haki  kwa kusikiliza na kuheshimu maamuzi ya
umma .
>
>
Vinginevyo  alitoa kauli hiyo kwa sababu  hajaishi
maisha
wanayoishi  Watanzania walio wengi ambao wanateseka kwa
umaskini.
>
> Hata
hivyo ni vema Rais mstaafu Benjamin Mkapa akatambua kuwa 
wajibu wake  kama Rais mstaafu kwa taifa hii kwa sasa 
siyo  kulinda maslahi ya watawala wachache wa  CCM 
ambao
wanadhani  kwa CCM kuondoka madaraka  Tanzania
itaharibikiwa.
>
>
Mkapa pia anapaswa kuwaonya  baadhi ya viongozi wa CCM
wanaopanda majukwaani na  kuweweseka  kwa kusema kuwa 
CCM  kamwe haiwezi kuviachia vyama vya upinzani 
kuongoza
nchi.
>
>
Wanaoweweseka  na kusema  CCM  haiwezi kuviachia vyama
vya upinzani  kuongoza nchi wanathibitisha kuwa 
serikali
ya CCM inaendesha mfumo wa  vyama vingi  kama geresha
lakini watawala wa serikali ya  CCM hawako tayari kuona
CCM
inaondoka  madarakani kwa amani hata kama wananchi
watakuwa
wameamua hivyo kupitia sanduku huru la kura. Hii
haikubaliki.
>
>
Ndiyo sababu  baadhi ya wananchi  wanajiuliza: Je CCM 
na  serikali ya CCM yake  mwaka huu  2015  watatumia
kwa
'goli la mkono' kuzuia maamuzi  ambayo wananchi wa
Tanzania  watakuwa wamefanya  kupitia sanduku huru la
kura
kuhusu hatma ya uongozi wa nchi yao ?
>

> Kama  serikali  ya CCM  watafanya
hivyo, watakuwa wamejidanganya na kudanganya Watanzania na
ulimwengu kuwa  Tanzania nchi nchi ya vyama vingi vya
siasa.
>
> Badala
yake Tanzania itakuwa inaendelea kuwa nchi ya chama kimoja
cha siasa maana vyama vingi vya siasa havitaweza 
kuendeshwa kwa uhuru na ufanisi unaopaswa  bila  kuwekwa
misingi ya kuondoa umaskini nchini  --misingi ambayo 
itawekwa na  Katiba Mpya inayotokana na maoni ya wananchi
haitaandikwa.
>
>
Lakini zaidi  CCM na serikali yake watakuwa
wamejidanganya
kwa sababu watakuwa wamefanya maamuzi mabaya  ya kutaka
kuendelea  kutengeneza bomu la mamilioni ya Watanzania
maskini na kikundi kidogo cha watawala matajiri wa kutisha
hali  ambayo  itahatarisha  zaidi amani na utulivu wa
Tanzania tuendako.
>
> Tukifika  hapo wawekezaji wa kigeni  na
wafadhili (wakoloni wa zama hizi mpya za utandawazi wizi

watachekelea sana  maana watakuwa wamepata mwanya mpya
wa 
kuibia zaidi Tanzania . Mungu ibariki Tanzania tusifike
huko
>
> Note:
Naruhusu  anayetaka kuchapisha Makala hii afanye hivyo.
Lengo tuelemishane kwa manufaa ya nchi yetu na wananchi
wote.
>
> Ananilea
Nkya
E-mail:ananilea_nkya@yahoo.com
>
> --
> Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
>
> Kujiondoa Tuma Email
kwenda
> wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com 
Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
>
> Disclaimer:
> Everyone posting to this Forum bears the
sole responsibility for any legal consequences of his or
her
postings, and hence statements and facts must be presented
responsibly. Your continued membership signifies that you
agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules
and Guidelines.
> ---
> You received this message because you are
subscribed to the Google Groups "Wanabidii"
group.
> To unsubscribe from this group
and stop receiving emails from it, send an email to
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
> For more options, visit
https://groups.google.com/d/optout.
>
<CCM WANAJIDANGANYA.docx>

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda

wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com 
Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to
this Forum bears the sole responsibility for any legal
consequences of his or her postings, and hence statements
and facts must be presented responsibly. Your continued
membership signifies that you agree to this disclaimer and
pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message
because you are subscribed to the Google Groups
"Wanabidii" group.
To unsubscribe
from this group and stop receiving emails from it, send an
email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit
https://groups.google.com/d/optout.

     


--

Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

 

Kujiondoa Tuma Email kwenda

wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com 
Utapata Email ya
kudhibitisha ukishatuma

 

Disclaimer:

Everyone posting to this Forum bears the sole
responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and
hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and
Guidelines.

---

You received this message because you are subscribed to
the
Google Groups "Wanabidii" group.

To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.

For more options, visit
https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com 
Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the
Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit
https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment