Thursday 26 February 2015

[wanabidii] KANISA LISILO RASMI LA MCHUNGAJI JOSEPHAT GWAJIMA LAVUNJWA KAWE

KANISA LISILO RASMI LAVUNJWA KAWE

Mchungaji Josephat Gwajima afungishwa virago Kawe!



Kanisa la lisilo rasmi la mchungaji Mchungaji Josephat Gwajima  lililokuwa likiendesha shughuli zake kinyume na taratibu katika viwanja vya Tanganyika Packers  Kawe,wilaya ya Kinondoni,jiji Dar limeamuriwa kuondoka mara moja  na kuwacha eneo hilo wazi kwa ajili ya maendeleo ya watu wa kawe. Kanisa hilo ambalo kwa muda mrefu  lemekuwa likiendesha shughuli zake kinyume na taratibu na kusababisha usumbufu na kero kubwa za makelele kwa wakazi wa maeneo hayo.  Katika Barua iliosainiwa na Meneja wa Mkoa wa Kinondoni wa shirika la nyumba  la Taifa  imesisitiza kwamba pamoja na kutambuliwa umuhimu wa kanisa hilo kuendesha  shughuli zake lakini shirika hilo  halitaweza kutoa ruhusa  kwa  kanisa hilo kuendelea kufanya  mahubiri katika viwanja hivyo,kwani shirika hilo limeshaanza  kutumia Viwanja hivyo kwa maendeleo ya wananchi wa KAWE ikiwa ni ujenzi wa makazi  n.k  Bw Masika ametoa siku 30 tu  ili Mchungaji Gwajima kujitayarisha na kuwacha viwanja hivyo wazi kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.

Mchungaji Josephat Gwajima afunge virago

--
Send Emails to wanabidii@googlegroups.com
 
Kujiondoa Tuma Email kwenda
wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com Utapata Email ya kudhibitisha ukishatuma
 
Disclaimer:
Everyone posting to this Forum bears the sole responsibility for any legal consequences of his or her postings, and hence statements and facts must be presented responsibly. Your continued membership signifies that you agree to this disclaimer and pledge to abide by our Rules and Guidelines.
---
You received this message because you are subscribed to the Google Groups "Wanabidii" group.
To unsubscribe from this group and stop receiving emails from it, send an email to wanabidii+unsubscribe@googlegroups.com.
For more options, visit https://groups.google.com/d/optout.

0 comments:

Post a Comment