Tuesday, 10 February 2015

Re: [wanabidii] Lowassa anadanganywa na wabunge wanaonyemelea mamilioni aliyonayo

dadaaaaaa
mlete wako anaefaaaa, cc huyo ndio anatufaaa mnaponda tuuuu lakini haji na majibu so nani atafaaaaa, to us EDO fit the post


From: 'Hildegarda Kiwasila' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com>
To: wanabidii@googlegroups.com
Sent: Tuesday, February 10, 2015 2:45 PM
Subject: Re: [wanabidii] Lowassa anadanganywa na wabunge wanaonyemelea mamilioni aliyonayo


Baba wa Taifa alisema "Pokea na kula hela zake lakini ikifika wakati wa Kura usimpigie au kumchagua!!"
Ataona kupigiwa makofi na watu kujaa halafu kura NIL lakini walimpamba na kura hawakumpa. Ni fundisho kwa vizee vinavyong'ang'ania madaraka. Abaki Monduli akiwafundisha nduguze kwa lugha ya kwao wafuge kisasa, waache kuhamahama na kuharibu amani na uchumi wa wenzao. Toka Monduli, simanjiro, Loliondo, ngorongoro na maelfu ya mifugo to Morogoro, Kilosa-Kilombero, Mgeta Juu milimani
kukausha mto Ruvu, hadi kisarawe-Rufiji, Kilwa-Lindi au Iringa-Mbararli, Mbeya-Sumbawaka kote huko kulishia mashamba, kupiga watu, kuua na kuharibu vyanzo vya maji eti wanaonewa hawana ardhi kwao. Huko simanjiro na ndani ya mbuga hifadhi ya ngorongoro-wanalima kwa plough na trekta. Hela za Tanzanite mererani na vijiji vyao wanachimba madini-wanalimbikiza mifugo. Wanakaribisha wenzao wa Kenya wanajazana NCAA na Loliondo na maeneo mengine. ardhi yao inakuwa kame mifugo imezidi na wanalima wanyamapori wanakosa chakula nao waliwekwa nao kwa vile hawalimi sasa wanalima hawanunui mahindi tena. Hata mkulima hawezi kuachwa analima misitu hifadhi anafukuzwa na kuadhibiwa. Wao wataua watashinda kesi si wanahela za kuhonga? Ranchi za ufugaji kisasa zipo kibao na misaada ya wazungu kuwasaidia kujikimu kibao ila kubadirika utata. Hata ardhi ilikopimwa makwao hawazingatii. Kila mtu akae kwao na atumie ardhi sustainably hakuna kuhamahama kwa kilimo wala mifugo. Wabunge
wasioonyesha mfano bora katika kusaidia kuboresha maisha wa watuwao majina yao yasipitishwe na vyama vyao. Huwezi ukaendelea kumchagua Diwani na Mbunge ambaye atakuwa anaandamana tu daima kupinga serikali ila sio yeye kuamka kuingia mtaani aishipo na kwenda jimboni kuhamasisha watu wake na kuongoza mabadiliko. Mbunge na diwani wanaona kinyesi kinatiririshwa na wakazi mtaani kwake na kutupa taka ngumu ndani ya mitaro tena mipya ya halmashauri-naye anaruka kinyesi haongei na wanaotiririsha; mbunge anahudhuria ndoa ya msichana mtoto wa kiaka 12 kwa libaba la miaka 68 naye anakuwa ngeni rasmi!? Anaona raia wanaziba njia na kuweka usalama mdogo moto ukiwaka-anapita anawasalimia kwa kuwachekea na kuwapungia mkono. Unahangaika na Urais, uwaziri wakati pale ulipo hatuoni tofauti kimaendeleo kwa raia wako-Hufai!!

--------------------------------------------
On Tue, 10/2/15, 'godfred mbanyi' via Wanabidii <wanabidii@googlegroups.com> wrote:

Subject: Re: [wanabidii] Lowassa anadanganywa na wabunge wanaonyemelea mamilioni aliyonayo
To: wanabidii@googlegroups.com
Date: Tuesday, 10 February, 2015, 14:hagua12


Declare interest first! Upo kundi gani??? Membe, Makamba
Jnr, Pinda, au???


--------------------------------------------
On Tue, 2/10/15, Juma Mzuri <jumamzuri@gmail.com>
wrote:

  Subject: [wanabidii] Lowassa anadanganywa na wabunge
wanaonyemelea mamilioni aliyonayo
  To: wanabidii@googlegroups.com
  Date: Tuesday, February 10, 2015, 1:10 PM
 
  Lowassa
  anadanganywa na wabunge wanaonyemelea mamilioni
  aliyonayoNa
  Mwandishi MaalumMAGAZETI
  kadhaa yatolewayo kila siku nchini, Jumatatu Februari 9,
  2015, yaliongozwa na habari kuu kuhusu
  Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa kwamba 'anang'ara
  katika mbio za urais'.Katika habari hiyo, magazeti hayo
  yote yalinukuu kauli za wabunge saba wa CCM wanazodaiwa
kuwa
  walizitoa katika hafla iliyotajwa kuwa "ya aina yake"
ya
  chakula cha jioni, Jumamosi iliyopita.Lakini katika hali
isiyokuwa ya
  kawaida, hafla hiyo kamwe haikutaja ilikofanyika zaidi ya
  kuelezwa tu kuwa "nyumbani kwa kigogo mmoja wa CCM",
  Kilimani mjini Dodoma.Kwa
  nini kigogo huyo alifichwa utadhani hafla hiyo ilikuwa
  haramu au kwamba iliambatana na vitendo vya
kihalifu?Wabunge waliotajwa na kunukuliwa
  wakizungumza ni Deogratius Ntukamazina (Ngara), Diana
  Chilolo (Viti Maalum – Singida), Stephen Ngonyani au
  'Profesa Maji Marefu' (Korogwe Vijijini) na Mary
  Chatanda ambaye pia wa Viti Maalum (Tanga) na Katibu wa
CCM
  wa Mkoa wa Singida.Wengine ni
  Kapteni John Komba (Mbinga Magharibi), Mussa Azzan Zungu
  (Ilala) na Yahya Kassim Issa ambaye ni mbunge wa Chwaka,
  Zanzibar.Wote walinukuliwa
  wakimwelezea Lowassa ambaye pia ni Waziri Mkuu wa zamani
  kwamba "ni kiongozi bora, kiongozi makini, chaguo la
  Watanzania" na kadhalika.Ntukamazina kwa mfano alisema:
  "Kule kwangu Ngara wananiuliza yule waziri mkuu
aliyeleta
  hizi shule za kata yuko wapi? Mimi nawajibu atarudi na
kila
  mtu mitaani anataja jina lako, kwa hiyo sauti ya wengi ni
  sauti ya Mungu".Wasiwasi
  kuhusu habari hiyo
  Kila gazeti, licha ya habari hiyo kuandikiwa ukumbini na
  isiyokuwa ya uchunguzi, yote hayakutaja jina la mwandishi
  kwa kusema ni "Mwandishi Wetu, Dodoma", halafu zote
  zinafanana kwa kila kitu katika mambo yafuatayo:
  (i) Kutotaja jina la kigogo wa CCM aliyeandaa hafla hiyo
  kuwa ni nani;(ii) Idadi ya
  wabunge waliohudhuria hafla hiyo imetajwa na kila gazeti
  kuwa 150 utadhani kila mwandishi aliwahesabu au
walihesabiwa
  mlangoni, kisha hesabu yao ikatangazwa hadharani;(iii)
Wabunge waliotajwa kwenye
  magazeti hayo kuwa waliongea ni walewale; na(iv) Wabunge
hao pia wametajwa kwa
  mtiririko uleule, nukuu zilezile, namna ileile huku kila
  kitu kikiwa kinafanana kama barua iliyopigwa photocopy na
  kusambazwa huko kote;Katika
  hali hiyo, yapo mambo kadhaa ya kutilia wasiwasi kwa
  wasomaji makini ambayo ni pamoja na haya yafuatayo:
  (i) Kuna kila mwelekeo wa kuwa hafla hiyo iliandaliwa kwa
  agizo au kwa gharama za Lowassa mwenyewe;(ii) Kuna kila
mwelekeo wa kuwa
  hafla hiyo iliandaliwa maalum kwa ajili ya kampeni za
urais
  za Lowassa, lakini ukakosekana umakini wa kutosha ili
  kufanikisha siri iliyolenga kuwadanganya Watanzania;(iii)
Wabunge waliozungumza
  inaelekea kwamba waliandaliwa maalum, halafu inawezekana
  kuwa maneno waliyozungumza walipewa au walielekezwa na
  Lowassa mwenyewe ama na washauri wake; na(iv) Habari hiyo
imeandikwa na
  mwandishi mmoja, kisha ikasambazwa katika magazeti hayo
yote
  kwa gharama za mwanasiasa na mbunge huyo ikiwa ni sehemu
ya
  kampeni zake za urais.Ili
  kuthibitisha vinginevyo, magazeti hayo inabidi yajibu
  maswali makubwa yafuatayo kwa wasomaji wake ambao ni
pamoja
  na mimi kwamba ilikuwaje habari hiyo ifanane kwa zaidi ya
  asilimia 75 kuhusu:(i)
  Mpangilio wa wabunge walivyozungumza katika hafla
  hiyo?(ii) Ilikuwaje idadi ya
  wabunge waliozungumza na kunukuliwa na magazeti hayo yote
  iwe ileile?(iii) Ilikuwaje
  mtiririko wa habari hiyo ufanane kiasi hicho kwa magazeti
  yote na kuonekana kuwa imeandikwa na mwandishi mmoja kama
  kweli ni tofauti?(iv) Kama
  habari hiyo iliandikwa na waandishi tofauti, wapi
  walikokutana, kisha wakakubaliana kuwa nukuu zao zote ziwe
  ni zilezile?(v) Wapi
  waandishi hao walikokutana na kukubaliana kuwa vilevile
  mtiririko wa nukuu zote hizo ufanane kama mayai?Mfano
ninaomaanisha ni kama pale
  Mbunge wa Ngara, Deogratius Ntukamazina aliponukuliwa na
  magazeti hayo yote akisema:"…Oktoba tutakuwa na
uchaguzi
  mkuu wa kumchagua kiongozi atakayesukuma mbele nchi
  yetu."Sote tunafahamu chama
  chetu bado hakijatangaza utaratibu, lakini sisi wabunge
  marafiki zako tunakuomba muda ukifika uchukue fomu kwa
  sababu unatosha".Nukuu hiyo
  ya neno kwa neno ipo katika kila gazeti, halafu imeandikwa
  kwa staili ileile na kwa aya zinazofanana utadhani
ilipigwa
  'photocopy' na kusambazwa huko kote.Mbali na hapo,
habari hiyo pia
  inafanana kwa kila kitu katika magazeti hayo yote ambapo,
  pale palipoandikwa bila ya kunukuu neno kwa neno inakuwa
  hivyo kwa kila gazeti, na pia kila paliponukuliwa (quoted)
  napo panakuwa vilevile utadhani pamefanyiwa
  'scanning'.Aidha,
  magazeti hayo yote yamemwandika Chilolo kwa aya moja yenye
  maneno 22 tu kama ifuatavyo:"Kwa upande wake, Mbunge wa
Viti
  Maalum, Diana Chilolo (CCM) aliunga mkono kauli ya
  Ntukamazina kwa kusema Lowassa ni chaguo la
wengi".Wasomaji wote makini walioisoma
  habari hiyo ndani ya magazeti hayo au baadhi yake hakuna
  mashaka kwamba waligundua kuwa ilitengenezwa maalum kwa
  ajili ya kumbeba Lowassa katika harakati zake za
  urais.Pamoja na ukweli kuwa
  kila mwanasiasa anayetafuta madaraka ya uongozi wa umma
huwa
  na njia zake mwenyewe za kutafuta ushindi, lakini mbinu
hiyo
  ya Lowassa haiwezi kuwadanganya walengwa ambao hasa ni
  viongozi waandamizi wa CCM.Wabunge aliowatumia kutaka
  kufanikisha mkakati wake huo wa kuitisha CCM ili iogope
kuwa
  isipomteua kugombea urais itaondoshwa madarakani na
  wapinzani, kwamba asipoteuliwa yeye ili kusimama katika
  kinyang'anyiro hicho basi chama hicho kitashindwa kuna
  wengine wamekubali kutumika kiasi hicho kwa sababu
inaelezwa
  kwamba ana pesa nyingi.Ukimwondoa mtu kama Ntukamazina
  ambaye ameshasema kuwa hagombei tena ubunge mwaka huu,
  Chatanda anajipanga kutaka kugombea ubunge wa jimbo la
  Korogwe Mjini huku Komba au 'Maji Marefu' nao
  wakikabiliwa na hali ngumu majimboni kwao.Ili waweze kupata
ushindi kwanza
  kwenye kura za maoni za ndani ya CCM, wabunge hao inabidi
  kila mmoja awe na kiwango kikubwa kabisa cha pesa za
  kampeni, fedha ambazo hakuna hata mmoja aliyenazo.Wote
wanategemea kiinua mgongo
  ambacho kila mmoja atalipwa na serikali baada ya muda wao
wa
  sasa kumalizika kiasi cha miezi mine ijayo, lakini
  wanafahamu kwamba hazitoshi kuwapa ushindi
  wanaoutafuta.Kwa mfano, Komba
  amekuwa akitishiwa hadi kufilisiwa na benki anakodaiwa
mamia
  ya mamilioni ya fedha alizokopa pamoja na riba, deni
  linalotishia hadi kukamatwa kwa mali zake kwa sababu
  ameshindwa kulipa.Wote
  walijitolea mhanga kumsifia hadharani mbele yake mwenyewe
  siyo kwa sababu eti wanamuunga mkono kwelikweli, bali
  walifanya hivyo kwa sababu wanayataka mamilioni ya pesa
  zake.Wanataka kumdanganya kwa
  sababu wanataka fedha hizo ili nao pia wakahangaikie
ubunge
  kwa muhula mwingine kwenye majimbo yao. Walikuwa hawamsifu
  eti kwa sababu anatakiwa kiasi hicho kuwa Rais wa Serikali
  ya Awamu ya Tano.Wote
  wananyemelea mamilioni ya fedha anazodaiwa kufadhiliwa au
  kwa yeye mwenyewe kujikusanyia kwa namna moja ama
  nyingine.NI MTAZAMO WANGU
 
 
 
  --
 
  Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
   
 
  Kujiondoa Tuma Email kwenda
 
  wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com 
Utapata Email ya
  kudhibitisha ukishatuma
 
   
 
  Disclaimer:
 
  Everyone posting to this Forum bears the sole
responsibility
  for any legal consequences of his or her postings, and
hence
  statements and facts must be presented responsibly. Your
  continued membership signifies that you agree to this
  disclaimer and pledge to abide by our Rules and
Guidelines.
 
  ---
 
  You received this message because you are subscribed to
the
  Google Groups "Wanabidii" group.
 
  To unsubscribe from this group and stop receiving emails
  from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
 
  For more options, visit
https://groups.google.com/d/optout.



 

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com 
Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility
for any legal consequences of his or her postings, and hence
statements and facts must be presented responsibly. Your
continued membership signifies that you agree to this
disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the
Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails
from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit
https://groups.google.com/d/optout.

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com

Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com  Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma

Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.


0 comments:

Post a Comment